Dr. Nchimbi kaniacha kinywa wazi

Dr. Nchimbi kaniacha kinywa wazi

Ndio maana anasema 'piganieni' ujue kuna ka mkwamo mahala. CCM ni dude kubwa Lina mizizi iliyojichimbia.
 
Hata sijui, sisi huku kijijini naona vumbi linatimka tu watu wanachimbia nguzo za kusambaza umeme kwenye vitongoji. Wananchi akiwemo bibi hasemi chochote zaidi ya kutaka matibabu ya mgongo wake.
Mkuu umewahi kujiuliza mbona nguzo zinachimbiwa, lakini zahanati ya kijiji haina dawa zinazoweza kumsaidia bibi shida yake ya mgong au haina daktari wa maana?

Jibu ni rahisi, ni kwa sababu katiba yetu ya sasa haimlazimishi Rais au Waziri kupeleka huduma bora za afya vijijini kama haki ya kikatiba. Kwenye katiba mpya, tunataka huduma za afya ziwe ni haki ya lazima ya mwananchi na sio fadhila au hisani ya kiongozi akijisikia.
Kama Museveni yuko kwa miaka yote ile kumbe hata CCM ina afadhali kubwa kwa kubadilisha viongozi kila miaka 10. Serikali ya nusu mkate kati ya CCM na Jeshi nadhani ndilo suluhisho kwasasa hadi 2050 tutakapokuwa tumekomaa zaidi kisiasa
Upo sahihi, sisi tuna afadhali Lakini mzee wangu, kubadilisha dereva huku gari lilelile likiendelea kuwa na rejeta mbovu na breki zilizokatika bado ni hatari. Suala sio tu nani anatawala bali ni je, huyo anayetawala anaongozwa na sheria gani? Kama mifumo ni ileile, hata sura mpya ikiingia madudu yanabaki kuendelea kuwatesa wananchi.
 
Samuya akiwa makamu wa Raisi alikwenda Nairobi Hospitali kumjulia hali Mhe. LISSU ALIYEKUWA AMEPIGWA RISASI 36.

Wakati huo huo, "Jiwe" ambaye ndiye aliyekuwa Rais, alikataza watu wasimchangie chochote Mhe.Lissu—ambaye jiwe alimuita "msaliti"

Kwa logic rahisi ungeweza kuhisi kwamba Makamu wa Rais(samuya) na Rais (jiwe) hawaelewani.

Lakini huenda yote hayo yalikuwa yamepangwa na samuya na jiwe ili kuwafanya watu kutozungumzia madhila ya Lissu na badala yake waanze kuwazungumzia wao (jiwe na samuya) kwamba hawaelewani.

Hali kama hiyo imejitokeza tena jana pale Imma alipowashauri Watanganyika wadai khatiba mpya kwa nguvu kubwa huku wakati huo huo samuya akiwapa vijana kesi ya ugaidi kwa kudai haki yao: khatiba mpya.
 
Athari hutokana na kutoijua katiba. Tuhakikishe kila mtanzania au angalau ¾ ya watanzania wanaijua katiba iliyopo. Ili wakati tunajadiri mapungufu, iwe rahisi kulibeba kwa pamoja.

Leo hii mtanzania wa kawaida haoni umuhimu wa kudai katiba kwasababu hata haelewi katiba ni nini. Ndio maana unaona wanaachiwa wanaharakati na vyama vya siasa kwasababu wao wanafuatilia kuhusu haki zao.

Mtanzania wa kawaida anapambania hela ya madawa hospitalini, hela ya chakula kwa familia, hela ya mahitaji ya shule kwa mtoto wake. Kula yake anaipata kwa siku. Akitoka ndo ale. Ukimuambia habari za kudai katiba anakushangaa kwasababu anadhani sio hitaji lake la msingi
Nachomaanisha ni kwamba hata hii katiba iliyopo sasa uzuri na ubaya wake unatuathiri wote bila kujali wenye kuijua au kutokuijua, hata kama mimi siijui hii katiba iliyopo ila yale yenye kuelezwa kama mapungufu ya hii katiba inabaki kuwa ndio ukweli huo hata kama mimi sina uelewa nalo hilo, na endapo ikija katiba mpya ambayo imerekebisha yale mapungufu yaliyokuwepo kwenye katiba ya sasa faida zake tutazipata wote na si kwa wale wenye uelewa na hiyo katiba tu.

