Mh. Zitto,
Ni kweli ni kanuni na sio sheria. Nilisema kwenye post yangu uliyonukuu kwamba, kanuni ni sehemu ya hiyo sheria husika kwa kuwa zimetungwa kwa mujibu wa sheria mama, ndo maana zinatumika zote kwa pamoja katika taratibu za manunuzi. Utakubaliana nami kuwa kwenye taratibu za "tender" na matangazo hizo kanuni na sheria hutumika sambamba. Ndio maana kwenye matangazo huandikwa maneno haya hapa chini nanukuu;
"A consultant will be selected in accordance with the procedures set out in the Public Procurement Act No. 21 of 2004 and the Public Procurement (Goods, Works,Non-consultant services and disposal of public assets by tender) Regulations, 2005 Government Notice No. 97 of 15th April, 2005"
Kwa hiyo sheria na kanuni zinaenda pamoja na hazitenganishwi. Ukienda kinyume na kanuni ambayo imetungwa kwa mujibu wa sheria mama, unahesabika mkosaji. Katika kushughurikia mambo mbalimbali ya serikali, lugha hii hutumika sana kwamba je, " Sheria, Kanuni na Taratibu" zimefuatwa?
Mh. Zitto, tuendelee na mjadala.