DOWANS (BEHIND THE SHADOWS): What you were not supposed to know...!

DOWANS (BEHIND THE SHADOWS): What you were not supposed to know...!

Tatizo hapo sio Mkataba mbovu au Mkataba Mzima. Tatizo hapo ni umeme! Umeme leo Tanzania hatuna wa kututosha na wakati wa kuingia hii mikataba tulikuwa desperate, Richmond wakafanya madudu, Dowans wakasema sisi tutafanya, wakafanya kweli, sasa hata ukiwa na mkataba ambao si mbovu, utakataa kuwalipa gharama zao? mitambo wameleta, wameijaribu, tena wameileta kwa haraka sana kuliko ilivyokuwa Richmond, halafu umeshapata mvuwa, huna tatizo la umeme, ukurupuke tu, useme sasa hatuihitaji hii mitambo! khaa, hiyo mahakama ipi itakayo kwambia haya umeshinda usilipe ondoka. Haiiingiiii akilini. Tuwe wa kweli.

Nadhani umekosa kuona nilichokuwa nakisemea:Nilichangia HOJA ya Ruta kuhusu ukinzani wa arbitration na Katiba. Maana yangu ni kuwa kilichopitishwa kwenye arbitration kitabakia final.

Kuhusu hii hoja yako kwenye bold ambayo ni nje ya kile nilichokuwa nakisemea, nasikitika kuona msimamo kama huu kwa mzalendo unless uwe siyo mzalendo.

Ina maana desperation itakufanya uue mtoto wako kwa vile tu unahitaji kitu fulani?
Kwani tusingeweza kupata deal nzuri zaidi ya hii inayotuingiza hasara ya mabilioni? Ni watu wangapi wangeweza kufaidika na pesa hizo tunazolazimika kulipa leo needlessly? Umeshajiuliza kwa mfano ni watu wangapi wanapoteza maisha kwa sababu ya kutokumudu gharama za matibabu ya magonjwa yanayotibika kirahisi tu?

Umeshajiuliza kwanini nchi yetu inaendelea kudidimia kwenye lindi la umasikini ilhali tumejaaliwa rasilimali za kila aina? Moja ya sababu kubwa ni uzembe wa namna hii - uzembe unaotokana na kutokujali kuweka maslahi ya taifa mbele!
 
Tafadhali angalia tena post ya awali kuna editing nimefanya na kuongeza document nyingine kuchangia clarity.
 
Napenda kukufahamisha kuwa the point was,ikiwa hawa watu wanaoweka transformer mara tano kwa ajili ya kuibiwa mafuta na hao ndio wanaamuwa kuwa hatulipi baada kuingia mkataba, kweli hawa ni watu wa kawaida hao?

Kuhusu Artumas, wala usiseme hilo, naijuwa Artunas kuliko unavyifikiria, tena nje ndani na for your information, sijui kama ushawahi kumsikia mtu anaitwa Tony (Anthony Lee) katika wa anzilishi wa hiyo Artumas, kama unamjuwa naweza kuendelea kuongea na wewe kuhusu Artumas, kama haumjuwi sina haja ya kukupa faida ya bure. Kuhusu subsidy, kama kweli ipo, basi hayo ndio mambo ya Kikwete, au na hilo litakukera?

Ewura iwepo kuweka kanuni na standards na kulinda maslahi ya consumers, hapo hatuna utata. Leo ji kampuni kama Tanesco, limekaa miaka yote hata asilimia 20% tu ya wa Tanzania imeshindwa kuwafikishia umeme, na hao inaowafikishia umeme hauna uhakika, si ndio hao wanaoanzisha mpaka nchi inaingia mikataba isiyokuwa na mpango.

Sasa huyo Mhando alikuwa hajui kama kuna transfomer ambazo ni Dry, mpaka akae abadili mpaka zifikie tano? kama si uzembe ni nini huo? halafu anajisifu kwenye TV kwa hoja kama hiyo!

Unafikiri hawa Tanesco wangekuwa competent kwa miaka yote aliokuwepo, leo tungisikia Dowans au Richmond au IPTL.

