Dr Slaa atingisha Kigoma Kaskazini

Dr Slaa atingisha Kigoma Kaskazini

cjaelewa hizi picha na kichwa cha habari mbona cnapishana, nyingi zimepigwa hotelini alipofikia na ndipo anasalimiana na polisi tayari kwenda kufanya mikutano, hizo zingine zimepigwa kwenye mikutano ya vijijini, huo ni mtupu.
 
Slaa aliambiwa na Wanakigoma, kuwa hali haijatulia, asiende, akataka kushindana Ubavu na Zitto kwa kumuonesha kwamba yeye yuko Juu, sasa ona anaibika anahutubia upepo!. HUYU MZEE HAAMBILIKI, HAFAI HATA KIDOGO!
teh teh,mkuu nani anaambilika?
 
natural justice?acha utani,zitto katuumiwa kwenye kikao

kinachokusumbua ni mahaba wa si kingine,mahaba ya pupa hupofusha akili.na inaonekana hujui chochote umeingia kwnye ushabik kwa mkumbo,zitto na wenzake walipewa nafasi ya kujieleza na kujitetea juu ya tuhuma zilzowakabili,ndio maana wakaomba kujiuzulu,lakn wajumbe wakataa uamuz huo kwan ilionekana wangebak na heshima ambayo hawakustahili.we kama ni maamuma soma tu usichangie kwa lengo la kupotosha
 
Dr. Slaa ni rais anayeongoza wananchi kupitia kwenye mioyo, wakati Kikwete ni rais abayetawala nchi kupitia nec
rais wa nini?? wasafi clasics??,,,,,tff?,,,,,,,,bavicha? si kila mtu anaweza kuwa rais
 
kinachokusumbua ni mahaba wa si kingine,mahaba ya pupa hupofusha akili.na inaonekana hujui chochote umeingia kwnye ushabik kwa mkumbo,zitto na wenzake walipewa nafasi ya kujieleza na kujitetea juu ya tuhuma zilzowakabili,ndio maana wakaomba kujiuzulu,lakn wajumbe wakataa uamuz huo kwan ilionekana wangebak na heshima ambayo hawakustahili.we kama ni maamuma soma tu usichangie kwa lengo la kupotosha
acha uongo mangi zitto mmemtimua kwa kuhofia atatwaa madaraka ndani ya chadema na hivyo kupoteza dhumuni halisi la kuanzishwa kwa chama chenu
 
hahahaaa....... mkuu umeingia shift ya usiki siyo! karibu tulikumiss muda
siko cheap kama nyie mnaolipwa na babu ili mumlambe viatu kiasi cha kuvumilia uzinzi,,,,chuki ,,,na uwizi wa rudhuku
 
siko cheap kama nyie mnaolipwa na babu ili mumlambe viatu kiasi cha kuvumilia uzinzi,,,,chuki ,,,na uwizi wa rudhuku

CHADEMA hakuna malipo, ni makamanda tunapambana kwa jasho mpaka tuikomboe nchi!
 
Mkuu unapoteza muda wako hujui FaizaFoxy akili zake zimedumaa? hawezi kuhoji wala kudadisi

Hahahaaaaaa, mkuu Mungi nimekumbuka kuwa hata chama chake ni CHAKAVU na KIMEDUMAA! Kuanzia leo nafuata ushauri wako kutomjibu huyu kikongwe foxy.
 
Last edited by a moderator:
Foxy,hata house girl wako ndo angekuwa rais wa TZ angetunukiwa hayo matuzo ya bure. Naongelea udr wa kuchimba darasani sio wa kupewa bure.

Unashindwa kuelewa kuwa madarasa yanaweza kukujaza ujinga huku unajiona kama ulivyo wewe. Hakuna PhD bora na yenye thamani zaidi ya ile ya kutunukiwa, kumbuka hilo. Kwa ufinyu wako wa mawazo sijui kama unaweza kuliona hilo leo au kesho.

House Girl wangu nyumbani ana hadhi ya PhD au zaidi. Alianza kazi kwangu kwa mshahara wa 40,000 kwa mwezi, miaka 7 nyuma, leo hii ana bajaj 3 ana bodaboda 12 ana fundi wake na ana duka la spare za bodaboda. Na alianza kwa bodaboda moja ya mkopo niliomdhamini. Kumbuka hilo pia.

ops, kuna madaktari wa "kuchimba" wakaenda kumchimba mtu kichwa badala ya mguu. Au umesahau hilo?
 
