Dkt. Mpango awaalika SADC Kutuma Timu ya Uangalizi wa Uchaguzi

Dkt. Mpango awaalika SADC Kutuma Timu ya Uangalizi wa Uchaguzi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
WhatsApp Image 2025-08-16 at 15.28.34_269ad64a.jpg

WhatsApp Image 2025-08-16 at 15.28.34_f9d97d6b.jpg
Makamu wa Rais wa Tanzania, Dr. Philip Isdor Mpango amesema kuwa maandalizi muhimu kwa ajili ya kufanya uchaguzi mkuu wa haki, huru na wazi yanaendelea vizuri nchini Tanzania na kutoa mwaliko kwa SADC kutuma timu ya waangalizi kwenye uchaguzi huo uliopangwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Dkt. Mpango ametoa wito huo wakati anasoma hotuba ya ufunguzi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama jijini Antananarivo, Madagascar Agosti 16, 2025.

Dkt. Mpango ambaye anamwakilisha Rais Dr. Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano huo ametaja mafanikio kadhaa ya uenyekiti wa Tanzania katika Asasi hiyo, iliyopewa jukumu la kusimamia masuala ya ulinzi, amani na usalama katika kanda ya SADC.
WhatsApp Image 2025-08-16 at 15.28.37_0b7765aa.jpg

WhatsApp Image 2025-08-16 at 15.28.47_6cbfa1e8.jpg
Akibainisha mafanikio hayo, Dr. Mpango alieleza kuwa mwaka mmoja wa Rais Samia katika Asasi hiyo, eneo la SADC limesalia kuwa tulivu, isipokuwa mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambapo jitihada za kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huo zinaendelea.

Jitihada hizo ni pamoja na majadiliano kupitia Mpango wa Luanda na Nairobi na hatua zilizochukuliwa na Wakuu wa Nchi katika mikutano ya pamoja ya EAC na SADC. Alisema kupitia mikutano hiyo jopo la Wazee wa Hekima kusuluhisha mgogoro huo limeundwa, timu za wataalamu kutoka EAC, SADC na AU zimeunganishwa ili zifanye kazi kwa pamoja, utaratibu (roadmap) na hadidu za rejea za namna ya kusghulikia mgogoro huo zimetayarishwa.

Dkt. Mpango alisisitiza umuhimu wa migogoro inayoibuka Afrika kutafutiwa suluhu na Waafrika wenyewe, kwa nchi hizo kuwa na dhamira ya dhati na kujitoa kwa hali na mali.

Aliendelea kwa kueleza kuwa katika kipindi cha uenyekiti, Tanzania pia imeongoza programu mbalimbali zinahusu uzuiaji na usuluhishi wa migogoro, upelekaji wa vikosi vya kulinda amani kwenye maeneo ya machafuko ya kisisasa, uimarishwaji wa taasisi imara za kidemokrasia ikiwa ni pamoja na kuongoza timu za waangalizi wa uchaguzi katika nchi za Botswana, Namibia, Mauritius na Msumbiji.

Amehitimisha kwa kueleza kuwa Tanzania imejitahidi kwa kiasi kikubwa kuhakikisha kuwa kanda ya SADC inasalia kuwa tulivu na salama na kuahid kuwa nchi yake itaendelea kutoa ushirikiano unaohitajika kwa mwenyekiti mpya wa asasi hiyo ambayo ni Malawi.
 
Tanzania inaonesha hofu kupitia makamu wa rais Dr. Philip Isidori Nzabhayanga Mpango kuwa maigizo ya ushiriki katika uchaguzi October 2025, serikali ya chama kongwe dola na vyama rafiki wa CCM vitaaibika kikanda na kimataifa.

Hivyo watakaojipitisha kuwa wameshinda watakosa uhalali / legitimacy mbele ya dunia mara baada ya maigizo ya uchaguzi.
 
Dkt. Mpango awaalika SADC Kutuma Timu ya Uangalizi wa Uchaguzi

Makamu wa Rais wa Tanzania, Mhe. Dr. Philip Isdor Mpango amesema kuwa maandalizi muhimu kwa ajili ya kufanya uchaguzi mkuu wa haki, huru na wazi yanaendelea vizuri nchini Tanzania na kutoa mwaliko kwa SADC kutuma timu ya waangalizi kwenye uchaguzi huo uliopangwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Dkt. Mpango ametoa wito huo wakati anasoma hotuba ya ufunguzi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama jijini Antananarivo, Madagascar Agosti 16, 2025.

