Kwa hiyo watu wasiokuwa watumishi wa kanisa au misikiti wamejitenga na mungu? ushauri wa Dr ndio suluhisho la kidiplomasia na si risasii..listen them! Kuwe na transparency kwenye mikataba watu waelewe faida zake...simple! USHIRIKISHAJI UMMA-Maendeleo kwa kila mtu!
au umesahau Mtwar wengi ni CUF na slogan yao inasema HAKI SAWA KWA KILA MTU!!
Wakoloni walipokuja Africa na kwa tamaa zao za kuzoa Mali za Waafrika zilipozidi,walitunga Mkakati wa kuwamaliza waafrika taratibu ili angalau kupunguza resistance ya kuwakataa.....ili wabaki waafrika wachache...na walifanya hivyo kwa kuja wenyewe na kuwaua waafrika,
Baadaye wakagundua njia ya Kisayansi zaidi,kuwagombanisha waafrika ili waanze kupigana wenyewe kwa wenyewe...wao wakawa wanasaidia hili kwa kutengeneza silaha na kuwauzia makundi yote mawili yanayopigana
Walipoona waafrika wanapigana wenyewe kwa wenyewe,halafu likaja na balaa jingine la kupunguza kizazi cha waafrika kutokana na maradhi hasa ya Ukimwi....wakaona sasa inatosha,haina haja ya wao kutumia nguvu sana za kuwaua waafrika,kwani sasa mnauana na mnajiua wenyewe na ngono zembe...lengo lao la kuhakikisha kizazi cha waafrika kinavurugika na kinapotea linatimia.
SASA HIVI,WAMEKUJA NA MBINU MAHSUSI ZAIDI,HASA KATIKA NCHI ZILE WANAZIONA ZIKO STABLE SANA UTAWALA WAKE....MBINU HIZI NI KUWAINGILIA BAADHI YA MAKUNDI YA WATU KUPITIA MIGONGO YA WANAHARAKATI,VYAMA VYA SIASA,WAFANYABIASHARA WAKUBWA,VIKUNDI VYA DINI NA TAASISI NYINGINEZO,KUWEZA KULETA VURUGU NA CHOKOCHOKO MBALIMBALI KILA KUKICHA,KWA JINA LA "KUTETEA MASLAHI YA WANYONGE"!
NINASEMA KWAMBA,DHAMBI HII YA KUPANDIKIZA CHUKI KWA WANANCHI DHIDI YA SERIKALI YEYOTE DUNIANI,HATA KAMA ITAFANIKISHA LENGO LA KUWAWEKA WATU MADARAKANI,KAMWE HAITATOKA KWA WANANCHI VIZAZI NA VIZAZI.....UKIINGIA KWA UPINDE UTATOKA KWA UPINDE...UKIIINGIA KWA DAMU UTATOKA KWA DAMU!
Watu wanawashawishi Wananchi kufanya mambo ambayo wao tu ndio wanajua malengo halisi,wakiwahadaa wananchi kwamba watapata maisha bora......
Sakata la Mtwara kuna Watu ambao wanalala usiku na mchana wakiombea likuzwe na kukuzwa ili labda machafuko yatokee nchini na kuonyesha serikali iliyopo madarakani haifai......ili labda wananchi wachukie serikali yao,katika hali hiyo,makundi hayo yatapata ULAJI katika patashika hizo.
Na kinachonitia wasiwasi...kuna wasemaji na waandikaji na wakumbushiaji wazuri sana wa suala la Mtwara kuanzia hapa jukwaani mpaka mitaani,ambao ukifuatilia thread zao,utajua kwamba wao ndio pia wahamasishaji wakubwa sana na wazuri wa vyama fulani vya siasa hasa kunapokuwa na mikutano ya vyama hivyo......hili ni lazima mtu kama mimi linipe mwanga kwamba kuna vyama viko nyuma ya sakata hili,na lengo lao kubwa ni kuchochea mgogoro huu kwa faida yao wenyewe.....
Nina hakika kwamba watu wenye nia OVU na Taifa letu watashindwa....wawe wanatoka serikalini,wawe wanatoka katika makundi mengine,watashindwa....Tanzania ni ya kwetu sote....Tanzania ni nchi ya Kidemokrasia,ndio maana kila mmoja anafanya kwa raha zake anachokifanya sasa hivi...lakini daima siku zote ukweli hushinda....kundi lililo na ukweli katika vita hii ndilo litakaloshinda....hatutaki vurugu Mtwara.