Dkt. Mathayo na Ana Kilango: Same "Wachina" wa Tanzania mpaka "VILAZA" wa Kilimanjaro

bangusule

JF-Expert Member
Feb 9, 2008
291
190
hali ya maendeleo katika wilaya ya Same imedorora tangu Dr.Mathayo na Anna Kilango wachaguliwe kuwa wabunge wa same magharibi na same mashariki. hali ya ELIMU ni mbaya sana. wilaya ya same imeshika mkia katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba na ule wa kidato cha nne. katika suala la KILIMO ule mradi maarufu wa kilimo cha umwagiliaji Ndungu una hali mbaya sana. kuna maradhi ya mpunga yameingia na wakulima hawana msaada wowote toka kwa mbunge wao Anna Kilango. milimani upande wa Dr.Mathayo ukataji MITI na uharibifu wa MISITU ambayo ni vyanzo vya maji umezidi kuongeza. BARABARA ya mkomazi-bendera-ndungu-gonja-kisiwani-same bado ni kero kubwa kwa wananchi.

Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kuisifu wilaya yetu na kutuita "Wachina" wa Tanzania. nina hakika akifufuka leo na kushuhudia uongozi mbovu wa Dr.Mathayo na Anna Kilango, akaona na matokeo ya mitihani ya watoto wetu atageuza kauli yake na kutuita "VILAZA" WA KILIMANJARO.
 
Of all the people to be blamed,you have chose the two MP's!!!Kwanini usizungumzie maafisa taaluma,maafisa elimu,walimu(kama kuna upungufu),mazingira ya kujifunzia na vitu vingine vingi tu....May be you might be having the valid arguments to collerate the poor
examination results and the inefficience of these MPs...As for now,I see your just making some baseless attacks!!We unadhani laiti Mwalimu akafufuka leo hii kitu kitakachomstaajabisha kiuhakika ni hicho???La hasha,pana mambo mengi sana...
 
Ngoja Fmes aamke ndo utakiona cha mtema kuni,, mi simoooo mchanga wa pwani huoo
 
There is something fishy in it... It has to do with 2010!. Haya tayarishe line up yako tuwaone. Mama Malechela atarudi, Dr. mathayo na Ph.D yake fake ikiumbuliwa, ndio basi tena.
 
kuhamasisha shughuli za maendeleo ndiyo jukumu kuu la mbunge yeyote yule. mbunge ndiyo muongoza njia[kilongola] ktk harakati zote za wananchi kuboresha maisha yao. mbunge anapigiwa kura na wananchi, ili asukume ajenda ya wananchi kujitafutia maendeleo.

kama maafisa elimu, maafisa misitu, maafisa kilimo, tulioletewa na serikali hawafanya kazi yao, mnatarajia wananchi tumuulize nani kama siyo wabunge wetu? nani anapaswa kuelezea kilio cha wananchi kuhusu utendaji mbovu wa maafisa hao kwa serikali? labda niongeze: ni lini mmesikia wabunge wetu hawa wakiwasukuma maafisa elimu, maafisa misitu, maafisa kilimo wa Same, kutekeleza wajibu wao?

Mwalimu akifufuka atastajaabishwa na mambo mengi sana, kati ya hayo ni hili la wilaya ya Same kuwa ya ndiyo vilaza wa Kilimanjaro. watu wa kwanza atakaowahoji kutokana na hali mbaya ya elimu Same watakuwa ni Dr.Mathayo na Anna Kilango.


kwa wale tunaoijua wilaya Same na mwamko wa maendeleo wa wananchi wake, tunajua kwamba kinachopelea na kuirudisha nyuma wilaya yetu ni uongozi mbovu wa wabunge wetu.
 
hali ya maendeleo katika wilaya ya Same imedorora tangu Dr.Mathayo na Anna Kilango wachaguliwe kuwa wabunge wa same magharibi na same mashariki. .

It could be that you are very right. However, we need more information to make a comparative analysis. That is, more data is required to compare the development path before and after Dr.Mathayo and Lady Kilango took office

. hali ya ELIMU ni mbaya sana. wilaya ya same imeshika mkia katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba na ule wa kidato cha nne. .

