Dkt. Mathayo na Ana Kilango: Same "Wachina" wa Tanzania mpaka "VILAZA" wa Kilimanjaro

Kiswahili kinaeleweka vizuri kabisa Mkuu, 'uwakilishi' ni neno lisilo tata.

Wasomi kweli mna kazi. Kama linaeleweka vizuri, kigugumizi cha nini? Kwa vile unasema hili ndilo jukumu kubwa la mbunge basi ungeliweka wazi! Ninavyokuelewa mimi niliyekwepa umande ni kuwa kazi ya mbunge ni kukaa bungeni kwa niaba ya wananchi wa jimbo lake. Yeye ni mtu wa kutimiza hesabu na si kingine.

Ni haki ya mwananchi kumuuliza Mbunge juu ya masuala ya maendeleo kwani ndiyo mwakilishi wao. Kinachokataliwa hapa ni kumuona Mbunge ndiye aliyepaswa kuleta maendeleo au kuona kwamba mhusika namba moja ni Mbunge kwa lugha rahisi kumuona Mbunge ndiye kipaumbele (answerable) badala ya Mkurugenzi wa Halmashauri, Tanroads (ktk barabara), Mamlaka za Maji safi na maji taka (kwenye miji) nk.

Kumpatia uwajibikaji huu mbunge ni kujenga Taifa linalowategemea wanasiasa badala ya kuwategemea wataalam.

Mhusika namba moja wa matatizo ya wananchi katika jimbo lake yenye utatuzi kitaifa ni mbunge.

Mbunge (na diwani na Rais) ndiyo viongozi pekee walio answerable moja kwa moja kwa mpiga kura. Hawa wasipo-deliver mwananchi anaweza kuonyesha kutoridhika kwake kwa kuwanyima kura zake. Wakiwepo wa kutosha, waheshimiwa kibarua kinaingia mchanga. Ndiyo maana pale huyo unaemwita mtendaji anapoteleza au asipo tekeleza wajibu wake, mwananchi ana haki ya kum-pressurise mbunge wake ili nae awasukume watendaji. Si wananchi wote wana access na hao watendaji wakuu kama aliyokuwa nayo mbunge.

Wabunge wanapewa ofisi katika majimbo yao na usafiri wa kutembelea jimbo lao ili wananchi waweze kuwafikia kiurahisi na yeye mwenyewe kuwafikia wananchi wake kiurahisi.

Kuna mwenzangu alinyimwa viza ya kwenda marekani ambako alialikwa na rafiki yake alie raia wa huko. Alipomwambia rafiki yake, yeye akamwandikia seneta wake, ambae akawasiliana na State Department, viza ikapatikana!

Tofauti na unavyosema, kudai kuwajibika kutoka kwa wabunge wetu ndiko kutakakofanya wataalam wetu wawajibike zaidi
.


bangusilo anayohaki ya kuhoji, anayetoa matusi anakosea na amekosa ustaarabu. Bangusilo anakosea kuweka mategemeo pekee kwa Mbunge, anaendeleza dhana ya kujenga Taifa la wanasiasa. Hapo ndo kosa lilipo.

Bangusule hajatukana mtu. Bangusule kama mpiga kura ana haki na wajibu wa kumwandama mbunge wake pale anapoona kuwa amekosea. Mbona anaposifiwa hamlalamiki kuwa hizo sifa za kujenga barabara zingeenda kwa CEO wa Tanroad? Hapana. Anapomsukuma mtendaji akatimiza wajibu wake ana haki ya kusifiwa. Vile vile anapoonekana kushindwa kuwasukumiza watendaji ( na wananchi) ana haki ya kukosolewa. Yote haya ni sehemu ya territory yake.

....kwa upande wangu niko interested na hii mada kwani nimeishi kwa kipindi fulani pale same...zamani hizo.....hata juzi juzi nilikuwa pale wilayani i.e. Same.....trust me kwa juhudi anazofanya yule mama huwezi ku-justfy kum-blame Kilango eti kwa watu wamefeli vile au eti kwa kuwa mashambani watu hawawajibiki ipasavyo............kama ni juhudi hizo za ku-mobilze resources........huyu mama vilevile anazifanya........so whats the fuss here!.........au ndio politics as usual....attack your opponent......and you guys joined the game blindly.......huh!

Mkuu, Ogah. Kama nilivyomjibu Nziku, kukosolewa si attack. Ishu alizozileta Bangusule zina umuhimu kama hizi nyingine ambazo mbunge amefanikiwa. In fact, watu kama Bangusule wanawafanyia favour wabunge hawa kwa ku-highlight pale ambapo anaona pana mapungufu. Mbunge makini, badala ya kukasirika, angeenda kuchungua na kufanyia kazi tuhuma hizi.

Matatizo yetu tuna kaugonjwa ka kupenda. Bangusule amewasema wabunge wawili lakini watu wanamuona Kilango peke yake!

Nchi yetu itafika mbali kama sote tutaanza desturi ya kukubali criticism. Si kila anae ku-criticize ni adui wako. Au ana agenda ya siri. Na sisi wananchi tuanze kudai wale tunaowapa kura zetu wawajibike katika kila nyanja iliyomo katika jimbo letu. Tusiridhike na haya maendeleo ambayo basically ni photo-op kwa ajili ya wabunge wetu. Tuendelee kudai watupe uongozi katika kutatua matatizo yetu yaliyosalia. Ndiyo kazi waliyoiomba. Ndiyo kazi tuliyowapa.

Amandla........
 
