Don't Shout Argue - Mbowe ameitendea haki falsafa hii

Don't Shout Argue - Mbowe ameitendea haki falsafa hii

Yule Mama kanifurahisha sana. Simuiti Mh. Yaani yupo mjengoni halafu hajui kinachoendelea!! Hawa watu wanachaguliwaje jamani tena anadai ni mjumbe wa kamati ya madini!!!!

Nami nimeshikwa na butwaa kuwa yule mama ni mjumbe wa kamati ya madini. Yeye na yule Ndasa sijui, wamejitambulisha pia kama wajumbe wa bodi ya nishati na madini, kweli kwa hoja kama zile??? Si ajabu mikataba yetu upande wa madini ni mibovu!
 
Wanaojua kusoma na kuandika tu. Ndo matokeo yake hayo.

Kwenye ishu nzito wanaongea wale, kwamba wale ni angalau au wengi wao wako vile?? Kuanzia Chombo, yule mmama, Ndassa, lusinde ni uozo mtupuu! Ni mwijage na yule wa mtwara ndo angalau waliongea kama wanaojitambua.
 
Una maanisha mama mmoja mwl.aliyesema 300bn -700bn=0,jina kama Mariam Msangi kama sijakosea,atakuwa viti maalum kutoka jiji kubwa kabisa Tz.

Ujue nimegundua kitu,vyama vya siasa ni mhimu sana kuwa na watu kama huyu mama,pamoja na kutokujua anachoongea lakini watu kama hawa hawezi ona aibu kuongea chochote atakachoambiwa hata kama hana uelewa hata kidogo suala husika.

Pamoja na Deo Filikujombe kutoa taarifa kwamba kodi ilisamehewa na AG,mama huyo alizidi kukazia eti kuwa TRA waende wakachukue tu kodi sababu alijicomiti

ha ha ha ha! mkuu ni hatari tupu, halafu eti ni mjumbe wa kamati nyeti ya madini!! kwa nini asingepelekwa kamati ya mzingira labda pangemfaa!!
 
Yule mama alikuwa mwl mkuu wa shule ya msingi Rangi tatu mbagala huko!!sio mbuge wa kuchaguliwa ni wale wa viti maalum.Elimu yake ni darasa la saba.

Ndio maana basi alikuwa anatetea kwa nguvu zote pasipo kujua nini kinaendelea.
 
Mchango wa Mheshimiwa Freeman Mbowe ni mchango bora kabisa ulio kuwa kwenye viwango vya hali ya juu kwenye mjadala wa leo, hoja murua zilizo chagizwa na vielelezo ambavyo vilimuacha hoi AG na akabaki kutikisa kichwa kukubali.
 
Wakuu wanaJF, Kwa siku ya Leo Nimefurahishwa kwa jinsi ambavyo Mbowe, Kafulila na Lissu walivyoweza kuwasilisha hoja zao kizalendo... Kibajaji Lusinde, Ndassa, Chambo, Kisangi hawastahili kamwe kurejea Bungeni! Hawa wamedhihirisha jinsi ambavyo matumbo yao yanatawala akili zao...
 
Hatuna haja ya kushangaa Mirabaha ya kijinga ya 4% kwenye madini ya Watanzania, Hatuwezi kushangaa Prof Mzima anakuwa dalali wa kuuza na kukwapua fedha za Wananchi via ESCROW a/c... Huyu Prof anajiona Mungu mbele ya vilaza kama huyu kisangi... RIP CCM...
ha ha ha ha! mkuu ni hatari tupu, halafu eti ni mjumbe wa kamati nyeti ya madini!! kwa nini asingepelekwa kamati ya mzingira labda pangemfaa!!
 
Hatuna haja ya kushangaa Mirabaha ya kijinga ya 4% kwenye madini ya Watanzania, Hatuwezi kushangaa Prof Mzima anakuwa dalali wa kuuza na kukwapua fedha za Wananchi via ESCROW a/c... Huyu Prof anajiona Mungu mbele ya vilaza kama huyu kisangi... RIP CCM...

watawala wamesha waona wananch ni mazoba.
 
Mbowe kazungumza vizuri alichemka anapotumia ung'eng'e confidence kwisha.

Bado uko utumwani sana. Ung'eng'e ni lugha yako wewe??
Akija mzungu hapa akibofoa kiswahili huwa analose confidence au ndiyo unazidi kumpapatikia akupakate vizuri?
 
Nashindwa hata kuandika kwa kweli, Mbowe kaonyesha njia, inauma sana nikifikiria Tanzania inakoelekea.
 
Siku zote namkubali mbowe, lusinde alimgusa lakini hajaangaika nae. Huwa anaongea kiuzalendo zaidi, maana ccm wote walikuwa kimya.

Lusinde wote tunamfahamu pia yeye mwenyewe kasema hakusoma hana elimu. UNategemea nini. Ila mipasho yake ilikuwa na nafuu kuliko hata engineer
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom