DOGMA ndio msingi wa dini ya ukristo

DOGMA ndio msingi wa dini ya ukristo

Quran Haina matini ya asili acha kudanganya watu

Hata hizo za sanaa na Birmingham zinatofautiana sana na Leo

Quran iliyopo Leo ni hii iliyoundwa na wahuni wachache wakiongozwa na mfalme Fuad wa misri 1924

Hiyo ya Uingereza haizingatiwi kwetu sisi.

Matini ya asili ya Qur'an tuko nayo mpaka Kiyama kinasimama, sababu sisi tuna chain ya upokezi mpaka kwa Mtume.

Nilikwambia tu kule ulete chain ya Matayo na utathibitishie nani aliandika Injili ya Matayo ukakimbia.

Usilinganishe Qur'an na Biblia kijana.

Huyo Mfalme DFuad hatajwi katika uandishwi wa Qur'an, shida huwa mnajitungia habari. Msome mwanazuoni aitwae al-Jazari, amedhibiti viraa saba na kuviandikia kitabu, Viraa ambavyo mpake kesho vinasomeshwa, unakuja kumtaja Fuad, hivi una akili wewe ?
 
miaka mingi baada ya Muhammad kufa,

Miaka mingi mingapi ? Qur'an ilikusanywa mwanzo kabisa na Swahaba Abu Bakar, nakala ikaenda kwa Swahaba Umar, Umar aliikabidhi kwa mwanae Hafs, aliposhika hatamu swahaba Uthman, ikachukuliwa toka kwa mtoto wa Swahaba Umar, ambaye alikuwa ameihifadhi, ndio zikaandikwa nakala 5 nyingine na kusambazwa katika miji ile mitano.

Lengo la kuandikwa ni kwa sababu ya vizazi vijavyo kwani kwa wao maswahaba walikuwa wameshaihifadhi moyoni. Kwahiyo angalia unachokiandika, hakikisha unakijua.
 
karne nyingi baadaye, na hata hizo zina tofauti katika usomaji (qira’at). Hivyo kusema kuwa maandiko haya yamehifadhiwa bila mabadiliko ni propaganda za Uislamu kama zile za Adamu alikuwa muislamu 🤣🤣🤣.

Karne nyingi ngapi ? Usiandike mambo jumla jumla ainisha.

Weka ushahidi na utuonyeshe hizo tofauti, usije kukimbia tena kama kawaida yako.

Maandiko yamehifadhiwa ndio maana mpaka viraa kumi vipo na vinasomeshwa, na ziada ya maneno sio Qur'an tu kuhifadhiwa bali mpaka Hadithi za Mtume zimehifadhiwa.

Maana ya kuhifadhiwa ni :
1. Kuhifadhi matini kama ilivyo pokelewa kwa Mtume
2. Uwepo wa sanadi (chain) ya upokezi ambayo haijakatika mpaka kwa mtume
3. Kuthibiti kwa usomaji kama alivyo soma Mtume
4. Uwepo wa viraa
5. Kujulikana kwa lolote la uongo linalo ongezwa au kupunguzwa katika Qur'an
6. Kuhifadhi maana kama alivyo fasiri Mtume, Maswahaba, Wanafunzi wa maswahaba na Maimamu.

Hii ndio maana ya kuhifadhiwa.

Sasa Adamu alikuwa Mkristo au Myahudi ? Sio tu Adamu, bali hakuna Mtume wala nabii wa Allah ambaye hakuwa Muislamu.
 
Mimi na wewe nan kakimbia ? Nenda kajibu maswali lukuki uliyozalisha ,hujajibu hata moja

Huwezi kunikimbiza na hautoweza, hakuna swali hata moja nililo kimbia na swali gani sijakujibu ? Ukiona sijakujibu ujue sijaliona au umerudia swali ambalo nimeshakujibu.
 
DOGMA ni kitendo Cha kuufanya uongo kuwa ukweli na kutumia Mbinu za kisaikolojia kukupandikiza huo uongo katika akili za watu

DOGMA ndani ya ukristo

1) wameaminishwa kuwa Yesu amezaliwa katika hori la kulishia ng'ombe wakati hakuna andiko linalosema hivyo

2) wameaminishwa kuwa ukristo ni dini wakati hakuna andiko linalosema hivyo

3) wameaminishwa kuwa Mungu ana nafsi 3 wakati hakuna andiko linalosema hivyo

4) wameaminishwa kuwa wakiwa na shida wamuombe Yesu wakati hakuna andiko linalosema hivyo

5) wameaminishwa kuwa Yesu ni Mungu wakati Yesu mwenyewe amekana kuwa yeye sio Mungu

