Ben Saanane
JF-Expert Member
- Jan 18, 2007
- 14,580
- 18,222
mkuu mkandara na wengine, zitto amenishangaza mno na kwa kweli sababu sisi wote ni watoto wa mjini, hakuna njia bali kuconclude blackmail/corruption imetumika.
Halafu cha kushangaza mh. Zitto anasema yeye anasimamia ukweli na hayumbi kwenye utekelezaji na hata akibaki mwenyewe sawa. Hivi huyu mtu anaendesha shirika lake binafsi au ni dhamana hiyo wananchi tulimpa kwa kura? Yaani kuwa chairman tu wa kamati amekuwa arrogant hivi, eti kamati yangu blah blah!!! Hivi ni nini hiki??? Nkiki jamani??? Zitto anadhani msimamo wa mwanasiasa ni wa kwake binafsi au ni wa wananchi?? Unadhani obama anapenda gaza wapigwe mabomu au ni reality kuwa bila kusupport israel huwezi kuwa rais??
Sasa zitto na misimamo yako binafsi ungetusaidia kama ungejiuzulu huo uchairman wa hiyo kamati uliyopata sababu ni mpinzani wa serikali na wananchi tulikuweka juu, then ukeep misimamo yako binafsi, sio unatumia position uliyopata sababu ya wananchi kukuweka juu, halafu unawaambia wananchi wewe unajali uamuzi binafsi. kumbuka wabunge wengi wanaharibu lakini sisi hatujali sababu tunajua hao wabunge ni hovyo, but u and dr.slaa, huwezi jua disappointment na majonzi uliyotuletea sababu tuliwategemea mno, and then kwenye hili bado unatunyanyasa na kutupiga vijembe wakati tunajaribu kwa udi na uvumba kukusaidia wewe binafsi na position yako kwa wananchi wa tanzania. Sisi hapa tunajua hili litakumnaliza kabisa in the next few weeks na tunajaribu kukuomba kwa faida yako mwenyewe lakini mwenzetu sijui vipi.
jamani nimeweka manyanga chini na ni afadhali tutawaliwe na ccm milele maana
at least wao wametuonyesha hawatujali wala hawana haja ya mawazo yetu, kuliko hawa wapinzani waliotumia mgongo wa support kubwa ya wananchi especially sisi wasomi kuja juu, halafu hawajafika popote wameanza kuonyesha huu wazimu.
Hivi huyu zitto angekuwa na power ya utendaji kwa mfano tungepush serikali ya mseto na yeye ndio pm, si tungekoma.
Mimi nimeishiwa nguvu na kwa kweli tanzania tumekwisha.
Hichi kitu straight forward ambacho kila mtu mpaka wabunge wa ccm wanajua ni bomu, leo huyu tunayemwamini anatutukana na kungangania mambo ya ajabu.
Tufanye assumption kwamba sisi wananchi ndio tunamakosa na kweli dowans ni nzuri, je zitto haoni kuwa whether tuko wrong au right, bado tanesco haitapata hasara yeyote kubwa kwa kununua mitambo mipya kwa sababu even best case scenario dowans watafikia tu level ya mitambo mipya lakini hawawezi kuipita, lakini kama tuko right then dowans wataleta hasara. Sasa premise hii tu inaonyesha kungangania dowans kuna downside kubwa kuliko upside, na bado zitto anangangana, ama kweli tanzania hovyoooooooo including mimi mwenyewe.!!!!!!
Nik kweli kwenye taarifa za saa 2 usiku huko nyumbani Waziri Ngeleja amesema serikali wameiamuru Tanesco kutoshiriki kwenye zabuni ya ununuzi wa mitambo hiyo kufuatia ushauri wa kamati ya bunge.
Nadhani uamuzi wa awali ulichochewa na ushawishi wa watu fulani ambao wanaaminika kuimiliki Dowans; bila shaka ni mzimu wa Richmond bado unaiandama serikali.
Nashauri tu,tukitaka kuwa na consistent Debate,we must avoid childish speculation.
Kwanini tutangulize hisia za mtu kununuliwa? kwa mtindo huu,hatuwezi kuwa na mjadala wenye tija.Let us just dwell katika debate
Is being pragmatic means kununua zigo la lililiopatikana kifisadi? Kwa hiyo kamati yenu inakubaliana na ufisadi? Kisheria inakuwaje?
nimepata nafasi ya kuzungumza kwa kirefu na waziri wa nishati na madini mhe. William ngeleja kuhusu suala la ununuzi wa mitambo ya kuzalisha umeme ambayo inauzwa na kampuni ya dowans. Kuna mambo kadhaa ambayo bila ya shaka wengi wetu hatujayasoma kwenye magazeti au tumeyasoma akiwa amenukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari.
