Dr. Nchimbi kaniacha kinywa wazi

Dr. Nchimbi kaniacha kinywa wazi

Mwishoni kasema "mpaka utashi wa raisi. "

Hilo ni dongo kwa samia kwamba kwa sasa anaonekana ndie kizingiti
Mantiki ya kuwaza kuwa ni 'dongo kwa Samia' umeitoa wapi?

Kuna jambo Nchimbi anaweza kulifanya against samia?

Haujawahi sikia mtu na mkewe wanapanga njama za fumanizi kwa mbaya wao, yaani mke ashikishwe ugoni ili kumkomoa mbaya wao huku mahusiano yao yakiimarika?

Ndicho kinachofanyika hapa.

Picha la nje lionekana kuna masigano ndani ya kaya, kumbe ni mfarakano bandia wa kupangwa ili kufikia lengo flani, ni usanii kindaki ndaki huu!
 
Kama Rais na Mwenyekiti wa CCM, Dr. Samia anataka Katiba mpya, Makamu wa Rais anataka Katiba mpya, sasa ni nani anapinga Katiba mpya kiasi cha Makamu wa Rais Dr Nchimbi kuwataka wananchi wapambane kudai katiba mpya?.

Angalau sasa tunajua ni nani aliyechomekeza kwenye Ilani ya CCM agenda ya Kuandika katiba Mpya. Ambacho ameniacha mdomo wazi ni kuhusu:

1. Nani hataki katiba mpya pale CCM na serikalini kama Rais na Makamu wake wanataka Katiba mpya?
2. Kama mwenyekiti wa CCM anataka Katiba mpya nani pale CCM hataki Katiba Mpya?
3. Wananchi wapambane dhidi ya nani ili wapate Katiba mpya?
4. Wananchi wapambaneje ili kuwazidi nguvu hao wasiotaka katiba Mpya?
5. Tunataka Katiba mpya nzuri kama ya taifa gani Afrika ili tuone wao ni bora kiasi gani wapi kuliko sisi?
6. Je, ubaya wa Katiba hii ya 1977 ni nini?

Nionavyo mimi kama mimi, watu wetu, uchumi wetu, uelewa wetu, kiwango cha elimu cha watu wetu, mila na ustaraabu wetu kupanua kiwango cha demokrasia na haki za watu wetu kuliko hivi tulivyo sasa kutaenda kulitumbukiza taifa kwenye migogoro mingi itakayoidumaza Tanzania. Tunakwenda kutanua uchochoro ambao wakoloni watapitia kuichukua tena Tanzania.

Mwl. Nyerere alikataa kuruhusu wazungu kuchimba sana madini yetu kwakuwa alikuwa anawafahamu watu wake kuwa hawakuwa na utaalamu wa kuyachimba wala elimu ya kujadiliana kuhusu mikataba ya uchimbaji. Watu wetu hawa wengi wao bado hawana uelewa mpana kuhusu demokrasia na haki. Bado kuna maeneo watu wanaona ni haki kwa mwanamke kunyimwa kumiliki hiki na kile, bado mpaka leo kuna watu wanaamini viungo vya binadamu vinaleta utajiri kwa njia za giza. bado kuna watu asubuhi kabisa wanakunywa pombe na kucheza pool siku za kazi.

Sipingi kuandika katiba mpya lakini Makamu Rais Dr Nchimbi ndiye aliyeniogopesha zaidi.


View: https://youtu.be/Y30BPBHftaE?si=E11qcCE9cMml3Wfw

Chawa wahedi with zero credibility, usitupotezee muda please 👎
 
Mantiki ya kuwaza kuwa ni 'dongo kwa Samia' umeitoa wapi?

Kuna jambo Nchimbi anaweza kulifanya against samia?

Haujawahi sikia mtu na mkewe wanapanga njama za fumanizi kwa mbaya wao, yaani mke ashikishwe ugoni ili kumkomoa mbaya wao huku mahusiano yao yakiimarika?

Ndicho kinachofanyika hapa.

Picha la nje lionekana kuna masigano ndani ya kaya, kumbe ni mfarakano bandia wa kupangwa ili kufikia lengo flani, ni usanii kindaki ndaki huu!
SAbabu kubwa ni Urais 2030, kampeni zinaanza sasa.
 
