Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,103
- 43,350
Tatizo kubwa ni kwamba kweli serikali ilijenga hoja nzuri za kuanzia lakini haikuwa na backup ya hoja hizo ni kama mtu ambaye hakujiandaa na kesi na badala yake wao wakawa wanasubiri majibu ya Dowans. Matokeo ya hili ni kuwa Dowans waliwagaragaza kama watoto wadogo katika mchezo wa chandimu.
Atakuwa amejichanganya. Amefurahia kupata Document akasahau kuandika vizuri masaa
Mazingira ya ushindi kwa dowans ilikuwa niTatizo kubwa ni kwamba kweli serikali ilijenga hoja nzuri za kuanzia lakini haikuwa na backup ya hoja hizo ni kama mtu ambaye hakujiandaa na kesi na badala yake wao wakawa wanasubiri majibu ya Dowans. Matokeo ya hili ni kuwa Dowans waliwagaragaza kama watoto wadogo katika mchezo wa chandimu.
Yaani, inasikitisha kama utetezi wetu wa Tanesco ndio ulikuwa hivyo. Hata ningekuwa mimi ningewakatalia hoja zao.
Baada ya kuisoma Document hiyo nina haya machache..
1. TANESCO sijui kwanini hawakufanya Due diligence katika kujihakikishia kwamba; yes, Richmond au Dowans walikuwa hawawezi kazi na walikuwa wanategemea kampuni nyingine ya Singapore kwa ajili ya uzalishai umeme?
2. Iweje wakakubali au walikubali Richmond ajivue mzigo na kukabidhiwa Dowans? Hapa ndio mchezo ulichezwa na bao kufungwa..
3. Sijui kamati ya akina Mwakyembe na PhD zao hawakuyaona haya? Au huko shuleni walikuwa wanafundisha wanafunzi kukariri?
4. Katiba yetu inafaa ifanyiwe marekebisho katika kipengere hicho cha 19 (1) na 19(2) ILI Effect ya Fraud au misrepresantion iwe kwamba contract inakuwa Void na sio Voidable kama ilivyo English Law KWAMBA kama ni contract ni void, no void from the start (ab nitio) na kama ni voidable basi hii itategemea na seriuosness of the breach of warrant kama ni too serious basi contract is voidable...
5. MWISHO Wanasheria wa TANESCO yafaa wafukuzwe kazi kwa uzembe kwa kusinzia na kutofanya yale waliyotakiwa kufanya ili ku-defend interest za kampuni yetu na pia kwamba TANESCO ni lazima position yake ijulikane kama ni independent organisation with full autonomy to decide its own affairs na kwamba serikali sio controling mind ya TANESCO..
Iliyopo sasa kwa TANESCO ni kusema hatuwezi kulipa na kampuni inakuwa mfilisi na kuanza upya .. Full stop..
Na wataendelea kuwagaragaza tu kama mchezo wa MAKIDA maana hapa naona TANESCO na serikali wanatafuta mahala pa kutokea ili isije ikaonekana kwamba kazini walikuwa wamelala ndo maana utasikia mara Uduwanzi/Dowans hatujui mmiliki wake, mara Dowans walitulaghai, mara Dowans wanataka hela nyingi... hizi zote ni kelele za mfa maji...
1. Pamoja na kwamba tumeshindwa katika hukumu hiyo kuna ulazima wa wazi mambo haya yawekwe na yaelezwe waziwazi na kwa lugha itakayoelekwa kwa wengi maana jamii inafaa ya wengi yafaa kujua nini maana halisi ya voidable na void contract, misrepresantion na Fraud katika Mikataba na mapungufu ya katiba yetu inayosema wazi au kutoa mwanya kwa Makampuni ya aina ya Ki-KIDOWANS kula kiulani.. Kipengere 19 (1) na 19 (2) cha misrepresantion yetu kimesema wazi kwamba contract haiwezi kuwa void.. hii inafaa ibadilishwe haraka sana...
2. Wanasheria wa TANESCO wajiuzuru haraka sana kwa kutojua wajibu wao na Due diligence ya kujua kana kwamba Richmond/Dowans hawawezi kazi na kwamba wao shida yao ilikuwa ku-sign tu mikataba na kutegemea kampuni nyingine ya Singapore kuja kuzalisha umeme...Mambo ya ajabu sana haya...
3. Haya ndio matokeo ya kufichaficha mambo... kama kila kitu kingewekwa wazi tangu mwanzo na hata kama tungeshindwa mbeleni haya ya kulalamikia malipo yangetokea wapi...
4. TANESCO hawana kesi na ndio maana Werema mjadara umefungwa bila kufafanua...
5. Mwisho kuna ambao wanasema kwamba ni lazima tulipe...mimi siwaelewi: Hivi Thamani ya TANESCO kwa sasa yaweza fikia hizo au kuzidi Bil 185? Kama jibu ni NDIO basi tulipe na kama jibu si ndio, cha kufanya ni kuji-declare bankrupt na hao Dowans wajue wa kumkaba maana kama nijuavyo mimi Serikali sio controling mind ya TANESCO na haiwezi kulazimishwa kuwalipia TANESCO... Kama TANESCO sio independent power supply company basi tujue kwamba kulikuwa hakuna sababu ya akina EWURA kuwa-regulate...
Please TANESCO go BANKRUPTCY AND START AFRESH ...IS THAT TOO MUCH TO ASK?
Ingepatikana document nzima ingetuweka pazuri zaidihii doz haitoshi ongeza nyingine mkuu
Baada ya kuisoma Document hiyo nina haya machache..
3. Sijui kamati ya akina Mwakyembe na PhD zao hawakuyaona haya? Au huko shuleni walikuwa wanafundisha wanafunzi kukariri?
Iliyopo sasa kwa TANESCO ni kusema hatuwezi kulipa na kampuni inakuwa mfilisi na kuanza upya .. Full stop..
Mkuu MKJJ.......ilishasemwa hapa......wewe ulifikiri utani..................watu walijiandaa kushindwa...............inaonekana wazi kabisa kwneye hii document................yaani..........basi tu!......inauma sana
Sawa sawa Mkuu... Kamati ya Mwakyembe waliona hayo yote na ndio maana Rostam/Lowassa wanamtafuta kwa udi na uvumba, uliposikia Mwakyembe akilia hakuwa anacheza makida, na alivyosema kuna mengi aliyaacha i.e. hawakuweka kwenye ripoti, nafikiri sasa utamuelewa ni kwanini alisema vile......
Nimeisoma hii document, nikampata kisawasawa Dr. Mwakyembe na kamati yake; kwakweli walifanya kazi nzuri... Sijui Lowassa alikuwa anataka kujitetea/angejitetea kitu gani?
Otherwise heshima mbele Mkuu...
Kwa mara nyingine heshima mbele Mkuu..............Yaani watendaji kibao wa TANESCO inabidi waachie ngazi sio wanasheria peke yao...........
BTW hivi Accounting Officer alikuwa nani?.....................kwa kawaida Wizarani Accounting Offcer ni Permanent Secretary
Kwa haraka haraka nilivyoiangalia hii document, PPRA ama hawakuishauri vizuri serikali, ama kulikuwa na njama fulani nyuma ya pazia...