6) wameaminishwa kuwa Mungu aligeuka kuwa mtu akacheza kombolela na watoto wenzake katika mitaa ya Galilaya

7) wameaminishwa kuwa ukristo alianzisha Yesu wakati maandiko na historia zinasema kuwa ukristo ulianzishwa baada ya Yesu kuondoka

8) wameaminishwa kuwa wakifanya ibada wasisujudu wakati maandiko yanawataka wasujudu na manabii wote walikuwa wanasujudu

9) wameaminishwa kuwa Yesu alisurubiwa Kwa ajili ya dhambi zao wakati maandiko yanasema Kila mtu atabeba mzigo wake

10) wameaminishwa kuwa msalaba ni neema Hadi wanavaa shingoni mwao wakati maandiko yanasema msalaba ni laana

11) wameaminishwa kuwa kuoa wake wengi ni kosa wakati hakuna andiko linalosema hivyo

12) wameaminishwa kuwa ukristo ulianzishwa nchini Jerusalem wakati maandiko yanasema ulianzishwa nchini ugiriki

14) wameaminishwa kuwa Injili ni kitabu Cha wakristo wakati hakuna andiko linalosema hivyo

15) wameaminishwa kuwa Paulo ni mtume wakati Yesu alisema yeye ndio mtume wa mwisho katika kizazi Cha Israel

16) wameaminishwa kuwa Jumapili ni siku ya ibada wakati hakuna andiko linalosema hivyo

Wazungu watu wabaya sana
Yaani eti Mungu ksmuumba binadamu kisha , Mungu huyu huyo azaliwe duniani kisha ateswe na kufa msalaba ni kwa ajili ya binadamu....

Ndio maana ukijadili na mkristo kuhusu hoja za kiimani haiufiki mwisho ...
Ni imani iliyojengwa ktk matamanio zaidi kuliko uhalisia...
 
Huwezi kunikimbiza na hautoweza, hakuna swali hata moja nililo kimbia na swali gani sijakujibu ? Ukiona sijakujibu ujue sijaliona au umerudia swali ambalo nimeshakujibu.
Nenda kajibu maswali mzigo kule ,🤣🤣
 
Karne nyingi ngapi ? Usiandike mambo jumla jumla ainisha.

Weka ushahidi na utuonyeshe hizo tofauti, usije kukimbia tena kama kawaida yako.

Maandiko yamehifadhiwa ndio maana mpaka viraa kumi vipo na vinasomeshwa, na ziada ya maneno sio Qur'an tu kuhifadhiwa bali mpaka Hadithi za Mtume zimehifadhiwa.

Maana ya kuhifadhiwa ni :
1. Kuhifadhi matini kama ilivyo pokelewa kwa Mtume
2. Uwepo wa sanadi (chain) ya upokezi ambayo haijakatika mpaka kwa mtume
3. Kuthibiti kwa usomaji kama alivyo soma Mtume
4. Uwepo wa viraa
5. Kujulikana kwa lolote la uongo linalo ongezwa au kupunguzwa katika Qur'an
6. Kuhifadhi maana kama alivyo fasiri Mtume, Maswahaba, Wanafunzi wa maswahaba na Maimamu.

Hii ndio maana ya kuhifadhiwa.

Sasa Adamu alikuwa Mkristo au Myahudi ? Sio tu Adamu, bali hakuna Mtume wala nabii wa Allah ambaye hakuwa Muislamu.
Tatizo huna elimu ,umeshadanganywa na wewe unataka kudanganya watu

Kwanza Kihistoria, Qur’an haikupokelewa na kubaki katika maandiko ya awali moja kwa moja kutoka kwa Muhammad, bali iliandikwa miaka kadhaa baada ya kifo chake, chini ya ukarani wa viongozi wa kisiasa (kama Abu Bakr na Uthman).

Wenyewe wanakiri kuwa kulikuwa na nakala tofauti zilizochomwa ili kubaki na toleo moja rasmi, jambo linaloonesha kulikuwa na utofauti wa matini. Hata “viraa” unavyosema ni ushahidi kuwa kulikuwa na tofauti katika usomaji, na si kielelezo cha uhifadhi mkamilifu.

Ukisema sanadi haijakatika, kumbuka sanadi ni simulizi za mdomo, na historia imetuonyesha simulizi za mdomo zinabadilika kulingana na mazingira na maslahi ya wapokezi.

Aidha, hoja kwamba “Adamu” alikuwa Muislamu ni kutoelewa historia ya imani.

Hakuna ushahidi wowote wa maandiko au wa kihistoria unaoonesha kuwa dini iitwayo “Uislamu” ilikuwepo kabla ya Muhammad. Maandiko ya kale Torah, Zaburi, Injili hayataji popote “Uislamu” wala Qur’an.