Dkt. Mpango ambaye anamwakilisha Rais Dr. Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano huo ametaja mafanikio kadhaa ya uenyekiti wa Tanzania katika Asasi hiyo, iliyopewa jukumu la kusimamia masuala ya ulinzi, amani na usalama katika kanda ya SADC.

Akibainisha mafanikio hayo, Dr. Mpango alieleza kuwa mwaka mmoja wa Rais Samia katika Asasi hiyo, eneo la SADC limesalia kuwa tulivu, isipokuwa mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambapo jitihada za kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huo zinaendelea.

Jitihada hizo ni pamoja na majadiliano kupitia Mpango wa Luanda na Nairobi na hatua zilizochukuliwa na Wakuu wa Nchi katika mikutano ya pamoja ya EAC na SADC. Alisema kupitia mikutano hiyo jopo la Wazee wa Hekima kusuluhisha mgogoro huo limeundwa, timu za wataalamu kutoka EAC, SADC na AU zimeunganishwa ili zifanye kazi kwa pamoja, utaratibu (roadmap) na hadidu za rejea za namna ya kusghulikia mgogoro huo zimetayarishwa.

Dkt. Mpango alisisitiza umuhimu wa migogoro inayoibuka Afrika kutafutiwa suluhu na Waafrika wenyewe, kwa nchi hizo kuwa na dhamira ya dhati na kujitoa kwa hali na mali.

Aliendelea kwa kueleza kuwa katika kipindi cha uenyekiti, Tanzania pia imeongoza programu mbalimbali zinahusu uzuiaji na usuluhishi wa migogoro, upelekaji wa vikosi vya kulinda amani kwenye maeneo ya machafuko ya kisisasa, uimarishwaji wa taasisi imara za kidemokrasia ikiwa ni pamoja na kuongoza timu za waangalizi wa uchaguzi katika nchi za Botswana, Namibia, Mauritius na Msumbiji.

Amehitimisha kwa kueleza kuwa Tanzania imejitahidi kwa kiasi kikubwa kuhakikisha kuwa kanda ya SADC inasalia kuwa tulivu na salama na kuahid kuwa nchi yake itaendelea kutoa ushirikiano unaohitajika kwa mwenyekiti mpya wa asasi hiyo ambayo ni Malawi.
 

Attachments

  • IMG-20250816-WA0174.jpg
    IMG-20250816-WA0174.jpg
    411.4 KB · Views: 13
  • IMG-20250816-WA0169.jpg
    IMG-20250816-WA0169.jpg
    623.7 KB · Views: 15
  • IMG-20250816-WA0148.jpg
    IMG-20250816-WA0148.jpg
    599.8 KB · Views: 13
  • IMG-20250816-WA0173.jpg
    IMG-20250816-WA0173.jpg
    590.1 KB · Views: 10
  • IMG-20250816-WA0183.jpg
    IMG-20250816-WA0183.jpg
    623.2 KB · Views: 13
  • IMG-20250816-WA0185.jpg
    IMG-20250816-WA0185.jpg
    553.5 KB · Views: 20
  • IMG-20250816-WA0184.jpg
    IMG-20250816-WA0184.jpg
    676.9 KB · Views: 11
  • IMG-20250816-WA0179.jpg
    IMG-20250816-WA0179.jpg
    664.1 KB · Views: 10
  • IMG-20250816-WA0188.jpg
    IMG-20250816-WA0188.jpg
    868.8 KB · Views: 15
  • IMG-20250816-WA0187.jpg
    IMG-20250816-WA0187.jpg
    699.5 KB · Views: 15
  • IMG-20250816-WA0150.jpg
    IMG-20250816-WA0150.jpg
    746.9 KB · Views: 11
  • IMG-20250816-WA0186.jpg
    IMG-20250816-WA0186.jpg
    650.1 KB · Views: 10
  • IMG-20250816-WA0181.jpg
    IMG-20250816-WA0181.jpg
    588.5 KB · Views: 11
  • IMG-20250816-WA0145.jpg
    IMG-20250816-WA0145.jpg
    635.7 KB · Views: 17
  • IMG-20250816-WA0177.jpg
    IMG-20250816-WA0177.jpg
    615.8 KB · Views: 12
  • IMG-20250816-WA0180.jpg
    IMG-20250816-WA0180.jpg
    625.8 KB · Views: 14
  • IMG-20250816-WA0156.jpg
    IMG-20250816-WA0156.jpg
    550.8 KB · Views: 16
  • IMG-20250816-WA0168.jpg
    IMG-20250816-WA0168.jpg
    451.5 KB · Views: 14
  • IMG-20250816-WA0171.jpg
    IMG-20250816-WA0171.jpg
    614.6 KB · Views: 17
  • IMG-20250816-WA0143.jpg
    IMG-20250816-WA0143.jpg
    407.2 KB · Views: 10
  • IMG-20250816-WA0176.jpg
    IMG-20250816-WA0176.jpg
    582.2 KB · Views: 12
  • IMG-20250816-WA0163.jpg
    IMG-20250816-WA0163.jpg
    396.4 KB · Views: 14
  • IMG-20250816-WA0151.jpg
    IMG-20250816-WA0151.jpg
    331.7 KB · Views: 13
  • IMG-20250816-WA0178.jpg
    IMG-20250816-WA0178.jpg
    718.7 KB · Views: 15
  • IMG-20250816-WA0182.jpg
    IMG-20250816-WA0182.jpg
    674.3 KB · Views: 15
  • IMG-20250816-WA0155.jpg
    IMG-20250816-WA0155.jpg
    552.4 KB · Views: 11
  • IMG-20250816-WA0175.jpg
    IMG-20250816-WA0175.jpg
    502.2 KB · Views: 10
Kwamba sadc waje kuangalia CHAUMA na ACT wakiibiwa kura😂
 
