Dkt. Kipilimba, sasa yatosha!

Dkt. Kipilimba, sasa yatosha!

Usichokijua ni bora tu kukaa kimya. Una uhakika gani kuwa hizi allegations zako TISS walikuwa hawazifahamu?

Una uhakika gani kuwa TISS hawakushauri lolote kabla ya haya kutokea?

Tanzania tuna bahati ya kuwa na taasisi imara. Hata wewe wakiamua kudeploy resources na kukufikia usiku huu wanakupata.

Usiku mwema!!
Ni kweli mkuu
Mimi naamini TISS wako vizuri kwenye operation za kupambana na raia wanaokosoa serikali hasa hasa wanasiasa ndani ya nchi basi na siyo nje ya nchi, tofauti na hapo, mkuu tutadanganyana.
Tuwe wakweli tu mkuu,
Raia wengi wanaamini kuwa usalama wa taifa ni usalama wa raia, ardhi na mipaka ya nchi yetu akini nionavyo mimi tafsiri hii si sahihi kama inavyotafsiriwa na Tiss ambapo wao usalama wa taifa huenda wanatafsiri kuwa ni usalama wa Rais na serikali yake!
Nimefikiria hivyo kutokana na mwenendo wa matendo yanayofanywa na baadhi ya viongozi kama RC Chalamila, Bashite na wengine wengi ambao ukiwafuatilia kwa karibu utabaini kuwa hotuba zao nyingi zinalenga kuvunja amani ya nchi, lakini Tiss wapo hawachukui hatua yoyote ile dhidi yao kwa kuwa ni viongozi serikalini lakin vitendo hivyo vingefanywa na wengine ambao siyo viongozi wa serikali ni dhahiri wangeshughurikiwa mapema sana.
 
Sasa hivi hata Comoro anaweza akatest zali lake kwa Tz ili waichukue Mafia 😂😂😂
Nalog off
 
Akina Chenge, Ndugai na wengine waliotuingiza mkenge kwa mikataba mibovu wote walipitia JKT

Wametusaidia nini hao zaidi ya kututia hasara?

Uzalendo ni tunda la haki siyo kwata

Mimi sizungumzii kupita JKT kwa mujibu wa sheria ambapo wengi tu wamepita na wengine walikuwa ni watoro kutwa kucha wapo uraiani.

Nazungumzia kupita JKT halafu waangaliwa kama wafaa kusogea hatua zingine muhimu kabla ya kupelekwa kwenye idara.
 
Kama TakaTaka za Aina yako ndio zimejazana Huko Idarani basi TZ imekwisha.
Usichokijua ni bora tu kukaa kimya. Una uhakika gani kuwa hizi allegations zako TISS walikuwa hawazifahamu?

Una uhakika gani kuwa TISS hawakushauri lolote kabla ya haya kutokea?

Tanzania tuna bahati ya kuwa na taasisi imara. Hata wewe wakiamua kudeploy resources na kukufikia usiku huu wanakupata.

Usiku mwema!!
 
Kwani huko Ubalozi wa TZ south Hamna Mtu wa TISS? Hamna Military Attachee?? TISS hawawezi Kukwepa Hizi Lawama Boss.
Nadhan lawama zinapaswa kwenda ubalozi Kwetu south
Na sio hao unaowasema

Sidhan hivyo Ila kama Unataka kuleta ujuaji kwamba unaifahamu kiundani sawa pia
 
Nyote wawili mnazungumzia kitu kimoja.

Kwanini TISS 'inadeploy resources' kuwafikia Wapinzani wa CCM na wanaomsema JPM wakati inashindwa 'kudeploy resources' kulinda maslahi ya Taifa mpaka ndege inakamatwa Afrika Kusini?

Au unasema TISS walijua wakakaa kimya?

Kama walikuwa na taarifa hizi, basi wameichoka serikali au hawana tena maamuzi, bali wanapokea maelekezo toka juu.

Ufalme ukifitinika ndani yake, basi huo ufalme hauta simama.
 
