activisty
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 315
- 107
Nitakuwa wa mwisho kabisa kuubeza, kudharau mchango wa dr slaa ndani ya Chadema na taifa kwa ujumla katika safari ya mabadiliko. Kazi aliyoifanya 2010 ndiyo iliyozaa nguvu hii ya ushawishi wa mabadiliko kwa watanzania. Nasema nitakua wa mwisho kuungana na Mbowe, ati dr slaa apumzike. Nitakuwa mnafiki kufanya hivo na muongo kabisa. Naamini na nitasimama imara katika kufanya lolote kuhakikisha mabadiliko yanapatikana.lakini pia natambua nguvu ya Lowassa na umuhimu wake katika safari hii ya mabadiliko makubwa lakini pia kwa hekima kabisa ingekuwa vyema Mbowe angeeleza kwanza hoja iliyopelekea kuleta maamuzi hayo kisha tukamsikiliza dr slaa kwani nitamshangaa sana mwanachadema aliyeishangilia kauli ile bila hata kuuliza, kutafakari majibu, na kupima athari zake.
Tunayahitaji mabadiliko kwa gharama yeyote ile ila si kwa kukubali kuitenganisha nguvu tuliyonayo katika safari hii ya mabadiliko."mchango wa lowassa ni mkubwa katika safari hii ya mabadiliko lakini pia nguvu ya dr slaa ndiyo daraja kuu litakaloiunganisha nguvu ya chadema na nguvu ya Lowassa"
By Fikra mfumo.
Tunayahitaji mabadiliko kwa gharama yeyote ile ila si kwa kukubali kuitenganisha nguvu tuliyonayo katika safari hii ya mabadiliko."mchango wa lowassa ni mkubwa katika safari hii ya mabadiliko lakini pia nguvu ya dr slaa ndiyo daraja kuu litakaloiunganisha nguvu ya chadema na nguvu ya Lowassa"
By Fikra mfumo.