Head teacher
JF-Expert Member
- Mar 10, 2012
- 1,796
- 413
Mwenye akili na aelewe.....Hongera Dr. You are a great thinker indeed!!
Nashawishika kusema huyu ni dr wa madesa, ndo amesema nini hapa.I am sorry...
Mwenye akili na aelewe.....Hongera Dr. You are a great thinker indeed!!
kitila mkumbo!!!, mtu ambaye nilikuheshimu na kukuamini sana, umenishangaza na ninakuomba uache kupotosha umma!!
Ninajiuliza, wewe si ni dr, kwa maana una phd!!!??, inakuwaje unarubuniwa kirahisi na mtu kama zitto!?
Dr. Kitila, ninaomba uuambie umma, hivi kuwarubuni wadiwani wa chadema arusha na kuwafanya wagomee maamuzi halali ya chama hatimae wakafukuzwa na mahakamani wakashindwa kesi, ndio njia halali za kutaka uongozi ndani ya chama?
Hivi kutembea majukwaani ukitukana chama na viongozi wakuu wa chama ndio demokrasia?
Swahiba wako uliekuwa unampigania bwana zitto, alikuambia kuwa kuhujumu chama kwa kuengua wagombea wa chama chake ili ccm ipite bila kupingwa ndio demokrasia muliokuwa mukiihitaji ndani ya chadema?
Kwenda kinyume na maazimio ya kambi rasmi ya upinzani kama vile;
1)kususia hotuba ya kikwete,
2)kutoshiriki na wenzie kwenye tukio la bomu mkutano wa chadema arusha,
3)kutotimiza majukumu ya naibu katibu mkuu na kutofika makuu makuu ya chama kwa zaidi ya mwaka, ndio unachohalalisha kuwa ni mbinu za ushindi?
Kitila, watanzania sio wajinga, ni bora tu ukakaa kimya kuliko kuendelea kujivunjia hiyo heshima kidogo uliyobakiza.
Nashawishika kusema huyu ni dr wa madesa, ndo amesema nini hapa.I am sorry...
we mjinga soma kwanza makala yote ndio ucomment!! Nyie ndo wale wale mnaoifanya cdm kionekane ni chama cha vilaza
Kwa mashabiki wa viongozi au niwaite vibaraka hiyo makala hawawezi kuielewa hata kidogo, wamejaa Upofu. Ila kwa mashabiki wa CHAMA imetukuna hasa. Na mimi niongeze hapo juu, hauhitaji ushabiki wa chama tu ili kuielewa makala kama hiyo hapo juu, unahitaji pia ushabiki wa NCHI YAKO. Cdm mmewa dissapoint watu wengi sana kwa hicho kinachoendelea kwenu. Mwenye macho haambiwi tazama
Tatizo mwenzangu hapa umeegemea kwenye facts ambazo hutaki kuziacha! nimeishakwambia kuwa siasa ni dynamic! Leo unaweza shirikiana na shetan kesho ukashirikiana na malaika! Hata Zitto mwenyewe unayemtolea mfano before aliwahi kushirikiana na hao wahafidhina katika kumuangamiza kisiasa Chacha Wangwe but leo Zitto hayupo pamoja nao!
JE UNAFAHAMU KWAMBA KITILA NA WENZAKE WALILIPWA ILI KUUPINDUA UONGOZI wa cdm ? NA KWAMBA WARAKA WA MABADILIKO UMEJAA MATUSI KWA VIONGOZI WAKUU WA CHAMA ? UNAFIKIRI NI KWANINI WANAUNGWA MKONO SANA NA CHAMA CHAKAVU CCM ? TAFAKARI KABLA YA KUAMUA KUWAUNGA MKONO !
Tumeikataa CCM kwasababu inakumbatia makosa kwa kuogopa watu eti watayumbisha nchi. Lazima tujifunze kutoa adhabu na kupokea adhabu lazima tuanze na ZZK ili kutengeneza std zinazokubalika. NCCR haikuwa taasisi ilikuwa ni viongozi wenye uchu mkubwa sana wa madaraka na fedha, usalama wa taifa nk. Mazingira yamebadilika sana hatuwezi kuacha kuadhibiana kwa kuogopa kivuli cha NCCR. Dr ingebidi kwanza useme wazi je kwenye sakata lenu kwa vyovyote vile mlivunja katiba ya chama na kama mlivunja adhabu yake ilikuwa nini kwa mujibu wa katiba?
Lazima tuzifuate sheria zetu tulizokubaliana nazo. Sioni upofu wa wanachama ila naona tamaa ya tuliowaamini.
Hivi kwa nini you people mnapenda kumezeshwa maneno na nyinyi mnayapokea mazima mazima!? mnashindwa hata kuhoji ndani ya nafsi zenu kimya kimya? Kinachotokea cdm ni makosa ya pande zote mbili, Zitto na Mbowe wote wanamakosa na inabidi wajichunguze upya waangalie walipoangukia! Kila binadamu ana haki ya kukosea na kujirekebisha
Nakushauri nawe uwapime viongozi wako wapo salama?
Mkumbo usidanganyike,Zitto akifukuzwa uanachama Chadema haitayumba hata kama wafuasi wa Zitto wataondoka.Biblia inasema "Nitampiga mchungaji kondoo watatawanyika" Zitto siyo mchungaji wa Chadema.NCCR ilitawanyika kwa sababu alipigwa mchungaji.Ni makosa makubwa kumlinganisha mrema na Zitto kwa sababu nafasi zao katika vyama vyao zilitofautiana sana.Kama mikakati yenu ilikuwa sahihi,kwa nini ilikuwa ya siri sana huku mkiwachafua viongozi? Zitto alipewa hela kudhoofisha Chadema na hilo liko wazi.Msidanganye watu.Inashangaza msomi kama wewe unajiunga kwenye kundi la wasaliti.Elimu yako inakusaidia nini? Mbona kina Juliana Shonza,Kafulila,Mtela Mwampamba,Mchange na wengineo walioasisiwa na Zitto hukuwatetea walipofukuzwa Chadema? Mbona siku ile mlipoandaa press conference na Zitto mlipovuliwa uongozi,akina Mwampamba,Mchange ndiyo waliandaa sehemu yenu ya mkutano hukusema chochote ilihali ukijua ni wanachama wa ccm?
...Unamjua vizuri Kitila Mkumbo ww au umemfahamia CDM???