Dowans: Another Richmond in making?

zitto bado yuko sahihi kwani ushauri wake hauna hisia kama wafanyavyo sitta, mwakyembe na wenzao.

ccm wana mambo yao na zitto amewashika patamu kwani tabia yao mbaya ya kuendekeza ushabiki kwenye masilahi ya nchi imepitwa na wakati.

zitto asonge mbele na maoni yake kwani hata ile ya buzwagi sitta alimkebehi na kumwadhibu kupitia genge laooooo.

kwa nn akina sitta na wenzao hawakemei mambo chungu mbovu yaliyomo zaidi ya dowans ila kwa kuwa hili wana masilahi bianafsi wanajifanya vinara???

mangapi ushabiki wa ccm unaendelea kukumbatia na sitta kama kada amayanyamaziaaaa...

Zitto waeleimishe kuwa hizo kamati sio siasa ni utendaji na utaalamu tena unaotakiwa kuwa muwazi kila mambo kwa mustakabali wa taifa letuuu..

kwa hili zitto anazidi kuijenga chadema kwa watu MAKINI.....
 

Heshima yako Mkuu.

Mimi nadhani suala la posho nalo ni muhimu likatizamwa. Kwani kamati ya bunge inapaswa kupewa posho na nani? kwa nini Tanesco waliwapa posho kamati ya Zitto? Je ilitoa posho pia kwa kamati ya Shelukindo? Je wamepewa posho kiasi gani? Posho ya mwenyekiti wa kamati ni tofauti na wajumbe wengine wa kamati? Kwa nini kamati ya Zitto (na zaidi Zitto mwenyewe binafsi) inaelekea ku'side' na MD wa Tanesco? Je ni hiyo posho peke yake au kuna zaidi?

Mwakyembe pia ameibua kitu kingine muhimu sana. Kwamba bodi ya Tanesco imekataa kununuliwa kwa mitambo ya Dowans. Bodi kisheria ndio iko responsible kwa uendeshaji wa kampuni. Dr. Rashid yeye ni nani hadi akatae maamuzi ya bodi ya Tanesco? Kamati ya kina Zitto mbona haikuwauliza kina Dr Rashid ni kwa nini wanataka kwenda kinyume na maamuzi ya bodi yao?

Sheria(na kanuni) ya manunuzi ipo wazi kabisa. Mitambo lazima iwe mipya, full stop.Lazima Tanesco waitishe tender na kama Dowans wanataka ku'bid', wa'bid' tu (sheria inasisitiza uwepo wa ushindani).

Kama kamati ya Zitto walipata data/maelezo ambayo yanawafanya watoe ushauri tofauti na ushauri wa kamati ya Shelukindo, nini kinawazuia kutoa ushauri huo. Kwani ni lazima ushauri wao ufanane na ule wa kamati ya Shelukindo hata kama wanatofautiana basis? Wanataka mjadala na kamati ya Shelkukindo, kwa kanuni ipi ya Bunge? Kanuni za Bunge zipo wazi ni nini wanatakiwa kufanya, kwa nini wantaka kupindishwa kwa sheria/kanuni? Wanatakiwa wapeleke taarifa yao Bungeni na siyo kujadiliana na kamati nyingine au kulalama kwenye vyombo vya habari.

Zitto anatuambia hatuhitaji kufahamu Dowans ni kina nani, tunahitaji mitambo tu bila kujali tunauziwa na nani. Hili si kweli. Je kama anaetuuzia hana mamlaka kisheria kutuuzia itakuwaje? Inashangaza kwamba amesahau yaliyotokea kwenye saga la Richmond. Moja kati ya hadidu za rejea za kamati ya Mwakyembe ilikuwa ni kupata ukweli juu ya nani ni mmiliki wa Richmond. Mpaka leo majibu bado hayaridhishi sana, at least to me.

Naamini Mhe. Zitto atajutia msimamo wake katika hili.
 
Last edited:

Ndugu yangu Nyauba, naweza kukubaliana nawe kwenye moja tu kati ya ninayoamini unamaanisha. Nalo ni kuwa, Zitto anayo haki ya kusema anachokiamini. Basi.

Mkuu, nimesikiliza mahojiano ya waheshimiwa wote watatu (Dr. W. Slaa, Zitto na Mwakyembe) kupitia ITV jana jioni. Nilichokiona kutoka kwao ni uelewa usiolingana wa issue iliyoko mbele yetu.