Wasomi kweli mna kazi. Kama linaeleweka vizuri, kigugumizi cha nini? Kwa vile unasema hili ndilo jukumu kubwa la mbunge basi ungeliweka wazi! Ninavyokuelewa mimi niliyekwepa umande ni kuwa kazi ya mbunge ni kukaa bungeni kwa niaba ya wananchi wa jimbo lake. Yeye ni mtu wa kutimiza hesabu na si kingine.

ummh mimi sita-define 'uwakilishi' ila maelezo yangu yataonyesha maana ya uwakilishi. Tuendelee na mjadala...

Wabunge wanapewa ofisi katika majimbo yao na usafiri wa kutembelea jimbo lao ili wananchi waweze kuwafikia kiurahisi na yeye mwenyewe kuwafikia wananchi wake kiurahisi.

Wabunge wanatakiwa kuishi na wananchi huko huko mikoani/wilayani labda kama anaofisi nyingine let say ni Waziri.

Mbunge anatakiwa kuhudhuria vikao vya Halmashauri hasa Kamati ya Fedha na Uongozi (ambayo inavikao kila mwezi) na Full Council (inavikao kila robo mwaka).

Mbunge anapaswa kufanya mikutano ya wananchi ili kujua shida zao, mawazo yao mitazamo yao na kuiwasilisha Serikali kuu au Halmashauri kwa kupitia vikao au mawasiliano ya kawaida ya kiofisi.

Mbunge anatakiwa kuhudhuria vikao vya RCC (kamati ya Ushauri ya Mkoa).

Nchi yetu itafika mbali kama sote tutaanza desturi ya kukubali criticism. Si kila anae ku-criticize ni adui wako. Au ana agenda ya siri. Na sisi wananchi tuanze kudai wale tunaowapa kura zetu wawajibike katika kila nyanja iliyomo katika jimbo letu. Tusiridhike na haya maendeleo ambayo basically ni photo-op kwa ajili ya wabunge wetu. Tuendelee kudai watupe uongozi katika kutatua matatizo yetu yaliyosalia. Ndiyo kazi waliyoiomba. Ndiyo kazi tuliyowapa.

Fundi Mchundo, upo sahihi mzee, ila tatizo langu lipo pale tunapotaka ku-invest masuala yote kwa Mbunge, pale tunapoona Mbunge pekee ndiyo jibu la masuala ya maendeleo, pale tunapotoa kipaumbele kwa wanasiasa badala ya watendaji husika.

Dhana yangu ipo pale pale kwamba katika ufahamu wetu, tuache kuipa siasa first priority, tuache kuwa kama Wakenya au waganda (i'm sorry) kuwafuata nyuma wanasiasa kama suluhisho la mambo yetu yote, bali tujenga ufahamu wa kuwafuata watalaam.

Tujenge Taifa linalowekeza katika taaluma, wananchi tuweke kipaumbele wataalamu/watendaji zaidi. Huko Same tuhoji Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya, Afisa Elimu, nk. Ili tupate majibu ya kitaalam.
 
Mbunge wa Tanzania anakuwa wa "maana" zaidi pale anapoukwaa uwaziri wa wizara muhimu kama ya ELIMU, FEDHA, MIUNDOMBINU.
 
Wabunge wanatakiwa kuishi na wananchi huko huko mikoani/wilayani labda kama anaofisi nyingine let say ni Waziri.

Mbunge anatakiwa kuhudhuria vikao vya Halmashauri hasa Kamati ya Fedha na Uongozi (ambayo inavikao kila mwezi) na Full Council (inavikao kila robo mwaka).

Mbunge anapaswa kufanya mikutano ya wananchi ili kujua shida zao, mawazo yao mitazamo yao na kuiwasilisha Serikali kuu au Halmashauri kwa kupitia vikao au mawasiliano ya kawaida ya kiofisi.

Mbunge anatakiwa kuhudhuria vikao vya RCC (kamati ya Ushauri ya Mkoa).

Ninavyojua mimi palikuwa na sera ya kila jimbo kuwa na ofisi ya mbunge. Ofiisi hii inatakiwa iwe wazi kwa constituents wake.

Ninapotofautiana na wewe ni hapo unapodai kuwa kuhudhuria vikao ( kwenye vibahasha) na kuita mikutano ( ambapo yeye anakaa high table) ndizo kazi pekee za mbunge. Mbunge anatakiwa kuwatembelea waliomchagua bila kungoja vikao au mikutano ya hadhara. Mbunge anapaswa kuwa na watu wake jimboni mwake watakaomweleza mahali popote panapotokea tatizo. Si matatizo yote yatakuwa ndani ya uwezo wake lakini ni muhimu ayajue na yale anayoweza kusaidia kutatua afanye hivyo na pale panaposhindikana awaeleze watu wake kwa nini pameshindikana. Kwa mbunge makini hakuna shida inayotokea katika jimbo lake ambayo haimhusu.


Fundi Mchundo, upo sahihi mzee, ila tatizo langu lipo pale tunapotaka ku-invest masuala yote kwa Mbunge, pale tunapoona Mbunge pekee ndiyo jibu la masuala ya maendeleo, pale tunapotoa kipaumbele kwa wanasiasa badala ya watendaji husika.

Dhana yangu ipo pale pale kwamba katika ufahamu wetu, tuache kuipa siasa first priority, tuache kuwa kama Wakenya au waganda (i'm sorry) kuwafuata nyuma wanasiasa kama suluhisho la mambo yetu yote, bali tujenga ufahamu wa kuwafuata watalaam.

