DOWANS vs TANESCO - Why TANESCO Lost?

Tatizo kubwa ni kwamba kweli serikali ilijenga hoja nzuri za kuanzia lakini haikuwa na backup ya hoja hizo ni kama mtu ambaye hakujiandaa na kesi na badala yake wao wakawa wanasubiri majibu ya Dowans. Matokeo ya hili ni kuwa Dowans waliwagaragaza kama watoto wadogo katika mchezo wa chandimu.
 

Na wataendelea kuwagaragaza tu kama mchezo wa MAKIDA maana hapa naona TANESCO na serikali wanatafuta mahala pa kutokea ili isije ikaonekana kwamba kazini walikuwa wamelala ndo maana utasikia mara Uduwanzi/Dowans hatujui mmiliki wake, mara Dowans walitulaghai, mara Dowans wanataka hela nyingi... hizi zote ni kelele za mfa maji...

1. Pamoja na kwamba tumeshindwa katika hukumu hiyo kuna ulazima wa wazi mambo haya yawekwe na yaelezwe waziwazi na kwa lugha itakayoelekwa kwa wengi maana jamii inafaa ya wengi yafaa kujua nini maana halisi ya voidable na void contract, misrepresantion na Fraud katika Mikataba na mapungufu ya katiba yetu inayosema wazi au kutoa mwanya kwa Makampuni ya aina ya Ki-KIDOWANS kula kiulani.. Kipengere 19 (1) na 19 (2) cha misrepresantion yetu kimesema wazi kwamba contract haiwezi kuwa void.. hii inafaa ibadilishwe haraka sana...

2. Wanasheria wa TANESCO wajiuzuru haraka sana kwa kutojua wajibu wao na Due diligence ya kujua kana kwamba Richmond/Dowans hawawezi kazi na kwamba wao shida yao ilikuwa ku-sign tu mikataba na kutegemea kampuni nyingine ya Singapore kuja kuzalisha umeme...Mambo ya ajabu sana haya...

3. Haya ndio matokeo ya kufichaficha mambo... kama kila kitu kingewekwa wazi tangu mwanzo na hata kama tungeshindwa mbeleni haya ya kulalamikia malipo yangetokea wapi...

4. TANESCO hawana kesi na ndio maana Werema mjadara umefungwa bila kufafanua...

5. Mwisho kuna ambao wanasema kwamba ni lazima tulipe...mimi siwaelewi: Hivi Thamani ya TANESCO kwa sasa yaweza fikia hizo au kuzidi Bil 185? Kama jibu ni NDIO basi tulipe na kama jibu si ndio, cha kufanya ni kuji-declare bankrupt na hao Dowans wajue wa kumkaba maana kama nijuavyo mimi Serikali sio controling mind ya TANESCO na haiwezi kulazimishwa kuwalipia TANESCO... Kama TANESCO sio independent power supply company basi tujue kwamba kulikuwa hakuna sababu ya akina EWURA kuwa-regulate...

Please TANESCO go BANKRUPTCY AND START AFRESH ...IS THAT TOO MUCH TO ASK?
 
Atakuwa amejichanganya. Amefurahia kupata Document akasahau kuandika vizuri masaa

What he meant is "he still has two hours to wait before midnight, it got nothin to do with Tanzanian hours"
 
Mungu awabariki na kuwazidishia maisha mema ya furaha na amani. Tunafaidika sana na jitihada zenu za kutufunulia siri.

Happy New Year 2011.
 
Asante sna heri ya mwaka mpya wadau
ngoja niichukue nitasoma vizuri baadae jmni Pombe kweli si maji:teeth::teeth::teeth:
 
Mazingira ya ushindi kwa dowans ilikuwa ni
1. PPRA ilikuwa na weakness ambayo majudge walikubali kuwa japo tender haikuwa awarded na tender board ila Govt negotiation team wana mandate ..na ukiisoma sheria hii ya manunuzi unaona kabisa majudge 'waliamua' tu kuchukua weakness, sheria inasema 'nobody shall award tender without tender board' walioaward hawakuwa TB
2. Sheria ya texas inaruhusu kufungua kampuni under assumed name
3.Mkataba huu uliruhusu icc arbritation na si sheria za TZ
4.Walikubali dowans iliingia dubiously but argued kuwa kwao TZ ni kwa manufaa ya public iliyokuwa gizani, thus uwepo wa dowans ni benefit kwa waTZ
.....Nitaendelea....
 
Asante sana Invisible.

Hata kama document siyo kamili, ni wazi ya kuwa mazingira yote hayo yaliwekwa mapema ya TANESCO (na kwa hivyo TZ) kuliwa. Siyo ajali hata kidogo!

Never believe for a moment that all the bad contracts we entered into as a country were fruitous, but were deliberately so laid out. The real issue is how high this gets up to and why the higher authorities are always treating us mortal as kids- that this or that contract must be complied with without any heads rolling. I think we have a much bigger problem with this government than we dare imagine.

Dawa ni kuweka Serekali inayowajibika kwa watu madarakani, na ndipo swala la Tume Huru ya Uchahguzi na Katiba Mpya linapokuwa la kufa na kupona.

Angalia historia ya nchi hizi zote tunazoziita za kidemokrasia- zilifika hapo baada ya kufisadiwa sana, watu wakaamka na kuwapindua/ua wafisadi ndipo UHURU kamili ulivyopatikana.
 