Kwa sababu sisi hatutafuti habari kutoka nukuu za waliosikia au simuliwe tunakwenda moja kwa moja kwa wenye habari wenyewe. Usikose kijarida cha cheche kesho na kusikiliza mahojiano hayo na bw. Ngeleja na uone kama na wewe unaweza kushawishika na msimamo wa serikali.
Snapshots:
- asema siyo lazima kununua mitambo ya dowans, ni ulazima wa hali ya mahitaji iliyopo
- asema dowans ndiyo wametangaza tenda ya kuuza mitambo yao hivyo sheria ya ppra inaingia kwa namna tofauti
- arudia suala la kununua mitambo iliyotumika, asema siyo 'geni'
- atolea mfano hali ya kiuchumi marekani na jinsi serikali ya huko ilivyoingilia hali ya uchumi wake..
Za zaidi sana...
ulipomuuliza kuwa, downs watatangazaje tenda ya kuuza mitanmbo amabayo inashikiliwa na serikali ili ije kuwa fidia pindi wakishindwa kesi waliyo fungua dhidi ya serikali kasema nini? Au na wewe maswali ayko leo yalikuwa ya kupangwa mzee.
Tutapenda tujue kabisa maswali uliyomuuliza na majibu yake vingine mchezo huu utakuwa unachezwa na watu wengi. Wenzio wametangulia inawezekana na wewe ukawa umefata, bila ya maswali uliyomuuliza, na majibu aliyotoa kuyaweka kwenye cheche hatutakuelewa.
Mwana kijiji, kama na wewe unataka kuwa Zitto, sema mapema tukuachie JF yako. Hashawishiki mtu hapa.
mbona una wasiwasi, mimi siandiki maswali wala majibu yake, utasikia mwenyewe haya mambo ya kunukuliwa ndiyo niliyoyakwepa. Kama kuna maswali ya ziada baada ya wewe kusikia niandikie halafu tutamtafuta kumuuliza tena.
Hakuna anayekataa option ya kununua mitambo mipya kabisa. Hakuna na hakna sehemu nimesema lazima Dowans. Unatukana wabunge kuwa ni ****** na flip flop? Natumai umeropoka tu katika hili.
Tupo wabunge makini, tumesoma vizuri na kuendele kujisomea na tunaelewa. TANESCO wamesema waziwazi kuwa mbadala wa kununua mitambo ya dowans ni kununua mitambo mipya kabisa.
Kamati ya Bunge imesema kamati mbili zikae na kujadili kupata mwafaka. Sijui la ziasa ni nini hapa.
Kama wanataka kununua mtambo mmoja chakavu kwa Tshs 70 billion kwa nini wasinunua toka GE mitambo 2 mipya kwa gharama hiyo hiyo wangepata 200MW badala ya 100MW. GE wanazo mitambo mipya tayari kwenye stock. kwa nini wanang'ang'ania mtambo chakavu toka dowan. Na dowan siyo manufacture wa hii mitambo, GE ni manufacture na wangepata na warrant for 5 years plus commissioning for another 30 years. shipping cost ya 100MW toka USA mpaka Tanzania by ship line siyo zaidi ya US$100,000.00. Pia kusoma hakumaanishi kwamba unaelewa na kukifanyia kazi, Chenge from Harvard Law Shool, si unaona madudu anayoyafanya, Dr. Rashidi wote hawa ni wasomi wazuri, angalia njisi walivyoshikwa kama kuku.
sasa huu ndiyo wasiwasi wenu.. ni kutokuwa open minded kama mtu hayuko tayari kushawishiwa. Mimi nimemsikiliza kwa kirefu na hajabadilisha msimamo wangu zaidi ya kuuthibitisha na kuuweka sawasawa.
Mtu makini atasema "i reserve my judgment hadi nimsikie" na baada ya hapo nitakuwa na picha ya kutosha kuweza kujua.
Wangapi wanajua kuwa Serikali haiwezi kutangaza zabuni au kuishindanisha Dowans katika suala hili kwa sababu habari zilizoripotiwa hazijaripotiwa kwa usahihi?
Suala la habari kutoripotiwa kwa ushaihi linawezekana(nina uhakika ndio hivy),maana baadhi ya waandishi wetu wa Tanzania tunawajua jinsi walivyo na uwaezo wa kupotosha habari/kupindisha ka malengo wanayoyajua wao...So let's wait and listen alichokisema Waziri Ngeleja