Dr Shein amtolea uvivu Rais Mstaafu Karume!

Dr Shein amtolea uvivu Rais Mstaafu Karume!

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,621
Reaction score
14,577
Katika hali isiyo ya kawaida na kuonyesha kuwa uvumilivu unaenda kufikia kikomo,Dr Shein ameanza kufunguka kuonyesha asivyoridhika na mambo anayofanya Rais Msaafu Amani Karume katika masuala ya kisiasa, hususan Muungano.


Amani karume inaelekea ameingia ubia wa kisiasa na Maalim Seif Sharrif Hamad katika kudai Muungano wa mkataba, sera ambayo si ya chama chake cha CCM.


Katika gazeti la leo Nipashe ,9/07/2013 nanukuu:
"Na Mwinyi Sadallah, Zanzibar

Katika hali inayoelekea kumlenga mtangulizi wake katika Ikule ya Zanzibar, Rais Ali Mohammed Shein , amesema hawezi kumzunguka Rais wa Jamhuri ya Muungano, Jakaya Mrisho Kikwete kwa kupigia debe Muungano wa mkatabakama mwanavyotaka baadhi ya Wazanzibari
......
Akizungumza huku akionyesha kuchukizwa na kamati hiyo( ya akina Sef Sharrif Hamad na Karume),Dk Shein alisema Serikali ya Jamhuri ya Muungano na ile ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ), haina mawazo wala msimamo bali inachokingojan ni ni mawazo ya wananchi wenyewe kwa vile katiba ni chombo cha umma wenye maamuzi kuhusu Muungano wanao utaka."

Alimaliza
...
Wasiniingize mimi katika mpango wao wala wasitake kufika waendako kwa kutumia mabega yangu,wamelipika sasa walinywe wenyewe"

Huko Zenji mbichi na mbovu za Malim na swahiba wake Amani Karume zinaanza kujitokeza.
 
huyo Amani si amewai kuzomewa Dodoma kwenye kikao cha NEC kwa kuitwa "mwanauamusho" yeye akawajibu wanamzomea "wanavichwa vya samaki"!!!
 
hao wote wahuni karume hakujiandaa kustaafu sasa anahangaika tu.
 
Hayo yao wenyewe , mimi Mtanganyika wa Katumbasongwe wala hayanihusu !
 
Ukweli ukoje? Hao viongozi wa Zanzibar waliomtangulia Shein walipokuwa madarakani walishindwa kutoa mawazo yao ya ndani kuhusu muungano kutokana na mazingira ya kisiasa yenye hofu na woga ulioasisiwa na Nyerere kwa misingi aliyokuwa akiitetea! Kuanzia Karume ambaye alimsumbua sana Nyerere kuhusu Muungano hewa, kisha Abood Jumbe aliyetoswa kwa kujifanya jasiri, njoo kwa Salmin Amour aliyewaambia wazi Watz msiingilie mambo ya Zanzibar na OIC, hakuna aliyekuwa anaukubali muungano moyoni mwake! Na Shein akiondoka madarakani huenda akawa wa kwanza kuipokea Zanzibar "mpya na huru"
 
Hayo yao wenyewe , mimi Mtanganyika wa Katumbasongwe wala hayanihusu ![/ QUOTE]

Ewe Mtanganyika wa huko Ziwa Nyasa, kumbuka kodi unayolipa kwa biashara zako za Kasumulu ndizo zinazobeba gharama za kuuendesha matumizi na matanuzi ya serikali ya Zenj! Waache waendelee kushoboana huko visiwani hadi wajitoe tupate nafuu yetu!
 
Ukweli ukoje? Hao viongozi wa Zanzibar waliomtangulia Shein walipokuwa madarakani walishindwa kutoa mawazo yao ya ndani kuhusu muungano kutokana na mazingira ya kisiasa yenye hofu na woga ulioasisiwa na Nyerere kwa misingi aliyokuwa akiitetea! Kuanzia Karume ambaye alimsumbua sana Nyerere kuhusu Muungano hewa, kisha Abood Jumbe aliyetoswa kwa kujifanya jasiri, njoo kwa Salmin Amour aliyewaambia wazi Watz msiingilie mambo ya Zanzibar na OIC, hakuna aliyekuwa anaukubali muungano moyoni mwake! Na Shein akiondoka madarakani huenda akawa wa kwanza kuipokea Zanzibar "mpya na huru"

umefafanua vizuri sana mdau
 
Hawa viongozi wa zenji ni vigeu geu sana!

Sita shangaa hata na yeye Shein kuupiga vita muungano baada ya kumaliza kipindi chake cha uraisi!
 
Dr. Shein ni Kibaraka tu na anachojali yeye ni maslahi Yake tu yaende ili asirudi alikotoka kuwa Boi wa Wahindi
 
Karume naye mnafiki wakati akiwa kwenye madaraka mbona hakusema hayo au alikaa kimya kwa vile urais wake aliupata baada ya kubebwa na CCM bara.
 
Hawa viongozi wa zenji ni vigeu geu sana!

Sita shangaa hata na yeye Shein kuupiga vita muungano baada ya kumaliza kipindi chake cha uraisi!

