Dr. Slaa bado anayo kadi ya CCM?

Dr. Slaa bado anayo kadi ya CCM?

Huyu Dr. Slaa ni ndumilakuwili; CCM anataka na CDM anatamani
 
Naona kama title haibebi ujumbe uliowasilishwa. Nafikiri Dr. Slaa ametoa ufafanuzi juu hasa ya suala zima la umiliki wa kadi na kuonyesha kwamba ni kitu kidogo kisichohitaji mjadala. Lakini hajakanusha kumiliki kadi. However, naungana na Dr. Slaa kwamba ni uendawazimu kuligeuza suala la kadi kuwa ni agenda inayohitaji attention ya kitaifa.
 
  • Thanks
Reactions: kix
Masinikini CCM.Ndio inakufa vibaya hivi?Lini kinana anaondoka ?anaonekana kaja mshikia JK nafasi wakati akijiandaa tafuta mtu mwingine.Inaelekea line haziendi through ili awapigie wengine simu kama Mangula. Uongozi wa CCM kuanzia taifa siku hizi hauna tena mvuto kwa watu wakachukue kadi wenyewe.
 
Waambieni CCM chini ya mzee wa fitna- Nape waanzishe lingine.

Hawana jipya kwa sasa PakaJimmy, labda tusubiri kile chungu cha majungu kiive wakilete mezani na kuanza mambo yao ya kuwalisha wadanganyika majungu.
 
Last edited by a moderator:
Mduda nenda kwenu Kalenga kachukue jimbo....Kipera wanakufahamu,kabebe hata udiwani uache chaki
Ni kweli kabisa Watanzania ni watu wa ajabu sana. Yanapo kuja mambo ya msingi kama polisi kujichukulia sheria mkononi, watu kuiba raslimali za taifa, viongozi kushindwa kutimiza ahadi walizotoa wakati wa kampeni hakuna anayejadili maswala hayo kiundani. Yanapokuja mambo ya kipuuzi kama mtu kutangaza kutokewa na mwujiza, mtu kuwa na kadi ya CCM wakati yeye si CCM watu wengi sana wanaingia kwenye mjadala. Hili linatufanya tuibiwe mchana kweupe. Yaani ni shida maana vijana wote maskini wako kijiweni wanajadili mpira. Kweli aliyetuloga roho yake ilishaacha mwili muda mrefu sana.
 
Miongoni mwa viashiria vinavyo onyesha kuwa ccm inakufa ni propaganda za kijinga zisizo msaidia mtanzania kutoka kwenye lindi na mzingo wa umaskini huku ikitegemea watetezi wa propaganda hizo wawe watu aina ya Ritz na chama na muenda zake TUNTEMEKE.

Kinacho zidi kuipa heshima chadema na propaganda za ccm ni jinsi propaganda hizo zinavyojibiwa kwa nguvu za hoja na mashiko yaliyo jaa kauli mujarabu huku zikionyesha obwe la kiuongozi na mtindio wa ubungo kwenye nyuso za magamba.

Naanza kuamini ule usemi wenye ncha kali "Wanao tetea ccm wana akili za maiti".

Kwa nini?
1. Hawashupalii elimu bora kwa watoto wetu kwenye hizi shule za ukata (st kayumba), wao wanashupalia kadi.

2. Hawataki kukilazimisha chama chao kuwataja na kuwachukulia hatua wamiliki wa kagoda, meremeta, deep green finance, epa, rada na trilioni zilizo Uswis. Wao wanalia na kadi ya Dr slaa bila kujali kuwa ni mali yake.

3. Hawashinikizi chama chao kutekeleza ahadi za Trilioni 13 ili kuifanya Kigoma iwe Dubai ya Afrika, barabara za hewani DSM na Tanga jiji la viwanda, wao muhimu kwao ni kadi ya Dr slaa.

4. Mwenyekiti wao amekiri kuwa ccm iache kutegemea polisi, hawashinikizi polisi walio uwa raia wenzao wachukuliwe hatua. Wao chenye umuhimu ni kadi ya Dr slaa.

5. Hawashinikizi wajumbe waliopatikana kwa rushwa na yale magamba yaondolewe kwenye chama chao. Wao akili zinapinga mbizi kufikiria kadi ya Dr slaa tu!

