Dr. Slaa anastahili kuheshimiwa

Dr. Slaa anastahili kuheshimiwa

kwanza hoja ya ufisadi imefikia mwisho utambue hilo. na ACT ndo chama makini cha upinzani kwa sasa.
 
Kama unataka uthibitisho kwamba sisi wengine ni CDM basi sema tukutumie namba za kadi zetu ukaprove ..usiwasakizie CCM kila jambo kwa ujinga wenu wenyewe kwani ndo waliowatuma mkauze chama chetu?

Nyie wapuuzi hamtakiwi hata kupewa uwezo wa kumiliki simu sa we unasema chama kimeuzwa we unaushahidi wowote wa mauzo na manunuzi cha chama au unaongea kwakuwa unamdomo na hulipii
 
WanaJF na hasa wana CHADEMA wenzangu tuwe makini sana na maandishi yetu hapa jukwaani kuhusu huu ukimya wa DR SLAA, tafadhalini sana, DR ni kiongozi mkubwa sana anastahili kuheshimiwa, wale wenye uchungu na CHADEMA na tunaofahamu tulipotoka hatuwezi kumkashifu huyu mtu, kwa lipi hasa ?

Acheni kabisa jambo hilo, sikupenda kuandika jambo hili maana linaweza kuendeleza malumbano zaidi lakini nimelazimika kuliweka kama angalizo.

Hata ww unastahili kuheshimiwa..ni haki ya kila mtanzania kikatiba
 
Leo lowasa awe mgombea kupitia chadema chama ilimwandaa lini?kwanini mwonzoni lowasa hakufunguka na aje chadema mpaka akatwe ccm kama siyo uroho wa madaraka?

Mkuu, Lowassa alifunguka kuhusu hili suala la Richmond hata alivyokuwa bado yuko ndani ya CCM. Kuna kipindi CCM walikuwa na mkutano mkuu, Edward Lowassa alikuwa analalamika jinsi Nape anavyomchafua na CCM imekaa kimya bila kumnyamazisha Nape. Edward Lowassa akaendelea kusema kwamba kama suala lenyewe analolitumia Nape kumchafua ni la Richmond, "kuna kitu gani nilichofanya katika Richmond ambacho Mh Raisi na mwenyekiti wa Chama hukukijua", Lowassa aliuliza. Mh Mkapa aliingilia kati haraka sana na kuomba mkutano uishe ili kumkinga mwenekiti.


Lowassa kuja Chadema na kupewa nafasi ya kugombea Uraisi hii imetoka na kimkakati zaidi. Lowassa ana watu wengi sana nyuma yake wanaomkubali, hilo tumeshuhudia wakati anazunguka mikoani kuomba wadhamini kwa tiketi ya CCM.
Watu wote wanaomkubali Lowassa ndani ya CCM watampa kura Lowassa na sisi tulio nje ya CCM tutampa kura Lowassa kwa lengo la kuiondoa CCM madarakani. Kuja kwa Lowassa Chadema amekuja na wanachama wengi sana, ushahidi ni kwamba kwa sasa tumeishiwa kadi za chama karibu katika ofisi zetu zote, watu wanajiunga Chadema kwa speed ya roketi. Naomba mkuu usitishike kwa hili la Lowassa kupeperusha bendera yetu, naomba tushikamane pamoja ili tushinde vita hii. "Sisi sote ni ndugu, adui yetu ni CCM"
 
Mkuu amani iwe nawe.
Naomba niandike machache labda utanielewa kidogo. Nami nilikuwa kama wewe katika kumchukia Edward Lowassa kwamba ni Fisadi, na nilimchukia kwa sababu "kusikia kwamba ni Fisadi" wakati sikuwa na ushahidi wowote.

Katika suala la Richmond kama utaangalia kiundani na kusikia kile Edward Lowassa alichosema utaona wazi kwamba ilikuwa ni mpango maalumu wa kumchafua na kumuondoa Edward Lowassa katika kiti cha Uwaziri mkuu. Kilichompoza Lowassa mpaka kusukiwa mpango huo mchafu ni ukali, umakini wa kufuatilia mambo na usimamizi wa yale anayoyaamini. Alipokuwa waziri mkuu tuliona wazi kwamba mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya walikuwa wanawajibika kisawasawa tokana na ukali wa Lowassa. Walikuwa hawaondoki vituo vyao vya kazi bila ruhusa maalumu toka ofisi ya waziri mkuu.
Muheshimiwa pale magogoni akaona wazi kwamba anafunikwa na Lowassa kwani viongozi wengi walikuwa wanachukua maelekezo na maagizo toka kwa Lowassa, ndipo zengwe lilipikwa la kumuondoa Lowassa madarakani.
Jiulize kwa makini sana, kama kweli Lowassa alifanya uchafu ule na kama ushahidi upo kwanini asipelekwe mahakamani?

Chadema walimuingiza Lowassa kwenye list of shame sababu kama zako wewe leo unayemchukia Lowassa kwa sababu za kusikia na kuambiwa. Juzi Lowassa karudia live kwenye TV kwamba alitaka kuvunja mkataba wa Richmond baada ya kujua kwamba ulikuwa fake, lakini bosi wake hakutaka kumsikiliza. Ulitaka Lowassa afanye nini zaidi?. Unaamini kabisa suala kama la Richmond mkuu wa nchi hakulijua toka mwanzo?. Unakumbuka tume ya Mwakyembe ilisema wazi kabisa kwamba inaficha baadhi ya mambo ili kuinusuru serikali, unafikiri walimaanisha nini?. Tume hiyohiyo ya Mwakyembe ilipewa mamlaka makubwa sana ya kumuhoji mtu yeyote bila kuogopa cheo alichonacho. Tume iliweza kuwahoji wahusika karibu wote na iliweza kusafiri mpaka USA kuwahoji wahusika, kwanini ilishindwa kumuhoji Edward Lowassa aliyekuwa na ofisi zikitazamana na ofisi ya tume hiyo?

Ni kweli kabisa Dr Slaa amejitolea sana katika kuifikisha Chadema hapa ilipo leo. Amejitolea kwa kila hali na mali, na kuna muda aliweka rehani mpaka maisha yake, lakini kuiacha Chadema leo juhudi zake zote alizofanya kuijenga na kuifikisha chadema hapa ilipo zitakuwa hazina maana tena. Slaa kama padri nilitegemea sana kwamba angefurahi kuona watu kama Lowassa wanajiunga na Chadema huku wakieleza (kutubu) ukweli machafu yaliyomo ndani ya CCM na yale tuliyokuwa tunasikia wametenda.

Mimi, wewe, wale na yule bila ubishi tumeichoka CCM. Sasa ni wakati wa kuunganisha nguvu kuitoa CCM madarakani. Ujio wa Lowassa na wenzake ndani ya Chadema naona iwe ni baraka kwetu wala isiwe laana. Kama umepitia mafunzo ya kijeshi utakumbuka kwamba tulifundishwa mateka anaweza kukusaidia kushinda vita, anajua siri nyingi za adui zako hivyo ukimtumia vyema utashinda vita. Nasi tunataka kuishinda CCM na kuitoa madarakani, huyu mateka itabidi afuate matakwa yetu, aishi kama sisi ili awe salama. Lowassa na wenzake wamejiunga Chadema na si Chadema wamejiunga na Lowassa, hivyo Lowassa na wenzake itabidi waishi na kufuata matakwa na malengo ya Chadema.

Kiuhalisia ni kwamba CHADEMA na UKAWA wamejiunga na Lowassa na Lowassa hajajiunga na CHADEMA na UKAWA. Lowassa ana nguvu kubwa kuliko CHADEMA.

Mbowe ni bonge la mjasiria Mali, ana akili ya biashara. Katika hili mmachame huyu nampa big up. Hivyo ndivyo walivyo hasa linapokuja suala la kupiga hela hawaachi fursa ipite. Mbowe alishasema hawezi kuacha kumpokea Lowassa mtu anayekuja na wafuasi zaidi ya 1bill. Vinginevyo mtamuona kichaa kwa sababu maisha ya chama yanategemea watu. Kadi CDM inapatikana kwa Tshs 1,500/=, kwa watu zaidi ya 1 bill CDM wataingiza zaidi ya 1.5 bill za haraka. Ila ni kama kweli hao watu watajiunga CDM.

Tanzania ina fursa nyingi na Mbowe amegundua fursa, ambayo ni kutumia wananchi kupata ajira na fedha za kula bata duniani.
 
Umeongea kijazba bila kujenga hoja za maana by da way unamatatizo unaposema utafurahi ukawa wakishindwa inamaana hutaki mabadiliko alafu sisi tushaona mfumo wa ccm hautufai tunahitaji changamoto mpya nyie vilaza ndio maana hitler alikuwa hawaachi mzidi kuongea mihemko yenu hakuna uthibitisho lowassa ni fisadi kwa kauli yake na jibu la serikali kushindwa kumchukulia hatua inamaana alikuwa mkubwa kuzidi serikali au ?????

Ushahidi upo na anao Dr. Slaa kwani ndie aliyekuwa anamtangaza Lowasa Fisadi sasa tazameni mlipoweka ushahidi.
 
Kweli chizi kalogwa tena nani kamsafisha lowassa??? Nadhani juzi hukumsikia hata mh vai nahodha alikiri lowassa siyo fisadi kwakuwa hamna mwenye ushahidi je wewe unaushahidi wa lowassa ni fisadi ili twende mahakamani ndugu????? Usiwe kilaza lowassa anamapungufu yake kama slaa tuu mliekuwa mnamuita mzinifu mara malaya ila leo mnajifanya mnapenda sana ila tunajua nyie lumumba fc hamuwezi kututakia mema hvyo kile mnachopondea sisi ndio tunafanya kwakuwa ndio kitakachowaua jipangeni ukawa ndio tumaini letu wananchi pia pia kati ya ccm na chadema wapi kunawatuhumiwa wengi wa ufisadi......baada ya lowassa kuna epa, escrow, rada, uuzaji nyumba za serikali hao wahusika wote bado mmewakumbatia na bado mnaongea machizi

Ushahidi wanao Dk Slaa na Mbowe....waliomtangaza pale mwembeyanga.....
Au waliposema kuwa wana ushahidi kuwa Lowasa ni fisadi walikuwa wanatuongopea wananchi.....
 
