Dr.Kitila Mkumbo: Tunahitaji mbadala wa CCM na CHADEMA

Dr.Kitila Mkumbo: Tunahitaji mbadala wa CCM na CHADEMA

Hawa ndo wasomi wetu,anajaribu kuhalalisha uovu. Halafu nazidi kupata shida zaidi juu ya uwezo wa kufikiri wa huyu dr.kitila. Hapa ametoa mfano wa nccr-mageuzi na kafulila,eti wamemaliza kimyakimya wakati kafulila alishafukuzwa uanachama akakimbilia mahakamani. Ukimya hapo uko wapi!? Pole sana dr. Zito hana watu km wewe ambavyo huna,wote mlikuwa mnabebwa na chama na hamjawahi kukibeba chama kwa sababu ya njaa zenu. Wewe umri huo kweli ni wa kujipendekeza kwa mwanaume mwenzio ili utumiwe mpesa? Kweli nchi ngumu sana hii.
 
Dr. Mkumbo anaishi kwa kufuata mkumbo wa Zito na tayari ameshapigwa kikumbo na CDM.
 
Huyu anayejiita Dr muda wote ana hoja dhaifu sana zilizojaa ulaghai na utata!
 
Hata kule Ujerumani Hitler alikuja na maneno kama haya, kumbe alikuwa nayake nyuma ya pazia. Huyu Dr katumwa na Shetani ila Hajui na Kwa nguvu za Mungu hawezi Kushida.

Kiukweli yeye amafanya makosa kusema tunahitaji badala ya anahitaji. Na ana haki ya kusema hayo kwa kuwa kafukuzwa kwenye chama chake. Asepe kimya kimya asizidi kujitia aibu.
 
Nimeisoma makala hii kwa umakini mkubwa. Nadiriki kukubaliana na mtoa mada kwa msingi huu; kuwa Demokrasia ya kweli katika nchi hizi zinazoendelea inaminywa sana, kuna kosa gani kupanga mkakati wa ushindi? Maana rahisi ya Demokrasia ni uhuru wa watu kuchagua viongozi wanaowataka, sasa kwa nini kuwa na ndoto za kugombea nafasi fulani ndani ya chama iwe usaliti? Na laiti kama CDM ingekuwa imeshika dola basi akina ZZK na Dr. Kitila leo wangekuwa gerezani kwa kosa linalosemwa ni Uhaini....Mimi ni miongoni mwa watu waliokuwa wakivutiwa na siasa za CDM lakini kutokana na kinachoendelea sasa ndani ya CDM kwa hakika sifikirii kama naweza kushiriki katika shughuli za chama hiki kama hapo awali.

Tusiwe na haraka ya kuwashambulia akina ZZK bila kuweka mambo katika mizania, kitu cha kujiuliza kwanini kila anayetoka CDM anatoka akisema ubaya ule ule kwa Viongozi? Alisema hayo Nakaaya Sumari, Shonza, Mwampamba, nk na pia sasa Zito na Kitila wanasema hayo hayo. Hivi hawa wote ------------ kweli? Ushauri wangu kwa CDM, imalize huu mgogoro kwa suluhu ndani ya Chama. Niliishasema hapo awali uwepo wa Dr. Slaa kama Katibu Mkuu ambaye alipita Mikoani na kufukuza fukuza hovyo Viongozi wa Chama wa Wilaya, Mikoa na hata Madiwani akidhani anaimarisha Chama kumbe laah ni mzigo. Hana sifa za kuwa mgombea wa Urais, hana jipya zaidi ya wimbo wake uliozoeleka wa ufisadi, nje ya ufisadi ana jipya gani??

Kwa Upande wa Mhe. M/kiti Mbowe amefanya aliyoweza kufanya lakini tunahitaji Mwenyekiti atakayekisaidia Chama kutoa ushindani wa dhati katika kuelekea kuchukua dola. Siasa za kuchukua fedha za mafisadi haziwezi kutusaidia kukishinda chama kilichoko madarakani. Heshima ya Mbowe itaendelea kuwepo kama atachukua maamuzi magumu kujiudhulu mara moja. Tusidanganyane, CDM kwa sasa si imara kama ilivyokuwa 2010, kunahitajika mabadiliko makubwa sana ili kurudisha imani.

