Kuna mtu anaijiita engineer (wa fitna) bado hajaiona hii post!!!!
Endeleeni kumdanganya huyo jamaa yenu kwa mapambio ambayo hayamwongezei hata kura moja. Kama mnampenda nawashauri muje huku Kyela mumsaidie kabla boat haijazama.
Jamaa yupo Dar na wana vikao vingi vya siri hapa Kyela. Tatizo la Kyela ni mji mdogo na umejaa majungu. Hata ukutane na mtu mmoja, kesho hiyo habari inakuwa nje.
Bado wanapanga namna ya kufanya maandamano ya kushinda mafisadi kwa ajali ya gari. Kinachowaogopesha hakuna tena watu wengi wa kumshangilia kwenye maandamano.
Watch this space! na Kyela tutawashangaza sana watu wa Dar.
Bahati mbaya watu wengi hawamjui huyu Dk. Mwakyembe. Huyi ni bingwa wa fitina na uzushi! Alimfitini Mzee Mwakipesile mpaka akamshinda ubunge wa Kyela. Mzee Mwakipesile alivyoteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa, Dk. huyo akaendelea na fitina mpaka chama chao cha CCM kikaingilia kati na kikagundua uzushi mkubwa alioufanya Dk. Mwakyembe dhidi ya Mzee Mwakipesile! Rekodi zipo CCM kwa anayetaka uthibitisho zaidi. Kwa Lowassa, nani asiyejua fitina za Dk. Mwakyembe zilizoungwa mkono na Spika Sitta ambaye naye walikuwa hawaivi na Lowassa. Mwakyembe, kwa kushirikiana na Sitta, waliukataa kata kata na kuutupilia mbali hata ushahidi wa wazi maandishi wa Lowassa unaodhihirisha, pasi na shaka yoyote, hayumo Richmond! Mwakyembe alikataa hata kumhoji Lowassa!Mwakyembe mwenyewe ameshindwa, mpaka leo, kutangaza kuwa alikuwa na maslahi binafsi katika kuikandia Richmond, IPTL, Dowans n.k. kutokana na mipango yake ya kampuni ya kufua umeme kwa upepo, ambayo alikuwa anaifagilia njia ili, wakati ukiwadia, ipate kandarasi nono Tanesco! Kwenye hili la kushindwa kutangaza maslahi, Sitta anamsaidia Mwakyembe. Rekodi ziko bungeni, kwenye taarifa rasmi za Bunge, Hansard! Alijaribu kuzusha hata kuwa ajali yake ya gari hivi karibuni, ilipangwa, kinyume na ushahidi wa watalamu uliomwona dereva wake ndiye mkosaji,kwa kwenda kasi bila ya uangalifu! Rekodi ziko Polisi! Siyo mgonjwa, kwani wataalamu bingwa Muhimbili walithibitisha kuwa hakuumia sana. Rekodi ziko Muhimbili, MOI, alikolazwa! Leo mnauliza yuko wapi "shujaa" wetu? Haonekani kwa sababu: (1) anashughulikia mipango yake ya Kampuni ya umeme na miradi yake mingine ya kibinafsi; (2) anasutwa na kutishwa na kivuli chake mwenyewe na anakikimbia na hata Bungeni anapaona pachungu (3) Hajafanya lolote jimboni Kyela, zaidi ya yale aliyoyaacha Mzee Mwakipesile, na saa ya uchaguzi imefika! Watanzania lazima tuwe wakweli, hizi siasa za chuki, fitina, kuoneana gele ambazo Dk. Mwakyembe ni championi wake, hazitufikishi popote! Wapigaji kelele Bungeni, wanaojifanya "wanamgambo" wa Ufisadi wengi tunawafahamu: walikosa Uwaziri au Unaibu Waziri! Wanawaonea gele wenzao na ndiyo maana majimboni kwao hoi! Walitaka ubunge siyo kuwasaidia wananchi wao, bali kujisaidia wao wenyewe kwa vyeo! Wanaifanya hata Serikali yao isuesue na kupoteza muda kutekeleza Ilani ya Uchaguzi!
Bwassa.
Endeleeni kumdanganya huyo jamaa yenu kwa mapambio ambayo hayamwongezei hata kura moja. Kama mnampenda nawashauri muje huku Kyela mumsaidie kabla boat haijazama.
Jamaa yupo Dar na wana vikao vingi vya siri hapa Kyela. Tatizo la Kyela ni mji mdogo na umejaa majungu. Hata ukutane na mtu mmoja, kesho hiyo habari inakuwa nje.
Bado wanapanga namna ya kufanya maandamano ya kushinda mafisadi kwa ajali ya gari. Kinachowaogopesha hakuna tena watu wengi wa kumshangilia kwenye maandamano.
Watch this space! na Kyela tutawashangaza sana watu wa Dar.
Kwanza karibu jamvini maana naona ni post yako ya kwanza hii. inaelekea wewe ni member wa mtandao na pro fisadis au wewe mwenyewe ni miongoni mwa waliotuhumiwa katika uchunguzi wa tume ya Mwakyembe. Jaribu kumtendea haki Dr. Mwakyembe. inanipa taabu sana kufikiri kuwa huoni ufisadi unaohusishwa na Richmond, IPTL, Dowans! Loo kweli kuna kazi kama watu wenyewe ndiyo wa aina hii!
anaipendaaa sanaaa......Tunakuombea kila kheri Mheshimiwa (sina hakika km unaipenda sana hiyo prefix), naamini hujaenda kusaini mahuduhurio!