Yes, suala ni Dowans hapa na hao Dowans waliingia mkataba (ambao unatakiwa ulipwe) na nani? Au hujui kama ni Tanesco? sasa utaongea Dowansa usiwataje Dowans au waliingia mkataba na hewa? pole sana kwa umbali wako wa kuona.

Hiyo evidence uliyoitaka mwisho mimi sina wala hujanisikia nikiitaja.
Dsm nashindwa jinsi ya kujibu quote to quote hapa inatokea yote anaywas nikiweza nitajibu ila labda niweke in points

1. TANESCO ina mkataba na Tanalec wa kussply transformer kwa sheria ya manunuzi huwezi kubadili specs after issuing an order, so baada ya lot kuisha ndio waliomba zibadilishwe sije dry na kuna transformers aina ya takaoka ni msaada toka japan hizo ni fuel shirika haliwezi kuzikataa kwavile bado beo zipo juu

2. Kuhusu artumas simfahamu Tony Lee ila niliconsult mradi wa mnazi bay kwa miezi 2, niliandika PPA yao, ninafahamu wanapata subsidy toka hazina lengo ni kuvutia uwekezaji, sio kuwa sitaki, bali naonyesha si rahisi kama kila mtu anavyodhani kuwa mnaweza kuanzisha distribution companies

3. Kuhusu under 20% with access to electricity, mimi ni member wa SAPP ( Southern Power pool ) definition ya access ni hii, iwapo unamtaja mteja mmoja kuwakilisha % ya wananchi wote, ama unataja watakaonufaika na umeme ambao mteja mmoja amelipia? Tunadebate whether hiyo iwe ni x 4 people ( standard african hhold ) ama per person..

4.Kuihusisha TANESCO na kusema si competent kwa kuwa ni dowans ni kuionea, TANESCO waliikataa richmond na wakaomba kufanya international shopping...nina uhakika na ninachokiongea kwani kamati ya mwakyembe haikumnasa yeyote ndani ya tanesco kwa ufisadi...nimefanya kazi na wataalamu wa TANESCO katika levels tofauti na si kama hapa JF wanavyochukuliwa so repeat after me...hakuna mkataba wowote wa ppa tanesco iliingia bila serikali kuupitisha hata ukiwa umekataliwa kabla

5. Nilichokisema ni kile ulichoomba cha wafanyabiashara kurun tanesco, kumbuka kuna core business 3, kuna moja ambayo lazima serikali ihodhi, thts all, napenda sana watu wajue nishati ya umeme na simu au kukusanya kodi si sahihi kuvilinganisha

Lastly, this is a healthy debate and I would like us to explore facts bila kubezana wala kutumia kauli mbaya, japo mimi ni mtaalamu wa umeme bado waweza kunifundisha, so tafadhali tusibezane Eng Nsiande
 
Asante sana WoS, ndio maana mimi siamini kuwa hili ni matokeo ya bahati mbaya, kutokujua au kutokuwa na uwezo. Hakuna kitu chochote ambacho kilikuwa hakijulikani toka mwanzo. Nothing is new, ndio maana nimesema walipeni tu twende kwenye mkataba wa Airbus 320 tuwalipe.

Sikubaliani na wewe, sio kuwalipa na kuyamaliza. Suala ni namna gani tunakubali hizi standard arbitration provisions bila kuweka namna ya pa kutokea. Wanasheria wachache sana wa Tanzania wanajua masuala haya ya arbitration.
 
Dsm nashindwa jinsi ya kujibu quote to quote hapa inatokea yote anaywas nikiweza nitajibu ila labda niweke in points

1. TANESCO ina mkataba na Tanalec wa kussply transformer kwa sheria ya manunuzi huwezi kubadili specs after issuing an order, so baada ya lot kuisha ndio waliomba zibadilishwe sije dry na kuna transformers aina ya takaoka ni msaada toka japan hizo ni fuel shirika haliwezi kuzikataa kwavile bado beo zipo juu

2. Kuhusu artumas simfahamu Tony Lee ila niliconsult mradi wa mnazi bay kwa miezi 2, niliandika PPA yao, ninafahamu wanapata subsidy toka hazina lengo ni kuvutia uwekezaji, sio kuwa sitaki, bali naonyesha si rahisi kama kila mtu anavyodhani kuwa mnaweza kuanzisha distribution companies

3. Kuhusu under 20% with access to electricity, mimi ni member wa SAPP ( Southern Power pool ) definition ya access ni hii, iwapo unamtaja mteja mmoja kuwakilisha % ya wananchi wote, ama unataja watakaonufaika na umeme ambao mteja mmoja amelipia? Tunadebate whether hiyo iwe ni x 4 people ( standard african hhold ) ama per person..

4.Kuihusisha TANESCO na kusema si competent kwa kuwa ni dowans ni kuionea, TANESCO waliikataa richmond na wakaomba kufanya international shopping...nina uhakika na ninachokiongea kwani kamati ya mwakyembe haikumnasa yeyote ndani ya tanesco kwa ufisadi...nimefanya kazi na wataalamu wa TANESCO katika levels tofauti na si kama hapa JF wanavyochukuliwa so repeat after me...hakuna mkataba wowote wa ppa tanesco iliingia bila serikali kuupitisha hata ukiwa umekataliwa kabla

5. Nilichokisema ni kile ulichoomba cha wafanyabiashara kurun tanesco, kumbuka kuna core business 3, kuna moja ambayo lazima serikali ihodhi, thts all, napenda sana watu wajue nishati ya umeme na simu au kukusanya kodi si sahihi kuvilinganisha

Lastly, this is a healthy debate and I would like us to explore facts bila kubezana wala kutumia kauli mbaya, japo mimi ni mtaalamu wa umeme bado waweza kunifundisha, so tafadhali tusibezane Eng Nsiande

Jambo moja nakubaliana na wewe ni kuwa TANESCO hawahusiki kabisa na zabuni ya Richmond wala kufuta mkataba na Dowans. Kila kitu waliamuriwa na mamlaka za juu. Hawana lawama kabisaaaa.

ICC wanasema Richmond sio kampuni feki tofauti na Bunge lilivyoamua. Hili bado linanipa utata na nataka mwanakijiji atusaidie kesi iliyopo mahakamani texas ni ya dowans na richmond ipi?
 
Sikubaliani na wewe, sio kuwalipa na kuyamaliza. Suala ni namna gani tunakubali hizi standard arbitration provisions bila kuweka namna ya pa kutokea. Wanasheria wachache sana wa Tanzania wanajua masuala haya ya arbitration.

Nakupata vizuri sana;

Tofauti na watu wengine mimi siamini kuwa tumeingia kwa bahati mbaya kwa sababu haiitaji mtu uwe mkufunzi wa fizikia kujua implications ya vipengele vya mikataba unayoingia. Ndio maana binafsi ninaamini kabisa wanasheria wetu wanaoshiriki huko wanafanya wakijua kabisa. Na pale ambapo watu hawana utaalamu wa mambo fulani ndio wanatakiwa wapate consultancy ya wataalamu wa mambo haya. Kwa miaka yote hii tangu Loliondo hadi leo tunaposema kuwa hatuna wataalam wa kutosha wa mikataba au ujuzi wakati tumekuwa tukisisitiza uwekezaji ni almost oxymoronic.

Ndio maana miye pendekezo langu ni tuwalipe, na wakija Airbus tuwalipe, na wakija wengine nao tuwalipe hadi tutakapoona kuwa hizo fedha zinatuuma kweli na kuanza kuwawajibisha wale wote wanaotuingiza kwenye mikataba hii "mibovu". Kwani kilio cha "Mikataba mibovu" kimeanza leo? Mikataba mibovu si mikataba mibovu kwa bahati mbaya kwa sababu tungejua ubovu wake tungeweza kusahihisha lakini inaonekana hatusahihishi.

Tuwalipe yaishe si tumeingia wenyewe kwenye mkataba huo?
 
