Don't Shout Argue - Mbowe ameitendea haki falsafa hii

Don't Shout Argue - Mbowe ameitendea haki falsafa hii

Kwa namna alivyoongea jana , naamini muhongo na wenzake wataondoka. Alitumia busara ya ajabu.
 
Mbowe nimemkubali, na Kafulila. mibunge ya ccm ni bogus inaropoka tu haina point

Mkuu Laki si pesa nakupongeza sana kwa kuweka ushabiki pembeni toka nikufahamu leo umenifurahisha sana Mkuu.tuache ushabiki wa hovyo tusiwachekee hawa wezi
 
Ukifuatilia wabunge wengi wa CCM waliopayuka jana wana uhusiano na kamati ya nishati na madini. Nadhani unaelewa kwanini walipayuka vile.....

ewaaaa,sio wana uhusiano ni kwamba wale ni wajumbe wa kamati ya Nishati na madini kwa zaid ya 90% waloongea jioni si walikua wakijinasibu,including mama kidawa mwalim wa sayansi kimu
 
Mbowe pamoja na elimu ndogo aliyo nayo ame mwaga fact, akika jamaa amejitofautisha na viongozi wengi wanao jadili watu badala ya vitu. hongera mbowe, japo mm sio chadema, mbowe kwa mara ya kwanza nime kuunga mkono.

Mbowe amemwaga nondo mpaka maprofesa na mainjinia wanainamisha vichwa kwa aibu, kweli tamaa mbaya sana kuliko wizi.
 
Mbowe anauwezo Mkubwa sana. Mbowe pekee ni serikali yote ya jk plus mafisadi wote kwa akili
Hilo ni wazi..hawa kenge wa CCM huwa anawaambia vitu,wanapuuza kwa vile hawaelewi hadi inapita miaka ndio wanakauja kurupuka.Aliwaambia kuhusu Money lundering long time...hayakusikia hata wahindi wakawa wanachoda dola zetu nchi inabaki tupu..mitanzania mingine miataani ikawa inawapa wahindi hela dolar mkononi eti wakawanunulie vitu ulaya kwa cash.Hadi Marekani wamekuja ndio mipuuzi inajiafanya kuwa inajua ubaya wa maoney laundering.Mengi alikuwa anatoa hela km Jukumu la kijamii kwa makampuni na fadhila binafsi na shukrani kwa mafanikio.Maccm yakaanza jenga hoja za kijinga km za mbunge wa magomeni.Leo ipo mbio kutamka hovyo neno CORPORATE SOCIAL RESPONSIBILITY?etc.Hayakujua wengine walishaona na kujua mambo siku nyingi na sasa wanazidi tambua mambo.
 
Alafu jamani suti aliyovaa pinda nayo.jana bungeni utafili Mbowe ndio aliyekuwa waziri mkuu
 
Mkuu Laki si pesa nakupongeza sana kwa kuweka ushabiki pembeni toka nikufahamu leo umenifurahisha sana Mkuu.tuache ushabiki wa hovyo tusiwachekee hawa wezi

una uhakika huyo ni laki si pesa?
 
Yanayoendelea bungeni, ni dhahili kwamba Watanzania tunadharauliwa na viongozi waandamizai wa serikali na wabunge wetu, hasa wa chama cha mapinduzi. Yani Mh. Mbowe pamoja na ujumbe na ushahidi mzito wa nyaraka aliouwasilisha juu ya Mh. Rais kuhusika moja kwa moja katika ukwapuaji pesa za escrow, pia kuthibitisha uwongo uliosemwa jana na waziri Muhongo juu ya mwanasheria wa TANESCO ndugu Ngwilima kwamba hakufukuzwa kazi bali aliaacha mwenyewe, mtu aliyekuwa mzalendo kwa kutoa ushauri usio na maslahi kwa wachache bali kwa taifa, kisha uzalendo wake kusababishia kufukuzwa kazi, bado watu, yaani wabunge wengi wa CCM hawashituki, wameendelea na utetezi wa hoja za kufundishwa ambazo hazihitaji elimu ili kujua kwamba wamefundishwa, hii ni dharau kubwa hasa kwa sababu sisi twaonekana ni wajinga sana na hakuna tuwezalo kufanya. Tuamke NDUGU, tumebakiza moja tu, halihitaji kuunganishwa na vyama vya siasa bali na utanzania unaopambana dhidi ya dhuluma hii. Tuingie BARABARANI TUU NA KUUKATAA UPUUZI HUU. Binafsi nawapongeza wabunge wote wateteao masrahi ya watanzania kwa utashi wao wote.
 
Mimi sina ushabiki. Ila kwa jana there was only who spoke for the benefit of the nation and that person is Mbowe. Tuache ushabiki inchi inaporwa. Mnao fikiri kutumia matumbo badala ya ubongo mtaona matokeo ya hili hapo mwakani.
 
Mbali na kwamba mbowe na kafulila waliongea kwa facts vizuri, pia mwenyekiti aliendesha mijadala fairly sana.
 
Mbowe did an excellent job...plus zitto plus kafulila
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom