Ni wanafki hawawezi kushinda,washaonyesha sura zao
Dhama izo nizakale binti 2015 hii we luka luka tu
Ni wanafki hawawezi kushinda,washaonyesha sura zao
acha washindweee. Kwa kweli, Sipigi kura ukawa kama Lowasa ndo kasimamishwa na Slaa katimuliwa indirect. Nashawishi wafuasi wangu pia wasipigie kkura CDM ktk ngozi ya UKAWA
Dhama izo nizakale binti 2015 hii we luka luka tu
Maccm ayo yanakesha kuchochea hawajui kwamba tumeamua kuwaua rasmi wamepata chakuongea
Kwenye list of shame mlimleta ya nini kama mnamsimamisha Leo kama sio uwehu,hivi unajua hata unachosimamia?
Kama ilivyokuwa kwa Lowassa na wapambe wake ndani ya CCM, Dr. Slaa naye hajaridhika na mchakato ndani ya CHADEMA. Kama ilivyokuwa kwa Lowassa, Dr. Slaa na wafuasi wake nao vivyo hivyo wana haki ya kuachana na CHADEMA.
Kama kuondoka kwa Lowassa kumeikosti CCM, kuonda kwa Dr. Slaa hakuwezi kuiacha salama CHADEMA.
Bora CCM less Lowassa kuliko CHADEMA plus Lowassa.
Alipo fisadi mimi sipo!
Kama ilivyokuwa kwa Lowassa na wapambe wake ndani ya CCM, Dr. Slaa naye hajaridhika na mchakato ndani ya CHADEMA. Kama ilivyokuwa kwa Lowassa, Dr. Slaa na wafuasi wake nao vivyo hivyo wana haki ya kuachana na CHADEMA.
Kama kuondoka kwa Lowassa kumeikosti CCM, kuonda kwa Dr. Slaa hakuwezi kuiacha salama CHADEMA.
Bora CCM less Lowassa kuliko CHADEMA plus Lowassa.
Alipo fisadi mimi sipo!
Na usiwepo
Waliokuwa wanajipambanua kupinga ufisadi Leo wanasafisha mafisadi
Ndugu huna agenda nyingne ukiacha hyo ya ufisadi
Ndo mliwatangaza mafisadi na kuifanya agenda kwenye m4c nchi nzima Leo unaulizaje angenda lingine mbali na ufisadi?unajua hata unachosimamia ww?
Mbowe katudhalilisha sana wanachadema,ccm wameingia chadema baada ya mbowe kumleta lowasa na wale chadema wasafi wakiumiwa,Leo chadema imegeuka gafla chama cha kupokea mafisadi huku mbowe na wafuata upepo wakiongea tutoe kwanza CCM madarakani
.
Kweli tunaitoa ccm madarakani kwa UKAWA kumsimamisha lowasa aliyekuwa fisadi!
Bila uso wa haya mnamsafisha lowasa na kumwita mkombozi.
Mafisadi wameingia chadema na ccm imebaki bila mafisadi imewatema halafu chadema mliojipambanua mnapinga ufisadi Leo mnamleta fisadi asimame kwenye UKAWA .
Kama Dr Slaa hatakwepo kwenye safu ya UKAWA nitafurahi UKAWA washindwe kabisa heri ccm iendelee tu,mafisadi wamekuja kusimama kwa upande mwingine na tumewacha kuwathamini waliotoa maisha yao kwa ajili ya chama.
Wakati watu wakipigwa risasi,mabomu arusha,wakipigwa risasi ya moto morogoro na nzega lowasa alikuwa wapi Leo anaibuka tu kama mzimu.
Kina Dr Slaa wakipelekwa polisi,mpaka mke wa Slaa alipigwa na polisi na kumwagika damu,kina Tundu Lissu walichaniwa mpaka nguo kudhalilishwa na hawa ccm sera za majukwaani ilikuwa kuwaponda hao mafisadi wa ccm.
Leo lowasa kaingia chadema analeta jopo la mafisadi wa ccm watu mnashangilia.
NITAFURAHI UKAWA ISHINDWE UCHAGUZI MKUU KAMA DR SLAA HAYUPO NA KAMA Mgombea ni lowasa.
Nahakikisha mwaka huu kwa madudu anayofanya mbowe lowasa akisimama UKAWA na wakashindwa upinzani ndo utakuwa umekufa rasmi mpaka hapo itakapokuja chama makini na siyo ACT wazalendo
Tushike dola kwanza hayo mengne badae
Kama unataka uthibitisho kwamba sisi wengine ni CDM basi sema tukutumie namba za kadi zetu ukaprove ..usiwasakizie CCM kila jambo kwa ujinga wenu wenyewe kwani ndo waliowatuma mkauze chama chetu?