Mkuu umeongea Mambo makubwa na ya kizalendo Sana, Nina Shaka na Hawa watawala na huyo mkuu kuhusu Kama wanaelewa hasa dhana nzima ya kuwepo kwa TISS?? NCHI UNAENDELEA KUDHALILIKA KWA KUENDEKEZA MAMBO YA CCM.
Kwa mara ya tatu tena nakuandikia Mzee wangu Dr Modestus Kipilimba, mkurugenzi mkuu wa idara ya usalama wa taifa, TISS.

Natamani sana, Rais Magufuli awe wa kwanza kusoma hii mada kabla yako.

Nimeshindwa kuendelea na kazi niliyokuwa naifanya usiku huu kwenye Computer, moyo wangu umekosa amani kabisa hadi niandike hii mada.

Dr. Kipilimba, unadhani bado unastahili kuongoza Idara nyeti na muhimu Kama hii ya TISS?

Kwanini mikononi mwako serikali ya awamu ya tano inadhalilika sana kimataifa?

Kwanini Idara yako imeruhusu uwepo wa watu Kama Musiba wanaokashifu viongozi wakubwa hadharani?

Sikufundishi kazi, ila nashangaa kwanini hujui kuwa idara kama TISS ndo Roho kamili ya Tanzania.

Kifo cha TISS ni kifo cha Tanzania, kwanini hujifunzi magumashi ya CIA, MI5, Mossad na mashirika mengineyo kama TISS?

Ninaposema magumashi nadhani umeelewa vizuri kabisa, maana nikielezea itahitaji kitabu.

Uimara wa TISS ndo Uimara wa Tanzania, na udhaifu wa TISS ndo udhaifu wa Tanzania.

Tunajua ya kwamba dawa ya Deni ni kulipa, lakini ilikuwaje TISS ikashindwa kubaini kuwa Steyn kafungua shauri mahakamani dhidi ya Tanzania kudai mali yoyote ya nchi ikamatwe?

TISS ingeitaarifu serikali basi, ndege isingeenda SA, na hivyo wangetafuta namna nyingine ya ku-solve tatizo.

Ni aibu kubwa mno nchi kudaiwa na raia mmoja Halafu mali ya nchi kukamatwa kwa Deni nje ya nchi, hii fedheha kubwa.

TISS mngeweza kuepusha hii fedheha. Kama TISS, ilishindwa kubaini njama za kutaifisha mali ya nchi, je itaweza kujua nini kinapangwa Somalia na Alshabab kwa mfano juu ya nchi?

Dr Kipilimba, TISS chini yako ni dhaifu mno, nakushauri u resign tu. TISS chini ya Dr Hansy Kitine na hayati Imran Kombe ilikuwa imara kupindukia.

Nakumbuka Tukio moja (siwezi kulitaja) nilikuja kushtuka mission accomplished muda mrefu kumbe yule jamaa alikuwa TISS na akapotea kama jini.

TISS ya leo imejaa vijana wa UVCCM, wasiojua lolote kuhusu intelligence wala miiko yake. Idara hii imegeuzwa kuwa ya kisiasa ili CCM itimize ndoto zake za alinacha za kutawala milele. Inashangaza sana, yaani Idara haikuweza hata kuzuia maandamano ya kuharibu Diplomasia yetu na SA.

Watumishi wa Idara hii wanatakiwa wawe wafia nchi (wazalendo kweli kweli) siyo wafia CCM au CHADEMA.

CCM itakufa, CHADEMA itakufa, lakiniTanzania ipo tu!
 
hahah vijana wa sikuhizi wanajikuta wachambuzi wa kila kitu story wanazopiga vijiweni wanatuletea JF tupotezee muda
 
Usichokijua ni bora tu kukaa kimya. Una uhakika gani kuwa hizi allegations zako TISS walikuwa hawazifahamu?

Una uhakika gani kuwa TISS hawakushauri lolote kabla ya haya kutokea?

Tanzania tuna bahati ya kuwa na taasisi imara. Hata wewe wakiamua kudeploy resources na kukufikia usiku huu wanakupata.

Usiku mwema!!
Ok! Say walikuwa, matokeo ndio haya tunayaona????
 
Hebu waambieni hao walio against Government kwa sababu tu ya kubwanwa maslahi wajitafakari. Uzalendo kwanza. Actually JKT ingerudi tena ianzie form 4 maana kuna kizazi kwa kweli kinatishia amani ya nchi!
Kuna watu wanamaliza Form 4 na miaka 14 hadi 16 maana yake ni underage. Serikali haiwezi wapeleka huko
 
Mkuu shikamoo, nimesoma posti yako inaharufu ya utuuzima na busara fulani hivi zilizopitwa na wakati!!! Eti unatamani rais awe wa kwanza kulisoma hili!!!