Adamu, Nuhu, Ibrahimu, Musa na manabii wengine walimwabudu Mungu wa Israeli, YHWH, na walifuata agano na sheria alizotoa, si mafundisho ya Muhammad yaliyokuja karne nyingi baadaye.

Mimi kama Mkristo, naamini na kufuata huyo Mungu ambaye manabii hao walimfuata, tofauti na wewe ambaye unamfuata Muhammad na mfumo uliokuja baada ya karne nyingi.

Uislamu haukuwahi kuwepo kabla ya Muhammad, na hakuna hata kipande cha maandiko ya kale, maandishi ya historia, au ushahidi wa akiolojia unaothibitisha vinginevyo.

Hata Quran yenyewe inakiri kuwa Muhammad ndiye wa kwanza kuleta mfumo huo wa kufuata sheria na ibada ulioitwa “Uislamu.”


Haya kimbia Tena na haya maswali 👇👇

Kwa nini hakuna hati ya kale kabla ya Muhammad inayotaja Uislamu?

Ikiwa Qur’an ilihifadhiwa bila kosa, kwa nini baadhi ya sura na aya zilipotea baada ya vifo vya wapokezi?

Kwa nini kulikuwa na haja ya kuchoma nakala za Qur’an ikiwa zote zilikuwa sawa?

Kwa nini hakuna hata manuskripti ya Qur’an kutoka zama za Muhammad iliyosalia leo?

Ikiwa Adamu alikuwa Muislamu, kwa nini hakuandika wala kufundisha Qur’an?
 
Huwezi kunikimbiza na hautoweza, hakuna swali hata moja nililo kimbia na swali gani sijakujibu ? Ukiona sijakujibu ujue sijaliona au umerudia swali ambalo nimeshakujibu.
Umekimbia na maswali hukujibu, kama mwanaume ,Rudi kule
 
Yaani eti Mungu ksmuumba binadamu kisha , Mungu huyu huyo azaliwe duniani kisha ateswe na kufa msalaba ni kwa ajili ya binadamu....

Ndio maana ukijadili na mkristo kuhusu hoja za kiimani haiufiki mwisho ...
Ni imani iliyojengwa ktk matamanio zaidi kuliko uhalisia...
Shida waislamu hamna elimu ya mambo ya roho, hata Quran yenu inasema hivo, nimekuwa muislamu kwa miaka zaidi ya 15+ ,hakuna dini imejengwa kwa uongo, propaganda,na misingi dhaifu kama uislamu,

Quran tu imejaa story za kuokota kutoka kwa wasabai, wakureshi wakipagani, na story za vitabu vya apokrifa vya wayahudi na wakristo waasi,

Quran ni kihitabu kidogo sana ,imagine kanakaribiana tu na kitabu cha Zaburi ndani ya biblia ,sasa unategemea humo upate elimu kuhusu wokovu?

Imagine Quran haimjui mke wa Adam ni nani, 😂

Quran ikiandikwa kwa font za biblia,ni sawa na ka notebook kadogo tu .

Unachokosa kuelewa ni kwamba katika imani ya Kikristo, Mungu si kiumbe mdogo anayeshuka duniani kwa lazima, bali ni Mungu mwenye uwezo usio na kikomo aliyeamua mwenyewe kuingia katika historia ya wanadamu ili kuokoa.

Si matamanio bali ni mpango wa Mungu aliye juu ya muda na nafasi, ambaye anaweza kuvaa mwili bila kupoteza uungu wake. Hata katika maandiko yako, Mungu anaingilia historia kwa namna ya kibinafsi kwa nini basi unashangaa akifanya hivyo kwa wokovu

Ikiwa Mungu hawezi kushuka duniani, je, ana mipaka ya uwezo wake?

Kwa nini maandiko ya manabii (kama Isaya 53) miaka 700 kabla ya Yesu yanatabiri wazi mateso ya Mpakwa mafuta kwa ajili ya dhambi za watu? Au tumuamini tapeli Muhammad?😂

Kwa nini unakubali kwamba Mungu alionekana kwa Musa kwenye kichaka kinachowaka moto lakini hukubali akija katika mwili?

Ikiwa Mungu hawezi kufa kwa mwili, kwa nini unadhani hawezi kutumia kifo kumshinda kifo?
 
Hiyo ya Uingereza haizingatiwi kwetu sisi.

Matini ya asili ya Qur'an tuko nayo mpaka Kiyama kinasimama, sababu sisi tuna chain ya upokezi mpaka kwa Mtume.

Nilikwambia tu kule ulete chain ya Matayo na utathibitishie nani aliandika Injili ya Matayo ukakimbia.

Usilinganishe Qur'an na Biblia kijana.

