Dr Slaa: Mtwara wamepuuzwa!

Dr Slaa: Mtwara wamepuuzwa!

kwanza anatakiwa akamatwe kwa uchochezi na kauli mbiu zake za uchochezi mfano nchi haitatawalika,mpaka kieleweke.slaa ni janga la kitaifa.

Mkuu kuna uzi humu jamvini unaelezea jinsi membe alivyo nyuma ya huu mtanange huko mtwara vp yeye hatakiwi kukamatwa kwa uchochezi?
 
Unajipofusha na kuziba masikio kwa pamba ee??? Kuiba mke wa mtu na kuvunja ndoa, kuasi kanisa na kula pesa za ujio wa papa huku ukijiita padre kwako ni mazuri hayo??

Mkuu hujasikia kuwa Josephine ameshapewa talaka na hakimu wa wilaya ya kinondoni wiki hii?
Pili, Kanisa katoliki wameshasema mara nyingi kuwa Dr Slaa aliondoka kwa utaratibu na hawana ugomvi naye, wewe umetoa wapi habari hii?
Tatu, hiyo hoja ya fedha za ujio wa papa mbona Rais wa Maaskofu alishajibu wakati wa uchaguzi wa Arumeru hoja hii ilipoibuliwa na Stephen Wasira? Kwa kukumbusha Askofu Rwaichi alisema kuwa hakuna fedha zilizotumika vibaya wakati wa ujio wa papa. Hope umenielewa mpaka hapo, ukitaka zaidi pia ninaweza kukupa detailed information kwa kuwa mimi ni mzaliwa Mbulu ambayo kikatoliki Mbulu na Karatu ziko jimbo moja.
 
Nyinyi watu mna akili ndogo sana! Watanzania wa leo hawahitaji Dr. Slaa kuona ujinga unaofanywa na Serikali. Wanaangalia wenyewe kwenye TBC na kujua nini cha kufanya na upuuzi unaofanywa na hawa viongozi waliopewa nafasi katika Serikali kwa kigezo cha ku balance dini badala ya uwezo wao wa kufikiri.

Waambie wana CCM wenzio haya: kwamba kuna eneo zaidi ya moja katika Taifa ambako watu wanafikiri kama wana Mtwara. Watu hawa hawatatumwa na DR. Slaa. Watajituma wenyewe, na polisi hawatatosha....

wewe siyo mzima uanadhani watu hawajui kuwa slaa ndiye mchochezi namba moja ngoja wakati wake unakuja atakutana na watoto wa kiume atajuta kuacha upadri.
 
ndugu embu tumia akili uskurupuke tuu kma una hoja kaa kimya dr slaa akuhasi bali alijiuzulu kutokana na sheria za kanisa katholic

nani kakudanganya au alivyokuja chadema aliwadanya hivyo mwabieni aseme vizuri asiwatania, yani na wewe unapata nguvu ya kuja humu na kudanganya watu kuwa na aibu.
 
hapa kunahitajika elimu ya kuwafahamisha haki zao ni zipi na siyo mabomu.,alisema Dr Slaa.
Watu wana protest mpaka wanakufa kudai haki zao wewe unasema hawajui haki zao, wapewe elimu.

Viongozi wetu wanapokosea ni kutudhania Wanachi ni majuha wa kutupwa, Kikwete anasema vurugu ni za kuchochewa, yani sisi wenyewe wananchi anaamini hatuwezi kupinga mambo fyongo mpaka tuamshwe, tuchochewe.

Slaa nae, ungedhani angekuwa na falsafa tofauti kuhusu uelewa wa Wananchi, lakini nae anasema Wananchi hatujui haki zetu tupewe elimu!
 
Unataka Doctor mzima aanze kuzidumisha fikra sahihi (kwa maCCM) za mwenyekiti wakati facts zipo wazi kuwa mabavu hayatakiwi.

Top Down approach kwa maendeleo ya watanzania tena kwa manufaa ya viongozi wa CCM is coming to an end, na mtarudishwa kwenye mstari tu, mlijisahau sana nyie mkadhani hii nchi ni yenu na familia zenu.