Ni jambo la kusubiri na kuona lakini bila kutafuna maneno uongozi wote wa juu wa CDM umepoteza credibility unatakiwa ujitafakari na kuvua gwanda. Sioni kama kesho Mbowe anaweza kusimama kwa ujasiri ndani ya Bunge kukemea ufisadi wakati yeye mwenyewe amekiri kupokea fedha za mafisadi. Katu haiwezekani.

Bado fursa ipo, mjiuzuru mara moja.

Mmeshupalia dhana ya kuchukua pesa CCm bila kutafakari.. Kwani hujawahi kusikia usemi kuwa "Kula ccm kulala chadema?" au ulifikiri Ni kwa wapiga kura WA chini Tu. Sisi tunaamini hata kama kachukua kweli basi zimetumika kuimatisha chama kwanza Ni pesa za walipa kodi. Mbowe Ni kiongozi mbunifu hadi kuweza kuzichota pesa hizo
 
bona kila siku huu wimbo una imbwa ina maana wahusika hawasiki ,hakuna marefu yasiyo na ncha hii democrasia tunayo ihubili kila siku kwenye majukwaa iko wapi jamani
 
Mmeshupalia dhana ya kuchukua pesa CCm bila kutafakari.. Kwani hujawahi kusikia usemi kuwa "Kula ccm kulala chadema?" au ulifikiri Ni kwa wapiga kura WA chini Tu. Sisi tunaamini hata kama kachukua kweli basi zimetumika kuimatisha chama kwanza Ni pesa za walipa kodi. Mbowe Ni kiongozi mbunifu hadi kuweza kuzichota pesa hizo
unaweza kuthibitisha huo usemi au una toka povu bila evidance
 
Hapa akili za wasomi wetu wa Tanganyika ndipo zilipo tia nanga, kupanda kwa bei ya umeme na athari zake kwa wananchi na uchumi wa Taifa kwa ujumla yeye hayamuhusu. Ubinafsi na siasa tena za maji taka ndio ajenda yake kuu.Lakini siku yenu yaja na ikaribu sana, ni kwa wanasiasa wote bilakujali itikadi. Wananchi hatuwezi vumilia tena mateso tunayopata kiasi hiki sababu ya siasa zenu mbovu zilizokosa mwelekeo wa kulikomboa Taifa letu kiuchumi.
 
MAADILI NI NGUZO MHIMU YA UONGOZI.

Kumekwepo na jitihada ama za makusudi, ama za kutokujua, ama za kile kinachoitwa kumsafisha mbowe.

Niweke wazi kwamba sikumkosoa mbowe kuhusu mambo ya mahusiano anayosemekana kuwa nayo na wabunge wake wa viti maalumu, bali ni kuhusu KUKIUKA KWAKE MAADILI YA UONGOZI.

1) Kitendo cha kukatisha ziara ya mbunge wake wa kazi maalumu ili wakakutane Dubai kwa kazi maalumu badala ya kazi ya nchi aliyotumwa tena arudi toka marekani mpk Dubai kwa fedha za serikali ni matumizi mabaya ya fedha za umma na ni ukosefu wa maadili ya uongozi. Angemrudisha kwa gharama zake yaani kwa fedha zake hapo ingekuwa mambo binafsi. Kufanya mambo binafsi kwa fedha ya umma haiwezi ikawa jambo binfsi. Hivyo sikukosoa mapenzi yao bali matumizi ya kodi za masikini kwa mambo binafsi.

2) Kumlazimisha Afisa wa bunge abadili tiketi ileile iliyokuwa aende kwenye shughuli ya bunge sasa ageuze aende kwenye kazi maalumu hili sio jambo binafsi ni matumizi mabaya ya madaraka. Ni kukosa huruma kwa hali ya juu kwa watanzania.

3) Kumlazimisha mbunge wake wa kazi maalumu kuachana na safari ya kikazi na kuacha nchi ikose mwakilishi kwenye kikao hicho huku tayari akuwa ameshagharamiwa safari hiyo, huku tayari akiwa ameshaziba fursa hiyo ambaye mbunge mwingine angeweza kwenda kuliwakilisha taifa halafu mbowe na mtu wake wakaenda kwenye kipaombele chake cha kuburudika dubai ni ukosefu wa uzalendo kwa Taifa na ni ukosefu wa maadili ya kiuongozi.
Tumeongea kwakuwa wametumia fedha za umma, tumesema kwa sababu wameacha kazi ya umma huku wakiwa wamechukua fedha kwa ajili ya kwenda kuiwakilisha Tanzania na tunasema kwakuwa wamewanyima fursa wabunge wengene ambao wangekwenda kuwakilisha Taifa endapo fursa hiyo hangepewa mtu elibadilishiwa safari ya ya taifa na kuitwa kwa kazi maalumu.