I thought this is tripartite issue! You can not blame these folks for poor performance in both primary and secondary schools. What about District education officers? teachers? parents? And ofcourse, pupils themselves?

katika suala la KILIMO ule mradi maarufu wa kilimo cha umwagiliaji Ndungu una hali mbaya sana. SIZE]


Again, who is to blame here? Farmers? local councils? Ministry of Agriculture? Fisadis within the projects? why would you want to put the blame to these two folks?

kuna maradhi ya mpunga yameingia na wakulima hawana msaada wowote toka kwa mbunge wao Anna Kilango.

Who told you that the role of mbunge is distribute pesticides? What percentage of government budget is allocated to the agric sector as a whole, leave alone pesticides??

milimani upande wa Dr.Mathayo ukataji MITI na uharibifu wa MISITU ambayo ni vyanzo vya maji umezidi kuongeza. BARABARA ya mkomazi-bendera-ndungu-gonja-kisiwani-same bado ni kero kubwa kwa wananchi.


Oops!!, give me a break! Do you really want to tell us that Dr. Mathayo anashirikiana na wananchi wa same kukata MITI?? OMG!!! Next time, mvua isiponyesha, utamlaumu Dr.Mathayo. That is, since he took office same district, does not get enough rain!

The rest of your arguments are trivial and futile. Next time, bring serious accusations with relevant data. Not maneno ya vijiweni.
 
Mwanamalundi,

toka enzi za mababu zetu kilimo ktk wilaya same kinafanyika kwa njia ya umwagiliaji. kuna mfumo wa mifereji ya asili ambayo inateremsha maji mpaka maeneo ya mabondeni ambako kuna kilimo kikubwa sana cha mazao kama mpunga,mahindi,na maharage.

chanzo cha mito inayoteremsha maji kwa ajili ya kilimo kipo katika misitu ambayo inashambuliwa na wakataji miti hovyo. wengi wao hawana asili na hivyo uchungu na maisha ya wananchi wa Same.

mpaka sasa hivi wabunge hawana na ajenda yoyote ile kama kupigania misitu hiyo iwe hifadhi ya taifa. kwa kufanya hivyo itapata ulinzi wa serikali kuu, bajeti kubwa zaidi ya uhifadhi na upandaji miti etc etc. zaidi ya hayo hawajahamasisha kwa namna yoyote ile kampeni ya kupanda miti katika maeneo ya milimani na hata mabondeni.

MISITU, MAJI, MITO NDIYO LIFELINE YA WANANCHI WA SAME.

hivi waziri wa chakula halafu wilaya yako ndiyo inakuwa ya kwanza kuomba chakula kwa kushindwa kuwapatia wakulima pesticides? mama kilango alidai ndani ya bunge kwamba yeye siku zote anakula wali, ugali ni mara moja moja akijisikia hamu. labda leo hii mama kilango anakula wali uliotokana na mchele toka maeneo mengine ya Tanzania, lakini ni aibu kwa wakulima wa mpunga wa Ndungu(Same) kutelekezwa na mbunge anayejisifia kuwa mlaji mzuri wa wali.

inawezekana kabisa huko mwenye makaratasi mnayosoma haya ninayoyazungumzia si majukumu ya wabunge. wabunge wa Same ndiyo "vilongola" wa kusukuma gurudumu la maendeleo wilayani. kwani Chedieli Mgonja alipokuwa akichimba barabara na wananchi wake hiyo ilikuwa kwenye description ya kazi za mbunge?

wananchi tumeshahamasishwa kujenga shule za kata na kazi hiyo tulimaliza kabla hawa hawajachaguliwa. sasa wao wametoa mchango gani tangu shule hizo zifunguliwe?

tunachodai ni hawa waonyeshe njia. waelekeze na kuwahamasisha wananchi kusukuma gurudumu la maendeleo ktk elimu, misitu, maji, kilimo nk nk.
 
mkoa wa kilimanjaro umeongoza kwa kutoa shule zilizofanya vizuri ktk matokeo ya sekondari. wilaya ya same haina hata shule moja kati ya shule hizo. hivi kweli watu wazima mnataka wananchi wa same tusishikane mashati na kuulizana kulikoni?



