Dr. Slaa bado anayo kadi ya CCM?

Dr. Slaa bado anayo kadi ya CCM?

Nape hufikiri kwa kutumia masaburi
Hivi hata usiporudisha kadi Katiba ya CCM inasema hivi kuhusu uanachama:
7. (1) Mtu akikubali kuwa Mwanachama itabidi atekeleze haya yafuatayo:-
(a) Atatoa kiingilio cha Uanachama
(b) Atalipa ada ya Uanachama kila mwezi isipokuwa kama akipenda anaweza kulipa ada ya mwaka mzima mara moja.
(c) Atatoa michango yoyote itakayoamuliwa
(2) Viwango vya kiingilio, ada na michango vitawekwa na Halmashauri Kuu ya Taifa.
(3) Uanachama wa mwanachama utakwisha kwa:-
(a)Kufariki.
(b)Kujiuzulu mwenyewe.
(c)Kuachishwa kwa mujibu wa Katiba.
(d)Kufukuzwa kwa mujibu wa Katiba.
(e)Kutotimiza masharti ya uanachama.
(f)Kujiunga na Chama kingine chochote cha siasa.
(4) Mwanachama ambaye uanachama wake unakwisha kwa sababu yoyote ile hatarudishiwa kiingilio alichokitoa, ada aliyotoa wala michango yoyote aliyoitoa.

Nape, Katibu Mwenezi wa Chama anapaswa ajue haya.

My take:
Uongo na kuchafuana bado vinatumika kama mtaji wa kisiasa. Watu wameshaamka, tutumie mambo yenye maslahi ya nchi kufanya siasa.

Kama hajarudisha kadi, Nape anataka kuwaambia wana CCM kuwa Slaa bado mwana CCM?
Nnauye Jr, mtu akishaacha kulipa ada, au kujiunga rasmi na chama kingine si lazima arudishe kadi. Anakuwa si mwanachama kwa mujibu wa katiba ya CCM.
 
Slaa rudisha kadi ya watu kama hii habari ina ukweli wowote. Huwezi kame kuwatumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja.

Mkuu Radhia, kwani uanachama ni kuwa na kadi tu inatosha hata usipoilipia miaka kadhaa?
Kama ni hivyo basi asilimia kubwa ya wa-TZ ni wana CCM.
Lakini nijuavyo mimi ni kwamba mtu huhesabika kuwa mwana jumuia fulani iwapo anakuwa hai kwa maana ya kuhudhuria vikao na kutoa michango na ada kwa mujibu wa katiba ya jumuia husika.

Kwa mantiki hiyo tangu Dr. Slaa alipoondoka CCM yapata miaka kumi na ushee iliyopita, akaruhusiwa na NEC kugombea ubunge kule Karatu na kushinda mara mbili, na pia akagombea U-rais wa TZ kwa ruhusa ya NEC kwamba ana vigezo na bila kuwekewa pingamizi na CCM kwamba ana uwanachama kuwili!!!??? Inatia shaka.

Kama ni kweli basi NEC ni hatari na haifai kabisa, na kama si kweli basi aliyetoa kauli hiyo hastaili kuwa kiongozi wa chama au jumuia yoyote zaidi ya kupelekwa hospitali ya vichaa.
 
kweli shule na vyuo vyetu vina kazi sana kama ndio watu wanafikiri hivi. Kama hajarudisha manake kuwa anayo? Yaani hakuna uwezekano mwingine wowote ule? Mimi pia niliwahi kuwa na kadi ya CCM na hadi leo sijairudisha na sina mpango wa kuirudisha....

CLUE: Uanachama wa CCM unakomaje?

Kumbe mpo wengi ambao hamjarudisha! :becky:
 
Hata mi naskia ivo na anashirikiana vizuri tu na viongozi wa ccm na serikali ila kisiri sana

DR.SLAA ITUNZWE TU KAMA SOUVENIR KWA AJILI YA WATOTO WA WATOTO WAKO KWA MAKUSUDI YA KUWAJULISHA KUWA ONCE UPON A TIME KATIKA NCHI HII KULIKUWA NA CHAMA CHA MA......... KILICHOTUMIA KADI AINA HII KUFILISI NCHI HII AU:glasses-nerdy: UNAWEZA KUIPELEKA MAKUMBUSHO YA TAIFA KAMA UKIPENDA!
 
