Ulitaka tumpe nchi mburu slaa tumuache mtoto Wa mjini jakaya unatufanya sie wajinga mpeni ushirikiano ajenge nchi nyie mnamuharibia atafukuza wangapi ktk serikari
HATIMAYE Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemtaja Dk. Wilbroad Slaa ambaye ni katibu Mkuu wake kuwa ndiye mgombea wake wa Urais katika Uchaguzi Mkuu ujao wa Rais na Wabunge utakaofanyika 2015.
Chama hicho kinaamini ya kuwa kitashinda katika uchaguzi huo, na endapo kitashinda kweli, basi kitamteua Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe kuwa Waziri Mkuu.
Safu hiyo ya watawala wapya nchini ilitangazwa wiki iliyopita na Mbunge wa Nyamagana, Hezekiah Wenje, wakati akiwahutubia maelfu ya wananchi waliokusanyika katika viwanja vya Mbungani Jijini Mwanza kwenye mkutano wa wabunge wa CHADEMA waliosimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kwa siku tano.
Wenje katika mkutano huo alitangaza Zitto Kabwe, ambaye amepata kusema kwamba hatagombea tena ubunge, atakuwa Waziri wa Fedha, huku yeye akishika Wizara ya Mambo ya Nje.
Kwa mujibu wa Wenje, Waziri wa Maliasili na Utalii atakuwa Mchungaji Peter Msigwa huku nafasi ya Waziri wa Michezo na Utamaduni ikienda kwa Joseph Mbiliniyi, ama maarufu kama Sugu. Waziri wa Nishati na Madini atakuwa John Mnyika na Waziri wa Sheria atakuwa Tundu Lisu.
Alisema Wizara ya Mambo ya Ndani itashikwa na Godbless Lema, Wizara ya Kilimo itakuwa chini ya Meshack Opulukwa na ile ya Mazingira itasimamiwa na Halima Mdee wakati ya Viwanda na Biashara itashikwa na Highness Kiwia.
Wenje aliwahakikishia wananchi waliohudhuria mkutano huo kwamba chama chake kimejipanga na kwamba hakina wasiwasi hata kidogo kuongoza dola mwaka 2015 kwa kuwa kina wapiganaji imara wanaoweza kuwakwamua Watanzania kutoka katika lindi la umaskini.
"Nchi haifanyi ya kutosha kuimarisha shilingi yetu, yupo msomi mmoja wa CCM ambaye anaamini kuwekwa kwa picha ya Nyerere na Karume hela yetu itapanda thamani. Hawa watu ni hatari, tupeni dola 2015 ili Zitto (Zitto Kabwe) awe Waziri wa Fedha, ni kijana mwenye akili nzuri nchi itakwenda," alisema.
Inaendelea hapa Raia Mwema - Timu ya CHADEMA 2015
Kwani ikulu raisi anafanya kazi ya kubeba zege?you are right!! tatizo kubwa kwake by that time ni umri!!
By 2015 nazani atakuwa anakaribia miaka 80 na kama sio basi atakapomaliza mihula miwili atakuwa keshafikia umri huo!!! Hatuna haja na wa2 kama hao kwavile bado kuna vijana au wazee kidogo wengi tu wenye uwezo wa kuongoza!!!
Wadau mnamuonaje Dr. Salim, kwa uadilifu wake na taswira na haiba yake Kitaifa na Kimataifa haimtoshi kuongoza Nchi yetu ya Tanzania kwenye ngazi ya Urais?
wadau mnamuonaje dr. Salim, kwa uadilifu wake na taswira na haiba yake kitaifa na kimataifa haimtoshi kuongoza nchi yetu ya tanzania kwenye ngazi ya urais?
'mtoto wa mjini jakaya' unawajua vizuri watoto wa mjini? we ndo kichefuchefu kabisa. Hii nchi sio familia acha ubwege,viva chadema viva
Kwani swala walilo mzushia la kuhusika na kifo cha karume limeishia wapi 'hidsbora..." kama sijakosa? kwani hiyo siyo kashfa! CCM bwana wana chafuana vibaya sana wao kwa wao. maji yakiwafiak puani wanaanza kulambana miguu. jama wapuuzi sana
Kwani Padri Slaa ana miaka mingapi vile?
Wadau mnamuonaje Dr. Salim, kwa uadilifu wake na taswira na haiba yake Kitaifa na Kimataifa haimtoshi kuongoza Nchi yetu ya Tanzania kwenye ngazi ya Urais?
Tatizo chama alichomo; 2010 walimkataa kiulaini kabisa bila hata aibu! Kwenye chama chake uwezo wake mkubwa na uadilifu wake uliotukuka ni kikwazo!
CCM hatuna tabia ya kuteua mgombea wa kiti cha Uraisi kabla ya uchaguzi huru na wa haki. Hayo mambo ya kumteua mgombea wa Uraisi kabla hata ya uchaguzi yapo CHADEMA.
Right candidate ni yule atakayechaguliwa baada ya uchaguzi wa ndani ya chama chetu.
Slaa anaonekana mzee zaidi kuliko umri wake.....Salim is older than Slaa for at least 5 years!Kwani Padri Slaa ana miaka mingapi vile?