"Ukipewa kazi ya nchi lazima ujiheshimu" NITASHANGAA SANA NITAKAPORUDI BUNGE LIJALO NIKIKUTA MBOWE BADO NI KIONGOZI WA UPINZANI BUNGENI

...ninyi ndo mnafanya watu waanze kuhoji ubora wa elimu ya DUCE. Yaani kwa akili yako Mbowe anamamlaka ya kuiamlisha ofisi ya bunge kufuja pesa? akili yako ndo imeishia hapo? rudisha cheti usiendelee kikinajisi chuo cha DUCE. Au ndo akili ileile ya Zitto kushupalia vyama kutokaguliwa badala ya CAG na msajili wanaotakiwa kukagua.
 
wakuu huyu kitila kabakia kidampa tu hana maana yoyote anatumia kalamu kufanya defence mechanism akiingia lecture nitamueleza
 
Mrema alishapata kusema "ccm walifanikiwa kuvisambaratisha vyama vingine lakini chadema ni kisiki cha mpingo".Huyu kitila kawafadhaisha sana hata wapiga kura wake nilikuwa nimeeenda kwenye mazishi ya mzee mmoja maarufu sana maeneo ya Ulemo juzi kati hapa nilipojua lile nd'o jimbo analotoka mwigulu na kitila nikaanza kudodosadodosa kwa watu kadhaa kwa habari ya mbunge wao ambapo wengi wao walionyesha kutomtaka mwigulu kutokana na mambo yake mengi anayofanya na lugha chafu anazotumia zinazoonyesha kutindikiwa busara,lakini wakawa wanafadhaishwa na mtu wao waliyemuona kama mbadala wa Mwigulu yaani Kitila jinsi alivyofanya madudu kwenye chama.Kimsingi wale jamaa niligundua wanapenda chama kuliko mtu wao kwa maana wengi walionyesha kumlaumu dr.kitila.

Nimeisoma hiyo article ya Kitila kwenye gazeti la Raia Mwema hakuna ninachokiona anafanya zaidi ya kujikanyagakanyaga tu,unafanya demokrasia gani na watu waliothibitika wanapokea pesa toka kwenye chama pinzani iliwaje kushinda uchaguzi kwenye chama,ni lazima waendelee kudhibitiwa kwa mtindo huohuo wa kubanwa mpaka pale tu tutakapokuwa tumepata watu safi wa dhamira na matendo yao,lakini kwa sasa bado sana kuruhusu demokrasia ya hivyo kwenye chama kama chadema,vinginevyo tutajikuta kuna mapandikizi mengi ya ccm huko cdm,naikisha fikia hapo ni watz kusahau habari ya kukombolewa kutoka kwenye wanyonya damu hawa wa ccm.
 
Nimeisoma makala hii kwa umakini mkubwa. Nadiriki kukubaliana na mtoa mada kwa msingi huu; kuwa Demokrasia ya kweli katika nchi hizi zinazoendelea inaminywa sana, kuna kosa gani kupanga mkakati wa ushindi? Maana rahisi ya Demokrasia ni uhuru wa watu kuchagua viongozi wanaowataka, sasa kwa nini kuwa na ndoto za kugombea nafasi fulani ndani ya chama iwe usaliti? Na laiti kama CDM ingekuwa imeshika dola basi akina ZZK na Dr. Kitila leo wangekuwa gerezani kwa kosa linalosemwa ni Uhaini....Mimi ni miongoni mwa watu waliokuwa wakivutiwa na siasa za CDM lakini kutokana na kinachoendelea sasa ndani ya CDM kwa hakika sifikirii kama naweza kushiriki katika shughuli za chama hiki kama hapo awali.