Yaani, inasikitisha kama utetezi wetu wa Tanesco ndio ulikuwa hivyo. Hata ningekuwa mimi ningewakatalia hoja zao.

Mkuu MKJJ, ilishasemwa hapa..... wewe ulifikiri utani....... watu walijiandaa kushindwa..... inaonekana wazi kabisa kwneye hii document...... yaani..........basi tu!

Inauma sana
 

Sawa sawa Mkuu... Kamati ya Mwakyembe waliona hayo yote na ndio maana Rostam/Lowassa wanamtafuta kwa udi na uvumba, uliposikia Mwakyembe akilia hakuwa anacheza makida, na alivyosema kuna mengi aliyaacha i.e. hawakuweka kwenye ripoti, nafikiri sasa utamuelewa ni kwanini alisema vile......

Nimeisoma hii document, nikampata kisawasawa Dr. Mwakyembe na kamati yake; kwakweli walifanya kazi nzuri... Sijui Lowassa alikuwa anataka kujitetea/angejitetea kitu gani?

Otherwise heshima mbele Mkuu...


Kwa mara nyingine heshima mbele Mkuu..............Yaani watendaji kibao wa TANESCO inabidi waachie ngazi sio wanasheria peke yao...........

BTW hivi Accounting Officer alikuwa nani?.....................kwa kawaida Wizarani Accounting Offcer ni Permanent Secretary
 
Mkuu invisible asante ila sitashangaa baadae nisipoikuta humu.
 
Kama wiki leaks vile, hii nchi yetu sijui tunakwenda wapi. Asante mkuu!
 
naomba wataalamu wa washeria waidadavue hii hukumu na kutueleza/kutufafanulia vizuri maana mimi nimesoma lakini sijailewa vizuri.. nilichoelewa ni kuwa Rostam Aziz ana power of Attorney kwenye masuala ya DOWANS( Kifungu17.11 ukurasa wa 121).
 
Na kama ikieleweka naomba tuchukue hatua hata kwa maandamano ya amani humu humu jamvini
 
It is Shelukindo, Sitta na Kundi lao lililotufikisha hapa!

Tungeisikiliza TANESCO wakati ule na akina Zitto tungekuwa tunapata umeme sasa hivi... sasa umeme hakuna na pia tunatakiwa kulipa... sio kila kitu siasa wajameni.
 

Hapa huwa nachanganyikiwa na kazi ya hii kamati! Hawakuliona hili??

Mkuu MKJJ.......ilishasemwa hapa......wewe ulifikiri utani..................watu walijiandaa kushindwa...............inaonekana wazi kabisa kwneye hii document................yaani..........basi tu!......inauma sana

Mkuu Ogah! pole sana ni kilio cha wote, Kuna tatizo

1. Kufanya kazi kwa mazoea
2. Kutojua mikataba ya kimataifa
3. Kuzidiwa nguvu aidha kwa makusudi au bahati mbaya, ambapo naamini kabisa kwa shirika kubwa kama hili ni uzembe


Mkuu Ogah! Mwakyembe is responsible for this, tusitete watu wa aina yake

Kwa ufahamu wa Mwakyembe alitakiwa kuonya au
1. Aidha alikosa ushirikano wa ndani ya TANESCO
2. Aliwaamini kuwa alipoishia wao wateza
3. Au alijua wazi matokeo ya kesi hii na alishindwa atapambana nalo vipi. Na kama yuko serious na uzalendo he was supposed to speak out and alert Tanzanians the danger ahead! Leo angekuwa hero!

Lazima ifike muda professionals wawe accountable na matokeo yao,

Mwakyembe ameulizwa why this happened, au ndiyo yaleyale ya kuogopa baada ya kupewa uwaziri, OK, achilia mbali Mwakyembe hata mwanasheria nguli Sitta?

Bila kuwabana hawa watu tunaendelea na tabia hii, IFIKIE MUDA WATU KUKATAA KABISA kufanyika mgongo, while we are blaming Rostam we need to reveal this Network mpaka ngazi ya chini, watu tunaweka professionals mfukoni tunapofanya kazi serious kama hii.

Kibaya ni kuwa hawa wanasheria wa TANESCO HAWAKUPEWA NGUVU na serikali na backup za kutosha, kuna kila dalili wanasheria wa TANESCO waliuziwa mbuzi kwenye gunia na Dr. Rashid!
 
Naomba clarification hapa.... DOWANS head office ni Costa Rica..... Concern yangu ni... Je, establishment ya DOWANS hapa TZ ilikuwa under Company Ordinance (CAP 212) au DOWANS waliingia kama Offshore company....?
 
Kwa haraka haraka nilivyoiangalia hii document, PPRA ama hawakuishauri vizuri serikali, ama kulikuwa na njama fulani nyuma ya pazia...
 
MMILIKI au wamiliki wa DOWANS ni kina nani?
 
Kwa haraka haraka nilivyoiangalia hii document, PPRA ama hawakuishauri vizuri serikali, ama kulikuwa na njama fulani nyuma ya pazia...

mkuu... same as you..... PPRA walikuwa neglected na government through responsible ministry...... kwani waliamini TANESCO through its tender board wange implement PPRA procurement act properly.... lakini nahisi pale TANESCO hapakuwa na watu makini kwenye procurement Department ili waishauri tender board accordingly....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…