Dr. Slaa bado anayo kadi ya CCM?

Dr. Slaa bado anayo kadi ya CCM?

Mi namtaka TUNTEMEKE ajitokeze humu maana alikesha siku2 na huo upuuzi wake humu ndani.
Ameshakula ban safi, muangalie hapa TUNTEMEKE

[h=1]TUNTEMEKE
user-offline.png

Banned
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
[/h]
 
Nimejaribu kuangalia wapi Dr Slaa kakanusa sijaona.

Unachotakiwa kujiuliza kabla ya yote kadi ni mali ya nani? ya chama au ni mali ya mtu aliyeinunua hata kama si mwanachama wa chama husika kwa wakati huo?alichokanusha Dr. ni kumiliki kadi ambayo ni mali ya CCM ,kadi anayomiliki ilitolewa na CCM lakini ni mali yake ingawa si mwana CCM kwa sasa.
 
Haya ndo madhara yakuwapa vyeo wa2 wenye njaa, wenye tamaa na wepec kurubuniwa kama kina Mtela Mwampamba
 
Hizo Degree uchwara hata Chadema zipo, kuna Kilaza anaitwa Deo Kisandu kwa kweli anaiabisha sana Chadema hasa hapa JF kwa kuweka mabandiko ambayo hayana quality za Kichadema na hata mtoto mdogo wa Primary Shool hawezi kuwa Kilaza namna hiyo.

user-offline.png
Deogratius Kisandu

11th December 2012 11:49
#1
Member
verified.png
Array


Join Date : 2nd December 2012
Posts : 11
Rep Power : 305
Likes Received4
Likes Given8



icon1.png
January Makamba na Henry Shekiffu walinikimbia kwenye mahafali!


Tarehe 8/12/2012 siku ya jumamosi ilikuwa ni siku ya mahafali ya chuo kikuu kishiriki cha Tumaini cha Sebastian Kolowa, kilichopo Lushoto, Tanga.

Katika mahafali hayo mimi nilikuwa mhitimu mmojawapo wa mwaka huu. Mgeni rasmi alikuwa ni Rais mstaafu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ndugu Benjamin Mkapa.

Namshukru Mungu kwa kuniwezesha kumaliza masomo yangu japo kuwa nimekoswakoswa mara nyingi kufukuzwa chuo, Mungu aliniongoza nakila nilipo kuwa na pewa barua za tuhuma nilizijibu kwa makini sana japo wapo wenzangu ambao hawakumaliza chuo.

Nawashukru waandishi wa habari ambao kwa kiasi kikubwa walikuwa wakinifuatilia utaratibu wa masomo yangu na maisha yangu ya chuo kwa muda wote mpaka na maliza.

Ndugu yangu Januari Makamba Mbunge wa Jimbo la Bumbuli ambaye kwa sasa ni Waziri na Mpinzani wangu mkuu ambaye nilichuana naye uchaguzi mkuu wa ubunge 2010 ndugu yangu Henry Shekifu mbunge wa jimbo la Lushoto hawakufika kwenye tafrija yangu ndogo baada ya mahafali na hata kwenye mahafali yenyewe sikuwaona. Kama wabunge wanapunguza CREDIT kwa wananchi kwa kutokutokea maeneo mhimu kama haya.

Kwasababu mimi ni mpinzani wao huenda walishindwa kufika kwa kuniogopa maana ndio Rais wao ajaye wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kiukweli inanipa picha kuwa Mungu anampango wake juu yangu.


DEOGRATIUS KISANDU
Katibu wa Baraza la Vijana wa Chadema mkoa wa Tanga
attachment.php
attachment.php
Huyu Kisandu ana uwezo mdogo sana wa kujiongoza yeye mwenyewe,hajitambui,anazungumza kama vie ni monita wa arasa na sio kiongozi wa vijana katika mkoa,Sishangai kuona mkoa kama Tanga CDM haina ushawishi mkubwa kwa sababu watu wenye upeo mdogo kama Kisandu eti ndio viongozi!
 
Kazi kwelikweli hapa Tanganyika,yaani kadi ya zamani inakuwa mjadala na kuacha majambazi yakitorosha nyati,tembo na hata chui kupeleka nje. Maskini Tanganyika.
 
Pilau la Lumumba limekuvimbia hata hujui hapa watu wanajadili nini!!

Hahaaahaa huyo jamaa na wenzake hapa, huwa hawaangalii kilichoandikwa ndani bali kichwa cha habari tu kisha akili yao husimama kubisha tu!
 
Miongoni mwa viashiria vinavyo onyesha kuwa ccm inakufa ni propaganda za kijinga zisizo msaidia mtanzania kutoka kwenye lindi na mzingo wa umaskini huku ikitegemea watetezi wa propaganda hizo wawe watu aina ya Ritz na chama na muenda zake TUNTEMEKE.

Kinacho zidi kuipa heshima chadema na propaganda za ccm ni jinsi propaganda hizo zinavyojibiwa kwa nguvu za hoja na mashiko yaliyo jaa kauli mujarabu huku zikionyesha obwe la kiuongozi na mtindio wa ubungo kwenye nyuso za magamba.