Huyo Mfalme DFuad hatajwi katika uandishwi wa Qur'an, shida huwa mnajitungia habari. Msome mwanazuoni aitwae al-Jazari, amedhibiti viraa saba na kuviandikia kitabu, Viraa ambavyo mpake kesho vinasomeshwa, unakuja kumtaja Fuad, hivi una akili wewe ?
Hakuna matini ya Quran na huna ,huwezi kuiona, Uislamu ndio dini ya ajabu ,dini mpya lakini Haina manuscript zake za asili, na zilizopo zote zinapishana na Quran hii ya Al Azhar University 1924 mnayoitumia Leo ,ndio maana Huwa tunaishia kuwacheka tu


Unaposema matini ya asili ya Qur’an ipo mpaka Kiyama, hiyo ni kauli ya imani, si hoja ya kihistoria.

Ukweli ni kwamba hakuna hata manuscript ya Qur’an kutoka zama za Muhammad.

Yale yaliyopo kama Topkapi manuscript (Istanbul)

Sanaa manuscript (Yemen),

Samarkand manuscript (Uzbekistan), na Birmingham fragments yote yameandikwa angalau miaka mingi sana baada ya kifo cha Muhammad, na yana tofauti nyingi na Qur’an ya leo hii ya 1924 hapo Al Azhar University 😂😂

Tafiti za kisayansi za carbon dating na textual analysis zimeonyesha tofauti za maandishi, herufi, na hata maneno.,Kwahiyo mnapodanganya watu Quran ilishuka ,sijui imehifadhiwa ,tunaishia kuwacheka tu

Qur’an unayosomea leo ni matokeo ya mchakato wa kisiasa, ambapo toleo la Misri lililopangwa chini ya Mfalme Fuad (1924), kupitia Al-Azhar University, ndilo liliidhinishwa rasmi na kusambazwa duniani, likifuta matoleo mengine.

Hata kabla ya hapo, Uthman alichoma nakala zote tofauti ili kubaki na toleo moja, jambo linaloonyesha kuwa kulikuwa na utofauti mkubwa katika fasihi simulizi mliyoita “sanadi.”

Fasihi simulizi yenyewe haiepuki kupotoshwa, kuongezwa, au kupunguzwa ndiyo maana mlihitaji kuchoma maandiko yasiyolingana.,mfano mzuri kwenye hizo mnaita Hadith,tukiwabana mnasema ni dhaifu 😂😂

Unapomtaja al-Jazari na viraa saba, hiyo ni kuthibitisha kwamba kulikuwa na njia tofauti za usomaji na baadhi ya viraa hivyo havipo tena, vingine havilingani kabisa na Qur’an ya leo.

Kwa hiyo si uhifadhi wa asili bali ni usalimishaji wa toleo lililochaguliwa kisiasa na wahuni wachache hapo Al Azhar University 😂


Ikiwa Qur’an ilihifadhiwa kikamilifu, kwa nini Uthman alihitaji kuchoma nakala nyingine?

Kwa nini hakuna hata nakala kamili ya Qur’an kutoka enzi za Muhammad?

Kwa nini Qur’an ya Misri (1924) ililazimishwa kuwa rasmi na kuondoa matoleo mengine?

Je, viraa vilivyo potea vilikuwa si sehemu ya “uhifadhi”?

Ikiwa sanadi haina maandiko ya asili, unathibitishaje kuwa haijabadilishwa?
 
Miaka mingi mingapi ? Qur'an ilikusanywa mwanzo kabisa na Swahaba Abu Bakar, nakala ikaenda kwa Swahaba Umar, Umar aliikabidhi kwa mwanae Hafs, aliposhika hatamu swahaba Uthman, ikachukuliwa toka kwa mtoto wa Swahaba Umar, ambaye alikuwa ameihifadhi, ndio zikaandikwa nakala 5 nyingine na kusambazwa katika miji ile mitano.

Lengo la kuandikwa ni kwa sababu ya vizazi vijavyo kwani kwa wao maswahaba walikuwa wameshaihifadhi moyoni. Kwahiyo angalia unachokiandika, hakikisha unakijua.
Wewe mbona kwenye uislamu ni mweupe hivi ?

Unachokieleza kuhusu kukusanywa kwa Qur’an na Abu Bakr, Umar, kisha kuhifadhiwa kwa Hafsa na baadaye kuchukuliwa na Uthman, si ushahidi wa uhifadhi wa asili bali ni ushahidi wa mchakato wa kuondoa utofauti uliokuwepo.

Hata wanazuoni wenu wanakubali kwamba Uthman alichoma nakala zote zilizotofautiana na alizozikubali. Hilo lina maana moja tu kulikuwa na maandiko na usomaji ambao haukuafikiana, na Uthman aliamua kisiasa na kijeshi ni ipi ibaki.

