Mwalimu Kitila
Pole yaliyokukuta, ila naamini ulichelewa sana kutambua hilo. Kwa kweli kama umelitambua leo ama baada ya kukubwa na dhahama basi, siku nyingine ningekushauri utafute njia mbadala ambayo itakupa uwezo wa kuyabaini na kuyafanyia projection jinsi mambo yatakavyokua baadae. Kule kwetu, wavuvi kabla ya kuingia ktk mitumbwi na mashua yao hutimua kajivumbi fulani na kuweza kubashiri kwa hakika kabisa kwamba mda fulani upepo utakua wa kasi gani na utakuwa unavuma kutoka upande fulani kuelekea upande fulani, sasa swali kwanini tusijifunze busara za wavuvi hawa?. Lakini, bado nina uwalakini ya kwamba je ni kweli hasa tatizo umelibaini?
Mie naamini ni kweli tunahitaji mbadala wa CCM na CHADEMA, lakini huo mbadala huo unaongelea unatakiwa uwa na attributes za namna zipi? Je ni mbadala wa kubadili jina la chama, ama mbadala wa kuandika katiba ktk makatasi ya chama kipya? Mbadala wa namna hii mie kwa muono wangu sio mwarabani.
Huko nyuma, niliwahi kukubishia kwamba tatizo lilopo sio CCM na wala mwarobaini wake sio CHADEMA, kwa namna fulani uliniita "MNAFIKI", nilikaa kimya nikasema mwalimu mzuri ni kumpa mda, mwalimu Kitila.
Mwalimu Kitila, kosa wapinzani wanalofanya na wewe naona unaelekea kulifanya ni lilelile la kuaminisha watu kwamba tatizo la Tanzania ni kwa sababu ya entity ambayo hai-exists kama vile:CHADEMA, CCM,CUF nk.
Mwl Kitila, ngoja nirudie tena kujaribu kurudia muono wangu, wenda leo kwa vile upo huru kama mie hapa, unaweza japo kuangalia huu muono ktk jicho tofauti. Na nasem kuwa tatizo la Tanzania linasababishwa na linaendelezwa na ile existing entity, hii existsing entity ni watanzania wenyewe . Tatizo lilomo na linasobabisha matatizo ktk Tanzania ni watazania wenyewe na tatizo sugu ilikiwa limejikita ktk ile dhana ya mindset ya mtanzania.
Mwl Kitila, unaweza tengeneza chama kipya mbadala chenye jina zuri na katiba ktk makaratasi nzuri sana na hiyo katiba ikawa nzuri sana kupita zote duniani, lakini kama wanachama na viongozi wake watakuwa ndo sisi hawa watanzania hawa hawa kwa mindset hii iliyopo hii hii, basi tegemea maumivu tu. Kwani nini kitachowafanya wasisahau kuchapa baadhi ya vipengele kwenye katiba yako nzuri?
Ngonja, niishie hapa kwa kuvipumzisha vidole, lakini nachelea kuamini kwamba wenda chanzo cha tatizo haswa hujapata kukiona, ila nafurahi kuwa umelishuhudia kwa maandiko yako ya kwamba vyama hivi vilivyopo na wanachama wake hawa hawana msaada wowote kwa mtanzania mnyongeu. Hivyo, ukombozi wa kweli bado sana kuwaidia. Maana, hata CCM kesho wakianguka sioni tofauti ya mpokea kijiti atachofanya cha ziada.