Tujenge Taifa linalowekeza katika taaluma, wananchi tuweke kipaumbele wataalamu/watendaji zaidi. Huko Same tuhoji Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya, Afisa Elimu, nk. Ili tupate majibu ya kitaalam.

Mwenye urahisi wa kuwahoji hawa watendaji ni mbunge. Ni huyu ndiye tunatakiwa kumsukumiza ili awahoji kwa niaba yetu. Wanasiasa hawana majibu yote lakini wana uwezo mkubwa wa kupata majibu kuliko mwananchi wa kawaida. Ila tusipowasukuma, wengi wao nao wanatelezea. Kutokana na tabia hii ya kila wakati kumtupia lawama mwananchi ndiko kulikotufikisha mahali ukienda kuripoti shauri polisi posti unaambiwa nenda kamkamate mbaya wako uwaletee. Ebo!

Amandla.......
 
Last edited:
mkuu mwanamalundi,
nimesoma ulichoandika lakini nimeona huna point,
kwani kazi ya mbunge ni nini?
me nakubaliana na bangusule, hizo ni kazi za wabunge,

mbunge ndio kiini cha maendeleo kwenye jimbo...
mbunge ni mwakilishi wa wananchi kwenye serikali, kwa ishu ya pesticides, mbunge anatakiwa kuwasaidia wanakijiji kwakuwataftia njia rahisi za kuweza kupata hizo pestcides... serikali ipo kwaajili ya kusaidia wananchi, na kama inasera za ku promote kilimo, then inatakiwa kuwasaidia wanakijiji wa same kuweza kupata pestcides, hata kama hawatapewa bure ,ila wataftiwe njia rahisi ya kuzipata, sijui kama point yangu nimeiweka fresh.... but 4 my recommndation wabunge wanatakiwa kuwasaidia wananchi wa jimboni kwao kwa mambo kama hayo...

mwanamalundi fikiria kidogo sio unatetea tu...
 
Hapa kuna hoja mbili za msingi,Maendeleo Same yamedumaa,Na utendaji kazi wa Wabunge waliopo.Yote yanawagusa wananchi wa Same ,ambao waliitwa wachina wa Tanzania.La kwanza la kudorora kwa maendeleo ya Same mimi nakubaliana nalo kwa kiwango kidogo,Kwani zaidi ya kuwahimiza wananchi kujiletea maendeleo Anna na David hawana cha ziada!Kwa hiyo maendeleo ya hawa wachina ambao nadhani Mwalimu aliiwaita hivyo kwa ajili ya ufupi wao na si uchapaji kazi ni ya wao wenyewe wala si ya hao wabunge wawili.

Utendaji wa wabunge hawa kweli zaidi ya siasa za majukwaani a vyeti vya kugushi kuitwa Dr.sidhani kwa dhati kabisa hakuna utendaji kwa manufaa ya hawa wachina wa Tanzania.Anna ni mke wa Malechela kule Mvumi,sasa swali kwa wachina Mlijua wazi kuwa ana ni mkaazi wa Mvumi!Halaf mkamchagua kuwa Mbunge wenu,Hivi inaingia akilini nikisema alifuata kura tuu huko Same ahalalishe uchaguzi wa Chama Tawala?
Mtakubaliana nami kuwa kama David amewaingiza Mjini alipowaambia kuwa amefuzu kuitwa Daktari nanyi mkakubali ndipo alipowaona kuwa nyie siyo Wachina wa Tanzania ila nyie ni wafupi tu wa kufikiri?
Maendeleo yenu hata kama yangewategemea wabunge nawaambia hata karne tatu msingeambulia kitu.Je hamjifunzi kutoka kwa majirani zenu tena mwawaita Watani zenu?Kwani wao wanawategemea wabunge tuuu??Hebu achaeni huo ufupi wa mawazo muinuke kujiletea maendeleo.DC anza kazi ya kuwacharaza bakora ukijitoa mhanga ile ujumbe uwafikie.Shime Wapare wa Same inukeni kutafuta maendeleo na kuwakataa wababaishaji na vihiyo!!!
 
Mkuu FMES,

Soma tena hiyo statement uliyo quote, umeelewa kinyume na maana yake. Wapi umetoa hilo la kwamba ukivizia allowances kwenye kamati unaweza kulisaidia jimbo lako?

Hili la ukilaza nafikiri unamwonea bure Gabusile maana hakusema mama Kilango au Mathayo ni vilaza. Alikuwa ana maana Same imegeuka kuwa vilaza. Tusiwe tunapotosha maana ya kitu maana kama ni kuelemishana basi ni muhimu mno kujadili ukweli na sio kuanza kujadili statements ambazo zimepindishwa.

I have said this earlier in one of my posts. FMES anajaribu kuharibu mtiririko wa mada ambao hauendeani na kile kilichoulizwa. FMES anatoa ushahidi wa visima 30 vya maji na baiskeli 20 za walemavu, ilhali hoja ya Bangusule ni kuhusu ukatwaji wa misitu, kudorora kwa elimu, ubovu wa barabara na ugojwa uliokumba zao la mpunga.
 
YourNameismine,

Same Sec iko wilaya ya Same na matokeo yake nimekuwekea. hebu linganisha Same Sec ambayo ni shule kongwe na Chaangaja Msuya Sec iko wilaya ya Mwanga. msifikiri nimekurupuka ninaposema wilaya ya Same haina uongozi. wenzetu walao wana Div 1 na Div 2.

pia umeonyesha hisia kwamba labda suala hili linahusu kampeni ya 2010. jibu ni kwamba Mbunge asiposhughulikia masuala kama haya ndipo yanapogeuka kuwa ajenda za kampeni dhidi yake.

kama angeshughulikia tatizo la elimu na mambo yetu yakawa mazuri kama wenzetu wa wilaya nyingine za Kilimanjaro basi angeweza kutumia kigezo hicho kijizolea kura.