Kama wote wanataka basi kakumbusha funga kinywa nzi wasijae ukashiba bureee
Anataka sisi tupambaneje na tupambane na nani? Angetupa orodha ya watu ambao hawapendi katiba mpya angeturahisishia kazi
 
Kama Rais na Mwenyekiti wa CCM, Dr. Samia anataka Katiba mpya, Makamu wa Rais anataka Katiba mpya, sasa ni nani anapinga Katiba mpya kiasi cha Makamu wa Rais Dr Nchimbi kuwataka wananchi wapambane kudai katiba mpya?.

Angalau sasa tunajua ni nani aliyechomekeza kwenye Ilani ya CCM agenda ya Kuandika katiba Mpya. Ambacho ameniacha mdomo wazi ni kuhusu:

1. Nani hataki katiba mpya pale CCM na serikalini kama Rais na Makamu wake wanataka Katiba mpya?
2. Kama mwenyekiti wa CCM anataka Katiba mpya nani pale CCM hataki Katiba Mpya?
3. Wananchi wapambane dhidi ya nani ili wapate Katiba mpya?
4. Wananchi wapambaneje ili kuwazidi nguvu hao wasiotaka katiba Mpya?
5. Tunataka Katiba mpya nzuri kama ya taifa gani Afrika ili tuone wao ni bora kiasi gani wapi kuliko sisi?
6. Je, ubaya wa Katiba hii ya 1977 ni nini?

Nionavyo mimi kama mimi, watu wetu, uchumi wetu, uelewa wetu, kiwango cha elimu cha watu wetu, mila na ustaraabu wetu kupanua kiwango cha demokrasia na haki za watu wetu kuliko hivi tulivyo sasa kutaenda kulitumbukiza taifa kwenye migogoro mingi itakayoidumaza Tanzania. Tunakwenda kutanua uchochoro ambao wakoloni watapitia kuichukua tena Tanzania.

Mwl. Nyerere alikataa kuruhusu wazungu kuchimba sana madini yetu kwakuwa alikuwa anawafahamu watu wake kuwa hawakuwa na utaalamu wa kuyachimba wala elimu ya kujadiliana kuhusu mikataba ya uchimbaji. Watu wetu hawa wengi wao bado hawana uelewa mpana kuhusu demokrasia na haki. Bado kuna maeneo watu wanaona ni haki kwa mwanamke kunyimwa kumiliki hiki na kile, bado mpaka leo kuna watu wanaamini viungo vya binadamu vinaleta utajiri kwa njia za giza. bado kuna watu asubuhi kabisa wanakunywa pombe na kucheza pool siku za kazi.

Sipingi kuandika katiba mpya lakini Makamu Rais Dr Nchimbi ndiye aliyeniogopesha zaidi.


View: https://youtu.be/Y30BPBHftaE?si=E11qcCE9cMml3Wfw

Kumbuka kabla ya kuwa Makamu wa Rais, alikuwa Balozi kisha Katibu Mkuu wa CCM. Kwa hiyo ni mtu mwenye taarifa nyingi nyeti ndani ya chama chake na serikali yake.

Anatambuwa misimamo binafsi ya wahafidhina waliopo ndani ya chama chake, na misimamo yao jinsi inavyokigharimu chama chake, serikali, na maslahi ya nchi kwa ujumla.

Kutofautiana maono na misimamo kwa viongozi ni jambo lenye afya. Lakini ndani ya utawala wa sasa wa CCM ni dhambi kubwa sana. Katika Ibada ya kipagani ya CCM, ni mwendo wa kusifu na kuabudu kinafiki tu.

"Constructive or critical thinking" haina tena nafasi ndani ya chama. Hata kama mfalme kakaa uchi mbele ya hadhara, hakuna mwenye uthubutu wa kumwambia juu ya aibu yake.
 
Kama Rais na Mwenyekiti wa CCM, Dr. Samia anataka Katiba mpya, Makamu wa Rais anataka Katiba mpya, sasa ni nani anapinga Katiba mpya kiasi cha Makamu wa Rais Dr Nchimbi kuwataka wananchi wapambane kudai katiba mpya?.
 
