Dodoma: Pamoja na katazo la Kiongozi wao, Wabunge kadhaa wa CHADEMA wakiwemo Silinde na Lijualikali wahudhuria bungeni

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,810
11,980
1588594688530.png

Wabunge wawili wa Chadema, David Silende (Momba) na Peter Lijualikali (Kilombero) wamehudhuria bungeni leo licha ya chama chao kuwataka wabunge wake kutohudhuria vikao vya Bunge ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona
1588594582130.png

Mbunge wa Kilombero (Chadema), Peter Lijualikali,

Hivi karibuni Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya amesema kutokana na hali ya Corona kuwa mbaya, Kwamba wabunge wa Chadema walikubaliana kutohudhuria Bungeni na wamekubaiana kujeweka Karantini.

"Hali ya Corona ni mbaya sana, wabunge kupitia Chadema, leo tumefikia makubaliano ya kutoingia Bungeni na kila mbunge kubaki nyumbani kwake Dodoma, niwatake wananchi huko mlipo mchukue tahadhari kubwa." alisema Bulaya.
1588594385704.png

Mbunge wa Momba kwa tiketi ya CHADEMA , Silinde Ernest David

Pia soma: Wabunge wa CHADEMA wakubaliana kutohudhuria tena vikao vya Bunge kutokana na janga la COVID-9, Kujiweka Karantini kwa wiki 2 - JamiiForums

Kufuatia wabunge wa CHADEMA kwenda Karantini, Spika Ndugai amshukia Mbowe kama mwewe - JamiiForums
 
Siasa ni maisha yao na ndio mustakabali wao, kwa kipindi hiki akili kichwani kumfuata Mbowe ama Serikali.
 
..waliosema Mbowe ni dikteta wameumbuka.

..waliosema Mbowe anawaburuza wabunge wamekosa hoja.

..waliosema ndani ya CDM hakuna demokrasia na uhuru wa mawazo watajificha wapi?
 
Back
Top Bottom