PakavuNateleza
JF-Expert Member
- Sep 9, 2009
- 1,106
- 1,297
Faiza, unaweza kusema mengi lakini ukweli ambao huwezi kuukwepa ni kuwa kuna tofauti kubwa kati ya safari aliyoifanya Mwigulu na Dr. Slaa. Hii safari ya Dr. ukiitazama kiundani ilijielekeza zaidi katika elimu, tekinolojia na uchumi lakini safari ya Mwigulu ilikaa kiupambe wa kisiasa. Hapo kuna tofauti kubwa sana katika vision.
Japo Dr. Slaa siyo kiongozi wa kiserikali lakini mtazamo wa safari yake umekaa kitaifa na kiuongozi zaidi kuliko safari ya Mwigulu. Lakini pia ukiangalia safari za Rais wetu, Nazo ni tofauti sana kimtazamo na hizi za Dr. Slaa. Safari za Kikwete zimekaa zaidi kisherehe, kuufurahia Urais, na ndiyo maana kulikuwa na taarifa hapa kuwa Prof. Muhongo alikwishawahi kutamka kuwa haelewi inakuwaje mtu mwenye upeo kama wa JK ameweza kuwa Rais wa nchi kwa sababu yeye anamwona ni mtu asiyejua mambo mengi sana.
JK, kuna mambo ya kujifunza kutoka kwa Dr. Slaa, anapoenda nje ya nchi afanye nini kuliko kuzurura na kugeuka kuwa ombaomba asiyekuwa na malengo yoyote ya kubadilika toka kuwa unayesaidiwa na kila nchi na kuwa nchi inayoweza kuisadia Dunia. Leo Tanzania inaonekana kama ni burden kwa mataifa mengi anayoyazungukia Kikwete kwenda kuomba kila mara.
Chief umeongea Mambo ya msingi sana.