Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,274
Wasaidizi wa ndani wanahitajika duniani kote. Nchi za Magharibi zimeboresha mikataba na maslahi ya wafanya kazi wa ndani, matokeo yake ni wachache wenye uwezo wa kuajiri wafanya kazi hao. Hao wachache wanaopata ajira wana mikataba ya kazi, likizo kila mwaka, malipo wakiwa wagonjwa, kiinua mgongo na mishahara inayo wawezesha kumudu gharama za maisha.
Oman na nchi za Kiarabu wanatoa ajira sana za wafanyakazi wa ndani kutoka Tanzania. Bahati mbaya kuna wanaopitia mateso. Wengine mpaka mauti yanawakuta. Hii imefanya mpaka Serikali kufanya upatikanaji wa ajira hizi kuwa mgumu.
Si wote wanapata mateso na kurudi nyumbani bila mafanikio. Kuna binti ninaemfahamu aliweza kuwajengea wazazi wake nyumba, kusomesha watoto na kupata mtaji wa kibiashara chake kutokana na ajira yake Oman iliyodumu kwa miaka 10.
Tatizo la ajira nchini ni kubwa sana. Kuna haja ya Serikali kufikiria jinsi ya kushirikiana na Serikali za nchi kama Oman. Kupitia Balozi zetu, wabobezi wa Human Resources na wanasheria waandae mikataba yenye tija kwa raia wetu.
1. Mwajiri alazimike kukata bima itakayofidia nauli ya mwajiriwa kama kutatokea manyanyaso.
2. Kuwe na HR officer Ubalozini atakayesikiliza kero za wafanyakazi, awe na uwezo wa kuongea na waajiri kama mwakilishi wa wafanyakazi.
3. Ajira zote zipitie Ubalozini na ikiwezekana Balozi ziweke matangazo kwenye redio na runinga kuwa wanaweza kukupatia wafanyakazi.
Kama kila ajira, $10 kila mwezi itabaki ubalozini, itafidia gharama za uendeshaji wa zoezi zima.
Oman na nchi za Kiarabu wanatoa ajira sana za wafanyakazi wa ndani kutoka Tanzania. Bahati mbaya kuna wanaopitia mateso. Wengine mpaka mauti yanawakuta. Hii imefanya mpaka Serikali kufanya upatikanaji wa ajira hizi kuwa mgumu.
Si wote wanapata mateso na kurudi nyumbani bila mafanikio. Kuna binti ninaemfahamu aliweza kuwajengea wazazi wake nyumba, kusomesha watoto na kupata mtaji wa kibiashara chake kutokana na ajira yake Oman iliyodumu kwa miaka 10.
Tatizo la ajira nchini ni kubwa sana. Kuna haja ya Serikali kufikiria jinsi ya kushirikiana na Serikali za nchi kama Oman. Kupitia Balozi zetu, wabobezi wa Human Resources na wanasheria waandae mikataba yenye tija kwa raia wetu.
1. Mwajiri alazimike kukata bima itakayofidia nauli ya mwajiriwa kama kutatokea manyanyaso.
2. Kuwe na HR officer Ubalozini atakayesikiliza kero za wafanyakazi, awe na uwezo wa kuongea na waajiri kama mwakilishi wa wafanyakazi.
3. Ajira zote zipitie Ubalozini na ikiwezekana Balozi ziweke matangazo kwenye redio na runinga kuwa wanaweza kukupatia wafanyakazi.
Kama kila ajira, $10 kila mwezi itabaki ubalozini, itafidia gharama za uendeshaji wa zoezi zima.