Jambo moja nakubaliana na wewe ni kuwa TANESCO hawahusiki kabisa na zabuni ya Richmond wala kufuta mkataba na Dowans. Kila kitu waliamuriwa na mamlaka za juu. Hawana lawama kabisaaaa.

ICC wanasema Richmond sio kampuni feki tofauti na Bunge lilivyoamua. Hili bado linanipa utata na nataka mwanakijiji atusaidie kesi iliyopo mahakamani texas ni ya dowans na richmond ipi?
Sijakuelewa ni "DOWANS na Richmond ipi?" unauliza kwa maana ya kwamba kuna uwezekano ni kampuni mbili tofauti zisizohusiana na Dowans na Richmond za Tanzania?
 
zitto... kama Richmond na DOWANS ... wanashitakiana na kuwa na misunderstanding pamoja na REDVCO consultant wa Richmond.... huoni kuwa hawa jamaa wana interest upon the weakness ya contracting party ..yaani TANESCO..... to me generally arbitration was a proof of a calculated risk ambayo DOWANS walifaulu...... sasa who is a scape goat....... we need to know this.... do we need to advance to punish the media..... media is just an authenticated investigative journalism and not thorough legal practice... dont blame editorial section of the media
 
Mzee Mwanakijiji,

Nakubaliana na wewe kwa asilimia 100%. If you try to connect the dots, utaona kwamba bado kuna utata au kuna kitu kimejificha kuhusiana na umiliki halali wa Dowans Tanzania Limited (DTL). Nimesoma kwa umakini hio Arbitration Award pamoja na hio kesi ya Dowans Holding S.A (DHSA) na Dowans Tanzania Limited (DTL) dhidi ya REDVCO nikagundua kwamba there is something hidden behind.

Ukisoma hio Arbitration Award ukurasa wa 127 utakutana na maneno haya:
Finally, an authenticated certificate of Incorporation of DTL is presented, as well as Memorandum and Articles of Association indicating that the main business will be as "… produces, suppliers and distributors of electric power…" The memorandum of Association lists Portek as one of shareholders of DTL.

Hapo inamaanisha kwamba Arbitrators waliona kwa mujibu wa Memorandum and Articles of Association za Dowans Tanzania Limited kwamba one of the shareholders wa DTL ni Portek

Lakini ukija ukasoma Original Complaint ambayo hao hao Dowans wamei-file kwenye kesi yao dhidi ya REDVCO inaoyesha kwamba Dowans Tanzania Limited ni kampuni inayomilikiwa kwa asilimia 100% na Dowans Holding S.A

Ukurasa wa pili wa Plaintiff (DHSA and DTL) Original Complaint unaonyesha unadhibitisha haya.
1. Plaintiff Dowans Holding SA is a foreign corporation organised under the laws of Costa Rica with its principal place of business outside of the United States.

2. Plaintiff Dowans Tanzania Limited is a foreign limited liability company organised under the laws of the United Republic of Tanzania with its principal place of business outside of the United States. It is wholly owned subsidiary of Dowans Holding SA


Hivyo ukiangalia hapa kwa umakini utagundua kwamba bado mpaka sasa umiliki wa Dowans Tanzania Limited ni kitendawili. Kwenye kesi dhidi ya Tanesco Dowans hao hao Wanasema Dowans Tanzania Limited moja ya wamiliki ni Portek wakati huo huo kwenye kesi ambayo wao wenyewe wameifungua dhidi ya REDVCO wanasema Dowans Tanania Limited inamilikiwa kwa asilimia 100 na Dowans Holding S.A. Hapa kuna utata mkubwa sana.

Kuhusu hii kampuni ya Portek ni kampuni inayojihusisha na mambo ya bandari na wala sio umeme, unaweza ukapata details zake hapa: Portek International Limited
 
Hii issue ni utata mtupu hivi hizi Dowans zote mmiliki wake ni mmoja? Are we dealing the same Dowans with different branches or are we dealing with different branches who chose to use the name Dowans?