Mh. Dr. W. Slaa, alielezea jinsi anavyoona inafaa kushughulikia suala la manunuzi ya mitambo ya DOWANS. Alikuwa mwangalifu sana katika kauli zake. Ila ni dhahiri kuwa busara zake hazimtumi kukubaliana na mawazo ya Zitto katika kushughulikia suala hilo. Dr. Slaa alikwepa kukosoa moja kwa moja mtazamo wa mwenzake (Zitto) kuhusiana na suala hilo. Vile vile Dr. Slaa alielezea kama ambavyo imekuwa ikielezewa hapa JF na kuomba kupata maelezo zaidi ya reports za Kamati za Bunge (Madini na Nishati na Matumizi ya Umma) kuhusiana na sakata hili.

Mh. Zitto alinisikitisha sana. Maelezo yake yalikuwa yakipingana pingana kadiri alivyokuwa akiendelea kuzungumza. Alionyesha either kutokujua alichokuwa anakiongea, au kutokiamini alichokuwa akikisema. Kwa mfano, Mh. Zitto alisema "suala ni je, mitambo hiyo inafanya kazi au lah". Kwa mtazamo wangu, kufanya kazi au kutofanya kazi kwa mitambo ya DOWANS hakuifanyi ikubalike hasa kama inatakiwa kununuliwa kinyume cha sheria. Mitambo hata iliyo chakavu na inayouzwa duniani, pia inafanya kazi. Suala ni je tuko tayari kutupilia mbali sheria za nchi yetu kwa manufaa ya DOWANS? Kama jibu ni ndio. Swali la nyingeza tunalotakiwa kujiuliza ni "Kwa manufaa ya nani"?

Nakubaliana sana na maelezo ya Mwakyembe kuhusiana na issue ya TANESCO kukusudia kununua mitambo ya DOWANS. Mwakyembe alisema kuwa:
1. TANESCO wakitaka kununua mitambo hiyo wanaweza kufanya hivyo, kama wanavyofanya kwenye manunuzi mengine yote (Bunge halihusiki kuamua juu ya hilo)
2. Kamati ya Bunge (Nishati na Madini) haioni manunuzi hayo kuwa ni sahihi kwa kuzingatia mchakato mzima wa manunuzi hayo toka mwanzo (Richmond na sasa DOWANS). Mkataba uliorithishwa kwa DOWANS, ni batili na umevunjwa. Leo hauwezi kuwa halali bila kuusafisha.
3. Sheria za manunuzi ya umma zifuatwe ili kukidhi matakwa ya sheria.
4. Na mengine mengi aliyosema

Kwa maoni yangu, suala la manunuzi ya mitambo ya DOWANS litafufua tena scandal kubwa sana ambayo ilishaanza kufifia. Scandal hiyo haina manufaa yote zaidi ya kupoteza muda tu, na labda hatua za kisheria kuchukuliwa baadae kwa watakaohusika (hata kama itakuwa ni baada ya miaka 10).

Nadhani Zitto amejiingiza kwenye mtego mbaya wa kisiasa. Mtego ambao waliomwingiza ndio wanaofahamu madhara yake. Naamini hivyo kwa kuwa yeye ndie aliewaumiza kwenye scandals nyingi ikiwemo hii ya Richmond, Buzwagi n.k. Hivyo inawezekana wanataka aonje maumivu kidogo kabla uchaguzi haujafika, na hatimae apotee kisiasa. Kama mawazo yangu si sahihi, basi serikali ndio itakayokuwa inaingizwa mkenge na Zitto. Vyovyote iwavyo, kuna mmoja ataumia sana tu.

Naamini mtego anaoingia Mheshimiwa Zitto, si tu utamgharimu yeye binafsi kama mwanasiasa, bali pia chama chake ambacho hakionekani kuweka msimamo wake kuhusiana na suala hili.
 
nyambalaa

pia binafsi ningependa kufahamu ni kwa kiasi gani kamati ya nishati ya bunge imeweza kulisaidia shirika hili kiutendaji ili liweze kuwa na ufanisi zaidi hasa kwenye suala la kuondokana na mfumo wake wa sasa wa utendaji (generetaion, transmission and distribution of power).

pili uwezo mdogo wa kimenejiment unaotokana na unskilled labour, overstaffed,nk.

bottom line financial crisis inayoliumiza na kutishia uhai wa shirika hili kwanza kutokana na mfumo mbovu wa utendaji???

Halafu hizi kamati (nishati na mahesabu ya mashirika ya umma,), TANESCO, SERIKALI (WIZARA YA NISHATI) NA IKULU WANAFANYA MALUMBANO HAYA KWA AJILI/FAIDA YA NANI????????????????????????????????????????????
 
