Dr. Mwakyembe arejea Bungeni

Karibu sana Dr.Mwakyembe bungeni,usiwe na wasiwasi unae Yesu anakulinda,mafisadi walie tu.
 
Welcome back mkuu na bwana akutangulie katika kazi zako.
Kwa maana mtetezi wako yu hai....aluta continuaaaaa.
Mafisadi mle tuu labda mcollaborate na shetani tena kumuangamiza mtetezi wa haki za wanyonge.
 
Na waulizeni waliopo Dodoma wathibitishe, anaendesha Lexus! Huku watu wa Kyela, wanahangaika na maisha yao! Ametoka kuchekiwa afya yake Ujerumani!

Bwassa
 
wacheni na wenzetu waswahili wayaendeshe hayo ma-Lexus! Tumeshazowea kuona ni halali wageni tu wayaendeshe sababu nini??
 
Mhe.mwakyembe amerejea toka jana anaendelea vizuri na leo asubuhi amechangia kwenye bajeti ya wizara ya kilimo na kimsingi amemshukuru sana mungu kumuepusha na ajali ile mbaya sana pia kwa wananchi wote kwa maombezi yao truly mungu anawaona watu wema na watadumu kupambania rasilimali za wanyonge wa tanzania.
 
Jamaa zangu,nilipotea kidogo kwani nilikuwa kwenye msiba wa ndugu yetu ambaye polisi wamemwua bila sababu zozote hapa Kyela.

Nchi hii inataka mabadiliko ya kweli, sio hawa wasanii ambao wanashindwa kututetea sisi wanyonge.

Vijana tuliomba kukutana na RC, akakataa; tukaomba kukutana na DC naye kakataa; hata mbunge naye hakuna hata salaam.

Leo nimepigiwa sana simu kwamba eti kuna kampeni Kyela. Achaneni na hao watu wa propaganda wa Dr. Wanatumia kila njia kuonyesha huyo kijana wa UK kaingia Kyela na anapiga kampeni wakati hata Kyela hayupo.

Huyo jamaa hayuko hapa ila tumeambiwa kaingia TZ na anategemea kuja Kyela karibuni. Tunamkaribisha kwa mikono miwili maana ni mzalendo mwenzetu anayejali maslahi ya vijana wa Kyela.

Tunaendelea kufuatilia haki za mwenzetu aliyeuawa.
 
Na waulizeni waliopo Dodoma wathibitishe, anaendesha Lexus! Huku watu wa Kyela, wanahangaika na maisha yao! Ametoka kuchekiwa afya yake Ujerumani!

Bwassa

Nonsense! Kuna Mbunge anaendesha Bajaj au baiskeli? Na ulitaka akachekiwe Mlingotini wakati viongozi wote wanarushwa nje? By the way, Lowassa karudi jana toka Ujerumani kuchekiwa afya yake. Mbona huongelei maishan ya Wamasai wanaohangaika na maisha? Lets be fair!JM
 
Nonsense! Kuna Mbunge anaendesha Bajaj au baiskeli? Na ulitaka akachekiwe Mlingotini wakati viongozi wote wanarushwa nje? By the way, Lowassa karudi jana toka Ujerumani kuchekiwa afya yake. Mbona huongelei maishan ya Wamasai wanaohangaika na maisha? Lets be fair!JM


JM uko kazini ? Kuna mtu kakutonya juu ya habari hii ya Mwakyembe umeamua kumpandia huku huku ?
 
Re: Hivi Dk. Mwakyembe yuko Bungeni?

Nakubaliana na Engineer. Watu wanalishwa pumba nyingi na hawajui ukweli wa mambo ulivyo. Wananchi wa Kyela wana taabu kubwa katika maendeleo yao wakati Mbunge wao akihangaika na mambo yake binafsi na kutaka Uwaziri, ambao kwa kufanya hivyo anawakandia wenzake Nani alijua kuwa ana hisa nyingi, tena ni za thamani ya zaidi ya Tsh. Bilioni moja na nusu, zaidi ya vijisenti vya chenge, katika mradi wa "umeme wa upepo'?. Hata Bungeni alikataa kusema mpaka ilipobainika hadharani na yeye kukiri kibaguzi kuwa ni "mradi wa watu weusi"? Mwanzo hakusema, baadaye mambo yalipowekwa hadharani akakiri! Alishindwa hata kutangaza "interest" alipokuwa akijadili umeme Bungeni! Hayo mnayozungumza ya ushujaa wake, siyo lugha wanayozungumza Kyela! Engineer mwaga data zaidi kwa kuwa unajua hali halisi! Wanaoishi Marekani na kupata habari za udaku, wajirekebishe!

Bwassa


Ndugu yangu Bwassa, tuulize tunaoishi na kufanyakazi Kyela ambao tutampigia tena kura Mwakyembe! Huyo anayejiita Engineer ni mmoja wa hao wababaishaji wanaolipwa na Lowassa kwa kumchafua mbunge wetu!