P0150 SAME SECONDARY SCHOOL CENTRE

DIV-I = 0 DIV-II = 1 DIV-III = 0 DIV-IV = 33 FLD = 45 ABS = 4


S1070 CHAANGAJA CLEOPA MSUYA SEC SCHOOL

DIV-I = 2 DIV-II = 2 DIV-III = 12 DIV-IV = 73 FLD = 6 ABS = 0



Mkuu CHAANGAJA CLEOPA MSUYA SEC SCHOOL, haiko Same, iko wilaya ya Mwanga......usiiandame sana hiyo wilaya mkuu mpaka ukatumbukiza na data za uongo ili utimize adhma yako........toa data za ukweli ili hoja yako iwe na maana
 
Mkuu CHAANGAJA CLEOPA MSUYA SEC SCHOOL, haiko Same, iko wilaya ya Mwanga......usiiandame sana hiyo wilaya mkuu mpaka ukatumbukiza na data za uongo ili utimize adhma yako........toa data za ukweli ili hoja yako iwe na maana
soma vizuri alichokiandika.Amesema wazi kuwa shule hiyo ipo wilaya ya Mwanga.
 
- Zero na wanaakuunga mkono mnajaribu sana kulazimisha ishu hapa aaginst Mama kilango shujaa wa taifa lakini mnashindwa vinbaya sana, mnajaribu wee kulazimisha elimu ya Same, lakini again mnashindwa vibaya sana ni kwamba hamna hoja wala ishu, ila manataka kupoteza muda na none ishu, nimewaambia hivi wapiga kura wa jimbo la Mama Kilango sio wewe tu Zero/Bangusule, hapana wapo wengi sana tena wanaofuatilia sana jimbo lao na mara kwa mara kumkumbusha mbunge wao mahitaji ya jimbo lao, lakini sijawasikia wakimuita kilaza wala kumlilia kuhusu kushuka kwa elimu ya jimbo. Eti dataz za division one and two za shule huko Same ni tatizo la Mama Kilnago, please jaribuni kuwa reasonable japo kidogo na mnachojaribu kukijenga hapa maana hata ya Bulicheka ilijengwa kwa busara kidogo kuliko hizi hoja zenu uchwara, nia na madhumuni yenu ni kujifanya kwamba mna uchungu sana na jimbo la Same kuliko wananchi wa huko na in the process kumchafua jina Mama Kilango, kwa wale tunaoelewa vizuri siasa za hilo jimbo tunawaonea huruma sana, na pia poleni sana ila it was a good try lakini also a waste of time.

- Mnatuambia eti Same zamani walikuwa wanalima mpunga sana mpaka wakaitwa wachina wa Tanzania, mimi maisha yangu yote nasikia mchele wa Kyela sijawahi kusikia habari za mchele wa Same, kwa hiyo unaona hizi hoja zenu zilivyo mufilisi.

- Bwana Zero/Bangusule, unajaribu kuponda habari za visima 30 na baiskeli za vilema 20 as if kwenye hilo jimbo wewe umewahi kuwapatia wananchi zaidi ya haya, halafu huna huruma hata na hao wananchi vilema waliofadika na hizi baiskeli, huna huruma hata na wananchi waliofaidika na hivi visima vipya vya majia safi ila unachotaka ni kumchafua Mama Kilango ndio roho yako itatulia maana that s all you know na kuihsi kuchfua tu wengine hata bila sababu il mradi tu uchafue, no wonder taifa limekwama maana tuna wananchi wanaoamka na kutaka kuchafua tu. Sasa tunapokujibu sio kwamba tunaogopa eti umefanikiwa au unaweza kufanikiwa hapana record ziko very clear huko Same, kushuka kwa elimu ni tatizo la taif it has nothing to na mbunge wa Same East, kama una ushauri kuhusu hilo liepleke kwa waziri kwanza wa elimu, ila kumshupalia mbunge wa kiama mitatu wa Same East ni watse of time kuanzia ya wananchi hapa JF mpaka huko Same kwenyewe.

- Halafu naomba kukumbusha kwamba wananchi na viongozi wa Same they deserve better respect zaidi ya kuitwa vilaza, wewe hujui Tanzania ya leo what it takes kwa wananchi kupitisha mkono kinywani, na hasa mara tatu kwa siku kama kanuni za dunia za afya zinavyotaka. Mkuu wewe huko majuu uliko unaweza kula mara tatu kwa siku lakini usifikiri na wananchi wa vijijini huko Same wanaweza kufanya hilo kwa urahisi, licha ya kufukuzana na elimu sasa next time jaribu kuwa considerate na wananchi usiowajua na ambao hujui hata wanavyoishi maana bina-adam mwenye njaa hawezi kuheshimu elimu eti unahitaji kuwa professor kuelewa hilo?