Usiku wa jana nilibahatika kuangalia ITV Channel,sina kawaida ya kusearch Tv za bongo mara kwa mara,Lakini jana niliipata bila kutarajia.Tumeskiliza taarifa ya habari, na kipindi kilichofuatia kikiendeshwa na Stephen Chuwa ambaye ndiye mwenyewe alikiandaa.Hakika nilijawa na hofu jinsi wabunge na spika wao walivyokuwa wanatupiana mpira kuhusu mitambo ya Dowans na TANESCO.Manunuzi , ununuzi,Kanuni ,kazi na sheria na Kamati za Bunge!!!
Tena nikaona pale Ikulu Bwana S.Rweyemamu na ufafanuzi wa alichosema Kikwete.Jamani kuna ubabaishaji gani wa kiasi hicho?Kila mmoja analo jambo la kuongea? Hatuna utaratibu wa kuendesha serikali,mamlaka,na vyombo vyake.Wana-JF Nisaidieni hapa!!
 
bado naunga mkono hoja ya zitto kushauri tununue mitambo kama tanesco walivyoshaurii.

Hii imetusaidia tena kujua upeo wa viongozi wetu(bunge na serikali) kwa mapana zaidiii.

Kuna upuuzi mkubwa hapa unaendekezwaaaa bila kujali heshima ya wananchi wanaoweka watu madarakani...

Wote sasa wanafanya show down...... Ujinga mtupuuuu

mpaka sasa kamati ya nishati, wizara na ikulu hawajitambuiiiii.....cheap popularity..

Inaumaaa sanaaaaa
 
bado naunga mkono hoja ya zitto kushauri tununue mitambo kama tanesco walivyoshaurii.

Inaumaaa sanaaaaa

Mbona tunaambiwa bodi ya Tanesco imekataa. Hiyo Tanesco ambayo wewe (na Mh. Zitto) mnaizungumzia ni ipi? Au ya Dr Rashid? Bodi ndiyo iko responsible kwa maamuzi ya Tanesco.
 
Last edited:
Mbona tunaambiwa bodi ya Tanesco imekataa. Hiyo Tanesco ambayo wewe (na Mh. Zitto) mnaitungumzia ni ipi? Au ya Dr Rashid? Bodi ndiyo iko responsible kwa maamuzi ya Tanesco.
MD wa tanesco ni sehemu ya bodi kwa hiyo natumai mapendekezo aliyoyatoa anawakilisha bodi yake pia.

kama hawasikilizani hayo ni matatizo yao kwani mimi wala zitto hatumo ndani ya bodi ila dr idrissa natumai ni mjumbe muhimu.

lengo la bodi ni kuona taasisi wanayoisimamia inasonga mbele kwa kutoa huduma bora (in case is service based org)...kama wanakinzana waangalie corporate governace ikoje kama wanaifuataa..

hapa jamani kwa sasa SIASA imetawalaaa zaidiiiiii...
pia kwa taarifa tuu mtendaji mkuu ndo bottom line mhusika mkuu wa success au failure za organization yake kwani yeye ndo mtaalamu zaidi ya bodi....
 

Hii nadhani ni Corporate Governance mpya!
 
hapa jamani kwa sasa SIASA imetawalaaa zaidiiiiii...
pia kwa taarifa tuu mtendaji mkuu ndo bottom line mhusika mkuu wa success au failure za organization yake kwani yeye ndo mtaalamu zaidi ya bodi....

Umesikia mashitaka ya kesi ya Liyumba? Mojawapo ni kufanya maamuzi bila kuishirikisha Bodi ya BoT.

Kusema kwamba MD/CEO ndiyo mhusika mkuu hapo ni kutudanganya mchana kweupe. Yeye yuko responsible kwa Bodi na wao Bodi kazi yao ni kupokea mapendekezo/taarifa za maendeleo ya shirika/kampuni na then wanaweza kutoa ushauri, kugoma ama kukubali utekelezaji wa mependekezo yaliyotolewa na MD/CEO.
 

Mkuu Nyauba, nilitegemea kusoma jinsi gani unavyounga mkono hoja ya Zitto kuhusiana na ununuzi wa mitambo kama TANESCO wanavyoshauri.

Ni kweli kuwa Saga hili limesaidia kutambua mengi kuhusu utendaji wa viongozi wetu. Kinachosikitisha ni kwamba wengi wa viongozi hao inaelekea kujali zaidi maslahi binafsi kuliko maslahi ya Taifa. Uzalendo katika nchi yetu uko chini kuanzia kwa viongozi hadi kwa wananchi na hii ndio sababu kubwa ya matatizo yetu mengi. Mchezo unaoendelea ni wa kisiasa. Nchi inaendeshwa kisiasa kuliko kitaalam. Kadiri muda unavyokwenda na kukaribia uchaguzi, tutashuhudia mengi zaidi yanayotia shaka. Wanasiasa wataumizana sana. Ila watakaoweza kupita kipindi hicho kigumu kisiasa watakuwa imara sana. Ukweli na uwakilishi mzuri ndio takaowawezesha wanasiasa ku-survive kipindi hicho.
 

Waandishi wazuri mko JF!. Safi sana. Ingependeza uchambuzi huu ukawekwa kwenye gazeti lisomwalo na wananchi wengi,wakaelimika.Saidia Umma kuyajua haya. Asante Mkuu
 
Jeuri ya sitta kuitingisha serikali inatoka wapi?? Je ni mtu makini mwenye misimamo isiyoyumba na kutaka kuona uhuru wa mihimili mitatu ya umma inaheshimiwaaa???

Au ni mwanasiasa aliyepofuka na siasa za muda mrefu na kujijengea himaya ya kutingisha wenzake(serikali) alioshiriki kwa karibu kuwafikisha (mtandao) hapo walipoo...

Kwa hili la richmond/dowans amekuwa kinara sana kuhakikisha serikali na wadau wake (fisadis) hawapati upenyoo...je ana ajenda ya siri??
 

Msome tena Mwanakijiji kuhusu hilo,hukumwelewa!!!
 
Recta.

ni kweli tupu maoni yako ila sasa tufanyeje kuondokana na KAULI na KUTENDA?
Binafsi naunga mkono msimamo wa Zitto/Tanesco katika hili kwa sababu tuu wao wanatusaidia kutambua uwezo wa wengine (kamati ya nishati na spika) katika kubishana, umaarufuuu kwenye masuala muhimu...

naomba mwongozo...hivi suala la kamati mbili kutoleana/kujibizana katika vyombo vya habari, pia Spika anajibu kupitia vyombo hivyooo....ni SAHIHI??

Sikufurahia tabia ya Spika (muhimili wa umma) naye kuitisha press conference bila hata kuongea na hao wanaolumbanaaaa....kuna tatizo..

Tusisahau pia tabia ya spika kubwatukaaaaaaa...
 
Wanabodi,
Asalaam Aleikum, Bwana asifiwe!
Ama kweli ukipotea JF siku moja ni sawa na mwaka mzima, mambo mengi yamenipita..Haya tena ya huyu Mh. Ngeleja mapya kwa mtindo wa Ulanguzi -Kibongo bongo.
Wakuu, nimesikia mahojiano na hakika nimebakia domo wazi pengine inawezekana kabisa Tanzania haina wasomi.. Huyu ni waziri tena mwanasheria!.. damn..
Moelex23, mkuu kama ulikuwepo yaani mchezo huu wa kuigiza wala hautakwisha kesho!.. mchezo wa kina mama _ Young and the Restless!

Jamani swala la Dowans linaeleweka wazi kuwa ni bomu haikuhitaji Sitta wala Mwakyembe kulizungumzia, ni wazi kabisa kwa mtu yeyote mwenye akili timamu..Kuendelea kudai hatuna hila ni UJINGA mtupu na ufinyu wa kufikiri na ndio maana kumbe Afrika tumeshindwa kuendelea sii kwa sababu ya kukandamizwa na nchi tajiri isipokuwa adui wa maendeleo ya mwafrika ni mwafrika mwenyewe..