Mambo ya "ubilionea" wa Mwakyembe hayo mnayajua nyie mabilionea wenzake, lakini sisi hapa Kyela tunajua kuwa hakuna Mbunge aliyewahi kufanya mambo mengi makubwa wilayani hapa toka uhuru kama Mwakyembe. Nitataja machache: Amepokea kiti cha ubunge tukiwa na shule 7 za sekondari, sasa tunazo 24; hii lami kidogo katikati ya mji, kaileta Mwakyembe; mradi wa umeme kutoka Ipinda hadi Ntaba, Ipinda hadi Matema Beach, ni miradi ambayo Mwakyembe kaipigania sana na inatekelezwa; katujengea madaraja mapya makubwa mawili (Lusungo na Matema), madogodogo na suspension bridges zaidi ya 10; ameanzisha KDF ambayo imechangia ujenzi wa shule zote Kyela; alimwomba Kikwete ajengewe barabara ya lami kutoka Kikusya hadi Matema (38km), mchakato umeanza na Serikali kuu tayari imetumia zaidi ya sh. milioni 600 kuiboresha; amehamasisha wawekezaji wakubwa na sasa Kyela itakuwa na kiwanda kikubwa cha mpunga Kikusya; barabara mpya tatu kata za Matema na Makwale zimeanzishwa na kujengwa chini ya uongozi wake; ameanzisha vikundi vidogodogo vya ushirika (VICOBA) ambavyo vimeenea sehemu mbalimbali Kyela; na above all ameipa Kyela jina kubwa ambalo halikusikika huko nyuma. Hayo mengine anayoyasema huyo sijui Engineer kweli au Engineer wa maneno, sisi hatuyajui!
 
JM uko kazini ? Kuna mtu kakutonya juu ya habari hii ya Mwakyembe umeamua kumpandia huku huku ?

Mkuu, kimsingi mimi ni msomaji tu na msomaji mzuri wa majadiliano ndani ya JF. Nachangia pale tu ninapoona ukweli unapotoshwa kihunihuni tu. JM
 
Hivi hapa anaye ongelewa kuwa mpinzani wa Mwakyembe ni George Mwakaling Ambwene ambaye ni mwanachama wa JF tangia ina anza ?Au mie sijaelewa jamani mbona kuna mengi yamenipita ?
 
Tumehabarishwa yuko Arusha kukutana na Mh Edward Lowasa!


Duh amewachenga?nasikia nyie mkakurupuka kwenda Kyela yeye akaensda Arusha.Nimeambiwa mlikuwa mnamtafuta kyela ,kweli Kijana wa london kiboko,amewapiga chenga
 
Duh, Mkuu Masanilo ya kweli hayo ?!



=Maxence Melo;https://www.jamiiforums.com/members/maxence-melo.html527841]Nimefanikiwa kuongea na Mwakalinga ambaye yupo Tanzania kwa mapumziko na ameshtuka kusikia haya, kwa kifupi anasema SI KWELI na yeye yupo Tanzania kwa ajili ya mapumziko na familia yake.

Anasema ni maneno ya kutungwa yasiyo na ukweli wowote na anashauri hoja ifungwe kwakuwa kathibitisha kwa kauli yake kuwa hana mpango wa kugombea Kyela.

Kwa sasa yupo Arusha.


Haya Mkuu Maxence huwa ni mkweli habari zake!
 
Ndugu yangu Bwassa, tuulize tunaoishi na kufanyakazi Kyela ambao tutampigia tena kura Mwakyembe! Huyo anayejiita Engineer ni mmoja wa hao wababaishaji wanaolipwa na Lowassa kwa kumchafua mbunge wetu!

Mambo ya "ubilionea" wa Mwakyembe hayo mnayajua nyie mabilionea wenzake, lakini sisi hapa Kyela tunajua kuwa hakuna Mbunge aliyewahi kufanya mambo mengi makubwa wilayani hapa toka uhuru kama Mwakyembe. Nitataja machache: Amepokea kiti cha ubunge tukiwa na shule 7 za sekondari, sasa tunazo 24; hii lami kidogo katikati ya mji, kaileta Mwakyembe; mradi wa umeme kutoka Ipinda hadi Ntaba, Ipinda hadi Matema Beach, ni miradi ambayo Mwakyembe kaipigania sana na inatekelezwa; katujengea madaraja mapya makubwa mawili (Lusungo na Matema), madogodogo na suspension bridges zaidi ya 10; ameanzisha KDF ambayo imechangia ujenzi wa shule zote Kyela; alimwomba Kikwete ajengewe barabara ya lami kutoka Kikusya hadi Matema (38km), mchakato umeanza na Serikali kuu tayari imetumia zaidi ya sh. milioni 600 kuiboresha; amehamasisha wawekezaji wakubwa na sasa Kyela itakuwa na kiwanda kikubwa cha mpunga Kikusya; barabara mpya tatu kata za Matema na Makwale zimeanzishwa na kujengwa chini ya uongozi wake; ameanzisha vikundi vidogodogo vya ushirika (VICOBA) ambavyo vimeenea sehemu mbalimbali Kyela; na above all ameipa Kyela jina kubwa ambalo halikusikika huko nyuma. Hayo mengine anayoyasema huyo sijui Engineer kweli au Engineer wa maneno, sisi hatuyajui!


Hii mijitu ya Nsesi imeuza mpunga sasa imeanza kusumbua mjini hapa.. shule 24 bila Walimu ndo sifa?Si bora zingekuwa 10 lakini zina ubora.Shule tu ndo mnakubaliana na Lowassa?shule gani hizo div.1v na 0,katibu kata mwenyewe hapeleki mtoto wake...
 
Duh amewachenga?nasikia nyie mkakurupuka kwenda Kyela yeye akaensda Arusha.Nimeambiwa mlikuwa mnamtafuta kyela ,kweli Kijana wa london kiboko,amewapiga chenga

Kyela wamekwisha kwelikweli. Kumbe kelele zote hizi za kumsulubu Mwakyembe, mtu aliyewanyua juu kwenye chati ni fedha za Lowassa na Rostam! Duh ama kweli EPA na RICHMOND ni kiboko! Hata hivyo huyu mgombea wa Kyela kutoka London, asiwaumbue BANYAMBALA wa Kyela kwa kumfuatafuata Lowassa mpaka nyumbani kwake. Hajasikia yaliyomkuta yule Mbunge wa Kigoma, nanihii.... nanihii ......?
 
Back
Top Bottom