Kwahiyo inawezekana kabisa katika hayo ambayo mtanzania wa kawaida anayapambania kila siku akaja kuona mabadiliko katika hayo mambo anayoyapambania kama athari ya mabadiliko ya katiba.
 
Ndio maana mimi hakuna mtu yeyote kutoka ccm naweza kumwamini hata kama amekufa siwezi kumwanini kamwe
 
Nachomaanisha ni kwamba hata hii katiba iliyopo sasa uzuri na ubaya wake unatuathiri wote bila kujali wenye kuijua au kutokuijua, hata kama mimi siijui hii katiba iliyopo ila yale yenye kuelezwa kama mapungufu ya hii katiba inabaki kuwa ndio ukweli huo hata kama mimi sina uelewa nalo hilo, na endapo ikija katiba mpya ambayo imerekebisha yale mapungufu yaliyokuwepo kwenye katiba ya sasa faida zake tutazipata wote na si kwa wale wenye uelewa na hiyo katiba tu.

Kwahiyo inawezekana kabisa katika hayo ambayo mtanzania wa kawaida anayapambania kila siku akaja kuona mabadiliko katika hayo mambo anayoyapambania kama athari ya mabadiliko ya katiba.
Upo sahihi na huo ndio ukweli. Ila sasa utatumia njia gani kuwashawishi hawa wanaopata athari kutokana na katiba iliyopo? Waliopo madarakani inawanufaisha na hawana haja ya kubadilisha?
 
Mkuu umewahi kujiuliza mbona nguzo zinachimbiwa, lakini zahanati ya kijiji haina dawa zinazoweza kumsaidia bibi shida yake ya mgong au haina daktari wa maana?

Jibu ni rahisi, ni kwa sababu katiba yetu ya sasa haimlazimishi Rais au Waziri kupeleka huduma bora za afya vijijini kama haki ya kikatiba. Kwenye katiba mpya, tunataka huduma za afya ziwe ni haki ya lazima ya mwananchi na sio fadhila au hisani ya kiongozi akijisikia.

Upo sahihi, sisi tuna afadhali Lakini mzee wangu, kubadilisha dereva huku gari lilelile likiendelea kuwa na rejeta mbovu na breki zilizokatika bado ni hatari. Suala sio tu nani anatawala bali ni je, huyo anayetawala anaongozwa na sheria gani? Kama mifumo ni ileile, hata sura mpya ikiingia madudu yanabaki kuendelea kuwatesa wananchi.
Mimi ni mtanzania lakini sina wakati ambao nimejisikia kuwa sasa ninateseka kwasababu ya katiba. Kaka Katiba hii ni mbaya kwa mwanasiasa ambae anataka kwenda Ikulu baasi. Bahati mbaya wanasiasa wetu wa upinzani wanadhani kuwa hawaendi ikulu kwasababu ya Katiba na tume ya uchaguzi tu, lakini ukweli Katiba ni sehemu ndogo sana ya shida yao ya kutokwenda Ikulu. Tatizo lao vyama vyao havikubaliki kwa watu wengi wq mikoani, vimekaakaa kama vyama vya kikabila na kidini zaidi kuliko kitaifa. Mfano chadema kina msukumo wa kichagga na kipare zaidi kuliko kitaifa. Vimekaa kama saccos kiasi kwamba kiongozi akikosa nafasi ndani ya chama anahamia CCM kwa hasira au kwa kupewa fedha.
 
Upo sahihi na huo ndio ukweli. Ila sasa utatumia njia gani kuwashawishi hawa wanaopata athari kutokana na katiba iliyopo? Waliopo madarakani inawanufaisha na hawana haja ya kubadilisha?
Katiba hii ni tamu kwa CCM na kwa jeshi na majeshi yetu. Hebu ona afande Mabeyo na AFANDE IGP mstaafu, Siro wako wapi hivi sasa baada ya kustaafu. Usitarajie kuwa ni rahisi kupambana kama anavyotudanganya Dr. NCHIMBI, utapotea tukusahau. Hii nchi ni usilete kamdomo tumia fursa kama umeiona.
 
Upo sahihi na huo ndio ukweli. Ila sasa utatumia njia gani kuwashawishi hawa wanaopata athari kutokana na katiba iliyopo? Waliopo madarakani inawanufaisha na hawana haja ya kubadilisha?
yaani sisi hatunufaiki na hii Katiba? HEbu acheni hizo. Au hamjui maana na kazi ya Katiba?