Mkuu MAVUMBI kaisema vizuri hii; WOGA unawafanya wasiseme WANAYOWAZA.........Tusubiri akistaafu atakuja na msimamo gani!!!! Taabu ya wanasiasa wetu unafiki mtuupu; wanalolisema kwenye majukwaa na wanaloliamini au kulitaka mioyoni mwao ni tofauti kabisa kama mbingu na nchi!!!!!
 
Hivi karime si mjomba na maalimu ndo mana myu na mjombaake si wana maliza mambo. Shauri yao si tunasubili serikari ya tatu tuanze mizengwe nasi
 
Katika hali isiyo ya kawaida na kuonyesha kuwa uvumilivu unaenda kufikia kikomo,Dr Shein ameanza kufunguka kuonyesha asivyoridhika na mambo anayofanya Rais Msaafu Amani Karume katika masuala ya kisiasa, hususan Muungano.


Amani karume inaelekea ameingia ubia wa kisiasa na Maalim Seif Sharrif Hamad katika kudai Muungano wa mkataba, sera ambayo si ya chama chake cha CCM.


Katika gazeti la leo Nipashe ,9/07/2013 nanukuu:
"Na Mwinyi Sadallah, Zanzibar

Katika hali inayoelekea kumlenga mtangulizi wake katika Ikule ya Zanzibar, Rais Ali Mohammed Shein , amesema hawezi kumzunguka Rais wa Jamhuri ya Muungano, Jakaya Mrisho Kikwete kwa kupigia debe Muungano wa mkatabakama mwanavyotaka baadhi ya Wazanzibari
......
Akizungumza huku akionyesha kuchukizwa na kamati hiyo( ya akina Sef Sharrif Hamad na Karume),Dk Shein alisema Serikali ya Jamhuri ya Muungano na ile ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ), haina mawazo wala msimamo bali inachokingojan ni ni mawazo ya wananchi wenyewe kwa vile katiba ni chombo cha umma wenye maamuzi kuhusu Muungano wanao utaka."

Alimaliza
...
Wasiniingize mimi katika mpango wao wala wasitake kufika waendako kwa kutumia mabega yangu,wamelipika sasa walinywe wenyewe"

Huko Zenji mbichi na mbovu za Malim na swahiba wake Amani Karume zinaanza kujitokeza.
Karume yuko sawa hata sisi Watanganyika tunataka Tanganyika yetu, alafu tufanye muungano wa mkataba ikishindikana tuwe majirani wema kama tulivyo majirani na Kenya,Uganda, Malawi,Zambia,Burundi,Rwanda,Comoro na Kongo
 
Karume yuko sawa hata sisi Watanganyika tunataka Tanganyika yetu, alafu tufanye muungano wa mkataba ikishindikana tuwe majirani wema kama tulivyo majirani na Kenya,Uganda, Malawi,Zambia,Burundi,Rwanda,Comoro na Kongo

Tanganyika daima.
 
Tatizo la zenj wanakuzwa kihuni hata wakijaingia ktk ustaarabu uhuni na upuuzi hauwatoki...Nini sasa hawajaelewa kuhusu huo muungano na utatawake?Mbona hakufanya hivyo akiwa rais.Wazenj wakiingia ktk ustaarabu wanapata ustaarabu wa muda..halafu wakitoka wanauacha na kurudi mashenzini kwao.

Kwa nini asikumbuke dhana iliyomfanya akaukubali uzenj na muungano kw akipindni chote alichokuwa mwana CCM no moja wa ikulu.Na alihubiri muungano hadi alipotoka.Sasa km Kila anayeondoka anaamua blackmail serikali ya Tanganyika kwa kuchokonoa Muungano basi tutauza vingi sana kwa kutokuwa serious.
 
Ukweli ukoje? Hao viongozi wa Zanzibar waliomtangulia Shein walipokuwa madarakani walishindwa kutoa mawazo yao ya ndani kuhusu muungano kutokana na mazingira ya kisiasa yenye hofu na woga ulioasisiwa na Nyerere kwa misingi aliyokuwa akiitetea! Kuanzia Karume ambaye alimsumbua sana Nyerere kuhusu Muungano hewa, kisha Abood Jumbe aliyetoswa kwa kujifanya jasiri, njoo kwa Salmin Amour aliyewaambia wazi Watz msiingilie mambo ya Zanzibar na OIC, hakuna aliyekuwa anaukubali muungano moyoni mwake! Na Shein akiondoka madarakani huenda akawa wa kwanza kuipokea Zanzibar "mpya na huru"
Naona wewe hujui chimbuko la siasa za muungano.

Wanoutaka muungano Zanzibar ni wale waafrika halisi, kama mimi na wewe .
Wasioutaka muungano ni wale wenye asili ya kiarabu na walio na wajomba zao uarabuni.
Its as simple as that.

Ukweli ni kwamba baada ya muungano kushambuliwa kwa miaka mingi upande wa Tanganyika has decided to call a spade a spade, na ndio nionavyo rasimu ya Warioba ya katiba mpya.

Suala hili limewapanikisha waliouasisi maana hawakuutetea vilivyo katika medani za siasa.

Siyo siri Sherrif na Amani Karume wana uasili wa kiarabu na wameamua kuside na upande huo.

Tofauti na wengi wanavyofikiri ubaguzi Zanzibar upo na wanaouhitaji muungano ni waafrika zaidi kuliko wenye asili ya kiarabu.
 
Back
Top Bottom