kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 17,182
- 16,866
Kama Rais na Mwenyekiti wa CCM, Dr. Samia anataka Katiba mpya, Makamu wa Rais anataka Katiba mpya, sasa ni nani anapinga Katiba mpya kiasi cha Makamu wa Rais Dr Nchimbi kuwataka wananchi wapambane kudai katiba mpya?.
Angalau sasa tunajua ni nani aliyechomekeza kwenye Ilani ya CCM agenda ya Kuandika katiba Mpya. Ambacho ameniacha mdomo wazi ni kuhusu:
1. Nani hataki katiba mpya pale CCM na serikalini kama Rais na Makamu wake wanataka Katiba mpya?
2. Kama mwenyekiti wa CCM anataka Katiba mpya nani pale CCM hataki Katiba Mpya?
3. Wananchi wapambane dhidi ya nani ili wapate Katiba mpya?
4. Wananchi wapambaneje ili kuwazidi nguvu hao wasiotaka katiba Mpya?
5. Tunataka Katiba mpya nzuri kama ya taifa gani Afrika ili tuone wao ni bora kiasi gani wapi kuliko sisi?
6. Je, ubaya wa Katiba hii ya 1977 ni nini?
Nionavyo mimi kama mimi, watu wetu, uchumi wetu, uelewa wetu, kiwango cha elimu cha watu wetu, mila na ustaraabu wetu kupanua kiwango cha demokrasia na haki za watu wetu kuliko hivi tulivyo sasa kutaenda kulitumbukiza taifa kwenye migogoro mingi itakayoidumaza Tanzania. Tunakwenda kutanua uchochoro ambao wakoloni watapitia kuichukua tena Tanzania.
Mwl. Nyerere alikataa kuruhusu wazungu kuchimba sana madini yetu kwakuwa alikuwa anawafahamu watu wake kuwa hawakuwa na utaalamu wa kuyachimba wala elimu ya kujadiliana kuhusu mikataba ya uchimbaji. Watu wetu hawa wengi wao bado hawana uelewa mpana kuhusu demokrasia na haki. Bado kuna maeneo watu wanaona ni haki kwa mwanamke kunyimwa kumiliki hiki na kile, bado mpaka leo kuna watu wanaamini viungo vya binadamu vinaleta utajiri kwa njia za giza. bado kuna watu asubuhi kabisa wanakunywa pombe na kucheza pool siku za kazi.
Sipingi kuandika katiba mpya lakini Makamu Rais Dr Nchimbi ndiye aliyeniogopesha zaidi.
View: https://youtu.be/Y30BPBHftaE?si=E11qcCE9cMml3Wfw
Angalau sasa tunajua ni nani aliyechomekeza kwenye Ilani ya CCM agenda ya Kuandika katiba Mpya. Ambacho ameniacha mdomo wazi ni kuhusu:
1. Nani hataki katiba mpya pale CCM na serikalini kama Rais na Makamu wake wanataka Katiba mpya?
2. Kama mwenyekiti wa CCM anataka Katiba mpya nani pale CCM hataki Katiba Mpya?
3. Wananchi wapambane dhidi ya nani ili wapate Katiba mpya?
4. Wananchi wapambaneje ili kuwazidi nguvu hao wasiotaka katiba Mpya?
5. Tunataka Katiba mpya nzuri kama ya taifa gani Afrika ili tuone wao ni bora kiasi gani wapi kuliko sisi?
6. Je, ubaya wa Katiba hii ya 1977 ni nini?
Nionavyo mimi kama mimi, watu wetu, uchumi wetu, uelewa wetu, kiwango cha elimu cha watu wetu, mila na ustaraabu wetu kupanua kiwango cha demokrasia na haki za watu wetu kuliko hivi tulivyo sasa kutaenda kulitumbukiza taifa kwenye migogoro mingi itakayoidumaza Tanzania. Tunakwenda kutanua uchochoro ambao wakoloni watapitia kuichukua tena Tanzania.
Mwl. Nyerere alikataa kuruhusu wazungu kuchimba sana madini yetu kwakuwa alikuwa anawafahamu watu wake kuwa hawakuwa na utaalamu wa kuyachimba wala elimu ya kujadiliana kuhusu mikataba ya uchimbaji. Watu wetu hawa wengi wao bado hawana uelewa mpana kuhusu demokrasia na haki. Bado kuna maeneo watu wanaona ni haki kwa mwanamke kunyimwa kumiliki hiki na kile, bado mpaka leo kuna watu wanaamini viungo vya binadamu vinaleta utajiri kwa njia za giza. bado kuna watu asubuhi kabisa wanakunywa pombe na kucheza pool siku za kazi.
Sipingi kuandika katiba mpya lakini Makamu Rais Dr Nchimbi ndiye aliyeniogopesha zaidi.
View: https://youtu.be/Y30BPBHftaE?si=E11qcCE9cMml3Wfw