Na ndio maana umiliki wake ni wa muhimu zaidi, you cant fight a battle without knowing your enemy
 
Mhafidhina, ukiangalia kwenye company structure ya portek hapo juu utaona wameonesha makampuni yote duniani ambayo wao wana shares hata kama ni asilimia 30.

Kwa miaka yote hii ambayo nimefuatilia ripoti yao hiyo (inayotoka kila mwaka na unaweza kupata kwenye Portek International Limited) hakuna mahali ambapo wameonesha kuwa wana umiliki wa asilimia 40 (kama inavyodokezwa na hukumu ya ICC) kwenye Dowans Tanzania Limited.
 
Clause 14. 1 (b).....ndiyo msalaba wa DOWANS.............................walikubaliana ya kuwa sheria za Tanzania ndizo zitaongoza usuluhishi na sheria zetu zipo wazi.........no contractual agreement ousting the jurisdiction of Tanzanian Courts will ever be entertained...............

Kwa hiyo vifungu vyote vinavyozuia Mahakama zetu kuchunguza haya makubaliano vinakinzana na katiba yetu.....i.e they are unconstitutional.....................and ought to be stricken out with costs...................

Nani atekeleze hilo na kesi imeisha?
 
Hapo umenena, hiyo ni haki ya msingi ya kila mtu, nami nikiwemo! Ingawa awamu ya kwanza ilitubana na katiba yetu! Unafikiri wakati wa Nyerere tungekuwepo hapa JF? duhhh, hata TV tulikuwa hatuna, magazeti ndio hivyo tena, Uhuru, Mzalendo na Ngurumo!

Halafu leo JMK mbaya!
Wee acha hizo pumba zako. JF wala mtandao haukuwepo enzi za Nyerere, sasa unategemeaje watu wandike kupitia JF ambayo haikuwepo?? JMK hakuleta huu uhuru wa kuandika humu bali ni mageuzi ya mtandao ndiyo yamesababisha haya.

Kwa taarifa yako JF imeanza kabla ya JK kuwa rais na watu waliandika sana toka enzi za serikali ya Mkapa enzi za BCS bila matatizo na bila kuogopa. Ni serikali ya awamu hii unayoisifia ndiyo iliifungia JF kwa siku kadhaa. Kama ulikuwa bado huijui JF by then muombe Invisible akupe taarifa badala ya kuanza kumwaga misifa bila kuwa na data.
 
Mnasoma na kulinganisha na kuanza kuuona ukweli au mnasoma kuridhisha the intellectual curiosity? Wanasheria wa Tanesco kama wanataka zaidi wanajua pa kutupata.. Ila nina mashaka nao..

mmh hawa jamaa balaa, yaani wanashtakiana wao kwa wao ? Dowans Vs Richmond Development Company RDEVECO?
 
nilikuwa kigali wiki iliopita wapendwa nikaongea na mwansheria mkuu aliniumiza kichwa sana
akasema yoote haya ni src ya kikwete akasema anafwatilia sana ila alichosema kimoja
kama hawa wakina lowassa na wengineo wangekuwa KGL basi israel aangekuwa anawakaribia
ama kifungo cha maisha....tanzania bana inachezewa sana m nimeena kule dodoma watu wana mashangingi mi sijaamini HUKU KAGAME KANYANGANYA MAGARI YOTE AALAFU WAKAPELEKWA TOYOTA KUCHAGUA WANAYOTAKA WAKAKOPESHWA NAKWAMBIA KILA MTU ANA ADABU NA GARI YAKE
MWISHO WA MWEZI UNACHUKUA VOCHA YA MAFUTA WIZARANI IKIISHA KABLA JUU YAKO UTAJUA PA KUONGEZEA MAFUTA NI HESHIMA BANA SIO HAWA BATU BAJINGA BANA CHEZEA NCHI WATU WANAANGALIA
 