Tusiwe na haraka ya kuwashambulia akina ZZK bila kuweka mambo katika mizania, kitu cha kujiuliza kwanini kila anayetoka CDM anatoka akisema ubaya ule ule kwa Viongozi? Alisema hayo Nakaaya Sumari, Shonza, Mwampamba, nk na pia sasa Zito na Kitila wanasema hayo hayo. Hivi hawa wote ------------ kweli? Ushauri wangu kwa CDM, imalize huu mgogoro kwa suluhu ndani ya Chama. Niliishasema hapo awali uwepo wa Dr. Slaa kama Katibu Mkuu ambaye alipita Mikoani na kufukuza fukuza hovyo Viongozi wa Chama wa Wilaya, Mikoa na hata Madiwani akidhani anaimarisha Chama kumbe laah ni mzigo. Hana sifa za kuwa mgombea wa Urais, hana jipya zaidi ya wimbo wake uliozoeleka wa ufisadi, nje ya ufisadi ana jipya gani??

Kwa Upande wa Mhe. M/kiti Mbowe amefanya aliyoweza kufanya lakini tunahitaji Mwenyekiti atakayekisaidia Chama kutoa ushindani wa dhati katika kuelekea kuchukua dola. Siasa za kuchukua fedha za mafisadi haziwezi kutusaidia kukishinda chama kilichoko madarakani. Heshima ya Mbowe itaendelea kuwepo kama atachukua maamuzi magumu kujiudhulu mara moja. Tusidanganyane, CDM kwa sasa si imara kama ilivyokuwa 2010, kunahitajika mabadiliko makubwa sana ili kurudisha imani.

Ni jambo la kusubiri na kuona lakini bila kutafuna maneno uongozi wote wa juu wa CDM umepoteza credibility unatakiwa ujitafakari na kuvua gwanda. Sioni kama kesho Mbowe anaweza kusimama kwa ujasiri ndani ya Bunge kukemea ufisadi wakati yeye mwenyewe amekiri kupokea fedha za mafisadi. Katu haiwezekani.

Bado fursa ipo, mjiuzuru mara moja.

Ndugu yangu dala dala umeongea kwa hisia sana kuhusu mambo yanayoendelea ndani ya cdm, ili ukweli mmoja ambao nakubaliana nao ni kwamba haiwezekani tukubuliane kwa kila jambo ila tunaweza kukubaliana kwa mambo mengi.
Ni kweli Mbowe kama Mbowe kwasasa hawezi kuwa na nguvu kubwa ya kuwanyooshea vidole hao mafisadi kama mwanzo kwani udhaifu wake umewekwa hadharani ambapo ni faida kwa chama kujua madhaifu ya viongozi wake. Umegusia mambo mengi kwa hisia ambayo wewe na hata mimi ninaona ni madhaifu kwa chama. Ila hapo ulipoanza kuwataja akina Mtela, Juliana ndio kidogo nimetofautiana na wewe. Iweje hawa akina Mtela, Shonza nk waliokuwa wakituhumiwa na cdm kwamba ni wasaliti wajiunge na CCM ambayo imekuwa ikihusishwa na kuivuruga cdm. Hao akina Mtela, Shonza nk walikuwa wakiiponda sana CCM walivyokuwa cdm, lakini wamehamia CCM hatuwaoni wakikosoa hayo mapungufu ya ccm wala kuleta changamoto mpya ndani ya ccm ila na wao wameiga kila upuuzi unaofanywa na ccm dhidi ya cdm i.e siasa za maji taka.
Halafu nikupe tahadhari kubwa ambayo ninaiona kwa ZZK ni kwamba kwa uzoefu wangu mtu yoyote anayeyataka madaraka kwa nguvu kubwa huwa ni tatizo sana huko mbeleni. Kila ajikwezaye nadhaani unajua madhara yake. Huyu Mbowe tayari ana mapungufu na yameshaonekana ila kwa sasa yeye ndie kiongozi halali, apewe muda amalize kipindi chake na wakati wa uchaguzi ushindani uwe huru na haki.
Huyu Dr. Kitila nadhani ni kiongozi mzuri ila nadhani sio imara kwenye kupambana na siasa za majitaka. Lakini naye kwa sasa nadhani ameweza kuuona madhaifu ya ZZK ambaye anaonekana alikuwa chaguo lao kwenye waraka wa mabadiliko maana kwa mtazamo wangu kiongozi mzuri halazimishi kupata madaraka ila anashawishi kupewa uongozi.
 
niliwahi kusema humu JF kwamba vyama vyote vya siasa vinamfumo sawa na CCM....wanakopi na kupesti ktk demokrasia huwezi kufanya yanayofanwa na viongozi wetu wa vyama vya siasa...na ndio maana hawapendani na hawaezi kuungana wapo kimaslahi tu................kitila is right...................very right...mapinduzi tafsiri yake haiingii kabisa na kile kimkakati cha kitila na wenzie...uliwahi kuona mapinduzi yanasubiri uchaguzi jamani??????????????????????
 