Kwenye list of shame mlimleta ya nini kama mnamsimamisha Leo kama sio uwehu,hivi unajua hata unachosimamia?

Viongozi wa CHADEMA sio watu wa kuwaamini tena....bora nisipige kura tu nijipumzikie nyumbani....
Wao wenyewe kwa vinywa chao walituambia kuwa ushahidi wanao wa kuthibitisha kuwa Lowasa ni fisadi na kama anaona anaonewa awahi mahakamani... .leo wanatuambia kuwa ushahidi hawana na Lowasa ni msafi na kama kuna mtu mwenye ushahidi apeleke mahakamani.....sasa je ule ushahidi waliotuambia kuwa wanao ulikuwa ni wa uongo....??
Na kama ni uongo je hii inajenga picha gani kwa wapiga kama sio unafiki....???
SINA IMANI NA CHADEMA....
 
Kwa hili niko na wewe mkuu .
Bora CCM ichukue tena nchi kuliko
UKAWAna Lowasa .

Kumbukukeni Lowasa anapata fedha za kampeni
kutoka kwa watu wake ye anasema " marafiki" wa Lowasa .

Na hao marafiki watataka kurudishiwa fadhila
Lowasa akichukua ofisi . Ndo haposasa.
Hakuna cha bure siku hizi .
Bora Magufuli na CCM kuliko Lowasa UKAWA.
 
Kama ilivyokuwa kwa Lowassa na wapambe wake ndani ya CCM, Dr. Slaa naye hajaridhika na mchakato ndani ya CHADEMA. Kama ilivyokuwa kwa Lowassa, Dr. Slaa na wafuasi wake nao vivyo hivyo wana haki ya kuachana na CHADEMA.

Kama kuondoka kwa Lowassa kumeikosti CCM, kuonda kwa Dr. Slaa hakuwezi kuiacha salama CHADEMA.

Bora CCM less Lowassa kuliko CHADEMA plus Lowassa.

Alipo fisadi mimi sipo!

Mkuu nina kila sababu ya kuwaita viongozi wangu wa CHADEMA ni wanafki.....na sijui hao wanaowaunga mkono wanatumia kiungo gani cha mwili kufikiri....
Katika hali ya kawaida hata kama Lowasa ni msafi kama wanavyodai ingawa walituambia kuwa ni mchafu na ushahidi wanao.....lakini si kwa kutuaminisha kwa kauli nyepesi kama hizi eti systerm ndio mbovu na sio Lowasa.....ina maaana vibaka wote wakihamia CDM wanakuwa wasafi kwa kuwa kinachotakiwa ni kuiangusha CCM tu.....
Ukombozi wa kweli hauishii kwenye kuitoa tu CCM madarakani pekeeem..bali tunatakiwa tuweke watu makini wenye nia ya dhati ya kutufikisha kwenye nchi ya ahadi...na sio mamluki walio tayari kufanya lolote kwa ajili kupata uongozi kwa manufaa yao na vibaraka wao.....
 
Kwenye list of shame mlimleta ya nini kama mnamsimamisha Leo kama sio uwehu,hivi unajua hata unachosimamia?

Kwenye list of shame ata mkuu Wa kaya yupo kwa hiyo mwenyekiti wako ni fisadi ccm ni chama cha mafisadi ndio maana adi mwenyekiti fisadi
 
Kama kila ambaye hakubaliani na kamati kuu akifanya hivyo itakuwaje?Ni wangapi ambao huko nyuma waliwahi kutofautiana na kamati kuuvkatika maamuzi?je,nao walizira na kususia chama kama alivyofanya yeye?
 
Napenda kutoa rai kwa makamanda wenzangu, wanaharakati, na watanzania wote.

Uamuzi wa Dr . Slaa uheshimiwe..amefanya uamuzi sahihi kwa nafsi yake, na amesema hajaondoka kwenye chama..tumpe muda atafakari zaidi, atajoin nasi mbele ya safari.

Mchango wake kwenye chama chetu ni mkubwa sana..tuuheshimu kwa kufunga midomo yetu kumjadili, tufocus zaid kwenye uchaguzi mkuu wa oct 25.

Na uamuzi wa Mbowe kumruhusu Lowassa aingie kwenye chama nao ni sahihi kutokana na hali ya kisiasa ya wakati huu. Kila mtu aheshimu mawazo ya mwenzake.

Maccm yanaendeleza propaganda nyingi kana kwamba kuna mpasuko mkubwa, na chimvi nyingi juu ya Dr Slaa na juu ya Lowassa, na juu ya Mbowe na uamuzi wa Chama..tuwapuuze, tusiwape nafasi.

ALUTA KONTINUA..
 
Back
Top Bottom