Hivi kuna chembe ya shaka kwa hako ka usemi kwa mifano hiyo michache?! Kama jibu ndiyo hebu angalia orodha ya watetezi wa hoja zao.
1. ZeMarcopolo
2. Ritz
3. TUNTEMEKE
4. chama (angalau siku moja moja huwa anatumia kichwa kuwaza badala ya tumbo kama Ritz
5. Mwendazake Marilia sugu.
6. Mwendazake Faiza fox.

Ukisema hao watu wanatetea hoja za kadi kwa kutumia yale madude ya yule mayor wa darisalamu utakuwa umekosea sana.

*Samahani kama nitakuwa nimewakwaza bahati mbaya au kwa makusudi*

Kila jema na lenye kheri lisiwaponyoke na mbarikiwe hadi mpigwe na butwaa.

Mkuu Mtoi
pumba nyingi sana hizi kiza kimeingia fupisha maneno ni unataka kusema tukujibu kwa ufasaha; sisi tunatumia mistari 4 kwasababu tunakupa kweli tupu>

Chama
Gongo la mboto DSM
cc: Ritz
 
Last edited by a moderator:
Kweli sumu ya neno ni neno,tatizo ccm hawajatambua adui yao,wao wanafikiri adui yao ni chadema,adui wa ccm ni wenyenchi kupoteza imani nao.
Hii itawatafuna hadi mtakapo tambua adui yenu na kuchukua hatua.chadema ni distant cause,secondary cause ni nyie wenyewe na primary cause ni wananchi kupoteza imani na nyie kadiri siku zinavyokwenda.
Dawa ni nyie wenyewe,mkishindwa wananchi watawapumzisheni wandugu.
 
Kwa mujibu wa Star tv kuwa Dr. Slaa amewambia badala ya kujadili mambo ya kitaifa kama wizi wa nyara za serikali kama wizi wa tembo watanzania wanajaditi kadi, badala ya kujadili kwa nini watu wanalala njaa watu wanajadili kadi, watu wanauwawa na polisi watu wanajadili kadi.

Dr. Slaa kawauliza hivi hao wanaotoa matamko mmewachunguza na kuwajua ni kina nani??

Ukiwatazama watu hao ni mbumbumbu wa sheria na hawajui wanachokifanya na tunapoteza taifa kwa mambo ya kipuuzi tunaacha kujadili mambo ya kitaifa na mafisadi wanatumia mwanya huo kuiba zaidi raslimali za taifa

Maswali haya ya Dr Slaa hayawezi kujibiwa na CCM wala serikali yake, maana ushahidi wa alichosema Dr Slaa uko dhahiri
 
Huyu Kisandu ana uwezo mdogo sana wa kujiongoza yeye mwenyewe,hajitambui,anazungumza kama vie ni monita wa arasa na sio kiongozi wa vijana katika mkoa,Sishangai kuona mkoa kama Tanga CDM haina ushawishi mkubwa kwa sababu watu wenye upeo mdogo kama Kisandu eti ndio viongozi!
Mkuu, hakuna anayejua kila kitu, ni kumwelekeza atakuja kuwa jembe huko mbeleni. Na uhakika kuna wengine wengi tu wanapata maujanja kupitia hapa jamvini. Na pengine mazingira au sehemu aliyopo pamoja na kuwa kamaliza shule bado hakubahatika kupata kujifunza yaliyo nyuma ya pazia. Hivyo ushauri wangu ni kwake kuwa tayari kuchukua hizi kama changamoto za kujifunza zaidi. Otherwise, tumsaidie kijana ajifunze.
 
Huwezi kushindana na ukweli na haki.Tsunami ya kuibomoa CCM inakuja na hii ndio wataparanganyika kwelikweli!
 
Kwa mujibu wa Star tv kuwa Dr. Slaa amewambia badala ya kujadili mambo ya kitaifa kama wizi wa nyara za serikali kama wizi wa tembo watanzania wanajaditi kadi, badala ya kujadili kwa nini watu wanalala njaa watu wanajadili kadi, watu wanauwawa na polisi watu wanajadili kadi.

Dr. Slaa kawauliza hivi hao wanaotoa matamko mmewachunguza na kuwajua ni kina nani??

Ukiwatazama watu hao ni mbumbumbu wa sheria na hawajui wanachokifanya na tunapoteza taifa kwa mambo ya kipuuzi tunaacha kujadili mambo ya kitaifa na mafisadi wanatumia mwanya huo kuiba zaidi raslimali za taifa
Wapi kakanusha???
 
Back
Top Bottom