Ndugu yangu dala dala umeongea kwa hisia sana kuhusu mambo yanayoendelea ndani ya cdm, ili ukweli mmoja ambao nakubaliana nao ni kwamba haiwezekani tukubuliane kwa kila jambo ila tunaweza kukubaliana kwa mambo mengi.
Ni kweli Mbowe kama Mbowe kwasasa hawezi kuwa na nguvu kubwa ya kuwanyooshea vidole hao mafisadi kama mwanzo kwani udhaifu wake umewekwa hadharani ambapo ni faida kwa chama kujua madhaifu ya viongozi wake. Umegusia mambo mengi kwa hisia ambayo wewe na hata mimi ninaona ni madhaifu kwa chama. Ila hapo ulipoanza kuwataja akina Mtela, Juliana ndio kidogo nimetofautiana na wewe. Iweje hawa akina Mtela, Shonza nk waliokuwa wakituhumiwa na cdm kwamba ni wasaliti wajiunge na CCM ambayo imekuwa ikihusishwa na kuivuruga cdm. Hao akina Mtela, Shonza nk walikuwa wakiiponda sana CCM walivyokuwa cdm, lakini wamehamia CCM hatuwaoni wakikosoa hayo mapungufu ya ccm wala kuleta changamoto mpya ndani ya ccm ila na wao wameiga kila upuuzi unaofanywa na ccm dhidi ya cdm i.e siasa za maji taka.
Halafu nikupe tahadhari kubwa ambayo ninaiona kwa ZZK ni kwamba kwa uzoefu wangu mtu yoyote anayeyataka madaraka kwa nguvu kubwa huwa ni tatizo sana huko mbeleni. Kila ajikwezaye nadhaani unajua madhara yake. Huyu Mbowe tayari ana mapungufu na yameshaonekana ila kwa sasa yeye ndie kiongozi halali, apewe muda amalize kipindi chake na wakati wa uchaguzi ushindani uwe huru na haki.
Huyu Dr. Kitila nadhani ni kiongozi mzuri ila nadhani sio imara kwenye kupambana na siasa za majitaka. Lakini naye kwa sasa nadhani ameweza kuuona madhaifu ya ZZK ambaye anaonekana alikuwa chaguo lao kwenye waraka wa mabadiliko maana kwa mtazamo wangu kiongozi mzuri halazimishi kupata madaraka ila anashawishi kupewa uongozi.


usitoe hoja dhaifu mkuu ktk siasa hakuna adui wala rafiki wa kudumu..machali anasema ni upepo tu upitao..kubadili chama ni kawaid...shibuda alikuwa ccm nw ni cdm..je alikuwa kibaraka wa chadema hapo awali.....yule katibu wa ccm Arusha aliyehamia chaedema baada ya nassari kuwin Arumeru mashariki je alikuwa kibaraka wa chadema.........iweje ukihama kutoka ccm kwenda CDM iwe sahihi na kutoka CDM kwenda CCM uwe msaliti......hii ndio demokrasia na uheshimu wa haki za binadamu tunaoupigania....................mimi naamini ukombozi wa mtamzania haupo ktk Ballot pper au box...upo kichwani mwake...na ndiomaana tunatumia fedha nyingi nyakati za uchaguzi kusha madege ............lakini hukuti tukitoa michango kuchenga hata public libraries watu wasome vitabu waondokane na ujinga...tunawaburuza na kuwaaminisha...........CCM imeamisha watu bila yenyewe hamna amani..watu wanaandamana na mabomu yanapigwa ccm inapata credit wao hawaandamani kwani ni watu wa amani...----!!!!!!!!!! wengine ndio watu wa vurugu...vyama vyetu vimeshindwa kuutegua mtego huo.........shida 2pu
 
