don-oba
JF-Expert Member
- Dec 8, 2011
- 1,387
- 677
Swali kuhusu wanafunzi kukosa mkopo, amedai kila mwanafunzi chuo kikuu ana haki ya kupata mkopo na kuwaasa wanafunzi kudai haki zao hata kwa maandamano kwani serikali hii ya JK ni vipofu na viziwi. Swali kuhusu wamejiandaa vp kuingia madarakani 2015, amedai chama kina mkakati mathubuti amesema hawezi kuutaja hapa kwani ni kutoa mbinu kwa maadui. Amemgeukia mayor wa jiji la Mwanza na amemwambia yeye ndiye bosi wa manispaa anayetambulika kisheria. Mkuu wa mkoa yupo chini yake kwani mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya kazi yake ni ku-facilitate tu hawana lolote ndomana chama kimependekeza ktk katiba mpya ya sasa iwaondoe wakuu wa mkoa na wilaya kwani hawana tija ktk maeneo yao.