Hakika ccm wanaweweseka na kutapatapa wasijue la kufanya!! Leo asubuhi nilifungulia tbccm kwa bahati mbaya nikamsikia Lukuvi akisema kuanzia tar. 19 desemba hii wataanza kurusha mafanikio ya ccm kwenye vituo vyote vya runinga eti waTz wafahamu mafanikio ya ccm na serikali tokea uhuru hadi leo! Hivi kweli mafanikio kama yapo wananchi si wanayaona kwa macho yao? Kuna haja gani ya kutumia kodi zetu kulipia vipindi hivyo mfululizo katika vituo vyote vya runinga? Hizo fedha wangeenda kutengeneze madawati maana kuna wanafunzi hadi leo hii wanakaa chini? Hayo si matumizi sahihi ya kodi zetu hakika!
Mkuu wanajidanganya, maendeleo kama yapo wananchi wangeyaona na kupata unafuu wa maisha. Wananchi hawahitaji kuonyeshwa maendeleo kwenye tv!