View attachment 126024
Dr. Slaa
akiwa jimboni kwa Zitto


Awaambia wapiga kura wa Zitto kabwe:



  • `Chadema haijakurupuka kuwasimamisha Zitto, Kitila`

Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, ameanza ziara katika Jimbo la Kigoma Kaskazini linalowakilishwa na Zitto Kabwe, huku akiwaeleza wananchi kuwa chama hicho hakikirupuka kumsimamisha uongozi Zitto kama inavyoelezwa na baadhi ya watu.

Aidha, amewalipua wenyeviti wa Chadema waliojizulu baada ya sakata la Zitto kwa kusema kuwa wamefanya hivyo kutokana na kupewa fedha ambazo mmoja wao zimemsaidia kujenga nyumba haraka.

Wenyeviti wa Chadema waliojiuzulu ni Wilfred Kitandu wa mkoa wa Singida na Ally Chitanda wa Lindi, ambao walifikia uamuzi huo baada ya Zitto kuvuliwa nafasi ya Naibu Katibu Mkuu pamoja na Dk. Kitila Mkumbo, ambaye alivuliwa ujumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho.

Hata hivyo, Dk. Slaa hakufafanua kama wenyeviti hao walihogwa na nani.

Akizungumza jana na mamia ya wananchi wa kijiji cha Nyalubanda Jimbo la Kigoma Kaskazini waliohoji sababu za Chadema kuchukua hatua za kumsimamisha Zitto uongozi, alisema chama hicho kinafanya kazi kwa kuzingatia katiba yake.

Dk. Slaa akihutubia wananchi hao huku mvua ikinyesha iliyoambatana na ukungu mzito, alisema katiba ya Chadema haina kipengele kinachotaka chama hicho kinapotaka kuchukua hatua dhidi ya kiongozi au mwanachama aliyefanya kosa hadi suala hilo waulizwe wananchi.

"Nilichogundua wenyeviti waliojiuzulu nyadhifa zao wamenunuliwa kwa pesa na mmoja wao baada ya siku mbili tatu, alijenga nyumba na amekuja kupiga magoti akiomba arudi Chadema, lakini hatuwezi kumkubalia," alisema Dk. Slaa bila kumtaja jina.

Dk. Slaa alisema wananchi na wanachama lazima watambue kuwa Chadema haijawahi kutetereka toka mwaka 2011, hivyo wanaodhani inaweza kutokea hivyo baada ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya Zitto wanajidanganya.

Alisema kiongozi yeyote au mwanachama atakayekiuka au kuvunja maadili na misingi ya katiba ya chama hicho awe ni Dk. Slaa, Mbowe au Mtei, lazima atachukuliwa hatua za kinidhamu kulingana na katiba.

Alitoa mfano mwaka 2011 madiwani wa Chadema mkoa wa Arusha walipobainika kukiuka kanuni za chama, walichukuliwa hatua na hadi sasa chama hakijayumba na kinadunda.

Alisema wananchi wakiwamo wa Kigoma wasiumize kichwa kwa hatua zilizokwisha chukuliwa dhidi ya Zitto kwa sababu suala hilo siyo la kwanza kuchukuliwa kwa kiongozi anayebainika kukiuka katiba ya chama.

Dk. Slaa alisema kabla ya Zitto, Dk. Kitila na Samson Mwigamba, kuchukuliwa hatua hizo, waliitwa na kuhojiwa kwenye vikao vya chama.

"Utakuwa mtu wa ajabu una kansa inakutafuna unataka uiache iendelee kukutafuna hadi kwenye moyo ambako huwezi kukata ni bora kuikata kabla haijafika sehemu ambayo haitawezekana kukatwa," alisema.

Dk. Slaa alisema hatua zilizochukuliwa dhidi ya Zitto hazina uhusiano wowote na suala la Zitto kuhoji ukaguzi wa hesabu katika vyama.

Juzi, Dk. Slaa alipowasili mjini Kigoma alipokelewa kwa kishindo na mamia ya wananchi huku pikipiki zaidi ya 150 na magari zaidi ya 20 yakiandamana kumlaki.




CHANZO: NIPASHE

 
Nashangaa kuna mada kama hii nimeiweka kama dakika chache zilizopita na mara imefutwa, hii ni published news kutoka gazeti nipashe kila kitu ni copy and paste, hakuna kilichoongezwa wala kupungua. Just be patient kwa published news
 
Candid Scope umechelewa sana, picha za ukweli zimewekwa tayari. Na kama unalipwa na babu kupiga propaganda leo utamkoma Josephine.
 
Last edited by a moderator:
Hila za mwovu ccm zimeshindwa!
Naona wananchi wametulia sana wakisubiri kupewa matirio.
attachment.php
 
Back
Top Bottom