- Kwamba eti Mwakyembe ndio role model wa ubunge, please habari nilizonazo ni kwamba hata kurudi kwake bungeni ni kwa mashaka sana unless itokee miracle sasa how could this be possible kwamba yeye ndiye anyefaa as mfano wa kupeleka elimu ambayo haikuwepo huko lakini wanataka kumn'goa anyways tena wananchi na sio mafisadi? Mimi ninakumbuka toka zamani sana nikiwa mdogo tuliambiwa Mwalimu hapendi kuwapa uwaziri makabila yaliyoendelea kielimu, kama wahaya, wanyakyusa, wachagga na wengioneo meaning kwamba Mbeya kuna elimu kubwa sana toka siku nyingi, sasa eti leo ni Mwakyembe ndiye aliyepeleka elimu huko ambayo haikuwepo? Mwakyembe ambaye nasikia huko jimboni ameanza kukanyaga majuzi tu baada ya kusikia mafisadi wameanza kumuingilia huko jimboni? Sasa leo huyu ndiye role model I mean ninaheshimu sana kazi ya huyu shujaa kwenye taifa, lakini ya jimboni please!

- Elimu ni tatizo la taifa tena ni kubwa sana kuliko mnavyoijadili hii ishu as if ni tatizo la Same tu na Mama Kilango, nimemsikia Mwalimu in the 90s akilalamika kwamba elimu imekwisha sio kushuka tu sikumsikia akimlaumu mbunge yoyote sasa haya ya kwamba eti elimu Same imeshuka tatizo ni mbunge wao wa miaka mitatu tu kwa kweli ni maajabu na kweli. Mama Kilango amefanya mengi sana katika jimbo lake kwa miaka mitatu ya ubunge wake na wananchi wa jimbo hilo wanajua sana wala hawahitaji kuja kutukanwa huku JF kwamba ni vilaza ili kuelewa kazi nzito sana ya mbunge wao na jinsi anavyowajali, mimi sijwahai kusikia amemaliza mwezi bila kufika huko jimboni, tunawasikia viongozi wa taifa kila siku wakiongozana huko Same East, mpaka rais wa jamhuri toka awe ameshafika huko zaidi ya mara nne, sasa yote haya ni kwa sababu ya mbunge amabye hawajali wananchi wake jimboni? Eti kuna hata mtu anashauri kwamba Mama Kilango ni mkazi wa, sasa mumewe mwenye haishi huko sasa mke anawezaje kuishi kama sio nonesense!

Naomba kumaliza kwa ksuema hivi, JF panatakiwa kuwa mahali pa kubwa sana na pa kujadili reasonable ideas kwa taifa na wananchi wetu, sasa tukianza kuwaita wananchi tunaowalalia macho kuwasiidia kuwa eti ni vilaza, au viongozi wao ni vilaza bila sababu, tunajishusha hadhi wenyewe kwamba tuko mbali sana na ukweli wa maisha Tanzania, na kuhitimisha msemo wa wananchi wengi bongo kwamba hawa vijana wa nje, kama alivyoniambia ofisa moja wa serikali huko nyuma kwamba nasikia huko mnapiga kelele sana yaani mimi nina njaa nikatae kump kura mgombea anyenipa kilo tano za mchele kwa sababu ya maneno yenu huko kwenye internet, sasa kwa mwendo huu wa kuwaita wananchi vilaza ambao hata kuweza ku-afford mlo mmoja kwa siku ni a struggle kwa kweli tunashuka sana hadhi mbele ya wanyonge tunajaribu sana kuwasaidia.

Otherwise, sisi tunaendelea kuwasiadia wananchi wa Same na majimbo mengine pia ya Tanzania, next month Mbungewa Same anatakiwa kuwepo Iowa kuwakilisha makadirio ya mradi wa maji zaidi kwa jimbo lake na umwagiliaji wa kilimo huko jimboni kwa wafadhili waliotafutwa na kijana mmoja mdogo sana mwenye uchungu na jimbo lake la Same East, kwa hiyo si kweli kwamba wananchi wote wa Same East ni vilaza!

Respect FMES!
 
Respect FMES!

Thats the way to go buddy. You are coming up good. Sasa umeanza kujadili hoja na sio kushabikia tu. Just for the records, mimi sio mkazi wa Same na wala sijawahi kufika Same. Huwa naisikia kwenye media tu. Hoja zangu kuhusu huu thread sio personal attack kwa Kilango na Mathayo. Infact hoja zangu ni katika kukusahihisha wewe ujadili mada na sio kwenda nje ya mada. Bangusule alitoa hoja, na wewe kama mchangia hoja ulipaswa kujibu kupitia hii latest post yako. Hayo mengine ya visima vya maji na kutuletea archives za magazeti hapa havikuwa na maana sana kama hii latest post yako. Bangusule kama mwananchi yoyote ana kila haki ya kuhoji juu ya utendaji wa mbunge wake katika nyanja zote za maendeleo. Kama amefanya vizuri katika kuchimba visima na mengineyo, basi anastahili pongezi. Lakini bado mwananchi ana haki ya kudai zaidi na zaidi kutoka kwa mbunge wake.

Ninachokuomba hapa (maana naona wewe ni mtu wa karibu sana na Kilango) umshauri mbunge wako akasikilize hoja (kama kweli Bangusule anasema ukweli) na kujaribu kuzitafutia ufumbuzi. Kwa mfano, kama suala la ukataji misitu, ni jambo la hatari sana kwa wananchi wa huko. Otherwise mpe hongera sana kwa kuchimba visima na kuleta baiskeli za walemavu. I really and strongly support that.

Adios!
 