Makamu wa Rais wa Tanzania, Dr. Philip Isdor Mpango amesema kuwa maandalizi muhimu kwa ajili ya kufanya uchaguzi mkuu wa haki, huru na wazi yanaendelea vizuri nchini Tanzania na kutoa mwaliko kwa SADC kutuma timu ya waangalizi kwenye uchaguzi huo uliopangwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Dkt. Mpango ametoa wito huo wakati anasoma hotuba ya ufunguzi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama jijini Antananarivo, Madagascar Agosti 16, 2025.

Dkt. Mpango ambaye anamwakilisha Rais Dr. Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano huo ametaja mafanikio kadhaa ya uenyekiti wa Tanzania katika Asasi hiyo, iliyopewa jukumu la kusimamia masuala ya ulinzi, amani na usalama katika kanda ya SADC.
Akibainisha mafanikio hayo, Dr. Mpango alieleza kuwa mwaka mmoja wa Rais Samia katika Asasi hiyo, eneo la SADC limesalia kuwa tulivu, isipokuwa mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambapo jitihada za kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huo zinaendelea.

Jitihada hizo ni pamoja na majadiliano kupitia Mpango wa Luanda na Nairobi na hatua zilizochukuliwa na Wakuu wa Nchi katika mikutano ya pamoja ya EAC na SADC. Alisema kupitia mikutano hiyo jopo la Wazee wa Hekima kusuluhisha mgogoro huo limeundwa, timu za wataalamu kutoka EAC, SADC na AU zimeunganishwa ili zifanye kazi kwa pamoja, utaratibu (roadmap) na hadidu za rejea za namna ya kusghulikia mgogoro huo zimetayarishwa.

Dkt. Mpango alisisitiza umuhimu wa migogoro inayoibuka Afrika kutafutiwa suluhu na Waafrika wenyewe, kwa nchi hizo kuwa na dhamira ya dhati na kujitoa kwa hali na mali.

Aliendelea kwa kueleza kuwa katika kipindi cha uenyekiti, Tanzania pia imeongoza programu mbalimbali zinahusu uzuiaji na usuluhishi wa migogoro, upelekaji wa vikosi vya kulinda amani kwenye maeneo ya machafuko ya kisisasa, uimarishwaji wa taasisi imara za kidemokrasia ikiwa ni pamoja na kuongoza timu za waangalizi wa uchaguzi katika nchi za Botswana, Namibia, Mauritius na Msumbiji.

Amehitimisha kwa kueleza kuwa Tanzania imejitahidi kwa kiasi kikubwa kuhakikisha kuwa kanda ya SADC inasalia kuwa tulivu na salama na kuahid kuwa nchi yake itaendelea kutoa ushirikiano unaohitajika kwa mwenyekiti mpya wa asasi hiyo ambayo ni Malawi.
takataka rubbish conglomerate
 
Back
Top Bottom