Kwa uelewa wangu, njia kuu za kuzalisha umeme au vyanzo vikuu vya nishati hii ni kama ifuatavyo nikianza na njia yenye LOWEST OPERATIONAL COST
1/UMEME WA NGUVU ZA NYUKLIA-Unatumia madini ya URANIUM ambayo tunayo na BUSH alikuja kuyamiliki!
2/ UMEME UTOKANAO NA NGUVU ZA MAJI-tayari tunao na kuna vyanzo vingi tu vinahitaji kuendelezwa/kuanzishwa kama vile mito ya Rufiji, Kagera, Mara, mawimbi ya baharini, kujaa na kupwa kwa maji ya baharini, mikondo (current) ya bahari n.k.
3/ UMEME UTOKANAO NA MAKAA YA MAWE - Tayari tunautumia inahitajika uendelezaji/uwekezaji zaidi ili tuyafaidi haya makaa yaliyopo Kiwira, Mchuchuma nk.
4/ UMEME UTOKANAO NA GESI ASILIA AU UCHAFU/KINYESI CHA WANYAMA - unatumika tatizo gesi ni yetu, lakini kuna ma-midlemans weengi kabla ya kuzalisha umeme wa gesi hivyo kuongeza gharama za uzalishaji/uendeshaji. Hebu fikiria gesi ya wa TZ, anaichimba SONGAS, inasafirishwa sijui na bomba za nani, ananunuwa DOWANS kuzalisha umeme na kumuuzia TANESCO ambaye anausafirisha n.k. hadi kwa walala hoi!! Kwanini asichimbe gesi TANESCO?
5/ UMEME WA MAFUTA YA PETROLI/DIESEL NK - Upo tangu enzi za Mwalimu.
6/ UMEME WA NGUVU ZA UPEPO - Unavuma kila mahala
7/ UMEME WA NGUVU ZA JUA - Unatumika nchi nzima hadi kwenye taa za kuongozea magari toka kwa wachina!!
Iweje sasa huyo Daktari wa falsafa ashindwe kupata ufumbuzi wa muda mrefu anafikiria GESI pekee?