Dr. Slaa aomba ukimbizi Canada

Dr. Slaa aomba ukimbizi Canada

Kuna nyuzi hapa zilidai Dr. kapewa pesa nzito nafikiri sio chini ya dola au paundi milioni moja. Sasa hiyo nyumba ina thamani gani hadi ashindwe kuilipia? Kuna ukweli gani kwenye habari hizi? Au ndio kumsanifu?
sema ww. Na sasa zito waliye mfukuza ndo anawabeba bungeni.
 
We si umeshaoa....na una "mamichepuko mawili"...South na Botswana....
Zamaulid mpendwa, hao ni wawezeshaji na sio michepuko. Ukweli katika kuoa kunahitaji umakini. Kinachotokea kwa mzee wetu tuliyempenda sana ni ushauri mbovu toka kwa mama yetu Mshumbushi.
 
Dr. Slaa ni jina kubwa haijalishi wewe unamwonaje. Hakubaliani na unafiki kwa kuwa yeye si mnafiki. Habari za yeye kuomba ukimbizi Canada tunaitaka serikali ifuatilie na itupe mrejesho. Kama vitisho hivi vinatoka kwa Hugo rais wa wawahuni wanayesema anaishi kama rais hatua zichukuliwe kuuthibitishia umma kwamba ipo serikali makini yenye uwezo wa kulinda RAIA wake
Tatizo unachangia kwa mihemuko ya kisiasa.
 
Kama habari hii ni ya ukweli basi Dr.Slaa anahitaji msaada maana naona kama Josephina na @Mwanakijiji wanakompeleka huyu mzee siko.
.Hivi Dr.Slaa hana ndugu wa kuweza kumtoa kwa huyu mwanamama maana mzee wetu anaanguka na sisi tunaona. Pamoja na mambo yote yaliyotokea (yaani kutuletee mzigo wake na kuubwaga Chadema) lakini sisi wanachadema tunakubali mchango wake kwa chama chetu hivyo basi Dr.Slaa si mtu kwenda kuishi katika nchi za wenyewe achilia mbali kujilipua.
 
Imefika mahali anawakimbia hata usalama wa taifa? Kweli majuto mjukuu.
 
Me nadhani CDM ndo wanaomtishia maisha alishawahi kunukuliwa akisema tangia siku ametangaza nia yake ya kujiudhuru siasa amepata vitisho vingi kushinda hata kipindi amewataja mafisadi papa 10
 
Dah nzee anataka kula raha tu huko ughaibuni....
 
Pamoja na hayo, lakini huwezi kuwalinganisha Prof. Lipumba na Dr. Slaa

Iwe ki uzalendo au kielimu. Lipumba na PhD ya uchumi, anauzika mahali popote Duniani. Slaa ana PhD ya theology ( ya dini ya kikatoliki ) ni ngumu kupata kazi kama sio kwenye taasisi za dini hiyo na alishawaliza. Watapiga memo kila aendako ilimfaa siasa ya bongo tu nayo naona kama imemponyoka
 
Maadui wa Dr Slaa wanajipanga kwa 2020. Wanamwona paroko wa watu kama kirusi and they want to scan him
 
siku mtakapoona Chama Kipya kinazinduliwa basi rudini hapa na mzungumze vitu kama Hivi mnavyonena Hapa. Staili anayotumia Dk Slaa ni Staili ambayo Ilitumiwa na Mpelelezi Matata Joram Kiango katika Mkasa Ule uitwao Tutarudi na Roho Zetu pale alipoiba pesa benki na kwenda kuomba Hifadhi ya Ukimbizi Kule South. Kilichotokea nadhani Hata kwa Dk kitatokea kama kile.
 
Naogopa sana kitu kinaitwa Destiny ,pole yake ,umefanya uliyo yafanya yawe mema au mabaya lakini ndio hivyo mwisho wako umekua ,Mungu akutangulie
 
Ni aibu tu inayomsumbua,kachanganya sana madawa.Nani amdhuru Dr.Slaa.
Habari za kutoka magazetini leo asubuhi itv zimesema kuwa Dr. Slaa ameomba ukimbizi huko Canada kwa madai kuwa maisha yake yamo hatarini Tanzania!

Swali: Ni nani huyo anayetishia uhai wa Dr.Slaa?
 
Back
Top Bottom