S0354 JITENGENI SECONDARY SCHOOL

DIV-I = 0 DIV-II = 0 DIV-III = 2 DIV-IV = 61 FLD = 61 ABS = 0

shule ya Jitengeni iko kijiji alichozaliwa Mwalimu Anna Kilango. sasa hii si aibu kwa mbunge na jimbo?? kwanini tuufumbie macho uzembe wa namna hii?


P2514 CHUO CHA MAENDELEO YA WANANCHI SAME

DIV-I = 0 DIV-II = 0 DIV-III = 0 DIV-IV = 6 FLD = 16 ABS = 1

aibu nyingine hiyo hapo kwetu sisi na mbunge wetu Dr.Mathayo.
 
Last edited:
Tutaanza kukuita mheshimiwa Bangusule, unaombwa ukagombee jimbo hilo.
Hiyo miti isipoota, utaipata.
 
Lole Gwakisa,
endelea kunikejeli tu. lakini nakuomba uwahurumie wanavijiji waliodunduliza pesa zao na kuwapeleka watoto shule matokeo yake shule nzima Div 4 na Div 0. pia naomba kabla hujanikejeli ufikirie hatari ya misitu kuisha na mito kukauka katika wilaya inayotegemea kilimo cha umwagiliaji maji.
 
Huyu bwana Bangusule alikuwa na jambo zuri alitaka kutueleza kuhusu Same, lakini nadhani kwa kunyoosha vidole kwa waheshimiwa ndio maana anaonekana mbabaishaji. Kila mtu ana haki ya kutetea jimbo lake, kama vile tulivyo na haki ya kutetea TZ. Anapozungumzia mfano wa kukata miti, na kuharibu vyanzo vya maji, ni suala kweli linahitaji majibu kwa hao wabunge, ni vipi kama wawakilishi wa wananchi wamelitafutia tatizo hilo majibu yake. Kawa wabunge wanalijua hilo, na hawachukui jitihada zozote kuishauri Serikali, huo uharibifu utaendelea na Serikali kuendelea kukusanya kodi kwa hilo.

Mfano mzuri bonde oevu la Ihefu, Usangu, Wilaya ya Mbarali ambapo Serikali iliposimama kidete kusimamia shughuli za kibinadamu kama ufugaji na kilimo, sasa maji yanatiririka vizuri.
 
mfumwa,

wewe kwa jina lako inawezekana kabisa unalijua fika jimbo la Same, matatizo yake, na potential yake. haya madai siyo kama yanatoka hewani tu, lakini wilaya ya Same ilishapata kuwa na shule zinazoongoza ktk mitihani ya kitaifa. kumetokea nini leo ndiyo iwe wilaya "KILAZA" katika mkoa wa Kilimanjaro? mpunga wa mabonde ya Same ulikuwa maarufu mpaka mikoa ya Tanga, Dar Es Salaam. hata Kenya maeneo ya Mombasa walikuwa wanajua mpunga uliotoka Same. nakukumbusha habari ya Mgonja kuandikwa katika magazeti ya Kenya kwamba anazuia wananchi wake kuvusha mpunga kwenda Kenya.

Afisa Elimu, sijui na bwana misitu, anategemewa kuwa na uchungu na maendeleo ya elimu, na uhifadhi wa misitu, kuliko wabunge wazaliwa wilaya yetu?

NDUGU YANGU MFUMWA, KAMA NIMEKOSEA KUWAHOJI VIONGOZI WETU TULIOWACHAGUA KWA KURA, NISAIDIE KUNIFAHAMISHA NIMHOJI NANI.
 
NDUGU YANGU MFUMWA, KAMA NIMEKOSEA KUWAHOJI VIONGOZI WETU TULIOWACHAGUA KWA KURA, NISAIDIE KUNIFAHAMISHA NIMHOJI NANI.

Ukisoma post yangu iliyopita sijasema umekosea, kuna mambo Wabunge wakiwa wawakilishi wa wananchi wanatakiwa kuyafikisha Serikalini, ili Serikali ichukue hatua. Kama huo ukataji wa miti unaosababisha kuharibu vyanzo vya maji.
 