Katiba hii wazazi wake halisi wametoka China na Russia, wajomba zake wanaishi Cuba na N.Korea.

CCM ni kubwa sana kuliko Dr. SAMIA na Dr. Nchimbi, kama CCM ikikataa jambo sio Rais wala Makamu watakuwa na chakufanya. CCM ina wenyewe. Horace Kolimba alikuwa Katibu CCM aliposema CCM haina dira wala mwelekeo, alikutana uso kwa uso na wenye chama.
 
Nachomaanisha ni kwamba hata hii katiba iliyopo sasa uzuri na ubaya wake unatuathiri wote bila kujali wenye kuijua au kutokuijua, hata kama mimi siijui hii katiba iliyopo ila yale yenye kuelezwa kama mapungufu ya hii katiba inabaki kuwa ndio ukweli huo hata kama mimi sina uelewa nalo hilo, na endapo ikija katiba mpya ambayo imerekebisha yale mapungufu yaliyokuwepo kwenye katiba ya sasa faida zake tutazipata wote na si kwa wale wenye uelewa na hiyo katiba tu.

Kwahiyo inawezekana kabisa katika hayo ambayo mtanzania wa kawaida anayapambania kila siku akaja kuona mabadiliko katika hayo mambo anayoyapambania kama athari ya mabadiliko ya katiba.
Hebu tuambie, wewe kama wewe hii katiba inakuathilije?
 
Samuya akiwa makamu wa Raisi alikwenda Nairobi Hospitali kumjulia hali Mhe. LISSU ALIYEKUWA AMEPIGWA RISASI 36.

Wakati huo huo, "Jiwe" ambaye ndiye aliyekuwa Rais, alikataza watu wasimchangie chochote Mhe.Lissu—ambaye jiwe alimuita "msaliti"

Kwa logic rahisi ungeweza kuhisi kwamba Makamu wa Rais(samuya) na Rais (jiwe) hawaelewani.

Lakini huenda yote hayo yalikuwa yamepangwa na samuya na jiwe ili kuwafanya watu kutozungumzia madhila ya Lissu na badala yake waanze kuwazungumzia wao (jiwe na samuya) kwamba hawaelewani.

Hali kama hiyo imejitokeza tena jana pale Imma alipowashauri Watanganyika wadai khatiba mpya kwa nguvu kubwa huku wakati huo huo samuya akiwapa vijana kesi ya ugaidi kwa kudai haki yao: khatiba mpya.
Kosa lake hakutuambia tupambane na nani na njia za kupambania. Inawezekana wanaopinga Katiba mpya ndani ya CCM wana hoja. Hata Mwl Nyerere alizima kwa hoja uasi wa G55 waliokuwa wakitaka Katiba mpya yenye Tanganyika. Haya mambo sio mageni na muda wote wanashindwa.
 
Mkuu umewahi kujiuliza mbona nguzo zinachimbiwa, lakini zahanati ya kijiji haina dawa zinazoweza kumsaidia bibi shida yake ya mgong au haina daktari wa maana?

Jibu ni rahisi, ni kwa sababu katiba yetu ya sasa haimlazimishi Rais au Waziri kupeleka huduma bora za afya vijijini kama haki ya kikatiba. Kwenye katiba mpya, tunataka huduma za afya ziwe ni haki ya lazima ya mwananchi na sio fadhila au hisani ya kiongozi akijisikia.

Upo sahihi, sisi tuna afadhali Lakini mzee wangu, kubadilisha dereva huku gari lilelile likiendelea kuwa na rejeta mbovu na breki zilizokatika bado ni hatari. Suala sio tu nani anatawala bali ni je, huyo anayetawala anaongozwa na sheria gani? Kama mifumo ni ileile, hata sura mpya ikiingia madudu yanabaki kuendelea kuwatesa wananchi.
SHIDA YA Samia anafanya vyote kwa wakati mmoja. JPM alikuwa anafanya mambo mengi lakini kwa kusimamisha mambo mengia pia. Aliacha kulipa wastaafu, aliacha kuajili na kupandisha watumishi wote mishahara na madaraja kwa miaka 6 ili ajenge reli, bwawa, madaraja na kuhamia Dodoma. Rais Samia anafanya vyote kwa wakati mmoja kwenye uchumi mdogo kama wetu, ndio maana unaweza kukuta dawa ni chache kwenye zahanati.

