Dkt. Kipilimba, sasa yatosha!

Dkt. Kipilimba, sasa yatosha!

Ndo uko sawa kabisa JKT inapaswa kurudi kisawasawa na mimi napendekeza vijana wakae kambini kwa miaka miwili.

Hii wanafanya Israeli na Korea Kusini na baadhi ya nchi zingine.

Hii itasaidia watu kushika moyo na kuonyesha wanaipenda nchi yao na wako tayari kuitumikia "no matter what".

Hata kama kuna kiongozi ambae na kasoro zake lakini linapokuja suala la ndege kuzuiwa nchi nyingine khasa ndege mpya watanzania wanaungana pamoja kutafakari juu ya mstakabali wa mali hiyo ya taifa.

Marekani pamoja na Donald Trump kufanya anayofanya lakini wakaikung'uta Syria kwa mabomu na sasa wanaishughulikia Iran na Korea Kaskazini, hiyo yote ni kwa "maslahi ya taifa" hilo.

Unafahamu hata nchi zilizoendelea likija jambo la "kwa maslahi ya taifa" wanageuka na kuunga mkono, hayo utaona kwenye televisheni, radio na magazaeti.

Masuala kama ya ugaidi na kutishia usalama wa mataifa yao wanaweza wakayaongelea kwa siku kadhaa masaa 24 na ukijaribu kubadilisha chennels habari ni hizohizo mpaka kieleweke mbele ya wananchi.

Viongozi mbalimbali, wasomi na watu wengine wa kada mbalimbali kwenye jamii wataitwa kwa interviews.

Sisi Tanzania kuna kitu kimeharibika ndani ya miaka 20 ilopita na tunapaswa kujitafakari na kujifunza uzalendo na kulinda maslahi ya taifa.
Mawazo ya kimasikini haya.

Vijana wasitafute maisha wakakae jeshini kisa uzalendo?

Upumbavu wa hali ya juu.
 
Nyepesi nyepesi ni kwamba huyu Mzee mda sio mrefu atapumzishwa kutokana na afya yake, na pale kuna mnyukano kwani aliependekezwa na Mkulu wenyewe hawajamkubali kwamba amekaa nje ya Taasisi na ndani wapo wenye sifa za kakalia kiti ya Kapilimba, za chini chini mle ndani kuna two blocks Mona iko unataka atoke ndani upande mwingne unasema hata aliyependekezwa anafaa, tusubiri!
Ameshapumzishwa.
 
... Nakumbuka Tukio moja (siwezi kulitaja) nilikuja kushtuka mission accomplished muda mrefu kumbe yule jamaa alikuwa TISS na akapotea kama jini....

ACHA NIWE MTABIRI WA TUKIO HILO, NALO NI "TUKIO LA AJALI YA KUCHONGWA ILIYOTOKEA HUKO MOROGORO (1984), NA KUSABABISHA KIFO CHA KIGOGO MMOJA ALIYEKUWA WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA😛😛"

Ouch!!, kumbe naota!!!
 
Unauhakika gani kipilimba bado ni ceo wa tiss? Je unaweza kuamin kama ameshatenguliwa?
Jioni hii n njema.
achaneni na kigogo. Huyu jamaa aliandika hiki kitu tarehe 29.... mwezi uliopita
 
Usichokijua ni bora tu kukaa kimya. Una uhakika gani kuwa hizi allegations zako TISS walikuwa hawazifahamu?

Una uhakika gani kuwa TISS hawakushauri lolote kabla ya haya kutokea?

Tanzania tuna bahati ya kuwa na taasisi imara. Hata wewe wakiamua kudeploy resources na kukufikia usiku huu wanakupata.

Usiku mwema!!
.....
....Mkuu upo
 
Ungeendelea na hiyo kazi yako ya kuchafua serikali na taasisi zake. Mkurugenzi wa TISS atakuwa mtu wa mwisho kabisa kupokea lawama na kuwajibika, in fact Dr. Kipilimba anafanya kazi kutokana na mabadiliko makubwa ya kisiasa, kiuchumi na uongozi wa awamu ya tano.
Pole kwa kazi mkuu
 
Ujue binadamu sisi ni watu wa ajabu sana. Mwenzio akiandika mada ukiona imekaa upande mmoja na we huna info za kutosha basi jiwie msomaji tuu. Kuna watu wameumbuka kwenye huu uzi
 
Kwa mara ya tatu tena nakuandikia Mzee wangu Dr Modestus Kipilimba, mkurugenzi mkuu wa idara ya usalama wa taifa, TISS.

Natamani sana, Rais Magufuli awe wa kwanza kusoma hii mada kabla yako.

Nimeshindwa kuendelea na kazi niliyokuwa naifanya usiku huu kwenye Computer, moyo wangu umekosa amani kabisa hadi niandike hii mada.

Dr. Kipilimba, unadhani bado unastahili kuongoza Idara nyeti na muhimu Kama hii ya TISS?

Kwanini mikononi mwako serikali ya awamu ya tano inadhalilika sana kimataifa?

Kwanini Idara yako imeruhusu uwepo wa watu Kama Musiba wanaokashifu viongozi wakubwa hadharani?

Sikufundishi kazi, ila nashangaa kwanini hujui kuwa idara kama TISS ndo Roho kamili ya Tanzania.

Kifo cha TISS ni kifo cha Tanzania, kwanini hujifunzi magumashi ya CIA, MI5, Mossad na mashirika mengineyo kama TISS?

Ninaposema magumashi nadhani umeelewa vizuri kabisa, maana nikielezea itahitaji kitabu.

Uimara wa TISS ndo Uimara wa Tanzania, na udhaifu wa TISS ndo udhaifu wa Tanzania.

Tunajua ya kwamba dawa ya Deni ni kulipa, lakini ilikuwaje TISS ikashindwa kubaini kuwa Steyn kafungua shauri mahakamani dhidi ya Tanzania kudai mali yoyote ya nchi ikamatwe?

TISS ingeitaarifu serikali basi, ndege isingeenda SA, na hivyo wangetafuta namna nyingine ya ku-solve tatizo.

Ni aibu kubwa mno nchi kudaiwa na raia mmoja Halafu mali ya nchi kukamatwa kwa Deni nje ya nchi, hii fedheha kubwa.

TISS mngeweza kuepusha hii fedheha. Kama TISS, ilishindwa kubaini njama za kutaifisha mali ya nchi, je itaweza kujua nini kinapangwa Somalia na Alshabab kwa mfano juu ya nchi?

Dr Kipilimba, TISS chini yako ni dhaifu mno, nakushauri u resign tu. TISS chini ya Dr Hansy Kitine na hayati Imran Kombe ilikuwa imara kupindukia.

Nakumbuka Tukio moja (siwezi kulitaja) nilikuja kushtuka mission accomplished muda mrefu kumbe yule jamaa alikuwa TISS na akapotea kama jini.

TISS ya leo imejaa vijana wa UVCCM, wasiojua lolote kuhusu intelligence wala miiko yake. Idara hii imegeuzwa kuwa ya kisiasa ili CCM itimize ndoto zake za alinacha za kutawala milele. Inashangaza sana, yaani Idara haikuweza hata kuzuia maandamano ya kuharibu Diplomasia yetu na SA.

Watumishi wa Idara hii wanatakiwa wawe wafia nchi (wazalendo kweli kweli) siyo wafia CCM au CHADEMA.

CCM itakufa, CHADEMA itakufa, lakiniTanzania ipo tu!
Kiongozi umeadimika jukwaani
 
Usichokijua ni bora tu kukaa kimya. Una uhakika gani kuwa hizi allegations zako TISS walikuwa hawazifahamu?

Una uhakika gani kuwa TISS hawakushauri lolote kabla ya haya kutokea?

Tanzania tuna bahati ya kuwa na taasisi imara. Hata wewe wakiamua kudeploy resources na kukufikia usiku huu wanakupata.

Usiku mwema!!
Sio kweli.
 
Back
Top Bottom