S. S. Phares
JF-Expert Member
- Nov 27, 2006
- 2,138
- 88
Susuviri,
Kwanza kabisa nianze na swali lako ambalo umeuliza kama Dorwan's ni kampuni ya Rostam na Lowassa..
Mkuu, nitasema:- NB:- Hapana KISHERIA, na Ndiyo KIUJANJA...
Kuna mchezo ambao unatumiwa na viongozi wa Tanzania pamoja na nchi nyingi maskini..
Kama ilivyokuwa Richmond, hutafutwa mtu wa kuaminika mwenye uraia nje ambaye anaweza kuwa Mbongo au mtu wa nje ambaye anaweza kufungua kampuni huko nje kihalali kulingana na deal lilipo Tanzania. Shirika hufunguliwa na wanahisa ndio hao viongozi wenyewe lakini hakuna kabisa mikono yao ndani ya shirika hilo. Hata hapo Bongo kina Manji, Load Rajpar, Jeetu Patel na wahindi wengine wengi tu wametumiwa ktk masdeal kama haya.. nadhani unakumbuka ile list ya Mob ya Mkapa na M Bank.. ni ktk mchezo huo huo.
Sasa tatizo la uharamu wa deal la Richmond KISHERIA sio mkataba wenyewe isipokuwa ni shirika lenyewe. Richmond ni kampuni hewa kama ilivyobainika lakini mkataba wake ulifuata sheria zote pamoja na kwamba hazikuwa for the interest of our Country, yet kisheria mkataba wenyewe ni genuine kama ilivyo mikataba mingine such as Barricks.. Sasa kufungiwa kanyaboya ktk mkataba na tukakubali na kuweka sahihi inatufunga sisi ktk Mkataba huo isipokuwa tu tatizo likaja kwa shirika lenyewe Richmond... Na kama unakumbuka Mh. dr Slaa alipoanzisha vagi la Richmond tulikuwa na kila haki kisheria kuvunja Mkataba kwa sababu kwanza walishindwa ku deliver kisha tukaja gundua kuwa halikuwa shirika halali Marekani wala Tanzania...
Kwa Ujanja ujanja bila kufuata sheria na haki tukapigwa changa la macho, mkataba kuhamishiwa shirika la Dorwans (Halali)ambalo pia tayari lilikwisha pangwa ili kuvuruga ushahidi wa Richmond kama shirika feki..
Inawezekana vipi kusaini mkataba na "kampuni hewa" halafu mkataba uwe na uhalali kisheria?? Mkataba hufanywa kwa kuaminiana kwamba wewe ni X na mimi ni Y na kwamba katika muda wa mkataba, X ataendelea kutimiza majukumu yake kama X, na Y vivyo hivyo. Ikija kubainika kuwa X alitumia ulaghai kujifanya yeye ni X wakati ambapo yeye ni Z basi mkataba uliowekwa kati ya X na Y si unakuwa batili moja kwa moja??
Mnaposema Mkataba unasimama kama "independent entity" bila kuunganishwa na Richmond nashindwa kuelewa...naombeni mifano mingine kama hii ambapo mkataba ulisimama hata baada ya kubainika upande mmoja ulidanganya.