Jamani, huwezi kutenganisha issue ya Richmond na Dowans kwa kutumia mitambo ambayo ndiyo sababu ya sisi kuwaita Richmond nchini..hatukuwa na biashara na Richmond wala Dowans isipokuwa kupitia mitambo hiyo...
Hivi niulize gari likiwa limeingizwa nchini na mtu ambaye hana visa ya kuingia nchini na inefahamika kuwa hata passport yake ni bomu, huyu mtu anaruhusiwa kuuza hilo gari! tena kwa serikali yetu na kuliwekea vikao vya kujadili..Kwa kitambulisho gani alichotumia aliponunua hilo gari huko nje ikiwa hata pass yake ni fake na kaweza vipi kuliingiza nchini! . Haya sii ndio sawa na ununuzi wa Vogue toka Uingereza auBenz toka South..kutaka vya bure!..
Hata kama tukiacha swala la dowans nje ya mjadala huu bado hakuna kati yetu anayefahamu nani mmiliki wa mitambo hiyo kati ya Richond, Dowans au kule ilikonunuliwa au kukodishwa..Yawezekana kabisa kuwa Dowans wamerithi mkataba wa Richmond kwa ku lease mitambo hiyo toka Richond.. Na kuna uwezekano mkubwa hao Richmond wenyewe walipewa mkopo na benki ktk ununuzi wa mitambo hiyo..hivyo bado sii mali yao wanalipia deni. Na bila shaka kutokana na muda mfupi hawajaweza kumaliza deni na nina hakika Dowans wasingeweza kuinunua mitambo hiyo kwa cash ktk kipindi cha muda mfupi kama ule..(kumbukeni mapendekezo ya Lowassa)....
Inaonyesha wazi kwamba viongozi wetu wanajaribu sana kutenganisha Dowans na Richmond au Dowans kama shirika na mitambo hii wakati wanashindwa kabisa kuelezea kuwa shida yetu ni UMEME sio mitambo ya Dowans..hivyo kuvuta fikra za watu wafikirie kwamba bila mitambo hii tutakuwa tumekwama...
Kichekesho, ni kwamba sidhani kama huyo Ngeleja anaweza kununua nyumba toka kwa mtu anayefahamu kuwa ni Tapeli na kuweka madai kuwa shida yake ni mahala pa kulala..Hata kama ukihitaji nyumba kiasi gani, kumfahamu mmiliki wa nyumba ni swala linalokwenda sambamba na manunuzi yote huwezi kutenganisha laa sivyo utafungiwa kanya boya,,
By the way nimeambiwa kuwa majuzi huyo waziri alionekana akiwa karibu sana na Rostam kabla ya kutoa taarifa yake ktk vyombo vya habari!..
 
Astakafilah, mafisadi hatimaye wamejua bei ya Zitto!!!! Mh Zitto hawezi kutudanganya kwa hilo la Dowans, akumbuke maneno ya Mh mwenzake

'WATANZANIA SI MABWEGE TENA' - Dk. H. Mwakyembe (MB) Kyela, Mbeya.
 

Sidhani kama ana ajenda ya siri. Ni wajibu wake.

Vyovyote atakavyofanya baadhi wataona ni tatizo. Akinyamaza atalaumiwa (ataulizwa yuko upande gani). Akikemea ununuzi,kitu kinachotarajiwa na wengi ndo kama hivyo ataonekana ana ajenda.

Ukweli ni kwamba watanzania wamebadirika hawadanganywi tena, wenye kutaka kuendelea na uongozi lazima wawe upande wao(wananchi) La sivyo...
 

Mkuu Nyauba, Kamati mbili za Bunge kukosoana hadharani si jambo la kujivunia. Ila kwa kuwa Kamati moja iliamua kwenda public katika issue hii, ilikuwa ni jambo lisiloshangaza kwa Kamati nyingine kujibu public pia. Kamati ya Matumizi ya Umma iliamua kutoa mapendekezo yake kwenye vyombo vya habari na si Bungeni kama ilivyotegemewa. Kamati ya Madini na Nishati isingeweza kujibu mapendekezo ya kamati ya Matumizi ya umma kupitia Bunge, kwakuwa haikufikishwa huko. Kumbuka wote hawa ni wana siasa na kuzungumza ndio siasa yenyewe. Hivyo hapo ndipo walipofikia.

Speaker wa Bunge kama alivyo kiongozi mwingine yeyote, anao wajibu wa kuingilia kauli za Kamati zake wakati wowote anapoona inafaa. Speaker ana vikao vyake maalum vya kupokea taarifa za Kamati. Sidhani kuwa ingekuwa ni busara kwake kukutana na Kamati hizo ili kuweka hali sawa. Kwakuwa hakukuwa na hali isiyo sawa, bali Kamati moja imepitiliza katika majukumu yake. Mh. Sitta katika press conf jana alisema hawezi kukaa na kukutanisha kamati hizo mbili. Sababu ni kuwa, kuna miongozo ya utendaji wa Bunge. Kamati ya Matumizi inatakiwa ipeleke taarifa yake kwa Kamati ya Madini na Nishati ili waipitie na kuona kama kuna haja ya kubadilisha mapendekezo yao kwa serikali kuhusuiana na manunuzi ya mitambo hiyo.

Kumbuka issue hii kama ingeachwa iendelee, ingeweza kulidhalilisha Bunge na serikali. Zaidi ya hayo, serikali na Bunge vingejikuta vikitofautiana sana katika vikao vya Bunge (ambavyo vina muda usiotosha kujadili kila kitu) badala ya kushughulikia mambo yenye maslahi kwa Taifa. Nadhani Speaker ametumia busara kutoa mtazamo wake na angalizo katika issue nzima (kama Kiongozi, Mtanzania na mpenda nchi yake). Serikali mara nyingi hujikuta ikiteleza kwenye mambo mengi. Hili ni mojawapo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…