nilikuwa kigali wiki iliopita wapendwa nikaongea na mwansheria mkuu aliniumiza kichwa sana
akasema yoote haya ni src ya kikwete akasema anafwatilia sana ila alichosema kimoja
kama hawa wakina lowassa na wengineo wangekuwa KGL basi israel aangekuwa anawakaribia
ama kifungo cha maisha....tanzania bana inachezewa sana m nimeena kule dodoma watu wana mashangingi mi sijaamini HUKU KAGAME KANYANGANYA MAGARI YOTE AALAFU WAKAPELEKWA TOYOTA KUCHAGUA WANAYOTAKA WAKAKOPESHWA NAKWAMBIA KILA MTU ANA ADABU NA GARI YAKE
MWISHO WA MWEZI UNACHUKUA VOCHA YA MAFUTA WIZARANI IKIISHA KABLA JUU YAKO UTAJUA PA KUONGEZEA MAFUTA NI HESHIMA BANA SIO HAWA BATU BAJINGA BANA CHEZEA NCHI WATU WANAANGALIA


Viongozi wangekuwa wanaajiriwa au kuazimwa, TZ tulistahili tuajiri au tumwazime huyu Bwana Kagame walau kwa mwaka mmoja tu aja atutengenezee nchi.
 
Dawa ni KUMKAMATA RA na kumshtaki kama MHUJUMU WA UCHUMI.

Unampa Songombingo hadi aseme wenzie ni nani.

Mambo yakiharibika, utasikia amekimbia sasa hivi au watam-Kolimba.

Jamaa ajihurumie nafsi yake na akiweza basi akimbie sasa hivi, vinginevyo, TISS wako nyuma yake.

Si rahisi, hii dunia nyingine si ya kina Marehemu Sokoine.
 
Hizo doc zinaonyesha JK ndo mmiliki? au mambo yanayoandikwa ni uzushi????

Uzushi mtupu! Kwani watu humu hata huyo RA wanamchukia kwa rangi yake na dini yake tu, hana biashara haram, zote legal deals. Wanausongo tu. Mbona kina nanihii, wenye biashara za haramu kikweli hatuwasikii kufatwa-fatwa!
 
Nadhani umekosa kuona nilichokuwa nakisemea:Nilichangia HOJA ya Ruta kuhusu ukinzani wa arbitration na Katiba. Maana yangu ni kuwa kilichopitishwa kwenye arbitration kitabakia final.

Kuhusu hii hoja yako kwenye bold ambayo ni nje ya kile nilichokuwa nakisemea, nasikitika kuona msimamo kama huu kwa mzalendo unless uwe siyo mzalendo.

Ina maana desperation itakufanya uue mtoto wako kwa vile tu unahitaji kitu fulani?
Kwani tusingeweza kupata deal nzuri zaidi ya hii inayotuingiza hasara ya mabilioni? Ni watu wangapi wangeweza kufaidika na pesa hizo tunazolazimika kulipa leo needlessly? Umeshajiuliza kwa mfano ni watu wangapi wanapoteza maisha kwa sababu ya kutokumudu gharama za matibabu ya magonjwa yanayotibika kirahisi tu?

Umeshajiuliza kwanini nchi yetu inaendelea kudidimia kwenye lindi la umasikini ilhali tumejaaliwa rasilimali za kila aina? Moja ya sababu kubwa ni uzembe wa namna hii - uzembe unaotokana na kutokujali kuweka maslahi ya taifa mbele!

That's my point, tungeweza, swali tulikuwa wapi? Toka Uhuru? Nyerere, Mwinyi, Mkapa? Leo, Kikwete ndie anatutatulia matatizo ya umeme halafu tunamuona mbaya?

Desperation sio ya mkataba ya umeme, na si kwa kuwa tupo desperate basi tuingie mkataba mbovu. La, hiyo sio point yangu. Point yangu ni kuwa, hata mkataba ungekuwa ni mzuri kama wewe, ndio tungeufuta na watu washaleta mitambo, tena inafanya kazi, haina hitilafu technically ina meet au hata zaidi specs zilizowekwa na "wataalam" wetu wa Tanesco, halfu umwambie mtu, basi mkataba na uishe. Halafu usimlipe halafu ukashinde kwenye mahakama? Sijawahi kusikia.
 
Back
Top Bottom