Sababu kuu Uthman akachoma nakala hizo ni hofu ya migawanyiko kutokana na tofauti za usomaji na matini (Bukhari, Kitabu cha Fadhail al-Qur’an).

Hii ni kukiri kwamba fasihi simulizi haikuwa na uthabiti wa asilimia 100. Historia imetufundisha kwamba simulizi za mdomo kila mara hupoteza uhalisia wake kadri muda unavyopita na watu wanavyoongeza au kupunguza kulingana na kumbukumbu au maslahi yao.

Halafu hao unaowaita wapokeaji si watu wasio na dosari.

Kuna Hadith zinazoeleza baadhi yao walikuwa wakinywa pombe mfano,

Sahih al-Bukhari 5582 (kisa cha walevi katika jamii ya maswahaba). Kuna pia Hadith kwamba Shetani alimshawishi Muhammad kusoma “aya za Shetani” (Sahih al-Bukhari 4862, pia katika Tafsir al-Tabari), jambo linaloonyesha kuwa hata chanzo kilihusiana na udanganyifu wa kiroho.

Zaidi ya hapo, baadhi ya wapokeaji wakuu wa Qur’an walifia vitani kabla ya maandiko kukamilika mfano vita vya Yamama vilivyomuua wapokeaji wengi, jambo lililomsukuma Abu Bakr kuanza mchakato wa kukusanya maandishi.

Ikiwa walikuwa wamehifadhi moyoni, kwa nini vifo vyao vilileta hofu ya kupoteza Qur’an?

Uhalisia ni huu , Fasihi simulizi haijawahi kubaki salama kwa karne nyingi bila maandiko ya awali. Ndiyo maana Uthman alibidi kuifunga katika toleo moja na kuchoma zingine.

Hiyo si hoja ya uhifadhi ni hoja ya kudhibiti matoleo.

Quran unayoisoma Leo imetoka kwa wahuni wachache hapo Al Azhar University 1924,

Fikiria Hadi Saudi Arabia walikosa manuscript halisi😂😂

ikabidi mwaka 1985 waikubali Quran ya hapo Al Azhar University 😂
 
Weka ushahidi na utuonyeshe hizo tofauti, usije kukimbia tena kama kawaida yako.
Hakuna dini Nyepesi kuijadili huku unakula au umekaa tu kama uislamu,sababu ni dini mpya ,ni dini ambayo Haina msingi thabiti ,ni dini imejengwa kwa uongo, propaganda na historia ya uongo,

Ni dini ambayo inaabishwa sana historia,AKIOLOJIA ,ni dini ambayo imevuruga sana historia ,so ni rahisi sana kuiweka kwenye mizania na kugundua ni FABRICATION tu ya mudy .

Nakupa mifano michache ya Qirrat tofauti kubwa ambazo hata tafsiri haziwezi kuficha

1. Surat al-Baqarah 2:184

Qirā’a ya Hafs (iliyotawala leo): فدية طعام مسكين (fidya ya kumpa chakula masikini mmoja).

Qirā’a ya Nafi’: فدية طعام مساكين (fidya ya kuwapa chakula masikini wengi).

Tofauti,neno la umoja vs wingi linaathiri idadi ya wanaopaswa kupewa fidya.


2. Surat al-Baqarah 2:222

Hafs: حتى يطهرن (mpaka wajisafishe).

Warsh: حتى يطهرن (mpaka wasafishwe tofauti katika umbo na maana).
Moja inamaanisha tendo la kujisafisha binafsi, nyingine kusafishwa na mwingine.


3. Surat al-Isra 17:102

Hafs: قال لقد علمت (akasema: Hakika umeshasema/umeshajua).

Kisā’ī: قال لقد علمتُ (akasema: Hakika nimejua).
Hii inabadilisha anayejua Musa au Firauni.


4. Surat al-Hadid 57:24

Hafs: هو الغني الحميد (Yeye ndiye Mwenye utajiri, Mwenye kustahiki sifa).

Hamzah: هو الله الغني الحميد (Yeye ndiye Allah Mwenye utajiri, Mwenye kustahiki sifa).
Maneno yameongezwa katika baadhi ya qirā’āt.


5. Surat al-Fatiha 1:4

Hafs: مالك يوم الدين (Mmiliki wa Siku ya Malipo).

Warsh: ملك يوم الدين (Mfalme wa Siku ya Malipo).
Mmiliki” na “Mfalme” si maneno yenye maana sawa.



