Dr. Dau aingilia mchakato wa ugawaji viwanja Mafia

Tunaenda na jf style

invisible unaweza kuiweka top kama kiambatanishi.....
attachment.php

attachment.php


attachment.php

View attachment 41088

View attachment 41086

View attachment 41083

Mkuu SlidingRoof, kama list ya waliopata viwanja, basi Dr. Dau alikuwa na wajibu wa kutetea watu wake. Ingawaje nimeona majina ya wazawa wa mafia, lakini wengi wao hapo ni wale wateule. Mie enimetoka Mafia miaka 4 iliyopita, lakini pamoja na hayo nimeona majina mengi tu ya wafanyakazi wa halmashauri na mmoja wapo akiwa kutoka idara ya ardhi. Kuna baadhi ya majina siyafahamu; lakini kwa miaka minne amestbayo sipo hapo, sina shaka kwamba mengi ya majina hayo huenda ni ya wafanyakazi wa halmashauri walikokuja hapo after 2007! Hivi kweli, tuseme timu ya JF ikiongozwa na Invissible ndiyo iwe inagawa viwanja; halafu waliopata wawe Mwanakijiji, Maxcenello, Faisal Foxy, AshaDii, Crashwise, MTM na wengineo; halafu babangu wa pale Tandika akisema kwamba JF walipendeleana atakuwa amekosea?! Hapa hakuna cha sheria wala nini; hata kama sheria zilifuatwa, bado kulikuwa na conflict of interests.
 
mikakati ya ubunge 2015 hiyo.

Bila shaka unamaanisha ni staili za nitoke vipi za Dokta Dau!!!! Mkuu, Dr. Dau akitaka ubunge mafia wala hana haja ya kutumia viwanja na hata Buji (mbunge wa sasa analijuwa hilo)! Kuwepo kwa Buji ni kwavile tu Dau hajaamua kugombea na akifanya hivyo, wala hana haja ya kutumia msuri. Na wala siamini kwamba Dau kafanya hayo kwavile amekosa kiwanja; Dau sio mtu wa kukosa kiwanja mafia; cha kupima cha halmashauri anaweza kukosa; hata cha kununua?! Kule kijijini kwao Bweni ni miongoni mwa ardhi chache sana mafia zilizo bora kuilko hapo Kilindoni. Naamini, dhamira ya Dau ipo clear kwamba kutetea maslahi ya Wana-Mafia wenzake; jambo ambalo hata mimi naweza kufanya hasa kwa kuzingatia hali ya mafia yenye ufinyu wa ardhi na uhamiaji mkubwa wa watu kutoka bara.
 
Viwanja vimegawiwa sehem 3 ismailia,vunjanazi na magemani wengi wamafia waloomba magemani wamepata ila wengi wa wanamafia walioomba maeneo waliyoyachagua wamepata tuache ushabiki kama ni viwanja vimegaiwa hii ni awamu ya tatu malalamiko haya hayakuwepo tatizo yeye aliomba viwanja hakupata bwanamkubwa na yupo kwenye siasa zaid kwa sababu anataka mleta Ndugu yake kugombea ubunge Mafia cha msingi watumishi mkinyang'anywa viwanja msikubali fateni sheria kama si mdini dr dau angemnyang'anya KAdinali Pengo Tereniakidai anataka jenga chuo cha VETA ye ana mwaka wa tatu hajafanya lolote zaidi ya kumuweka mpambe wake RHUMBA....
 
Shule amejenga kwao BWeni hata walimu anapanga yeye kuh UDINI kwa Dau halina utata....

Charity begins at home broda! Ukumbuke kwamba, wakati Dr. Dau anajenga sekondari mafia, wakati huo Wilaya mzima ilikuwa na sekondari moja tu-Kitomondo! Mbaya zaidi, Kitomondo Sec ipo other side(mbali kabisa na Bweni-nyumbani kwa Dau)! Kwa asiyeijuwa Mafia, ni sawa na kusema Kijiji Cha Dau kipo Kiluvya/Mbezi Luis na Shule ya Kitomondo ipo Mbagala!!! Sasa hapo kuna ubaya gani ikiwa aliamua kujenga shule ku-save kijijini kwao na vijiji vya jirani ambavyo kimsingi ndiko eneo kubwa la mafia liliko?!
 
