Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
Dr. W. Slaa, Katibu Mkuu wa Chadema
Wiki iliyopita iliwekwa mada hapa kuhusu Dr. Slaa ambaye ni katibu mkuu wa Chadema kuhusu mvao wake kila anapotokea ni magwanda tu hata iwe katika hafla ya kitaifa au shughuli nyingine za umma. Wengi walimshambulia hapa mtoa mada bila kujali maudhui ya hoja zake.
Katika picha hii leo unaweza kuona anapotoa tamko la Chadema kuhusu mafuriko yaliyolikumba jiji la Dar amebadili mvao, ingawa ni sare ya Chadema, lakini mvao huo umembadili kwa kiasi kikumbwa mwonekano wake tuliozoea kumwona. Hapa anaonekana ni rais mtarajiwa atakavyokuwa anaonekana anapotoa ujumbe mahsusi kwa taifa.
Asante Dr. Slaa kwa kuwa na sikio sikivu, ni dalili nzuri za uongozi wenye kuleta matumaini mapya kwa kizazi cha leo. Tutajitahidi kila inapowezekana kutoa mapendekezo na ushauri wa kufaa kutokana na tabia yako ya kuwa flexable, Thanks again.