Kwa wafuatliaji wa siasa za hapa kwetu Tanzania, mtakumbuka ya kwamba Dr. Slaa alikuwa mwanachama mtiifu wa CCM kabla ya kuasi chama na kukimbilia CHADEMA.

Hata hivyo, mpaka leo hii Dr. Slaa hajawahi kukabidhi kadi ya CCM.

Huku ndo kufilisika kifikira na Kihoja.

Huyu NAPE anatuona sisi watanzania tukoje.

KADI ya Chama ni document ya mwenye kadi na sio kama kitambulisho ambacho kina clause inayosema ni maly ya mwajiri ikitokea kufukuzwa au kuacha kazi kwa njia yoyote ile kitambulisho kinarudishwa kwa mwajiri kwani ni mali yake.

Kadi ni kumbukumbu ya mwanachama, ikitokea kuhama au kuachana na hicho chama kadi inabaki kwake kwani hakuna kipengele cha kurudisha na uhai wa mwanachama umeahinishwa kwenye katiba ya chama.

mimi hapa nilikuwa mwanachama wa UVCCM, CCM, baadaye DP, MMD, UDP,NCCR, CHADEMA baadaye kuhachana na siasa na kadi zote bado ninazo kama documentary. Ila sijawahi kujiunga na CUF.

Wasira ya NCCR aliirudisha lini?
Kaburu ya CDM alirudishalini?
NAPE ya CCJ alirudisha lini?
Festo Limbu, NSANZUNGWAKO, MTEMVU, HIZA, Ngawahiya, nk. kadi za vyama walivyowahi kujiunga ziko wapi?

NAPE STOP KIDDING!!!!!!! we are not kids as you are!!!!!
 
nape hajui kazi yake akijua basi ccm itaendelea kutawala, mi navyothani jk alimchagua ili tu awe anamzungumzia dr slaa. Nape hapitishi wiki bila ya kumtaja dr slaa hata kama ni warsha ya serikali. kuwa kiongozi wa ccm lazima uwe mjinga ili uweze achana na ukweli ndo utaweza kuongoza, mi naamini hivyo.

Sio NAPE tu.

Nimeona VIDEO hapa jamvini ya KAGASHEKI akimsema MEYA wako kuwa mambo anayosema meya au kupanga yataleta maswali na ugumu wa maisha siku Dr. Slaa akifika BUKOBA.

Ona watu hawa wasivyo lala kwa ajili ya Dr. Slaa.
 
Nape has devilish mind! Watu wameficha mapesa Uswisi, Kagoda, Migodi, Wanyama hai, meno ya tembo! Umekaa kimya na unawasifu! Kila siku Dr. Slaa. Stupid boy
 
Duh yaani CDM kiboko wameanza kumchafua Dr. Slaa! Jana nilikuwa kijiweni na vijana tunakunywa kahawa nikasikia wanasema Dr. Slaa alitumwa na Nyerere kuingia upadri ili ajue huko mapadri wanafanya nini na hakuwa na utashi wa kweli. kwa kifupi wanasema alitumwa na serikali na ni mtu wao hadi leo. Vijana wakawa wanaonyesha wasiwasi juu ya Dr. Slaa na wakasema afadhali Mbowe. Leo naona hii post nimeshangaa. Naona mitandao ya Urais ndani ya CDM inafanya kazi kwa umakini mkuu.