Mfumwa,
umeniita mbabaishaji. lakini ndugu yangu umeona jinsi watoto walivyopukutika kwenye mitihani ya taifa? hawa itabidi warudi kwenye kilimo, wakati huohuo kilimo kinauawa kwa kuharibu vyanzo vya maji ya kumwagilia.

imeniuma sana. bora ningetukanwa na kina Gwakisa lakini siyo wewe.
 
Mfumwa,
umeniita mbabaishaji. lakini ndugu yangu umeona jinsi watoto walivyopukutika kwenye mitihani ya taifa? hawa itabidi warudi kwenye kilimo, wakati huohuo kilimo kinauawa kwa kuharibu vyanzo vya maji ya kumwagilia. imeniuma sana. bora ningetukanwa na kina Gwakisa lakini siyo wewe.

Ndugu yangu Bangusule, niliandika hivi "Huyu bwana Bangusule alikuwa na jambo zuri alitaka kutueleza kuhusu Same, lakini nadhani kwa kunyoosha vidole kwa waheshimiwa ndio maana anaonekana mbabaishaji.".

NAOMBA KUCHUKUA FURSA HII KUKUOMBA MSAMAHA KWA HILO NENO "MBABAISHAJI", LAKINI SIKUWA NA NIA MBAYA KABISA. Naomba urudie tena kusoma ile post yangu, uone jinsi nilivyokutetea katika suala lako. Naelewa matatizo ya hilo eneo vizuri sana.

Kwa mara nyingine, SAMAHANI SANA ndugu.
 
Mimi niko na Bangusule kwenye hili. Ni lazima tuanze kuwabana wabunge wetu tunapoona kuna upungufu kwenye jimbo letu. Hawa tumewapa kura zetu ili waangalie maslahi yetu. Ni lazima wawajibike kwetu.

Amandla......
 
Mfumwa,
tumeyamaliza. angalia private message yako. nashukuru kwa kurekebisha yale uliyojaribu kuyaeleza.
Fundi Mchundo,
asante sana. kuongeza tu mbunge wa Same ana nafasi na jukumu tofauti kabisa na wabunge wa maeneo mengine. wananchi wana ari kubwa tu ya kujitolea katika shughuli za maendeleo. wananchi wanaelewa umuhimu wa kupeleka watoto shuleni na wanafanya hivyo. elimu kwa mtoto wa kike inatiliwa mkazo na Mbunge Mama Kilango ni ushahidi wa hilo. sasa inakuwaje katika kipindi cha uongozi wa Dr.Mathayo na Anna Kilango sisi ndiyo tuwe "VILAZA" wa Kilimanjaro?

asilimia 60% ya wakazi wa Same wanategemea kilimo cha umwagiliaji kutokana na maji yanayotiririka toka milimani. kuna utaratibu wa asili wa kusimamia matumizi ya maji unaitwa NDIVA labda wachangiaji wengine wangejielimisha kuelewa undani wa suala hili. sasa kama maisha ya 60% ya wananchi yanachezewa kwanini tukae kimya?

WANANCHI WA SAME HATUTAKI KUWA MZIGO KWA WATANZANIA WENZETU. NDIYO MAANA SIJAMSHIKA SHATI RAISI, WAZIRI MKUU, AU KIONGOZI YOYOTE WA KITAIFA.
 
Bangusule,

Hawa waheshimiwa walio wengi hata hawajui kinachotokea kwenye majimbo yao. Nakubaliana na wewe mbunge apimwe kwa uwezo wa kuleta maendeleo kwenye wilaya yake.

Kuna wabunge wengi wanadhani kazi zao ni kupiga kelele Dodoma tu, kumbe wananchi wamewachagua kwasababu wanafikiri watasaidia kusukuma gurudumu la maendeleo kwenye wilaya zao.

Hiyo shule ni aibu kubwa kuwa kwenye jimbo la mpiganaji Kilango. Huo si upiganaji tena, badala yake unageuka kuwa usanii.
 
Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kuisifu wilaya yetu na kutuita "Wachina" wa Tanzania. nina hakika akifufuka leo na kushuhudia uongozi mbovu wa Dr.Mathayo na Anna Kilango, akaona na matokeo ya mitihani ya watoto wetu atageuza kauli yake na kutuita "VILAZA" WA KILIMANJARO.

MWITEN AFUFUKE AWALETEE MAENDELEO!!
 
Back
Top Bottom