MIfano ni mingi sana ,

Qirā’āt hizi zipo kwa sababu mchakato wa mapokezi ya Qur’an haukuwa wa maandiko ya awali yaliyothibitishwa moja kwa moja, bali wa simulizi na upokezi wa mdomo uliokumbwa na tofauti za lahaja na kumbukumbu.

Uthman alipochoma nakala zingine, hakuzifuta tofauti zote ndiyo maana leo bado kuna qirā’āt zinazotofautiana.
 
Maandiko yamehifadhiwa ndio maana mpaka viraa kumi vipo na vinasomeshwa, na ziada ya maneno sio Qur'an tu kuhifadhiwa bali mpaka Hadithi za Mtume zimehifadhiwa.

Maana ya kuhifadhiwa ni :
1. Kuhifadhi matini kama ilivyo pokelewa kwa Mtume
2. Uwepo wa sanadi (chain) ya upokezi ambayo haijakatika mpaka kwa mtume
3. Kuthibiti kwa usomaji kama alivyo soma Mtume
4. Uwepo wa viraa
5. Kujulikana kwa lolote la uongo linalo ongezwa au kupunguzwa katika Qur'an
6. Kuhifadhi maana kama alivyo fasiri Mtume, Maswahaba, Wanafunzi wa maswahaba na Maimamu.

Hii ndio maana ya kuhifadhiwa.
Wadanganye wasioujua uislamu na historia yake ,

Hao wapokeaji walikuwa WALEVI, WANAFIKI, WENGI WALIFIA VITANI ,

Sio maneno yangu ni vitabu vyenu 👇👇

Wapokeaji wa Qur’an walikufa vitani – kusababisha hofu ya kupoteza Qur’an
📜 Sahih al-Bukhari 4986
Zayd bin Thabit alisema


“Abu Bakr aliniita baada ya vita vya Yamama… Umar alikuwa naye. Umar alisema: ‘Vifo vingi vya wapokeaji wa Qur’an vimetokea kwenye vita vya Yamama, na ninaogopa iwapo vita kama hivi vitaendelea, sehemu kubwa ya Qur’an itapotea. Ninapendekeza ukusanye Qur’an.’”


Hii inaonyesha Qur’an haikuwa salama kichwani mwao kama mnavyodai vifo vyao vilihatarisha matini ya asili.😂

Baadhi ya Maswahaba waliokuwa sehemu ya wapokeaji walikunywa pombe
📜 Sahih al-Bukhari 5582 na Sahih Muslim 1980


Imepokewa kutoka kwa Anas bin Malik: “Nilikuwa nikimiminia kinywaji kwa Abu Talha, Abu Ubayda bin Jarrah, Ubayy bin Ka’b, Suhayl bin Bayda, na watu wengine. Pombe ilikuwa imeruhusiwa wakati huo, basi wakanywa… kisha Qur’an ikateremsha aya ya kuharamisha pombe.”


Hawa walikua wapokeaji na walimu wa Qur’an, lakini walikuwa walevi kabla ya aya fulani kushuka.😂😂

Hii inaonyesha hawakuwa “watakatifu wasiogusika” kama mnavyojaribu kuonyesha.


Hadith kuhusu Shetani kumtupia Muhammad “aya za Shetani”
📜 Sahih al-Bukhari 4862 na Tafsir al-Tabari (Surat al-Hajj 22:52)


“Mtume alipokuwa akisoma (Qur’an), Shetani alitupa maneno katika ulimi wake…”

Ikiwa Shetani aliweza kuingiza maneno kwenye ulimi wa Muhammad, hoja ya kuwa Qur’an ilihifadhiwa bila kosa inakufa kifo cha mende😂


Qur’an yenyewe inakiri baadhi waliokuwa karibu walikuwa wanafiki
📜 Surat at-Tawba 9:101


“Miongoni mwa wale walio karibu nawe wako wanafiki… hujui, sisi tunawajua.”


Ikiwa miongoni mwa waliokuwa karibu na Muhammad walikuwa wanafiki, ni dhahiri kuwa upokeaji wa simulizi haukuwa na ulinzi mkamilifu.


Halafu nakupa hii ulikuwa labda hujui Fasihi simulizi si salama kihistoria
Watafiti wote wa historia ya dini (ikiwemo Waislamu wa mwanzo kama Ibn Ishaq) wanakubali kuwa sababu kuu ya kukusanya Qur’an ilikuwa hofu ya kupotea kwake, jambo linaloonyesha kuwa njia ya simulizi pekee haikuwa na uhakika wa asilimia 100.

Sasa jiulize na kawaulize kina Sharif majini na firdaus

Ikiwa Qur’an ilihifadhiwa kikamilifu moyoni mwao, kwa nini kifo cha wapokeaji kilileta hofu ya kupotea kwake?
 