Upinzani kuna mazezeta ambayo muda wao wa kwenda Ikulu bado kabisa,
Hujajibu swali, hadi hizo points nilizokupa bado huoni uzezeta wako kusema katiba hii chakavu ina mapungufu mengi?
wacha wapate kwanza watu wenye akili. Nchi hii hakuna anaeshindwa kutoboa kwasabu ya Katiba.
CCM ndio kuna akili?

Polepole yupo wapi?

Mlishindwa nini kumjibu hoja zake mkaishia kumuua?
 
Kauli ya Dkt. Nchimbi ina uzito hasa ukiangalia mahali aliposema, kwenye Mkutano Mkuu wa Watetezi wa Haki za Binadamu, si jukwaa la chama.

Lakini baada ya kauli hiyo, baadhi ya watu wameanza kuuliza maswali mazito. Wanauliza:
01. Kama Rais anaitaka, kwa nini tuipambanie? "Yaani kuna vita baridi, wapo wanaoitaka na wasioitaka."
02. Tunapambana na nani ili tuipate? "Yaani adui ajulikane wazi, tusipigane vita ya gizani."
03. Kama Rais anaitaka, kwa nini asiseme yeye mwenyewe? "Yaani Rais aufikishe ujumbe huo kwa kauli yake mwenyewe, kwani kauli ya Rais ina uzito wa kutekelezwa moja kwa moja."

Maswali haya yanauma kisiasa, na yana mvuto wa kisiasa pia. Lakini ukweli ni kwamba yote yanabeba dhana moja iliyofichika, dhana kwamba tunasubiri ruhusa kutoka juu, na kwamba mtu fulani lazima aturuhusu kwanza ndipo tupate Katiba. Hapo ndipo mtego ulipo.

Katika msingi wa kikatiba, mamlaka ya kutunga Katiba ni ya wananchi wenyewe, siyo ya viongozi. Katiba haitoki kwa kupewa, inatoka kwa wananchi kuiunda. Kwa mantiki hiyo, swali sahihi si "adui ni nani," bali "sisi wananchi tumeshafanya nini kutumia mamlaka tuliyonayo." Ukiendelea kuwahoji viongozi nia zao, unabaki umesimama, unasubiri. Ukianza kushughulikia maudhui yenyewe, umeanza kutembea.
Ndiyo maana nasema hakuna haja ya kuendelea kuzunguka kwenye maswali hayo kama jibu tayari lipo mezani. Ipo rasimu kamili ya pendekezo la Katiba, ibara kwa ibara, inayojaribu kujibu tatizo la usimamizi wa madaraka kwa kuongeza muhimili wa nne, Baraza la Usimamizi wa Taifa, sambamba na Bunge, Mahakama na Serikali. Siyo kazi rasmi ya serikali, ni pendekezo la kujadiliwa na kupingwa.

Badala ya kuuliza nani anatuzuia, twende tukaone Katiba inaweza kuonekanaje kwa vitendo: www.katibampya.com. Isome, uihoji, uikosoe. Hapo ndipo mapambano ya kweli yalipo, kwenye maudhui, si kwenye maswali.

Angalizo: hoja hizi ni kwa lengo la kuelimisha, kuzua tafakari huru na kuibua mjadala wa muelekeo wa pamoja kama Taifa, si vinginevyo.
 
Kumbuka kabla ya kuwa Makamu wa Rais, alikuwa Balozi kisha Katibu Mkuu wa CCM. Kwa hiyo ni mtu mwenye taarifa nyingi nyeti ndani ya chama chake na serikali yake.

Anatambuwa misimamo binafsi ya wahafidhina waliopo ndani ya chama chake, na misimamo yao jinsi inavyokigharimu chama chake, serikali, na maslahi ya nchi kwa ujumla.

Kutofautiana maono na misimamo kwa viongozi ni jambo lenye afya. Lakini ndani ya utawala wa sasa wa CCM ni dhambi kubwa sana. Katika Ibada ya kipagani ya CCM, ni mwendo wa kusifu na kuabudu kinafiki tu.

"Constructive or critical thinking" haina tena nafasi ndani ya chama. Hata kama mfalme kakaa uchi mbele ya hadhara, hakuna mwenye uthubutu wa kumwambia juu ya aibu yake.
Mimi ni muumini wa mabadiliko lakini yale tunayoyaita planned change. Aina hii ya mabadiliko yanafanyika kwa kutumia takwimu (evidence based change) kutoka kwenye mazingira yanayokuzunguka yanayofanana na yako (benchmarking). Yaani unataka kufanya mabadiliko kwasababu gani yanayofanana kama ya nani mwenye mazingira kama ya kwangu?. Je, ninaetaka kumuiga ana hali nzuri kiasi gani kwenye nini iliyosababishwa na mabadiliko ninayotaka kuyafanya?

Sisi tuko Afrika ya chini ya jangwa la Sahara (third world). Shida kuu za nchi za chini ya jangwa la Sahara ni pamoja na:
1. Ukosefu wa technolojia za kuvunia rasilimali zetu ambazo tunazo nyingi tu.
2. Ukosefu wa fedha za kuendesha nchi zetu na kuzalisha zaidi.
3. Ukosefu wa masoko ya haki ya kuuza bidhaa zetu kwa bei nzuri na shindani. Bidhaa zetu zinategemea huruma na hisani zao kwenye masoko yao.
4. Bei kubwa za bidhaa zao kwenye masoko yao na masoko yetu pia. Yaani wao wako huru kuketa bidhaa zao kwetu lakini zenye bei kubwa mno.
5. Riba kubwa kwa mikopo tunayopewa kutoka mafuko ya dunia kama IMF na WB tunakopa sisi kuliko riba wanazotozwa nchi nyingine za ukanda mwingine kama wakikopa kwenye mifuko hiyohiyo.
6. Nguvu kazi yetu kuibiwa kwenda kwao kuwazalishia mali bila kutulipa sisi fidia yoyote. Vijana wetu tuliowalea na kuwasomesha kwa shida wanakimbilia Ulaya, Marekani na Asia kufanyakazi za uzalishaji na kulipa kodi huko bila sisi kupata fidia yoyote. Vijana wetu wengine wakifika wanawageuza kuwa vibaraka wao katika mataifa yetu, hasa wale wenye akili nyingi.

Sasa unapotaka kufanya mabadiliko yoyote makubwa kwenye Katiba, Sheria au sera lazima ujiulize mabadiliko hayo yatajibu maswali ya changamoto hizo 6 hapo juu au ndiyo yataongeza changamoto nyingine ya 7 na 8?

Je, unafanya mabadiliko kwakuwa wengine wamefanya au unataka kuboresha jambo la msingi kabisa?. Mfano, Kenya wanayo Katiba Mpya lakini sioni cha maana kutuzidi sisi, je tuwaige wao kwakuwa wamefanya?

Tujiulize ni mambo gani ya msingi ya kubadilisha kwenye Katiba yetu kama tunataka kubadilisha. Mfano, mimi naona kama tukiweka kifungu cha kuwapa adhabu kali viongizi na watumishi wa umma wezi tutakuwa tumepiga hatua sana kwa kuacha mambo mengine yabaki kama yalivyo.
 
Kama Rais na Mwenyekiti wa CCM, Dr. Samia anataka Katiba mpya, Makamu wa Rais anataka Katiba mpya, sasa ni nani anapinga Katiba mpya kiasi cha Makamu wa Rais Dr Nchimbi kuwataka wananchi wapambane kudai katiba mpya?.

Angalau sasa tunajua ni nani aliyechomekeza kwenye Ilani ya CCM agenda ya Kuandika katiba Mpya. Ambacho ameniacha mdomo wazi ni kuhusu:

1. Nani hataki katiba mpya pale CCM na serikalini kama Rais na Makamu wake wanataka Katiba mpya?
2. Kama mwenyekiti wa CCM anataka Katiba mpya nani pale CCM hataki Katiba Mpya?
3. Wananchi wapambane dhidi ya nani ili wapate Katiba mpya?
4. Wananchi wapambaneje ili kuwazidi nguvu hao wasiotaka katiba Mpya?
5. Tunataka Katiba mpya nzuri kama ya taifa gani Afrika ili tuone wao ni bora kiasi gani wapi kuliko sisi?
6. Je, ubaya wa Katiba hii ya 1977 ni nini?

Nionavyo mimi kama mimi, watu wetu, uchumi wetu, uelewa wetu, kiwango cha elimu cha watu wetu, mila na ustaraabu wetu kupanua kiwango cha demokrasia na haki za watu wetu kuliko hivi tulivyo sasa kutaenda kulitumbukiza taifa kwenye migogoro mingi itakayoidumaza Tanzania. Tunakwenda kutanua uchochoro ambao wakoloni watapitia kuichukua tena Tanzania.

Mwl. Nyerere alikataa kuruhusu wazungu kuchimba sana madini yetu kwakuwa alikuwa anawafahamu watu wake kuwa hawakuwa na utaalamu wa kuyachimba wala elimu ya kujadiliana kuhusu mikataba ya uchimbaji. Watu wetu hawa wengi wao bado hawana uelewa mpana kuhusu demokrasia na haki. Bado kuna maeneo watu wanaona ni haki kwa mwanamke kunyimwa kumiliki hiki na kile, bado mpaka leo kuna watu wanaamini viungo vya binadamu vinaleta utajiri kwa njia za giza. bado kuna watu asubuhi kabisa wanakunywa pombe na kucheza pool siku za kazi.

Sipingi kuandika katiba mpya lakini Makamu Rais Dr Nchimbi ndiye aliyeniogopesha zaidi.


View: https://youtu.be/Y30BPBHftaE?si=E11qcCE9cMml3Wfw

Sikia, acha janjajanja. Tunataka Katiba Mpya na sote tunamjua anayeikwepa!!

Na tunajua ni kwanini anaikwepa Sasa!!

Uhuru na RASILIMALI za nchi zinatakiwa kulindwa na Katiba!! Uhuru haupo na Rasilimali za Taifa kapewa Mwarabu!!

Kipande Cha nchi kimetumbukia Mikononi mwa Wageni, leo Ngorongoro siyo yetu tena!!

Usijitoe akili kwa Kutuletea Hekaya za Alinacha!! Unamjua sana anayeikataa Katiba!!

Nchimbi ni Namba mbili kwa Mamlaka hapa Tanzania!! Sasa hata kwa akili tu za kuvunia viazi unaweza kujua tatizo lipo!!

Au unataka mpaka Elon Musk ndo aje akufungue akili?
 
Kama anasema mawaziri na kila mtu akiwemo yeye mawazo yao kwenye vikao ni ushuri tu kwa Rais maana yake kikwazo cha Katiba ni Rais Samia. Hata kupambana anakoagiza watu wapambane ni dhidi ya Rais mfanya maamuzi mkuu. Walimchomekea agenda ya Katiba kwenye Ilani.

Kama sio uwepo wa Katiba hii serikali hii ingeshapinduliwa siku nyingi zilizopita na hata yeye asingekuwa Rais wa nchi hii. Ndio maana marais wote walikwepa swala la Katiba. Mzee wa Msoga karibu yamtokee puani alipojaribu kuigusa.

Kama mimi ningekuwq mshauri wake ningemshauri aachane nayo yeye kama Rais mwanamke wa kwanza nchini.
Sikuwai kufikiria jamaa una mawazo ya kiwango cha chini kiasi hiki.
Kweli ukitaka kujua uwezo wa akili ya mtu acha aongee.
 
Kichwa chake kimekaa upande kama koti lake.
Ana akili nyingi sana huyu mzee. Huwezi kumlinganisha na huyu ambae haeleweki majukwaani. Unaposema endelea kupambana mpate Katiba maana yake unasema chomeni tena nchi hadi mpate katiba. Kuna haja ya kuongeza bajeti ya kuongeza manunuzi ya risasi kukabiliana na ongezeko la watakaochoma tena.
 
Sikia, acha janjajanja. Tunataka Katiba Mpya na sote tunamjua anayeikwepa!!

Na tunajua ni kwanini anaikwepa Sasa!!