Mkuu Zero......hebu soma kw amakini maelezo haya ya bangusule......

hali ya maendeleo katika wilaya ya Same imedorora tangu Dr.Mathayo na Anna Kilango wachaguliwe kuwa wabunge wa same magharibi na same mashariki. hali ya ELIMU ni mbaya sana. wilaya ya same imeshika mkia katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba na ule wa kidato cha nne. katika suala la KILIMO ule mradi maarufu wa kilimo cha umwagiliaji Ndungu una hali mbaya sana. kuna maradhi ya mpunga yameingia na wakulima hawana msaada wowote toka kwa mbunge wao Anna Kilango. milimani upande wa Dr.Mathayo ukataji MITI na uharibifu wa MISITU ambayo ni vyanzo vya maji umezidi kuongeza. BARABARA ya mkomazi-bendera-ndungu-gonja-kisiwani-same bado ni kero kubwa kwa wananchi.

Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kuisifu wilaya yetu na kutuita "Wachina" wa Tanzania. nina hakika akifufuka leo na kushuhudia uongozi mbovu wa Dr.Mathayo na Anna Kilango, akaona na matokeo ya mitihani ya watoto wetu atageuza kauli yake na kutuita "VILAZA" WA KILIMANJARO.

............can you substantiate hizo claims...........? then bangusule kutaka kuonyesha kuwa argument yake ni valid akaja na matokeo ya mitihani ya shule mbali mbali..........hebu niambie statistically how do one come with such a support na ku-claim his/her argument kuwa true.........huh......eti hali ya elimu imedorora tangu Kilango na Mathayo wawe wabunge kule...........!!

....hakuna anayekataa tatizo la Same........lipo.........na kumwambia Mh Mbunge ni haki ya kila mwananchi wa huko Same........however check this...... ".......WAKULIMA HAWANA MSAADA WOWOTE TOKA KWA MBUNGE WAO ANNA KILANGO.........." eehh!!

.......otherwise nimeheshimu na ku-enjoy sana mchango wa wakuu Mtanzania, Nziku, Zakumi na Fundi Mchundo.......guys keep it up!
 
Mkuu Zero......hebu soma kw amakini maelezo haya ya bangusule......



............can you substantiate hizo claims...........? then bangusule kutaka kuonyesha kuwa argument yake ni valid akaja na matokeo ya mitihani ya shule mbali mbali..........hebu niambie statistically how do one come with such a support na ku-claim his/her argument kuwa true.........huh......eti hali ya elimu imedorora tangu Kilango na Mathayo wawe wabunge kule...........!!

....hakuna anayekataa tatizo la Same........lipo.........na kumwambia Mh Mbunge ni haki ya kila mwananchi wa huko Same........however check this...... ".......WAKULIMA HAWANA MSAADA WOWOTE TOKA KWA MBUNGE WAO ANNA KILANGO.........." eehh!!

.......otherwise nimeheshimu na ku-enjoy sana mchango wa wakuu Mtanzania, Nziku, Zakumi na Fundi Mchundo.......guys keep it up!

Ogah,

Naheshimu sana michango ya wachangiaji wote hapa JF. Kuna wengine wanakufanya ucheke hata kama hawana points. Huo ndio uzuri wa JF. Hoja hujibiwa kwa hoja.

Nashukuru umeanza kukubaliana na Bangusule baada ya kupewa stats za matokeo ya mitihani Kwenye hilo la wakulima kukosa msaada wowote kutoka kwa mbunge wao baada ya mpunga wao kupata maradhi sijui ulitaka ushahidi wa namna gani. Nadhani Bangusule akapige picha mashamba ya mpunga yaliyoharibiwa na huo ugonjwa ili picha hizo zibandikwe hapa JF kama ushahidi. Is that what you are up to?

Nachofurahi kuona ni hoja zinavyojibiwa kwa hoja. Inawezekana Bangusule alikuwa hafahamu mengi juu ya utendaji wa mbunge wake. Lakini kupitia FMES, sasa atakuwa anajua yale machache (mengi kwa FMES) aliyoyafanya mbunge wake. Na kupitia JF, wabunge Kilango na Mathayo, watakuwa wamejua kero chache (nyingi kwa Bangusule) za wananchi wao.

Hii ni changamoto kwa JF members wengine kuleta kero kutoka majimbo yao hasa kipindi hiki tunapoelekea 2010.
 
Mkuu Zakumi,

Nimecheka kuhusu mfano wako wa mpaka rangi na mfunga nati. Kwa taarifa tu kwenye uzalishaji wa kisasa mambo sio hivyo tena mkuu. Management ime kua mno kiasi kwamba sasa ownership ya kitu au jambo lolote ni wadau wote. Hakuna tena ya kwamba mimi mimi ni mpaka rangi, yule ni mfunga nati. Any way nisingetaka kwenda huko zaidi, huo unaweza kuwa mjadala mwingine na siku nyingine.

Unataka nikupe majina mara ngapi? Si nimekutajia mfano jimbo la Rungwe? Kwanini kwenye masuala ya shule na maendeleo liko mbele kuliko majimbo mengine Mbeya? Unafikiri ni bahati ya Mungu?

Sio mwanasiasa ila nakuhakikishia ningelikuwa kwenye hizo nafasi za Wabunge, nina uhakika ningeongeza kiwango cha elimu kwenye wilaya husika. Hakuna rocket science hapo, ni management tu. Kwa watu hao hao ambao leo wanasua sua kuchangia maendeleo yao, wakipata mtu anayejua anataka kufanya nini na akawa na nia ya kufanya hivyo, inawezekana kabisa mkuu wala sio kujisifu lakini nakuhakikishia ningekuwa kwenye wilaya hizo zenye elimu duni kwa nafasi yoyote ile, kuna kitu kitasogea.

