Duh! Rais Samia amkataa mama mnyonge aliyetaka kumlilia kama Magufuli. Nenda kakae…

Usiongee mambo usiyoyajua! Suala la Msingi Ni Moyo wa Mtu kuguswa na mambo ya watu wengine! Magufuli ukiachana na hao Waliokuwa wanam-face directly amesaidia watu wengi sana kimya kimya walioonewa. Sasa huyu ambaye hakurupuki ameshamsaidia nani?
Yaani nikuambie jamaa yangu! Huyu bibi kama unashida kubwa ya level ya kumuona huwezi kumuona labda uwe fisadi hapo sawa! Ila mganga njaa sahau! Ndo maana hatakiwi kabisa kufanyia ziara kuwatembelea wananchi! Labda kutembelea kwenye matukio tena mikoa mikubwa basi!
 
Yule jamaa angekuwepo leo watu wangefukuzwa kazi wengine kutukanwa matusi ya nguoni.
 
lakini ndio kashaongea kiukali mkuu na haliwezi kubadilika. Hili halina utofauti na watu wengi walivyokuwa wakimlalamikia kwa vitu vingi tu mtangulizi wake na bado hakuwasikiliza wala hakubadilika.
Tena Kama Ni ukali amesahau Magufuli alikua anawaambia wananchi waende wakakae na mavi Yao nyumbani.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Mama Samia yuko sahihi swala unakuta lilishaenda mahakamani au watendaji wanalifanyia kazi mtu sababu tu kaona raisi kaja anataka kubururuza taratibu ziheshimiwe si kwamba Mama Samia hatalifuatilia ila kitakachofuata kama huyo mama alionewa wahusika wajiandae

Hata Magufuli alilalamika sana mambo hayo kuwa watendaji wapo nawalipa mishahara na marupurupu kibao inakuwaje hawashughulikii kero za wananchi hadi mimi nije?

Huyu mama watendaji wasimchukulie poa hasa wale wanaopelekewa kero za wananchi na kuwadharau kitakachowakuta wasije kupiga yowe humu kuwa mama Mkororofi alishasema ukinizengua nakuzengua

Watendaji badilikeni
Magufuli alikuwa halipi watendaji mishahara, hakuwa ni hizo pesa. Mishahara yote ya wafanyakazi wa serikali nchi hii inalipwa na serikali kutoka kwenye kodi za wananchi.
 
Maadamu waandishi wa habari wameweza kuona tukio hili na kulirekodi, kazi kwenu mhimili wa 'nne' muende kumhoji kwa kina shida za mama huyu ili vyombo vinavyohisika pamoja na taasisi ya urais ifahamu matatizo ya watanzania.

Media House vyombo vya habari Tanzania msijiegemeze tu kuwahoji watu maarufu tu au ma celebrity , social influencer Kiki, zao au scandal zao na hili la mama huyu mlifuatilie ifahamike shida ni nini.

The term Fourth Estate or fourth power refers to the press and news media both in explicit capacity of advocacy and implicit ability to frame political issues
 
Usiongee mambo usiyoyajua! Suala la Msingi Ni Moyo wa Mtu kuguswa na mambo ya watu wengine! Magufuli ukiachana na hao Waliokuwa wanam-face directly amesaidia watu wengi sana kimya kimya walioonewa. Sasa huyu ambaye hakurupuki ameshamsaidia nani?
Ni kweli alikuwa anasaidia watu kimya kimya kama Ben Saanane na wenzake.
 
Back
Top Bottom