Umeongea kijazba bila kujenga hoja za maana by da way unamatatizo unaposema utafurahi ukawa wakishindwa inamaana hutaki mabadiliko alafu sisi tushaona mfumo wa ccm hautufai tunahitaji changamoto mpya nyie vilaza ndio maana hitler alikuwa hawaachi mzidi kuongea mihemko yenu hakuna uthibitisho lowassa ni fisadi kwa kauli yake na jibu la serikali kushindwa kumchukulia hatua inamaana alikuwa mkubwa kuzidi serikali au ?????
Mkuu amani iwe nawe.
Naomba niandike machache labda utanielewa kidogo. Nami nilikuwa kama wewe katika kumchukia Edward Lowassa kwamba ni Fisadi, na nilimchukia kwa sababu "kusikia kwamba ni Fisadi" wakati sikuwa na ushahidi wowote.
Katika suala la Richmond kama utaangalia kiundani na kusikia kile Edward Lowassa alichosema utaona wazi kwamba ilikuwa ni mpango maalumu wa kumchafua na kumuondoa Edward Lowassa katika kiti cha Uwaziri mkuu. Kilichompoza Lowassa mpaka kusukiwa mpango huo mchafu ni ukali, umakini wa kufuatilia mambo na usimamizi wa yale anayoyaamini. Alipokuwa waziri mkuu tuliona wazi kwamba mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya walikuwa wanawajibika kisawasawa tokana na ukali wa Lowassa. Walikuwa hawaondoki vituo vyao vya kazi bila ruhusa maalumu toka ofisi ya waziri mkuu.
Muheshimiwa pale magogoni akaona wazi kwamba anafunikwa na Lowassa kwani viongozi wengi walikuwa wanachukua maelekezo na maagizo toka kwa Lowassa, ndipo zengwe lilipikwa la kumuondoa Lowassa madarakani.
Jiulize kwa makini sana, kama kweli Lowassa alifanya uchafu ule na kama ushahidi upo kwanini asipelekwe mahakamani?
Chadema walimuingiza Lowassa kwenye list of shame sababu kama zako wewe leo unayemchukia Lowassa kwa sababu za kusikia na kuambiwa. Juzi Lowassa karudia live kwenye TV kwamba alitaka kuvunja mkataba wa Richmond baada ya kujua kwamba ulikuwa fake, lakini bosi wake hakutaka kumsikiliza. Ulitaka Lowassa afanye nini zaidi?. Unaamini kabisa suala kama la Richmond mkuu wa nchi hakulijua toka mwanzo?. Unakumbuka tume ya Mwakyembe ilisema wazi kabisa kwamba inaficha baadhi ya mambo ili kuinusuru serikali, unafikiri walimaanisha nini?. Tume hiyohiyo ya Mwakyembe ilipewa mamlaka makubwa sana ya kumuhoji mtu yeyote bila kuogopa cheo alichonacho. Tume iliweza kuwahoji wahusika karibu wote na iliweza kusafiri mpaka USA kuwahoji wahusika, kwanini ilishindwa kumuhoji Edward Lowassa aliyekuwa na ofisi zikitazamana na ofisi ya tume hiyo?
Ni kweli kabisa Dr Slaa amejitolea sana katika kuifikisha Chadema hapa ilipo leo. Amejitolea kwa kila hali na mali, na kuna muda aliweka rehani mpaka maisha yake, lakini kuiacha Chadema leo juhudi zake zote alizofanya kuijenga na kuifikisha chadema hapa ilipo zitakuwa hazina maana tena. Slaa kama padri nilitegemea sana kwamba angefurahi kuona watu kama Lowassa wanajiunga na Chadema huku wakieleza (kutubu) ukweli machafu yaliyomo ndani ya CCM na yale tuliyokuwa tunasikia wametenda.
Mimi, wewe, wale na yule bila ubishi tumeichoka CCM. Sasa ni wakati wa kuunganisha nguvu kuitoa CCM madarakani. Ujio wa Lowassa na wenzake ndani ya Chadema naona iwe ni baraka kwetu wala isiwe laana. Kama umepitia mafunzo ya kijeshi utakumbuka kwamba tulifundishwa mateka anaweza kukusaidia kushinda vita, anajua siri nyingi za adui zako hivyo ukimtumia vyema utashinda vita. Nasi tunataka kuishinda CCM na kuitoa madarakani, huyu mateka itabidi afuate matakwa yetu, aishi kama sisi ili awe salama. Lowassa na wenzake wamejiunga Chadema na si Chadema wamejiunga na Lowassa, hivyo Lowassa na wenzake itabidi waishi na kufuata matakwa na malengo ya Chadema.