Mimi ni mpenzi wa elimu na hata nikienda huko wilayani nakuwa frustrated na hali duni za shule nyingi. Naamini ni possible kabisa kuongeza huo ubora.

Mtanzania:

Upenzi wako elimu unaweza kuwa sawa na ushabiki wa Simba na Yanga. Watu wanataka Simba au Yanga ishinde bila kufuata taratibu zozote zile. Na wewe unataka maendeleo ya elimu bila kuangalia facts zingine.

Tukirudi kwenye mada. Nitarudia kuuliza swali ambao; JE NI KITU GANI KILICHOWAKATAZA WATU WA SAME KUFANYA KAZI KAMA WACHINA :confused:

Kwa sababu maendeleo siku zote, yakiwemo ya elimu, yako proportion na mapato ya watu.

Mpaka sasa inaonyesha kuwa watu wa Same hawafanyi kazi kama walivyokuwa miaka ya nyuma. Je unategemea nini :confused:
Je unataka mama Kilango awapige viboko :confused:


Kuna kitu mnakisahau, mtu huyohuyo aliyewasifia waPare kuwa ni waChina wa Tanzania alikuwa-responsible na kuanzisha sera ambazo zimeua uzalishaji vijijini. Alianzisha vijiji vya ujamaa, operasheni maduka na mamlaka za mazao ambazo ndio chanzo cha maisha duni kwa watu wengi vijiji.

Sasa badala ya kulaumu mama Kilango, anzeni kuchambua siasa zilizo sababisha uduni wa uzalishaji na maendeleo vijijini.
 
Hapa kuna hoja mbili za msingi,Maendeleo Same yamedumaa,Na utendaji kazi wa Wabunge waliopo.Yote yanawagusa wananchi wa Same ,ambao waliitwa wachina wa Tanzania.La kwanza la kudorora kwa maendeleo ya Same mimi nakubaliana nalo kwa kiwango kidogo,Kwani zaidi ya kuwahimiza wananchi kujiletea maendeleo Anna na David hawana cha ziada!Kwa hiyo maendeleo ya hawa wachina ambao nadhani Mwalimu aliiwaita hivyo kwa ajili ya ufupi wao na si uchapaji kazi ni ya wao wenyewe wala si ya hao wabunge wawili.

Utendaji wa wabunge hawa kweli zaidi ya siasa za majukwaani a vyeti vya kugushi kuitwa Dr.sidhani kwa dhati kabisa hakuna utendaji kwa manufaa ya hawa wachina wa Tanzania.Anna ni mke wa Malechela kule Mvumi,sasa swali kwa wachina Mlijua wazi kuwa ana ni mkaazi wa Mvumi!Halaf mkamchagua kuwa Mbunge wenu,Hivi inaingia akilini nikisema alifuata kura tuu huko Same ahalalishe uchaguzi wa Chama Tawala?
Mtakubaliana nami kuwa kama David amewaingiza Mjini alipowaambia kuwa amefuzu kuitwa Daktari nanyi mkakubali ndipo alipowaona kuwa nyie siyo Wachina wa Tanzania ila nyie ni wafupi tu wa kufikiri?
Maendeleo yenu hata kama yangewategemea wabunge nawaambia hata karne tatu msingeambulia kitu.Je hamjifunzi kutoka kwa majirani zenu tena mwawaita Watani zenu?Kwani wao wanawategemea wabunge tuuu??Hebu achaeni huo ufupi wa mawazo muinuke kujiletea maendeleo.DC anza kazi ya kuwacharaza bakora ukijitoa mhanga ile ujumbe uwafikie.Shime Wapare wa Same inukeni kutafuta maendeleo na kuwakataa wababaishaji na vihiyo!!!

Well said; waChina wa Tanzania kwa sababu ya urefu wa kwenda chini. Nasikia Nyerere alikwenda Same, wakati wa mapokezi, alifikiri waliokuja kumpokea ni watoto wa shule (kwa sababu ya ufupi). Hivyo Nyerere akauliza, wapo wapi wazazi wenu. Wapare wakajibu: Ni thithi (sisi) baba zao, ni thithi (sisi) mama zao.

Kujibu swali la kuchuka elimu; ni lazima ku-establish timeline. Kuna uwezekano mkubwa Mgonja akiwa waziri wa elimu aliwasaidia sana. Lakini toka influence ya wilaya ya Same kupungua katika wizara ya elimu, maendeleo ya elimu ya wilaya hiyo yamekuwa katika free fall.

Au kuna uwezekano waliokuwa wanafanya vizuri wamehama kutafuta fortune katika sehemu zingine na waliobakia Same ni vilaza shujaa.
 
Mkuu FMES,

Napata shida sana kuchangia hoja zako maana ni kama unaongelea kitu tofauti kabisa.

Ni nani katika thread hii aliyesema Dr. Mwakyembe ndio role model ya ubunge?

Umeitafsiri tofauti kabisa sehemu ambayo ilimtaja Dr. Mwakyembe. Hata kama wengine tulisema wanachofanya kuhusu hao watoto waliokwama kusoma ni jambo zuri haimfanyi yeye awe role model ya ubunge.

Kuwa role model unahitaji kufanya mambo mengi makubwa kwenye nyanja husika. Ningelikuwa mimi labda ningemsema prof. Mwandosya ndio role model kwi kwi kwi najua kuna watu hapo wanasema Mtanzania huyo mpambe wa prof.

Take easy mkuu hapa ni majadiliano tu. Tukikutana kwenye kampeni zenyewe kule Same 2010 wakati wengine tunampigia kampeni mheshimiwa Bangusule itakuwaje? Naona tutashikana masharti kabisa.
 
