kukukakara
JF-Expert Member
- Jul 31, 2012
- 496
- 164
Namuonea huruma Kitila na wenzake, wanatia aibu hata elimu yao pia wameitia aibu kuu. Wameshindwa kujua malengo ya chama chao na hata sababu ya kuwa Upinzani. Kitu ambacho hata mtoto wangu wa Darasa la kwanza analielezea vizuri. Huruma yangu ipo katika kona waliyonaswa tena vijana, alafu wasomi, ushauri kwao ni kukaa kimia Jamii iwasahau na wasirudi tena kwenye siasa. Waliingia kwenye mtego bila kujua wakijua ni Misaada ya kawaida ya kibinadamu mbaya zaidi walinashwa hata kabla hawajua kuwa watalazimishwa kufanya wasiyoyapenda na hawata kuwa na jinsi maana tayari wameneswa tunduni, wale Jamaa ni hatari ndio fani yao wapo makini na wanatumia akili nyingi sana, kama una akili za kalatasi huwezi kujua unapoperekwa maana mngelijua msingekubali kwa namna ninavyowajua Mwl. Kitila na mm.
Hakuna msomi aliye elimika ambaye hasingejua kuwa kwasasa priority nikuondoa CCM kwanza hata kama inafanyika bila chama kuwa na Mwenyekiti au hata kama Mwenyekiti aliopo anamapungufu ya aina yoyote achilia mbali upuuzi wanaoeleza sasa. Maneno ya Kitila na utetezi anaotoa ukilinganisha na umuhimu wa jambo lenyewe unaletashaka kama kweli ni Dr. Huwezi kuongelea kubadili Mkuu wa majeshi wakati mpo mstari wa Mbele vitani tena wakati ambapo umoja unahitajika ili kushinda vita husika, huo ni usaliti tosha inashangaza sana Dr mzima haoni hili. Watu wanaojua historia ya vita vya Rwanda vilivyomuingiza Kagame madaraka wanaojua fika nini kilifanyika kuweka askali katika morali ya ushindi baada ya Mkuu wa operation hiyo kufariki mwishoni kabisa wakati bado kidogo wapate ushindi. Kitila ni msomi anajua kwanini Mwl. Nyerere aliongoza TANU wakati wa mapambano ya Uhuru na hata baada ya Uhuru, sio kuwa hakuwepo mwenye kumshinda kiakili na ki mawazo.
Hakuna mjinga atakaye waelewa bora mnyamaze mnaweza kurudisha heshima yenu kwa ukimia.
Well said!!!