Kwanza naomba nirekebishe kidogo,
Dr. Isack Ndodi si Mchungaji bali ni Mwinjilisti. Kuna tofauti kati ya Mchungaji na Mwinjilisti. Dr. Ndodi hajawahi kuwekewa MKONO WA KICHUNGAJI, hivyo yeye si Mchungaji bali ni Mwinjilisti anayefanya kazi ya kueneza Injili ya Bwana Yesu. Pia, Dr. Ndodi ni Mganaga anayetumia Tiba Asilia hasa ya mimea amabayo hata ktk maandiko matakatifu yanashauriwa tuyatumie, kwani haya yenye kemikals yamekuwa na side effects nyingi sana kwetu. Dr. Ndodi hapigi Ramli na ndiyo maana yuko tofauti na Waganga wa Jadi/Kienyeji. Tatizo ni kwamba ni kweli Gharama yake ni kubwa sana, hivyo wengi wenye kuhitaji huduma yake wanashindwa kupata kutokana na gharama yake.
Nilitoa comments zangu muda mrefu kwamba UKIONA MWANAUME ANAONGEA KWA SPEED NAMNA HIYO UJUE NI TAPELI. NDODI HANA TOFAUTI NA MATAPELI WOWOTE WALIOPO MITAANI. Jambo hili litafahamika vizuri kadri siku zinavyokwenda.
Huyu Dokta/Mchungaji tena kijana ni mfano wa kuigwa.Napenda vipindi vyake vya redio na TV kwa maana anazungumzia mambo ya maisha ya kawaida kabisa.Kipindi chake cha juzi Jumatano kuhusu namna ya kuchagua mchumba kwa vijana wa kike na kiume kilinivutia sana.Laiti angejiunga hapa akaweza kuchangia hizi mada kwenye jukwaa la mahusiano na JF Dr.
Wakuu naomba muone angalizo hapa chini.
Inatakiwa tumzungumzie kwa wema!!!!!
Utaona moja kwa moja sina nafasi ya kuchangi wema juu ya mtu huyu. Naomba upanue wigo ya mada hii ili tuweze toa mabaya pia.
Are u kidding? Hv tangu lini binadam wa kawaida akawa mtume.....mhh naona sasa hv ataitwa mungu lol
Samahani wakubwa, nina shida na wimbo wa mafumu bilali unaitwa maya, kuna mtu anaweza kunisaidia?
Pdidy haueleweki! Kwanza unamlalamikia Dr Ndodi, Pili unaendelea kupeleka watu kwake; we ni mtu wa aina gani?
Hao unaowapeleka wanapona au ...? Kama yeye amekaa kibiashara hilo ndio jambo la muhimu. tatizo waTZ hatujali muda wa mtu. Inawezekana jamaa yako alikuwa amepewa maelekezo yote lakini akawa mgumu wa kuelewa na akawa anapoteza muda kutaka jambo hilo hilo lirudiwe rudiwe na Dr akaona anampotezea muda wa kulamba 20K.
Tujali muda, kila mtu ana 24hrs per day na usipotumia vizuri uta-lost
Jamani fuateni njia sahihi toka kwa watu sahihi waliothibitishwa na mamlaka sahihi!
How on earth unaanza kumconsult mtu kama Ndondi?..hadeserve kuitwa dokta!
Tatizo mamlaka husika zinamuacha tu aendelee kupotosha! Bongo tambarare!
dokta+ mchungaji+ mshauri+ mwalimu = tapeli
Hapana huyu Dr Ndodi ni ghali mno, Basi! Mambo ya kupanda ndege kwenda Mwanza au popote pale hayasababishi awe ghali kivile, dawa zenyewe limao, mapapai, kitunguu swaumu, tangawizi, ughali uko wapi hapa. Kutuibia tu!Hizo trip ni za kujitangaza zaidi. Wanaomwalika wangemchangia kidogo ili gharama zipungue. Kuhusu kumanipulate mawazo ya watu ni kweli kabisa. Wabongo tuna matatizo mengi ambapo ni fursa kwa wajanja kama hao.