Mbona Dr mwenyewe ni mshabiki wa zito.. Kutufundisha kutokuwa washabiki wa viongozi hali wewe umeonyesha kwa uwazi mkubwa kuwa ni mshabiki wa kiongozi fulani tutaelewa kweli hilo somo.. Ubiri unachoishi
Tatizo kubwa la nchi hii ni unafiki uliokithiri kama huo anaouonyesha Kitila. Wao walipanga waweke watu wao kwenye uongozi kuanzia ngazi ya shina hadi Taifa je hapo walikuwa wanajenga ufuasi wa chama au mtu? Mtu ambaye ni mwanademokrasia wa kweli kitu ambacho angefanya ni kuacha mwanachama wa ngazi yeyote muda wa uchaguzi ukifika achukue fomu na kugombea nafasi anayodhani anaitaka na wapiga kura wamchague bila ushawishi wa kimtandao ambao hutumia pesa kwa sababu huwezi kujenga mtandao bila pesa, na pesa hizo zinatoka kwa maadui wa mpinzani wako ambao wako nje ya chama , hivyo hapo hakuna kujenga chama ni kumjenga mtu. Mtu aliyekaa darasani muda mrefu kushindwa kuelemika kuliko mtu aliyekaa darasani muda mfupi ni jambo la aibu. Ingekuwa mimi ningekaa kimya kuliko kujidanganya kuwa ninaweza kuhadaa watu wote. Ulichotaka kufanya kimebumburuka kabla hakijatimia na kimekugharimu nafasi yako kisiasa na kazi kwako, labda fanya tahmini ya faida na hasara za kununuliwa.
 
Mkutano wa leo wa NCCR MAGEUZI unadhihirisha Watanzania tunaweza kujenga mfumo makini wa siasa za vyama vingi.
Chama cha NCCR kimealika vyama vyote na VIMEHESHIMU, VIMEHUDHURIA. HONGERA HONGERA SAAANA NCCR !!!!!
 
Mrema alipotimka, akatimka na mashabiki wake. Hicho ndicho kinachoendelea ndani ya CHADEMA. Kuna watu wenye mtazamo finyu wanaamini kwamba chama hiki ni imara sana kwa sasa kiasi kwamba hata wakimfukuza Zitto kitaendelea kubaki imara. Wamesahau kwamba wamejenga ufuasi kwa viongozi, na hivyo watakapomfukuza Zitto atatimka na wafuasi wake na chama kitayumba" Dr Mkumbo.

Hii paragraph pia Ina ujumbe ulionauzito mkubwa! Na ndicho kitakachowakuta CDM! Tusubiri.

mbona tayari ZITTO KISHATIMULIWA ! KWANI AMEONDOKA NA NANI ? ZAIDI YA WALE WANACHAMA WA CUF TEMEKE WAKIONGOZWA NA KAMBAYA AU KUNA WENGINE ?
 
Huyu anayejiita Dr muda wote ana hoja dhaifu sana zilizojaa ulaghai na utata!

Huyu mhadhiri mwenzangu amenisikitisha sana kwa kuonesha upeo finyu na tamaa. Alipaswa kujua kwmba chadema imeanza kukubalika sio zaid ya miaka saba iliyopita. tishio la cdm kwa chama tawala limekifanya chama tawala kutumia kila mbinukukimaliza. muda huu ulikuwa wa kuimarisha chama na kuongeza umoja kazika kukabiliana na mbinu za ccm. kinyume chake kina kitila and co. wanadhoofisha uongozi wa chama kichinichini ili wapate sababu ya kuwatoa.hii sii nia njema. this is pathetic. kitila umetuangusha sana. shame on you. mabadiliko ya uongoz kwenye chama ni jambo jema lakini kwa njia sahii na wakati muafaka. hovyo kabisa mwalim mwenzangu.
 
kuna babu mmoja nyarwanda aliwai kunambia mwaka 87 wakati naenda form 1 kwamba; ukwiga ntigutera ukumeya(elimu haifanyi mtu aache ujinga aliozaliwa nao). Kwa tafsiri hii, kamwe kitila hautakuja kutokwa na ujinga uliozaliwa nao ata kama umesoma. Baada ya kufukuzwa, dr lwaitama alisema kuwa wewe ni rafiki yake wewe na zitto. Mmesaidiana kwa mambo mengi ila kwa hili mmechemka na alisema mlipashwa kufukuzwa. Watu tunategemea mageuzi ya kweli nyie mnakuja na sera za kufifiza? Kama zitto alikuwa anakupa sh. Lak 2 kila mwezi, je ulikuwa na kazi gani special kwake? Kwa ujinga huu, angekupa milion moja kila mwezi, ungefanya ujinga mkuwa zaidi licha ya kuwa umesoma ila haujaelimika
 
Back
Top Bottom