Allah akulipe kila lililo jema
Asante Dr. Slaa kwa kutuunganisha watanzania
Allah akulipe kila lililo jema
Mumeo anaitwa Slaa?
unajibu swali kwa swali?
Eid Mubarak mkuu, Karibu CDM
mpeni matumaini afe kifo kisicho cha uchungu
Asante Dr. Slaa kwa kutuunganisha watanzania
Sasa Bakwata inahusika vipi na Chadema we mbwa mwenye udhu?
Lakini haukuhudhuria msiba wa mama zzk, hii yote kama mama yake zzk asingekuwa muislam, ama andekuwa mkristo, basi dr.slaa ungeenda, maana dr.slaa wewe ni mdini sana, na kila ufanyapo mikutano, huwa unaongelea dini ya kikristo tu, hii inaonesha huna upendo na dini ya kiislam, nakumbuka kuna siku ulikuja iringa viwanja vya mwembetogwa mwaka jana mwezi wa nne, ulitoa mfano kwa kusema, "sisi wakristo" tena mbele ya umati wa watu na kusahau kuwa pale kuna waislam wengi tu, sasa hii slaa nadhani wewe ni mnafiki wa kukejeri dini ya kiislamu
Hii michango nyenu imeonyesha ukomavu unao akisi mafundisho mema ya dini.
Mwenyezi Mungu awabariki nyinyi na familia zenu katika kipindi hiki cha sikukuu ya Eid.
Kila jema na lenye kheri lisiaponyoke.
Kafiri wewe kila mahali unawaka siasa hukui tuu au kwa sababu ya fadhila za kisiasa unazopata/ulizopata.Siasa si kila mahali hata ckukuu kama hizi unataka zimilikiwe na chama chako!Utakuwa lini.Hakuna jipya hapo drama za Chadema tu.
Kwenye chama hawawataki, salam za nini?
ﻭَﺩَّ ﻛَﺜِﻴﺮٌ ﻣِﻦْ ﺃَﻫْﻞِ ﺍﻟْﻜِﺘَﺎﺏِ ﻟَﻮْ ﻳَﺮُﺩُّﻭﻧَﻜُﻢْ ﻣِﻦْ ﺑَﻌْﺪِ ﺇِﻳﻤَﺎﻧِﻜُﻢْ ﻛُﻔَّﺎﺭًﺍ ﺣَﺴَﺪًﺍ ﻣِﻦْ ﻋِﻨْﺪِ ﺃَﻧْﻔُﺴِﻬِﻢْ ﻣِﻦْ ﺑَﻌْﺪِ ﻣَﺎ ﺗَﺒَﻴَّﻦَ ﻟَﻬُﻢُ ﺍﻟْﺤَﻖُّ ۖ ﻓَﺎﻋْﻔُﻮﺍ ﻭَﺍﺻْﻔَﺤُﻮﺍ ﺣَﺘَّﻰٰ ﻳَﺄْﺗِﻲَ ﺍﻟﻠَّﻪُ ﺑِﺄَﻣْﺮِﻩِ ۗ ﺇِﻥَّ ﺍﻟﻠَّﻪَ ﻋَﻠَﻰٰ ﻛُﻞِّ ﺷَﻲْءٍ ﻗَﺪِﻳﺮٌ
Wengi miongoni mwa watu wa Kitabu wanatamani lau wange kurudisheni nyinyi muwe makafiri baada ya kuamini kwenu, kwa ajili ya uhasidi uliomo ndani ya nafsi zao, baada ya kwisha wapambanukia Haki. Basi sameheni na wachilieni mbali mpaka Mwenyezi Mungu atapo leta amri yake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.
ﻭَﻟَﻦْ ﺗَﺮْﺿَﻰٰ ﻋَﻨْﻚَ ﺍﻟْﻴَﻬُﻮﺩُ ﻭَﻻَ ﺍﻟﻨَّﺼَﺎﺭَﻯٰ ﺣَﺘَّﻰٰ ﺗَﺘَّﺒِﻊَ ﻣِﻠَّﺘَﻬُﻢْ ۗ ﻗُﻞْ ﺇِﻥَّ ﻫُﺪَﻯ ﺍﻟﻠَّﻪِ ﻫُﻮَ ﺍﻟْﻬُﺪَﻯٰ ۗ ﻭَﻟَﺌِﻦِ ﺍﺗَّﺒَﻌْﺖَ ﺃَﻫْﻮَﺍءَﻫُﻢْ ﺑَﻌْﺪَ ﺍﻟَّﺬِﻱ ﺟَﺎءَﻙَ ﻣِﻦَ ﺍﻟْﻌِﻠْﻢِ ۙ ﻣَﺎ ﻟَﻚَ ﻣِﻦَ ﺍﻟﻠَّﻪِ ﻣِﻦْ ﻭَﻟِﻲٍّ ﻭَﻻَ ﻧَﺼِﻴﺮٍ
Mayahudi hawawi radhi nawe, wala Wakristo, mpaka ufuate mila yao. Sema: Hakika uwongofu wa Mwenyezi Mungu ndio uwongofu. Na kama ukifuata matamanio yao baada ya ujuzi ulio kwisha kujia, hutapata mlinzi wala msaidizi kwa Mwenyezi Mungu.