Kitu ambacho kinachotatiza hapa kama ileee ya TAMASHA LA MASHOGA MAFIA mwaka jana, (na ndiyo msingi wa malalamiko ya Dr Dau na wenzake ) ni kuwa ofisi ya Mkurugenzi haikuweka wazi vigezo vilivyotumika kugawa viwanja hivyo. Hali hii inatia mashaka hasa ukizingatia kuwa wengi waliopewa viwanja hivyo si wakazi wa Mafia ambayo ki jiografia ni kisiwa kidogo ambacho hakina raslimali yoyote ile zaidi ya ardhi ndogo iliopo na na baya zaidi wengi wa hao waliopewa ni watumishi wa Halmashauri na hasa watumishi wa Idara ya Ardhi, jambo ambalo ni kinyume kabisa na misingi ya Utawala Bora [principles of good governance].

Sasa hapa umesema kitu ambacho ndio nilikuwa naulizia kwa sababu mwanzoni uliingiza mambo ya uzawa n.k ambayo hayana msingi. Hata kama Mafia kuna ardhi kidogo haina maana Tanzania kuna ardhi kidogo. Wakazi wa Mafia wanaweza kupata ardhi sehemu yoyote ndio maana leo unaona watu kutoka Uchaggani (ambako ardhi huru haipo kwa miaka mingi) wameweza kwenda sehemu mbalimbali za Tanzania na kununua ardhi; ndio maana leo unaona Wamasai wamehama maeneo yao ya asili na kuwakuta kila kona ya nchi wakijipatia ardhi kwa ajili yao na mifugo yao. Wakati wa Mafia wasifungwe na fikra kuwa wanatakiwa kuishi Mafia tu na kuwa ni lazima wapate ardhi Mafia. Tanzania ni kubwa sana na watoto wake wote wanaweza kunufaika nayo.

Ila kwamba baadhi ya watu waliopatiwa ardhi ni watumishi wa ardhi hapo umeleta hoja nzuri na hii inaweza kuwa na msingi sana na kama kweli kuna uthibitisho wa watu kujipendelea basi ni hoja inahitaji kusimamiwa kwa karibu kabisa. Lakini pia ni lazima ioneshwe vizuri kwani mfanyakazi wa Ardhi naye ni Mtanzania je hana haki ya kupata ardhi Mafia? Ila at least kuna mahali pa kuanzia hapa.

Cha kijiuliza DC wa Mafia bwana Mangochie Manzie, Mbunge wa Mafia bwana Abdulkarim Shah (Bulji) pamoja na madiwani wanatekeleza ilani ya Chama gani? Kwa sababu ni wazi kuwa hawa hawa mwaka jana walipigania TAMASHA LA MASHOGA liende kisiwani Mafia, mwaka huu wameamua kujipatia viwanja wao na wake zao KIFISADI bila kuweka maslahi ya wana Mafia kwanza kama wakazi wa pale

Hili la Mashoga unalilazimisha sana - Mashoga wapo Tanzania, wamekuwepo na wataendelea kuwepo labda tuanze kuwatia pingu na kuwafunga wote tunaowahisi ni mashoga! Sidhani kama Dau au mtu mwingine yeyote anaweza kuendesha kampeni hiyo dhidi ya mashoga kama sehemu ya kisiasa. Kwani mashoga hawana haki ya kuwa na viwanja Tanzania? Ni lini tumesema kuwa mashoga hawana haki ya kuwa na tamasha lao!? Mbona yapo matamasha ya watu wazinifu au ngoma zote na burudani zinazofanyika Mafia zote zinafanywa na kufurahisha wana ndoa peke yao? Hili la mashoga labda limekuzwa sana na baadhi ya watu wamekuwa obsessed nalo kupita kiasi.

Na sijaona uhusiano wa hili la ardhi na suala hilo la mashoga.
 
Bila shaka unamaanisha ni staili za nitoke vipi za Dokta Dau!!!! Mkuu, Dr. Dau akitaka ubunge mafia wala hana haja ya kutumia viwanja na hata Buji (mbunge wa sasa analijuwa hilo)! Kuwepo kwa Buji ni kwavile tu Dau hajaamua kugombea na akifanya hivyo, wala hana haja ya kutumia msuri. Na wala siamini kwamba Dau kafanya hayo kwavile amekosa kiwanja; Dau sio mtu wa kukosa kiwanja mafia; cha kupima cha halmashauri anaweza kukosa; hata cha kununua?! Kule kijijini kwao Bweni ni miongoni mwa ardhi chache sana mafia zilizo bora kuilko hapo Kilindoni. Naamini, dhamira ya Dau ipo clear kwamba kutetea maslahi ya Wana-Mafia wenzake; jambo ambalo hata mimi naweza kufanya hasa kwa kuzingatia hali ya mafia yenye ufinyu wa ardhi na uhamiaji mkubwa wa watu kutoka bara.

Haya madudu ya ubaguzi haya..
 
Solution ni kuondoa huo ukiritimba wa upimaji na ugawaji wa viwanja ili watu wajipatie viwanja wakati wanapotaka badala ya kusubiri mpaka idara ya ardhi wanapopenda.
 
Haya madudu ya ubaguzi haya..

Hakuna cha madudu wala ubaguzi hapo mkuu; lazima tuiangalie tunawazungumzia watu wa aina gani! Ni maestkosa sana kusema eti wachaga mbona wanaweza kwenda popote!!! Mafia island nazani ndio wilaya ndogo kuliko zote TZ na yenye umaskini mkubwa. Sina shaka hata hiyo hadhi ya wilaya ilipata kwa sababu tu ya location yake kwamba ilibidi lazima ijitegemee kiutawala ili kuondoa hadha ya wakazi wake. Sasa watu kama hawa ambao hatatokea wa kuwatetea itafika wakati wenyeji wakawa ndio wapangaji kwenye ardhi yao.hakuna ubaya wowote wa kutetea interests za wenyeji, especially kama wenyewe wenyewe ni disadvantaged.....huo so ubaguzi na kamwe hauwezi kuwa ubaguzi na kinyume chake kutozinagatia maslahi ya wengi. Ni kweli, nchi hii M-TZ ana haki ya kwenda popote na kupata kiwanja popote; lakini tukiacha rules of the jungle i-apply kila mahali kwa kigezo ambacho kinyume chake ni ubaguzi kama unavyoita then hapoa maskini always watabaki masikini na kuwa watwana kwene ardhi yao. Generally speaking, as much as 50% ya wachaga wana uwezo wa kupata ardhi mafia (tuki-apply rules of the jungle) wakati ni less than 2% ya Wamafia wenye uwezo wa kupata ardhi Uchagani! So, hapo ubaguzi upo wapi ikiwa mtu anatokea kutetea hii disadvantaged population (in terms of size and economic power?). I stand on my point; hata ningekuwa mimi ningewatetea hata kama sheria zimefuiatwa hasa nikizingatia, ktk mazingira ya hapa kwe2; sheria zinawa-favor zaidi the powerfull than the powerless!
 
Mkuu SlidingRoof, kama list ya waliopata viwanja, basi Dr. Dau alikuwa na wajibu wa kutetea watu wake. Ingawaje nimeona majina ya wazawa wa mafia, lakini wengi wao hapo ni wale wateule. Mie enimetoka Mafia miaka 4 iliyopita, lakini pamoja na hayo nimeona majina mengi tu ya wafanyakazi wa halmashauri na mmoja wapo akiwa kutoka idara ya ardhi. Kuna baadhi ya majina siyafahamu; lakini kwa miaka minne amestbayo sipo hapo, sina shaka kwamba mengi ya majina hayo huenda ni ya wafanyakazi wa halmashauri walikokuja hapo after 2007! Hivi kweli, tuseme timu ya JF ikiongozwa na Invissible ndiyo iwe inagawa viwanja; halafu waliopata wawe Mwanakijiji, Maxcenello, Faisal Foxy, AshaDii, Crashwise, MTM na wengineo; halafu babangu wa pale Tandika akisema kwamba JF walipendeleana atakuwa amekosea?! Hapa hakuna cha sheria wala nini; hata kama sheria zilifuatwa, bado kulikuwa na conflict of interests.

He he heee ....watu wachokozi kweli.
 
Sasa hapa umesema kitu ambacho ndio nilikuwa naulizia kwa sababu mwanzoni uliingiza mambo ya uzawa n.k ambayo hayana msingi. Hata kama Mafia kuna ardhi kidogo haina maana Tanzania kuna ardhi kidogo. Wakazi wa Mafia wanaweza kupata ardhi sehemu yoyote ndio maana leo unaona watu kutoka Uchaggani (ambako ardhi huru haipo kwa miaka mingi) wameweza kwenda sehemu mbalimbali za Tanzania na kununua ardhi; ndio maana leo unaona Wamasai wamehama maeneo yao ya asili na kuwakuta kila kona ya nchi wakijipatia ardhi kwa ajili yao na mifugo yao. Wakati wa Mafia wasifungwe na fikra kuwa wanatakiwa kuishi Mafia tu na kuwa ni lazima wapate ardhi Mafia. Tanzania ni kubwa sana na watoto wake wote wanaweza kunufaika nayo.