Naanza kuamini ule usemi wenye ncha kali "Wanao tetea ccm wana akili za maiti".

Kwa nini?
1. Hawashupalii elimu bora kwa watoto wetu kwenye hizi shule za ukata (st kayumba), wao wanashupalia kadi.

2. Hawataki kukilazimisha chama chao kuwataja na kuwachukulia hatua wamiliki wa kagoda, meremeta, deep green finance, epa, rada na trilioni zilizo Uswis. Wao wanalia na kadi ya Dr slaa bila kujali kuwa ni mali yake.

3. Hawashinikizi chama chao kutekeleza ahadi za Trilioni 13 ili kuifanya Kigoma iwe Dubai ya Afrika, barabara za hewani DSM na Tanga jiji la viwanda, wao muhimu kwao ni kadi ya Dr slaa.

4. Mwenyekiti wao amekiri kuwa ccm iache kutegemea polisi, hawashinikizi polisi walio uwa raia wenzao wachukuliwe hatua. Wao chenye umuhimu ni kadi ya Dr slaa.

5. Hawashinikizi wajumbe waliopatikana kwa rushwa na yale magamba yaondolewe kwenye chama chao. Wao akili zinapinga mbizi kufikiria kadi ya Dr slaa tu!

Hivi kuna chembe ya shaka kwa hako ka usemi kwa mifano hiyo michache?! Kama jibu ndiyo hebu angalia orodha ya watetezi wa hoja zao.
1. ZeMarcopolo
2. Ritz
3. TUNTEMEKE
4. chama (angalau siku moja moja huwa anatumia kichwa kuwaza badala ya tumbo kama Ritz
5. Mwendazake Marilia sugu.
6. Mwendazake Faiza fox.

Ukisema hao watu wanatetea hoja za kadi kwa kutumia yale madude ya yule mayor wa darisalamu utakuwa umekosea sana.

*Samahani kama nitakuwa nimewakwaza bahati mbaya au kwa makusudi*

Kila jema na lenye kheri lisiwaponyoke na mbarikiwe hadi mpigwe na butwaa.
 
Last edited by a moderator:
Mimi hapa siwezi kumlahumu Nape Nauye hata chembe kwani yeye ni mpinzani wa CHADEMA na ndio kazi yake kipropaganda zaidi ili aweze mkono kinywani.
Hasira yangu ni kwa hawa baadhi ya vijana njaa kama Magafu, Mtela mwampamba co ambao eti ni wanaCHADEMA lakini ndio vinara wa kumchafua Dr.Slaa mitandaoni na kukipaka chama matope, Nilitarajia mwanzo kuona watu kama Beno Malisa au Martin Shigela au Mwigulu wakishikia bango swala hili lakini hali imegeuka kwa vijana wenyewe wa CDM kuharibu nyumba yao kwa mikono yao wenyewe.
 
Hivi ni kweli hao graduate wa sheria hawajui sheria?njaa mbaya sana,yaani kijana kama Magafu anakubali kujidhalilisha namna hii!

Ukiendekeza njaa, wallah tena unafededwa mchana wa juakali na mwanaume mwenzio,ndo walichomfanya Magafu, wamemtumia kupima upepo wameona mambo yamegoma watamwachia msala peke yake na mkewe mwisho yeye ndo ataonekana MSENGErema wenzie kina Nape wanafanya mengine,vijana jalini utu wenu,msiuze utu wenu kwa njaa ya siku moja afu mkabaki na laana maisha yenu yote
 
Sijaelewa vizuri.....Dr. Slaa kakanusha kumiliki kadi! lakini je ni nani aliywahi kunukuliwa akikiri (kama ndiye Dr.) kuwa alikuwa anamiliki kadi ya CCM? Maana itakuwa ni kasfa kubwa mno kwa "waandishi wa habari" waliopamba na kukuza suala lile.

Ni kweli ishu haikuwa na mashiko na pia ilikuwa ni hoja dhaifu sana ktk karne hii lakini kwa namna magazeti na mitandao ya kijamii ilivyosheheni mijadala......well nilifika mahali (nikiri wazi) niliona ktk hili CHADEMA itabidi kuwa "defensive" kwa muda. So nafarajika na pia nashukuru kuwa sasa Dr. Slaa amelisemea kwa upana na urefu na kuwaumbua wahaini. Na hapo hapo Dr. katuweka mguu sawa ktk mapambano dhidi ya CCM na mafisadi yanaendelea.

Lazima Tanzania ikombolewe, na hilo litawezekana tu endapo CCM itatokomezwa ktk siasa za Tanzania.
Propaganda mfu na chafu namna hii haziwafanyi CCM kustahili wala kuwa na uhalali wowote kuwemo ktk siasa za Tanzania ya sasa na tunayoitaka.
 
Hoja za magafu ni moto sana,kila anaejaribu kujitokeza anaishia kulalamika badala ya kujibu hoja za msingi
 
Back
Top Bottom