Allah akulipe kila lililo jema
Guys kuna vitu vya kushabikia na vile vya kutanguliza utaifa mbele, Sasa akitokea mtu akaingiza ushabiki kwenye mambo ya kitaifa na kijamii kama haya KUMPUUZA ni jambo la msingi sana
Wala haipendezi kwenye mitandao hii ya kijamii wapo Wakenya,Wauganda,Rwanda nk wanatusoma na kutujaji..Sipati picha wanatuona ni watu wa aina gani? Kama tunaweza kumtusi mtu kwa just salam Kheri na maombi kwa taifa zima basi ni nini KINATUUNGANISHA watanzania?
Ni vema tukawapuuza watu wa namna hii,, Kumpuuza mtu ni fimbo tosha na Karipio kali lisilo tumia nguvu, usipomjibu mtu ktk ujinga wake anao uandika hapa lazima atajigundua kwamba yeye nie mjinga kiasi gani..
Nikushukuru sana Dr Slaa kwa kuwatakia kheri wenzetu Waislam na Watanzania kwa ujumla ktk kusheherekea sikukuu hii muhimu kwa Waislam wote duniani, Niungane pia na Dr kuwatakia wenzetu Waislam sikukuu njema na yenye baraka tele..........Amin
BACK TANGANYIKA
Mkuu swala la waislamu kujisikia hawapendwi nchi hii ni kitu ambacho hakina uhalisia na kama ukipewa uhuru wa kwenda kuthibitisha haya kwenye mahakama huru kama za kimataifa wewe mwenyewe ndugu yangu hutakuwa na cha kusema maana ni kitu cha kuambiwa na wala hujawahi kukiishi wewe! Hebu toa experience yako binafsi ni lini na wapi ulishawahi kubaguliwa? Tumekuwa na maraisi wawili wakristo na wawili waislamu, kama kungekuwa na kunyanyasika kwa waislamu au wakristo basi tungekuwa tulishapigana maana kila Raisi angeingia madarakani na kupendelea dini yake na kuwanyanyasa wengine. Kama waislamu kweli wangekuwa wanayanyaswa basi Maraisi wa kiislamu wasingepigiwa kura na wakristo kwa sababu wangehofia kulipiziwa kisasi!
Mkuu tuache kufikiri kama watu ambao hawajaenda darasani maana kama sisi tulioenda darasani tunaanza kuchochea udini kwa maandishi hapa JF basi wale ndugu zetu ambao hawakubahatika kusoma wao watafanya nini? Hawa ni watu wakuambiwa na kutekeleza hawatapata muda hata wa kutafakari athari zake maana tayari kwa umasikini na shida zao hawana cha kupoteza!
Unaweza kuona ni vizuri kutumia propaganda za udini ukidhani unaiharibia chadema lakini kumbuka madhara yake ni zaidi ya kuiharibia chadema, hata hao ccm hawatapata kitu maana kama watu wakijua chadema ni wakristo tu basi wakristo wote wataisupport chadema na hapo ndo utakuwa mmwanzo wa utungu na mtakuwa mmeshachelewa hamtaweza kuwarudisha watu nyuma tena!
Lakini sishangai sana maana wapo watu nadhani hawana matumaini tena , wamefika mwisho na kwao sasa hivi ni "Bora tukose wote"
Kama sisi watu wa kawaida tungejua kinachotafutwa basi tungekuwa makini sana na kauli zetu za kuwagawa watanzania kwa dini zao maana zitatuasili wenyewe na wala sio wengine!
unatumia vigezo vipi kumjaji huyu ni muislam safi na huyu siye?sidhani hizi salam zinawahusu waislam alshabab,boroharam na genge la ponda,hizi ni salaam za waislam safi,wahubiri amani
Mkuu kati ya kikwete na Dr. Slaa mwisilamu ni yupi? Tuambie kikweta ana wake wangapi mbona watoto kibao na je mama wa hawa watoto wote alishawahi kuwaoa?
Acha kutumia argument za kitoto hapa sisi ni watu tunaoweza kupambanua mambo! Kawandanganyeni huko vijijini lakini siyo hapa JF! Na huko vijijini siku hizi shule za kata zimeamusha watu mtapata shida sana maana hamwezi kutawala kama mnavyotaka, ni either mkubali kupote heshima yenu na utajiri mlioupta kwa kuwanyonya masikini wa nchi hii or msipo kubali kubadilika mtang'olewa tu ni swala la muda tu and God is watching!