Kila mwenye akili zake timamu hapa, bila shaka yoyote kwa hii comment yako, anapaswa kukuelewa vyema. Aisee yaani it is extremely tooooooooooooooooooooo low and cheap mpaka kiasi cha mtu kufikiria mtu anayejiita GT anaweza kupoteza muda kuandika cheap kiasi hiki. Mwenzetu twaona kichwa watumia kuweka au kutunzia kofia kama unavyoonekana pichani. Pole mkuu Kimbunga, but honestly this is tooooooo low kwa mtu kama wewe hata kama bado unaamini katika CCMism au kuumia na CCMmonia.
 
mbona yule mwanamama diwani aliyefukuzwa uanachama CDM kadi yake kairudisha CCM ..... visa versa

Nape ... kwanini unapokea kadi za wanavhama wa CDM wanaohamia CCM na kwanini usiwaambie wazirudishe kwenye chama walichokuwa (walichohama)
 
Kila mwenye akili zake timamu hapa, bila shaka yoyote kwa hii comment yako, anapaswa kukuelewa vyema. Aisee yaani it is extremely tooooooooooooooooooooo low and cheap mpaka kiasi cha mtu kufikiria mtu anayejiita GT anaweza kupoteza muda kuandika cheap kiasi hiki. Mwenzetu twaona kichwa watumia kuweka au kutunzia kofia kama unavyoonekana pichani. Pole mkuu Kimbunga, but honestly this is tooooooo low kwa mtu kama wewe hata kama bado unaamini katika CCMism au kuumia na CCMmonia.

Mkuu Tumaini Makene hii post imekuwa tangia September kama sikosei. Kwa kuwa jana Nnape kasema hayo basi unanishambulia! Nilichokisema nilikisikia kwa wanywa kahawa wenzangu siyo mimi nimetunga. Mkuu kama unataka uthibitisho njoo kijiweni kwetu tunakokunywa kahawa; ni kijiwe cha vijana wa CDM
 
Last edited by a moderator:
Mimi sikurudisha kadi ya ccm,Niliichambia pamoja na ugumu wake.Sikujua watu tunaangaika kununua toilet paper wakati kuna kadi nyepesi za kijani.
 
Jamania akina nape tafuteni sera,acheni kuchezea akili za wasomi,mbona mnazididi kujichafua,hii si tz ya 1960 's when more poverty,ignorance and diseases.
 
Duh yaani CDM kiboko wameanza kumchafua Dr. Slaa! Jana nilikuwa kijiweni na vijana tunakunywa kahawa nikasikia wanasema Dr. Slaa alitumwa na Nyerere kuingia upadri ili ajue huko mapadri wanafanya nini na hakuwa na utashi wa kweli. kwa kifupi wanasema alitumwa na serikali na ni mtu wao hadi leo. Vijana wakawa wanaonyesha wasiwasi juu ya Dr. Slaa na wakasema afadhali Mbowe. Leo naona hii post nimeshangaa. Naona mitandao ya Urais ndani ya CDM inafanya kazi kwa umakini mkuu.
Wewe unayejiita Great thinker, waliposema hivyo ukakubali? Na umeona hili ndilo la kushirikisha Great thinkers.

Jamani huku ni kufilisika kubaya. Kama CCM imebaki na utoto wa namna hii kama mtaji, na ndio inaongoza nchi basi Watanzania tunapaswa kuhurumiwa sana!
 
Nnauye Jr naomba tuachane na ya huyo dr slaa; tuje kwenye chama chetu na nomba kuuliza hili:
- hivi wale mafisadi uliwapa SIKU 90 au MIAKA 90 YA KUJIVUA GAMBA!!?? Baada ya hapo sasa ndio tuamie kwa kina slaa hebu tuamie kwenye chama chetu
 
Last edited by a moderator:
Mimi siko CCM na ninazo kadi zao 5:........yaani bila kadi ulikuwa hupati haki yako....
  1. Niliyopewa nikiwa sekondari
  2. Niliyopewa nikiwa JKT
  3. Niliyopewa ili nijiunge Chuo Kikuu
  4. Niliyopewa ili nianze kazi
  5. Niliyopewa nilipo omba kiwanja

POrojo za vijiweni , watu siku hizi wanalewa kahawa.
Ili uaminike mkuu hebu ziscan utuwekee mtandaoni, mara tutasikia nilichana!

Uongo mtupu!
Sidhanii kama ulikuwa mjanja miaka hiyo.
 
Nyingine hizi hapa.
IMG_1589.JPG
 
Back
Top Bottom