Hamjishangai, kila siku mna mgogoro mara na CDM mara na waandishi wa habari, mara madaktari, mara wananchi; lazima mjitathmini haiwezekani makundi yote haya yakawa yanakosea tu na nyie ndio mpo right.

huyo unaye mwita dk muulize tofauti na elimu ya dini kasoma chuo gani na kozi ipi yawezekana unaita tu dk hata humjui vizuri.
 
huyu mzee anahangaika tu amechoka kuchochea suala la kuchinja sasa kahamia kwingine,swali dogo hivi mzee slaa na jk nani aliyejitenga na mungu,kwa sababu mzee slaa aliasi dini na kufanya uovu mwingi ndani ya kanisa sasa uko wapi uadilifu wa slaa.

Hebu tukumbushe kauli ya Slaa kuhusu kuchinja, alisemaje mkuu! Dr Slaa hajatoa kauli kuhusu kuchinja usimlishe maneno bila sababu. Kwa upande Mtwara Slaa na Mbowe wanataka wananchi wa mtwara wasikilizwe na wakubaliane na serikali kuhusu uwekezaji unaotaka kufanywa kwenye ardhi yao. Je, unakubali kuwa mtwara wamesahauliwa na serikali ya ccm kwa miaka yote ya uhuru?
 
Umeshatubu kuhodhi fedha za ujio wa papa? ,, Pia tambua mdomo wako una madhara sana ktk Taifa hili unapotoa kauli ambazo zinapelekea kuvunjika kwa Amani.
 
nani kakudanganya au alivyokuja chadema aliwadanya hivyo mwabieni aseme vizuri asiwatania, yani na wewe unapata nguvu ya kuja humu na kudanganya watu kuwa na aibu.

Wewe ndo umekuwa msemaji wa Kanisa siku hizi?Hiyo mada isha-expire ilikuwa ni mbinu tu ya Mafisadi kumchafua Dr.Vipi kuhusu ndoa ya Dr Slaa na huko nako mtakosa hoja ya kumchafua.Anawakata kilimi limi taratibu
 
huyu mzee anahangaika tu amechoka kuchochea suala la kuchinja sasa kahamia kwingine,swali dogo hivi mzee slaa na jk nani aliyejitenga na mungu,kwa sababu mzee slaa aliasi dini na kufanya uovu mwingi ndani ya kanisa sasa uko wapi uadilifu wa slaa.

Hivi na wewe unafuata dini gani ambayo inakufundisha uwongo? Swala la kuchinja bila aibu unasema alichochea Dr.Slaa? Kwa huyo wewe unajilidhisha kuwa huyo unayemshabikia hana dhambi au makosa. Haya ndugu yangu lakini Mungu hufanya kazi kupitia kwa watu. Mnawatesa WanaMtwara badala ya kuwasiliza na kuwaelimisha pale walipopotoka. Hakuna maendeleo bila maelewano na malidhiano. Nguvu ni swala la muda tu
 
kwanza anatakiwa akamatwe kwa uchochezi na kauli mbiu zake za uchochezi mfano nchi haitatawalika,mpaka kieleweke.slaa ni janga la kitaifa.

Wewe ni walewale, badala ya kutatua tatizo unashari kuongeza tatizo. To hell maCCM
 
Huu ni mtihani mwingine wa kifikra kwa slaa, hivi anadhani ataendelea kuwahadaa wananchi kupitia matatizo yao hadi lini??? Kwa hiyo anashangilia vifo vya askari na mali za umma zilizoharibiwa???


Hichi ulichokiandika kina uhusiano gani na kauli ya Slaa ya kwamba watu wa mtwara wasikilizwe? Kwani Slaa aliangusha gari?
 
pitia kauli ya rais na taarifa ya wazir mkuu ndani ya bunge, cdm wameinjinia vurugu za mtwara

Kwa hiyo Waziri Membe ni CHADEMA siku hizi?Sipati picha aibu aliyoipata yule Waziri wa Mambo ya Ndani kituko kuwahi kutokea katika historia ya Nchi hii tangu ipate Uhuru Bw Nchimbi kufuatia tuhuma zilizoibuliwa na Waziri mwingine Mh Hawa Ghasia.Yaani haya majitu kila kitu ni CHADEMA.
 
Back
Top Bottom