Uhuru na RASILIMALI za nchi zinatakiwa kulindwa na Katiba!! Uhuru haupo na Rasilimali za Taifa kapewa Mwarabu!!

Kipande Cha nchi kimetumbukia Mikononi mwa Wageni, leo Ngorongoro siyo yetu tena!!

Usijitoe akili kwa Kutuletea Hekaya za Alinacha!! Unamjua sana anayeikataa Katiba!!

Nchimbi ni Namba mbili kwa Mamlaka hapa Tanzania!! Sasa hata kwa akili tu za kuvunia viazi unaweza kujua tatizo lipo!!

Au unataka mpaka Elon Musk ndo aje akufungue akili?
ACheni janjajanja, hii Katiba ilikuwepo tabgu mwaka 1977 na Samia kaja mwakwa 2022. Tunaijua hiyo. Wacha tuongeze bajeti ya risasi kupambana na wakora kama nyie. Jitoeni ufahamu mkachome tena. Kwanza tunajua kuwa hamkutaka awe Rais tangu mwanzo, hizi nyingine ni ngonjela tu.
 
Sikuwai kufikiria jamaa una mawazo ya kiwango cha chini kiasi hiki.
Kweli ukitaka kujua uwezo wa akili ya mtu acha aongee.
Huna akili ya kunizidi mm wewe, hata kwa robo tu, unaendeshwa na mkumbo, mm sina upande wowote naongea facts tu kwakutumia uelewa wangu na uzoefu wangu tu baaasi.
 
Kama Rais na Mwenyekiti wa CCM, Dr. Samia anataka Katiba mpya, Makamu wa Rais anataka Katiba mpya, sasa ni nani anapinga Katiba mpya kiasi cha Makamu wa Rais Dr Nchimbi kuwataka wananchi wapambane kudai katiba mpya?.

Angalau sasa tunajua ni nani aliyechomekeza kwenye Ilani ya CCM agenda ya Kuandika katiba Mpya. Ambacho ameniacha mdomo wazi ni kuhusu:

1. Nani hataki katiba mpya pale CCM na serikalini kama Rais na Makamu wake wanataka Katiba mpya?
2. Kama mwenyekiti wa CCM anataka Katiba mpya nani pale CCM hataki Katiba Mpya?
3. Wananchi wapambane dhidi ya nani ili wapate Katiba mpya?
4. Wananchi wapambaneje ili kuwazidi nguvu hao wasiotaka katiba Mpya?
5. Tunataka Katiba mpya nzuri kama ya taifa gani Afrika ili tuone wao ni bora kiasi gani wapi kuliko sisi?
6. Je, ubaya wa Katiba hii ya 1977 ni nini?

Nionavyo mimi kama mimi, watu wetu, uchumi wetu, uelewa wetu, kiwango cha elimu cha watu wetu, mila na ustaraabu wetu kupanua kiwango cha demokrasia na haki za watu wetu kuliko hivi tulivyo sasa kutaenda kulitumbukiza taifa kwenye migogoro mingi itakayoidumaza Tanzania. Tunakwenda kutanua uchochoro ambao wakoloni watapitia kuichukua tena Tanzania.

Mwl. Nyerere alikataa kuruhusu wazungu kuchimba sana madini yetu kwakuwa alikuwa anawafahamu watu wake kuwa hawakuwa na utaalamu wa kuyachimba wala elimu ya kujadiliana kuhusu mikataba ya uchimbaji. Watu wetu hawa wengi wao bado hawana uelewa mpana kuhusu demokrasia na haki. Bado kuna maeneo watu wanaona ni haki kwa mwanamke kunyimwa kumiliki hiki na kile, bado mpaka leo kuna watu wanaamini viungo vya binadamu vinaleta utajiri kwa njia za giza. bado kuna watu asubuhi kabisa wanakunywa pombe na kucheza pool siku za kazi.

Sipingi kuandika katiba mpya lakini Makamu Rais Dr Nchimbi ndiye aliyeniogopesha zaidi.


View: https://youtu.be/Y30BPBHftaE?si=E11qcCE9cMml3Wfw

Tunaongozwa na vichaa!
 
Back
Top Bottom