Kama Katiba hii ndiyo inayofaa kwa kutujengea reli haraka basi tujenge reli haraka ili tupate fedha nyingi za kugharamia uandishi wa katiba kutokana na mapato ya SGR na miradi mingine kama bomba la mafuta na bandari.

Tuna kazi kubwa ya kujenga reli ndefu na ghali kwenda Kigoma, Mwanza, DRC na Burundi. Hebu watanzania tufanye haya kwanza kuliko kuongelea Katiba Katiba ambayo hata kesho tutaiandika tu, tusitoke kwenye reli.

Binafsi namuomba Rais Samia azibe masikio yake kwanza ajikite kwenye mambo ya haraka kama ujenzi wa SGR, gesi ya kupikia, kilimo cha kisasa, upanuzi wa bandari, kusambaza maji nchi nzima badala ya kuhangaika na Katiba ambayo hata Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli hawakuona ni kipaumbele cha watanzania namba moja. Hata wao wangeweza kuiandika lakini walikuwa na mambo muhimu kuliko Katiba. Je, Rais Samia anona Katiba ni kipaumbele namba ngapi kwake?

Kama Katiba hii inaruhusu kupitisha nguzo za umeme na mabomba ya maji kwenda kwa wananchi kwa gharama nafuu basi tuitumie hiihii kusambazia wananchi umeme na maji. Kama Katiba hii ndiyo inafaa kupanua viwanja vya ndege mijini kwa gharama ndogo basi tuitumie kwanza Katiba kupanua viwanja kwa manufaa ya watu wote. Magufuli aliweza kupanua barabara ya Kimara kwakuwa Katiba ilimuwezesha kufanya hivyo, barabara ambayo leo inatufaa wote.
 
Mimi ni mtanzania lakini sina wakati ambao nimejisikia kuwa sasa ninateseka kwasababu ya katiba. Kaka Katiba hii ni mbaya kwa mwanasiasa ambae anataka kwenda Ikulu baasi. Bahati mbaya wanasiasa wetu wa upinzani wanadhani kuwa hawaendi ikulu kwasababu ya Katiba na tume ya uchaguzi tu, lakini ukweli Katiba ni sehemu ndogo sana ya shida yao ya kutokwenda Ikulu. Tatizo lao vyama vyao havikubaliki kwa watu wengi wq mikoani, vimekaakaa kama vyama vya kikabila na kidini zaidi kuliko kitaifa. Mfano chadema kina msukumo wa kichagga na kipare zaidi kuliko kitaifa. Vimekaa kama saccos kiasi kwamba kiongozi akikosa nafasi ndani ya chama anahamia CCM kwa hasira au kwa kupewa fedha.
Kuna namna umeongea ukweli Mkuu, lakini hemu jiulize. Hivi kama katiba ingeruhusu mgombea binafsi, ungepoteza muda wako kusikiliza hivyo vyama unavyoviita vya kidini au kikabila?

Tatizo lililopo sio upinzani kwenda Ikulu au CCM kubaki madarakani Mkuu. Ishu ni jinsi mifumo inavyomlinda mwananchi wa kawaida asiyekuwa na chama wala cheo.
 
Nation-MBI anajichongea barabara ya kuupata urais 2030....uzuri wa WE-WE-m wanajua kwenda na beat wanalodance Watanzania.....Mchakato mpaka ukamilike ni miaka 10 ndani ya urais wa Nchimbi..atakayekuja tena 2040 nae ataimba wimbo huohuo wa katiba mpya
 
SHIDA YA Samia anafanya vyote kwa wakati mmoja. JPM alikuwa anafanya mambo mengi lakini kwa kusimamisha mambo mengia pia. Aliacha kulipa wastaafu, aliacha kuajili na kupandisha watumishi wote mishahara na madaraja kwa miaka 6 ili ajenge reli, bwawa, madaraja na kuhamia Dodoma. Rais Samia anafanya vyote kwa wakati mmoja kwenye uchumi mdogo kama wetu, ndio maana unaweza kukuta dawa ni chache kwenye zahanati.

Kama Katiba hii ndiyo inayofaa kwa kutujengea reli haraka basi tujenge reli haraka ili tupate fedha nyingi za kugharamia uandishi wa katiba kutokana na mapato ya SGR na miradi mingine kama bomba la mafuta na bandari.