Labda hulijui hili " U can't swim against the current". Sio Dr Kipilimba pekee wako mawaziri, makatibu, makamishna, wakurugenzi, mabalozi wanaoshindwa kama nansvyoshindwa Dr.
 
Mimi naona Dr Kipilimba anajitaidi sana kuifanya tiss kuwa ya kisasa.... Shida ni Siasa tu.
Ndio tiss wanapaswa kumonitor siasa za bongo ila isiwe too much.
Mm Binafsi naweza kutoa mchango mkubwa sana kwa mageuzi ya tiss.
Tiss ya leo ina vijina wa UVccm wanatoa vitambulisho hovyo hovyo hasa kwenye mabaa makubwa kama trpo 7, Element......ila bado naiman nayo.
 
Ndo uko sawa kabisa JKT inapaswa kurudi kisawasawa na mimi napendekeza vijana wakae kambini kwa miaka miwili.

Hii wanafanya Israeli na Korea Kusini na baadhi ya nchi zingine.

Hii itasaidia watu kushika moyo na kuonyesha wanaipenda nchi yao na wako tayari kuitumikia "no matter what".

Hata kama kuna kiongozi ambae na kasoro zake lakini linapokuja suala la ndege kuzuiwa nchi nyingine khasa ndege mpya watanzania wanaungana pamoja kutafakari juu ya mstakabali wa mali hiyo ya taifa.

Marekani pamoja na Donald Trump kufanya anayofanya lakini wakaikung'uta Syria kwa mabomu na sasa wanaishughulikia Iran na Korea Kaskazini, hiyo yote ni kwa "maslahi ya taifa" hilo.

Unafahamu hata nchi zilizoendelea likija jambo la "kwa maslahi ya taifa" wanageuka na kuunga mkono, hayo utaona kwenye televisheni, radio na magazaeti.

Masuala kama ya ugaidi na kutishia usalama wa mataifa yao wanaweza wakayaongelea kwa siku kadhaa masaa 24 na ukijaribu kubadilisha chennels habari ni hizohizo mpaka kieleweke mbele ya wananchi.

Viongozi mbalimbali, wasomi na watu wengine wa kada mbalimbali kwenye jamii wataitwa kwa interviews.

Sisi Tanzania kuna kitu kimeharibika ndani ya miaka 20 ilopita na tunapaswa kujitafakari na kujifunza uzalendo na kulinda maslahi ya taifa.
Uzalendo hautafutwi JKT bali ni matokeo ya haki katika taifa.
Leo wanaohubiri uzalendo ni wale waliopita JKT na wakapikwa huko miaka 2 lakini leo hii wao ndio hao hao
1) Mafisadi
2) Wauaji
3) Wanafiki wa kutupwa na wapenda vyeo
4) Wanaoamini mtu mmoja ndiyo pekee anaeweza kuitoa Tanzania mahali ilipo kiuchumi
5) Wanaokula njama njama za kubadili katiba ili wajiongezee muda wa kutawala.

Kama watu hawa walipita huko jkt na ndio wanatuongoza, unatarajia nini kutoka kwa waongozwaji? Lazima washangilie mali za nchi kushikwa maana wanaamini kufanya hivyo ni kuwakomesha watawala.
 
Ushauri wako haulengi kuondoa chanzo cha tatizo, ubovu wa TISS haujaanzia kwa Dkt. Kipilimba, mbona wakati nchi inafisidiwa kupitia kagoda mpaka escrow hamkusema TISS wanafanya nini?? hii ishu ndogo ya ndege inalingana na aibu ya watu kugawana pesa za nchi kwenye mifuko tena mitaani?? benki ndio zilikuwa kichaka cha kuficha uhalifu na TISS wapo, kuna aibu kubwa kushinda hizo??Kipilimba amerithi TISS mbovu..laumu waliokuwepo kabla yake!
Waandishi hawajaanza leo kuikosoa TISS,; mimi Nafanya marudio tu, magazeti ya Mwanahalisi na Mawio, yalifutwa kwa sababu ya kuikosoa TISS, Azori Gwanda, Ben Saanane, Kanguye nao wamepotezwa na TISS, Tundu Lissu alipigwa risasi na TISS.
Hata mimi eti wanaulizana ofisini namna ya kunipata, kuna wakati wanahisi mimi ni Chahali au Ngurumo, hebu jiulize kosa langu ni lipi hadi na mimi wanataka kuniua, kuwakosoa tu?
Bahati mbaya kwao nalala sebuleni kwao, kila wanachoongea nakijua
 