Tatizo la kuporomoka kwa elimu na maendeleo mengine kwa ujumla ni la nchi nzima (si Same peke yake), kwa mawazo yangu ufumbuzi wa matatizo haya utaanzia ktk ngazi ya familia...watu wachape kazi na wafuatilie kwa ukaribu elimu za watoto wao na kuacha kulialia kila siku kuwa serikali haijafanya hivi au vile....

...una point hapo wazazi ni muhimu sana,lakini mimi nina experience na jinsi uongozi wa shule na wanafunzi wenyewe wanavyoweza kubadilisha mambo for worse/better,hii ndio experience yangu.....high school kuna kipindi tulikuwa hatuna mwalimu wa chemistry na jinsi ilivyokuwa inaonekana tusingepata mwalimu mpaka tumalize shule,watu tukaanza kuhesabu F na panicking ikaanza tukajua tumekwisha maana miezi sita ilipita bila kuona mwalimu,basi akatokea mwanafunzi mmoja very smart akatushauri tutafute wenyewe mwalimu then tumlipe na shule imruhusu atufundishe darasani kwetu na kutumia laboratory kwa vipindi vyote vinavyohitaji,kweli tukaomba shule waturuhusu lakini shule ikakataa ikasema haiwezi kutoa madarasa kwa mtu ambaye sio mwalimu wa pale na hata hivyo wanafunzi wengine hawana hela kwa hiyo sio fair kufundisha wenye pesa tuu(tuliona wana point hapo ya wasio na pesa) basi ikabidi tukubaliane wasioweza kulipa tuwabebe tuu na yule mwalimu akakubali na kusema OK lakini walipe hata nusu wasioweza,anyway deal ikawa through kati yetu na mwalimu wa chemistry then tukarudi kwa uongozi wa shule still wakakataa kwa sababu ile ya kwanza eti sio mwalimu wa pale,frustration zikaingia maana muda unaenda na hakuna solution yeyote,baada ya kuona uongozi hakuna kitu watatusaidia ikabidi watu wachukue issue mikononi mwao ili kujiokoa,wajanja wachache(zaidi ya 30) wakakubaliana na mwalimu wakawa wanakutana naye mara tatu kwa week kwenye shule(primary jirani) na mwalimu alikuwa commited na machine kweli kweli,kwa ufupi jamaa wote waliosoma wote kwa yule mwalimu karibu wote walipata B na cha kusikitisha karibu darasa lote la PCM liliondoka na F maana hawakuwahi kuona chemistry teacher for 2 yrs...ni mfano tuu jinsi uongozi mbovu wa shule unavyoweza kuharibu future za wanafunzi wake bila sababu
 
Asante sana, naona madogo wamefanya vizuri ukizingatia ni shule ya serikali....lakini ukiangalia waliofaulu (div 1-3) kwa ujumla stats za Rungwe Sec (pass 58%) na Same Sec (pass 46%) hazipishani kihivyoo na hii ndio point yangu all along kuwa matokeo si mazuri karibu nchi nzima....Hapa ukija ukiweka (kama alivyofanya Bangusule) private candidate centers na vishule vya kata/kijiji, basi lazima matokeo ya form four ktk wilaya hizi mbili yatakuwa hayana tofauti kabisaaa!! Kwahivo lawama basi watupiwe wabunge wooote ktk Tanzania na sio kuwa-single out wabunge wa Same peke yao(hiyo sio fair..)!

Tatizo la kuporomoka kwa elimu na maendeleo mengine kwa ujumla ni la nchi nzima (si Same peke yake), kwa mawazo yangu ufumbuzi wa matatizo haya utaanzia ktk ngazi ya familia...watu wachape kazi na wafuatilie kwa ukaribu elimu za watoto wao na kuacha kulialia kila siku kuwa serikali haijafanya hivi au vile....

Yournameismine,

Tatizo la Bangusule halikuwa Same secondary school, tatizo lake lilikuwa kwenye zile shule ambazo katika kumi za mwisho kwa Kilimanjaro, tisa zimetoka Same.

Kwa shule za serikali matokeo kwa shule zote yako chini kuliko huko nyuma na kuna sababu nyingi ikiwemo kuongezeka kwa shule nzuri za private, wenye pesa wengi wanakimbilia huko, kuongezeka kwa wanafunzi, upungufu wa walimu, na huduma mbovu za vyakula kwa wanafunzi, ufisadi, ufundishaji mbaya nk.

Sasa ulitaka Bangusule awalaume wabunge wote kwa failures za Same? Yeye kaandika yanayomhusu kama wengine tunavyoandika mara nyingi yanayotuhusu.

Vinginevyo nimekuelewa na tuendelee kukata issues.
 
Ningependa tu kuuliza hivi matokeo ya kidato cha nne yana nini hasa Tanzania ??? maana yakichatoka tu, watu wanaanza kutoa taafsiri za ajabu ajabu.

Kuna watu wanachukua vitabu vya matokeo na kuvisoma kama novel ???

Kuna thread inayosema shule za Kilimanjaro zimefanya vizuri basi kuna Wachagga wameonyesha kuwa wao vichwa kuliko wazalendo wengi.

Na tatizo la Bangusule ni kuwa katika shule zilizofanya vibaya katika mkoa wa Kilimanjaro, kati ya kumi, tisa zimetoka Same.

Hivi kuna mystic gani za matokeo ya kidato cha nne :confused: Inaonyesha kuna euphoria fulani.
 
Back
Top Bottom