Tuna kazi kubwa ya kujenga reli ndefu na ghali kwenda Kigoma, Mwanza, DRC na Burundi. Hebu watanzania tufanye haya kwanza kuliko kuongelea Katiba Katiba ambayo hata kesho tutaiandika tu, tusitoke kwenye reli.

Binafsi namuomba Rais Samia azibe masikio yake kwanza ajikite kwenye mambo ya haraka kama ujenzi wa SGR, gesi ya kupikia, kilimo cha kisasa, upanuzi wa bandari, kusambaza maji nchi nzima badala ya kuhangaika na Katiba ambayo hata Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli hawakuona ni kipaumbele cha watanzania namba moja. Hata wao wangeweza kuiandika lakini walikuwa na mambo muhimu kuliko Katiba. Je, Rais Samia anona Katiba ni kipaumbele namba ngapi kwake?

Kama Katiba hii inaruhusu kupitisha nguzo za umeme na mabomba ya maji kwenda kwa wananchi kwa gharama nafuu basi tuitumie hiihii kusambazia wananchi umeme na maji. Kama Katiba hii ndiyo inafaa kupanua viwanja vya ndege mijini kwa gharama ndogo basi tuitumie kwanza Katiba kupanua viwanja kwa manufaa ya watu wote. Magufuli aliweza kupanua barabara ya Kimara kwakuwa Katiba ilimuwezesha kufanya hivyo, barabara ambayo leo inatufaa wote.
Mkuu kosa kubwa wanalofanya watu ni kudhani kudai katiba ni lazima uingie barabarani ,huko ni kujitafutia matatizo bure na hakuna anayetaka damu imwagike tena, njia ya kuwashawishi wananchi sio kuwambia twendeni tukapambane, bali ni kuwazindua kiakili tu. Raia wakijua haki zao wataanza kuunga mkono mabadiliko, shinikizo likiwa kubwa kuna uwezekano wa kupata mabadiliko pasipo hata kutumia nguvu kubwa.

Hata hao Maafande na wana CCM wanaihitaji Katiba imara sana tu Mkuu, kesi ngapi tumeona mtu akiwa mkubwa leo, kesho akitofautiana kidogo tu na wakubwa wenzake anaswekwa ndani au anafilisiwa mali zake zote? Katiba mbovu haina macho inavyomtafuna mpinzani leo, ndivyo itakavyomtafuna mwana-CCM kesho pindi upepo ukigeuka. Katiba mpya inapaswa kulinda usalama wa kila mtu, hadi wa hao wastaaafu. Katika historia ya dunia, hakuna utawala ulishawahi kuachia madaraka au mifumo kwa hiari yao eti kwa sababu wamependa. Mabadiliko huwa yanakuja pale ambapo shinikizo la kiuchumi na ufahamu wa wananchi unakuwa mkubwa kiasi kwamba watawala wanaona ni gharama kubwa zaidi kubaki na mfumo wa zamani kuliko kukubali tu mabadiliko.

Walioko madarakani hawawezi kuwa na hamu ya kubadilisha kitu ambacho kinawanufaisha wao wenyewe.
 
Samuya akiwa makamu wa Raisi alikwenda Nairobi Hospitali kumjulia hali Mhe. LISSU ALIYEKUWA AMEPIGWA RISASI 36.

Wakati huo huo, "Jiwe" ambaye ndiye aliyekuwa Rais, alikataza watu wasimchangie chochote Mhe.Lissu—ambaye jiwe alimuita "msaliti"

Kwa logic rahisi ungeweza kuhisi kwamba Makamu wa Rais(samuya) na Rais (jiwe) hawaelewani.

Lakini huenda yote hayo yalikuwa yamepangwa na samuya na jiwe ili kuwafanya watu kutozungumzia madhila ya Lissu na badala yake waanze kuwazungumzia wao (jiwe na samuya) kwamba hawaelewani.

Hali kama hiyo imejitokeza tena jana pale Imma alipowashauri Watanganyika wadai khatiba mpya kwa nguvu kubwa huku wakati huo huo samuya akiwapa vijana kesi ya ugaidi kwa kudai haki yao: khatiba mpya.
Mwisho ikawaje Magufuli akalamba udongo Samia akawa Rais ,je kama mtindo unafanana vipi MATOKEO YATAFANANA?
 
Back
Top Bottom