DOGMA ni kitendo Cha kuufanya uongo kuwa ukweli na kutumia Mbinu za kisaikolojia kukupandikiza huo uongo katika akili za watu

DOGMA ndani ya ukristo

1) wameaminishwa kuwa Yesu amezaliwa katika hori la kulishia ng'ombe wakati hakuna andiko linalosema hivyo

2) wameaminishwa kuwa ukristo ni dini wakati hakuna andiko linalosema hivyo

3) wameaminishwa kuwa Mungu ana nafsi 3 wakati hakuna andiko linalosema hivyo

4) wameaminishwa kuwa wakiwa na shida wamuombe Yesu wakati hakuna andiko linalosema hivyo

5) wameaminishwa kuwa Yesu ni Mungu wakati Yesu mwenyewe amekana kuwa yeye sio Mungu

6) wameaminishwa kuwa Mungu aligeuka kuwa mtu akacheza kombolela na watoto wenzake katika mitaa ya Galilaya

7) wameaminishwa kuwa ukristo alianzisha Yesu wakati maandiko na historia zinasema kuwa ukristo ulianzishwa baada ya Yesu kuondoka

8) wameaminishwa kuwa wakifanya ibada wasisujudu wakati maandiko yanawataka wasujudu na manabii wote walikuwa wanasujudu

9) wameaminishwa kuwa Yesu alisurubiwa Kwa ajili ya dhambi zao wakati maandiko yanasema Kila mtu atabeba mzigo wake

10) wameaminishwa kuwa msalaba ni neema Hadi wanavaa shingoni mwao wakati maandiko yanasema msalaba ni laana

11) wameaminishwa kuwa kuoa wake wengi ni kosa wakati hakuna andiko linalosema hivyo

12) wameaminishwa kuwa ukristo ulianzishwa nchini Jerusalem wakati maandiko yanasema ulianzishwa nchini ugiriki

14) wameaminishwa kuwa Injili ni kitabu Cha wakristo wakati hakuna andiko linalosema hivyo

15) wameaminishwa kuwa Paulo ni mtume wakati Yesu alisema yeye ndio mtume wa mwisho katika kizazi Cha Israel

16) wameaminishwa kuwa Jumapili ni siku ya ibada wakati hakuna andiko linalosema hivyo

Wazungu watu wabaya sana
Kweli ndio maana MAKOBAZI tunaganyagia mavi chooni lakini majini yanaendea kuswali .
 
DOGMA ni kitendo Cha kuufanya uongo kuwa ukweli na kutumia Mbinu za kisaikolojia kukupandikiza huo uongo katika akili za watu

DOGMA ndani ya ukristo

1) wameaminishwa kuwa Yesu amezaliwa katika hori la kulishia ng'ombe wakati hakuna andiko linalosema hivyo

2) wameaminishwa kuwa ukristo ni dini wakati hakuna andiko linalosema hivyo

3) wameaminishwa kuwa Mungu ana nafsi 3 wakati hakuna andiko linalosema hivyo

4) wameaminishwa kuwa wakiwa na shida wamuombe Yesu wakati hakuna andiko linalosema hivyo

5) wameaminishwa kuwa Yesu ni Mungu wakati Yesu mwenyewe amekana kuwa yeye sio Mungu

6) wameaminishwa kuwa Mungu aligeuka kuwa mtu akacheza kombolela na watoto wenzake katika mitaa ya Galilaya

7) wameaminishwa kuwa ukristo alianzisha Yesu wakati maandiko na historia zinasema kuwa ukristo ulianzishwa baada ya Yesu kuondoka

8) wameaminishwa kuwa wakifanya ibada wasisujudu wakati maandiko yanawataka wasujudu na manabii wote walikuwa wanasujudu

9) wameaminishwa kuwa Yesu alisurubiwa Kwa ajili ya dhambi zao wakati maandiko yanasema Kila mtu atabeba mzigo wake

10) wameaminishwa kuwa msalaba ni neema Hadi wanavaa shingoni mwao wakati maandiko yanasema msalaba ni laana

11) wameaminishwa kuwa kuoa wake wengi ni kosa wakati hakuna andiko linalosema hivyo

12) wameaminishwa kuwa ukristo ulianzishwa nchini Jerusalem wakati maandiko yanasema ulianzishwa nchini ugiriki

14) wameaminishwa kuwa Injili ni kitabu Cha wakristo wakati hakuna andiko linalosema hivyo

15) wameaminishwa kuwa Paulo ni mtume wakati Yesu alisema yeye ndio mtume wa mwisho katika kizazi Cha Israel

16) wameaminishwa kuwa Jumapili ni siku ya ibada wakati hakuna andiko linalosema hivyo

Wazungu watu wabaya sana
Umeongea vitu vya maana na vya msingi sana lakini ni wachache katika wao watayazingatia. Mkristo yeyote atakayetumia akili yake ataona kuna mambo hayako sawa katika dini yake.