Kweli mkuu ni aibu lakini ondoa Shaka mkuu watayafanyia kazi lakin turudi nyuma kuna mbunge wa kuitwa kubenea kutoka jimbo la segerea huku dar nilishawai kusikia sikumbuki tarehe Alitoa onyo jamani tunadaiwa tulipe point mpaka huyu mbunge alijua inawezekana TISS walijua ila viongozi waripuuza kwa sababu ya urafiki wetu na S A
 
Ni kweli mimi hakuna ninalolijua kuhusu TISS sababu mimi sio mtumishi wa idara hiyo.
Afadhari mimi najitambua sijui kuhusu TISS kuliko wewe unajinasibu unajua kuhusu TISS na intelijensia kiujumla huku unaongea usiyoyajua.

Huyo anaekupa hadithi anakulisha matango pori tu, hamna kitu hapo.
Unazidi kuonyesha umbumbumbu wako humu, pathetic kabisa wewe.
Kwanini CIA na NSA walishindwa kunusa mapema kuwa Edward Snowden alikuwa amejiandaa kuasi? ili wamdhibiti asitoe Siri nzito za nchi?
Narudia tena, huna unalojua wewe, kakojoe ulale.
 
Mkuu shikamoo, nimesoma posti yako inaharufu ya utuuzima na busara fulani hivi zilizopitwa na wakati!!! Eti unatamani rais awe wa kwanza kulisoma hili!!!

Labda hulijui hili " U can't swim against the current". Sio Dr Kipilimba pekee wako mawaziri, makatibu, makamishna, wakurugenzi, mabalozi wanaoshindwa kama nansvyoshindwa Dr.
Mkuu idara ya usalama wa taifa ikishindwa jambo lolote ujue hakuna tena nchi salama
 
Wewe tafuta pesa kwa njia halali, usibeze Tiss kwa kukuharibia shughuli zako haramu, kama akaunti ina pesa haramu ni wajibu wao kuifunga hata kama kufanya hivyo hakutaboresha uchumi!
Wewe m.pumbavu usiejua hata kuandika na wewe ni "think tank" ya TISS?
Hebu niambie wale mliosema wameficha sukari mliishia wapi?
Makinikia mmeishia wapi?
Zile korosho mmeshawalipa wakulima?
Safari za ATCL mnazo cancel kila siku nazo vp?
Dola imepanda baada ya kunyang'anya hela na kufunga bureau de change?
Ajira mpya zimeishia wapi?
C.A.G naye ni fisadi? Mnona mnamuwinda?
ENDELEENI KUMPA USHAURI WA KIPUMBAVU MEKO ILI KULINDA MATUMBO YENU. TIME WILL TELL!.
 
Tatizo lenu mna uwezo mdogo mno wa kufikiria ,unajuaje Kama na mimi nimeiva ktk masuala ya intelligence?
Halafu ni wapi nimetukana zaidi ya kushauri?
TISS haiko imara ,ni kichaka cha CCM kufanya upumbavu wao.
Tungekuwa na TISS imara, hata uchumi ungekuwa imara, kwa sababu kazi za Taasisi Kama TISS ni kuhujumu mataifa mengine kwa maslahi ya nchi na siyo kuhujumu vyama vya siasa.
Ningeandika mazito ila namwonea huruma Melo watamtesa bure, hapa mbona nimeshauri tu, nikiweka nondo nzito hadi ikulu watapoteana.
Wewe kula ukalale huna unalojua, Tuachie sisi wanaume tuikosoe serikali.
Well said!.wanadhani kila anayeshauri humu ni CHADEMA. Wengine wapo nao humo humo ofisini ila hawataki ujinga.
 
Back
Top Bottom