Ila kwamba baadhi ya watu waliopatiwa ardhi ni watumishi wa ardhi hapo umeleta hoja nzuri na hii inaweza kuwa na msingi sana na kama kweli kuna uthibitisho wa watu kujipendelea basi ni hoja inahitaji kusimamiwa kwa karibu kabisa. Lakini pia ni lazima ioneshwe vizuri kwani mfanyakazi wa Ardhi naye ni Mtanzania je hana haki ya kupata ardhi Mafia? Ila at least kuna mahali pa kuanzia hapa.
Wachaga na Wamasai walilazimika kutoka kwenye maeneo ya asili na kwenda maeneo mengine kutafuta ardhi/maeneo baada ya maeneo yao ya asili kwisha na walioyamaliza ni wao wenyewe pamoja na ukweli kwamba walikuwa na maeneo makubwa kijiografia! Hii ni tofauti sana na wala haikaribiani na ukweli kuhusu mafia! Mafia ardhi ni ndogo pengine kuliko sehemu yoyote ile hapa TZ. Lakini bado mtu useme; if u can't survive in the jungle then leave the fittest wa-play the role......no, tht is unacceptable!
 
Mafia Kuna matatizo makubwa sana. Na haya mambo ya Uongozi mbovu yana historia ndefu kisiwani Mafia, tangu enzi ya Mwalimu Nyerere, ambapo yeye aliifanya Mafia kama detention spot. Kwaa wale woote ambao walikosana na utawala wake basi aliwapeleka mafia kama adhabu na sehemu ya kuwapoza wasisikike. Baadaye Ikawa inatumika mafia kuwapeleka wafanya kazi wa serikali ambao wamefanya Makosa sehemu zingine za tanzania, ukipelekwa mafia maana yake umepewa adhabu, na ndiyo maana kisiwa hicho kikanyimwa fursa zote za miundombinu, kama viwanja vizuri vya ndege, barabara na bandari. Lakini hivi sasa Mafia imegeuzwa kuwa ni sehemu ya kupeleka ndugu au marafiki wa viongozi wa juu ambao uwezo wao mdogo kuongoza, na hivyo wasingeweza kukubalika sehemu zingine za tanzania ambako wananchi wake ni waelewa wa mambo na wasiovumilia ujinga. Kwamfano, mkuu wa wilaya ya mafia hana sifa hata moja ya kuwa kwenye nafasi hiyo, anachokifanya mafia ni upumbavu mtupu, amefanya madudu lukuki, amelazimisha wanachi wa kijiji cha chole kuuza magofu ya serikali kinyume na sheria za nchi, ameuza kwa mzungu madarasa ya shule yaliyojengwa na nguvu za wananchi, nyumba ya mwalimu pamoja na soko, ameshiriki kusababisha migogoro ya ardhi sehemu mbalimbali kisiwani Mafia,anavunja sheria za hifadhi za bahari kwa kuvua kwenye maeneo tengefu(marine reserves), hivi ninavyoandika kwa taarifa rasmi ni kwamba, nyavu zake na vifaa vingine vya uvuvi vimekamatwa na marengers wa hifadhi viko chini ya mikono ya sheria,lakini anaforce apewe vifaa vyake! Na mengine mengi, kuna mdau mmoja jana alitaka kumtia vibao pale airport mafia kwa ujinga wake!
 
Mhhh hivi ni kweli?????
  • Na kama ni kweli kulikuwa na tatizo ktk taratibu kwa nn mpaka Dr Dau ndio aingilie kuokoa janga. Ina maana katika mfumo mzima ya serikali halmashsuri, wilaya , Mkoa, wizara madudu hayo yamefinayika bila kuonekana kasoro? Yaani ama ni kweli basi waki reverse itabidi watu wawajibishwe otherwise itauwa ni siasa tu
  • Na watu kama kina Dr Dau ( National figures ) sauti zao tulitakiwa tuzisike sio tu kwa mambo ya mafia lakini tulitkiwa tusikie wakikosoa issues za mwaziri na vigogo kuziana nyumba. Tunatakiwa tuwasikie wakikosa utaratibu wa vigoro wakiuziana ma VX ya umma kwa bei chee
 
Sasa hapa umesema kitu ambacho ndio nilikuwa naulizia kwa sababu mwanzoni uliingiza mambo ya uzawa n.k ambayo hayana msingi. Hata kama Mafia kuna ardhi kidogo haina maana Tanzania kuna ardhi kidogo. Wakazi wa Mafia wanaweza kupata ardhi sehemu yoyote ndio maana leo unaona watu kutoka Uchaggani (ambako ardhi huru haipo kwa miaka mingi) wameweza kwenda sehemu mbalimbali za Tanzania na kununua ardhi; ndio maana leo unaona Wamasai wamehama maeneo yao ya asili na kuwakuta kila kona ya nchi wakijipatia ardhi kwa ajili yao na mifugo yao. Wakati wa Mafia wasifungwe na fikra kuwa wanatakiwa kuishi Mafia tu na kuwa ni lazima wapate ardhi Mafia. Tanzania ni kubwa sana na watoto wake wote wanaweza kunufaika nayo.

Ila kwamba baadhi ya watu waliopatiwa ardhi ni watumishi wa ardhi hapo umeleta hoja nzuri na hii inaweza kuwa na msingi sana na kama kweli kuna uthibitisho wa watu kujipendelea basi ni hoja inahitaji kusimamiwa kwa karibu kabisa. Lakini pia ni lazima ioneshwe vizuri kwani mfanyakazi wa Ardhi naye ni Mtanzania je hana haki ya kupata ardhi Mafia? Ila at least kuna mahali pa kuanzia hapa.



Hili la Mashoga unalilazimisha sana - Mashoga wapo Tanzania, wamekuwepo na wataendelea kuwepo labda tuanze kuwatia pingu na kuwafunga wote tunaowahisi ni mashoga! Sidhani kama Dau au mtu mwingine yeyote anaweza kuendesha kampeni hiyo dhidi ya mashoga kama sehemu ya kisiasa. Kwani mashoga hawana haki ya kuwa na viwanja Tanzania? Ni lini tumesema kuwa mashoga hawana haki ya kuwa na tamasha lao!? Mbona yapo matamasha ya watu wazinifu au ngoma zote na burudani zinazofanyika Mafia zote zinafanywa na kufurahisha wana ndoa peke yao? Hili la mashoga labda limekuzwa sana na baadhi ya watu wamekuwa obsessed nalo kupita kiasi.

Na sijaona uhusiano wa hili la ardhi na suala hilo la mashoga.


Tangu lini Tanzania ikaruhusu kuwa na ma GAY PRIDE FESTIVALS?

Chukulia uongozi wa kijiji chenu waamue tuu kuwa na GAY festival ambalo lingejaza mambo mengi tuu ya ambayo si mila na desturi zetu wewe unaona wananchi watalichukulia ni sawa?


Hakuna anayebisha kuwa mashoga wapo lakini jiulize why Mafia and not Mbeya au Iringa kwa mfano

You might find it fine with GAY lakini haya mambo ya ki homosexual Mafia tumeyakataa na viongozi waliambiwa hilo lakini hawakutaka kuwasikiliza wananchi kama ambavyo sasa hawataki kuwasilikiza juu ya hili la ugawaji viwanja
 
LATEST FROM THE GROUND ZINASEMA HIVI:

Mbunge wa Mafia bwana Shah amesema ataenda kushtaki kwa JK kuwa watu wanamharibia jimbo na kumpakazia kachukua ardhi

Ukweli ni kuwa JK hato muentertain na upuuzi wake huuu na mbaya zaidi if anything kati ya hao waliopewa viwanja kiupendeleo ni Mke wake wa pili ambaye ni ndugu yake na ROSTAM! (hii mambo ya ufisadi kinda runs in the family I guess)

Mwenyekiti wa Council Mkewe wamepewa

Mbunge na mkewe (ndugu yake rostam) wamepewa

Madiwani 5 wamepata!
 
Mafia Kuna matatizo makubwa sana. Na haya mambo ya Uongozi mbovu yana historia ndefu kisiwani Mafia, tangu enzi ya Mwalimu Nyerere, ambapo yeye aliifanya Mafia kama detention spot. Kwaa wale woote ambao walikosana na utawala wake basi aliwapeleka mafia kama adhabu na sehemu ya kuwapoza wasisikike.

Baadaye Ikawa inatumika mafia kuwapeleka wafanya kazi wa serikali ambao wamefanya Makosa sehemu zingine za tanzania, ukipelekwa mafia maana yake umepewa adhabu, na ndiyo maana kisiwa hicho kikanyimwa fursa zote za miundombinu, kama viwanja vizuri vya ndege, barabara na bandari.

Lakini hivi sasa Mafia imegeuzwa kuwa ni sehemu ya kupeleka ndugu au marafiki wa viongozi wa juu ambao uwezo wao mdogo kuongoza, na hivyo wasingeweza kukubalika sehemu zingine za tanzania ambako wananchi wake ni waelewa wa mambo na wasiovumilia ujinga. Kwamfano, mkuu wa wilaya ya mafia hana sifa hata moja ya kuwa kwenye nafasi hiyo, anachokifanya mafia ni upumbavu mtupu, amefanya madudu lukuki, amelazimisha wanachi wa kijiji cha chole kuuza magofu ya serikali kinyume na sheria za nchi, ameuza kwa mzungu madarasa ya shule yaliyojengwa na nguvu za wananchi, nyumba ya mwalimu pamoja na soko, ameshiriki kusababisha migogoro ya ardhi sehemu mbalimbali kisiwani Mafia,anavunja sheria za hifadhi za bahari kwa kuvua kwenye maeneo tengefu(marine reserves), hivi ninavyoandika kwa taarifa rasmi ni kwamba, nyavu zake na vifaa vingine vya uvuvi vimekamatwa na marengers wa hifadhi viko chini ya mikono ya sheria,lakini anaforce apewe vifaa vyake! Na mengine mengi, kuna mdau mmoja jana alitaka kumtia vibao pale airport mafia kwa ujinga wake!

Kati ya watu wanaorudisha nyuma Kimaendeleo Mafia ni DC bwana Mangochie Manzie

Bwana Membe njoo umchukue mtu wako umpeleke huko kusini sie tushamchoka

DC anaandika mabarua ya ya kutetea mafisadi na ukiisoma ripoti ya mkaguzi mkuu wa mahesabu utaona ufujaji mkubwa unaendelea chini ya ofisi yake

Tusisahau kuwa yeye ndiye aliyeruhusu Tamasha la Mashoga Mafia, jambo ambalo najua fika asingekubali hili huko kwao umachingani
 
Haya madudu ya ubaguzi haya..

Information zinazoendelea ni kuwa on this Dr Dau ameonyesha uadilifu ambao viongozi wengi hawana

mfano jioni hii mkurugenzi wa halmashauri anahaha kutafuta watu wambembeleze Dr aende akapewe ardhi ili yaishe

na hapo ndugu yake (Muba) kapewa sasa katika hali ya kawaida Dr alitakiwa kuwa kimya lakini ameamua kulalamika kwani haki haijatendeka

as we speak Dr amekataa hii rushwa ya kupewa kiwanja ili yaishe
 
LATEST FROM THE GROUND ZINASEMA HIVI:

Mbunge wa Mafia bwana Shah amesema ataenda kushtaki kwa JK kuwa watu wanamharibia jimbo na kumpakazia kachukua ardhi

Ukweli ni kuwa JK hato muentertain na upuuzi wake huuu na mbaya zaidi if anything kati ya hao waliopewa viwanja kiupendeleo ni Mke wake wa pili ambaye ni ndugu yake na ROSTAM! (hii mambo ya ufisadi kinda runs in the family I guess)

Mwenyekiti wa Council Mkewe wamepewa

Mbunge na mkewe wamepewa

Madiwani 5 wamepata!
Hawakukosea walionena "siku ya kufa kwa nyani miti yote uteleza"
 
Ndugu ngwendu nikutoa mashaka, udini wa Dr Dau is beyond words! Ongea na watu NSSF watakueleza ujio wake hapo na mtazamo wake kuhusu 'makafiri'. Sick sick sick!

Sio kweli kama Dr Dau nimdini, huyo mleta mada anachuki binafsii zake na akutukanae hakuchagulii tusi,yeye aendele na kumpaka tope lakini ikosiku ukweli utabainika au kama anakithibitisho cha analoliongea aende mahakamani.......
 
Back
Top Bottom