Haya mambo watu wanayapuuza hapa duniani, lakini kwa hakika ile saa ya kufariki kuna majuto makubwa sana ambayo wale walio puuza watayakumbuka, lakini kwa wakati ule muda wa kuamini unakuwa haupo tena, pale ni malipo kwa yale uliyo amini na kutenda hapa duniani.

Mimi honestly nawapenda wakristo ni watu wazuri tu na ni wema ukiondoa wachache wabaya ambao hata katika uislamu pia wapo. Ninatamani sana hawa ndugu zetu waongoke na wajue ukweli wa dini yao na wajue kuwa Yesu sio Mungu na wamuamini Mungu wa kweli. Lakini sasa anaye muongoza mtu ni Mwenyezi Mungu tu, kama mtu akitumia akili yake na akimuomba Mungu amuongoze bila shaka Mwenyezi Mungu atamuongoza.
 

Mwenye macho na aone, mwenye masikio na asikie


QURAN 4: 157-159

157. "Na kwa kusema kwao: Sisi tumemuuwa Masihi Isa, mwana wa Maryamu, Mtume wa Mwenyezi Mungu. Nao hawakumuuwa wala hawakumsulubu, bali walifananishiwa tu (wakamuua mtu mwingine). Na hakika walio hitalifiana katika haya wamo katika shaka nayo. Wao hawana ujuzi nayo wowote, ila ni kufuata dhana tu. Wala hawakumuuwa kwa yakini .

158. Bali Mwenyezi Mungu alimnyanyua Kwake, na hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye hekima.

159. Na hakuna yeyote katika watu wa Kitabu (Wakristo na Mayahudi) ila ataamini ukweli huu kuhusu yeye (Isa) wakati wa kifo chake (kabla ya kutoka roho). Naye Siku ya Kiyama atakuwa shahidi juu yao"
 
DOGMA ni kitendo Cha kuufanya uongo kuwa ukweli na kutumia Mbinu za kisaikolojia kukupandikiza huo uongo katika akili za watu

DOGMA ndani ya ukristo

1) wameaminishwa kuwa Yesu amezaliwa katika hori la kulishia ng'ombe wakati hakuna andiko linalosema hivyo

2) wameaminishwa kuwa ukristo ni dini wakati hakuna andiko linalosema hivyo

3) wameaminishwa kuwa Mungu ana nafsi 3 wakati hakuna andiko linalosema hivyo

4) wameaminishwa kuwa wakiwa na shida wamuombe Yesu wakati hakuna andiko linalosema hivyo

5) wameaminishwa kuwa Yesu ni Mungu wakati Yesu mwenyewe amekana kuwa yeye sio Mungu

6) wameaminishwa kuwa Mungu aligeuka kuwa mtu akacheza kombolela na watoto wenzake katika mitaa ya Galilaya

7) wameaminishwa kuwa ukristo alianzisha Yesu wakati maandiko na historia zinasema kuwa ukristo ulianzishwa baada ya Yesu kuondoka

8) wameaminishwa kuwa wakifanya ibada wasisujudu wakati maandiko yanawataka wasujudu na manabii wote walikuwa wanasujudu

9) wameaminishwa kuwa Yesu alisurubiwa Kwa ajili ya dhambi zao wakati maandiko yanasema Kila mtu atabeba mzigo wake

10) wameaminishwa kuwa msalaba ni neema Hadi wanavaa shingoni mwao wakati maandiko yanasema msalaba ni laana

11) wameaminishwa kuwa kuoa wake wengi ni kosa wakati hakuna andiko linalosema hivyo

12) wameaminishwa kuwa ukristo ulianzishwa nchini Jerusalem wakati maandiko yanasema ulianzishwa nchini ugiriki

14) wameaminishwa kuwa Injili ni kitabu Cha wakristo wakati hakuna andiko linalosema hivyo

15) wameaminishwa kuwa Paulo ni mtume wakati Yesu alisema yeye ndio mtume wa mwisho katika kizazi Cha Israel

16) wameaminishwa kuwa Jumapili ni siku ya ibada wakati hakuna andiko linalosema hivyo

Wazungu watu wabaya sana
Kwakuwa sisi ni Wakristu, basi tunaamini katika mafundisho ya Ukristu kupitia madhehebu mbalimbali. Wewe ambaye huyaamini ndio maana sio Mkristu.
 
Fanyeni kaz mlipe kodi msipoteze muda huko dinini hakunaga mwafaka.
 
Back
Top Bottom