Dini ni Utamaduni wa watu fulani

Dini ni Utamaduni wa watu fulani

Na mimi sikusudii mjumbe ni mtu yoyote, mimi namkusudia yule aliyezungumziwa katika aya.

Almuhimu unatakiwa usome fasiri za Qur'aan hasa zile za "Maathuri" zinazofasiri aya kwa hadithi, na soma kitabu cha Imaam Muhammad al Amin ash Shanwitwy kiitwacho "Da'fu Ihaam adh Twirasb 'an ayaat al Kitaab",uone namna wanavyo oanisha aya kwa aya au aya hadithi na kupata jibu moja.
Sasa wewe unajenga hoja alafu unanipa marejeo.

Wewe unatakiwa uweke hapa hayo marejeo na hizo hadithi.

Sioni kama ni sahihi unajadiliana na mtu alafu unajenga hoja kwa ushahidi ambao upo kwako.

Wewe ndo utoe hayo marejeo na sio unaniambia mimi nikapitie,wewe kwa nini usilete hapa.

Kama mjumbe unakubali kuwa ni mtume kwa nini unakataa kuwa kila umma walipata mjumbe ?
 
Umma, ukisoma aya katika matini yake, imekuja "Rasula" kwa maana ya mtume kilugha kama alivyofasiri Shaykhul Islaam katika majmui al Fatawa unawatoa manabii, lakini aya inajumuisha na manabii kadhalika, hii uone ya kuwa linalo kusudiwa hapo ni wingi wa watu.

Soma Kamusi uone maana ya umma, kwamba siyo lazima uwe wote duniani, ndiyo maana hata nabii Ibrahiim aliitwa "Ummah" japokuwa alikuwa peke yake, lakino aliitwa vile sababu alikuwa kwenye haq.
Kundi la watu wangapi ili waitwe ummah ?

Kwa sababu
Unajua kwamba mjumbe wapo walikuwa wanakuja kwa ajili ya mji au koo fulani, huo ni umma mzee, hata nabii Issa alitumwa kwa Wana wa Israeli na si katika umma wote wa dunia nzima, na ndiyo maana ule pia unaitwa umma, umma siyo lazima uwe dunia nzima mzee, hili unatakiwa uelewe, mtume pakee aliye tumwa kwa ajili ya ulimwengu mzima ni mtume Muhammad pekee.
Tunakubaliana kuwa kila ummah ulipewa Mtume.

Sasa nipe wewe maelezo yanayoonesha kuwa kuna nyumati ambazzo hazikupewa utume.

Na hayo maelezo uyaweke hapa yaseme kuwaa kuna ummah fulani haukupata mtume.

Maelezo yakisema kuwa kuna watu fulani hawakupata mtume hayo maelezo ni baatwil kwa sababu sio kila watu ni ummah.

Hayo marejeo yako yaweke hapa tuone usahihi wa mambo.
 
Umma, ukisoma aya katika matini yake, imekuja "Rasula" kwa maana ya mtume kilugha kama alivyofasiri Shaykhul Islaam katika majmui al Fatawa unawatoa manabii, lakini aya inajumuisha na manabii kadhalika, hii uone ya kuwa linalo kusudiwa hapo ni wingi wa watu.
Kwa hiyo kama ni hivyo sio kila watu ni ummah.

Na kila ummah lazima uwe na watu.

Sasa mbona hao watu ambao hawakupata mjumbe kwa nini uwatie katika ummah ilhali sio kila watu ni ummah ?
 
Kwa ufupi sana ili tusizongane..

Kwa mujibu wa uislamu umma ni nini na uweje ili uwe umma ?
Tamko umma katika Uislamu limekuja kwa minasaba zaidi ya mitani au minne, na munasaba wa chini zaidi ukikusudia mtu mmoja, kama ilivyokuja aya kumuongelea nabii Ibrahiim.

Kadhalika, tamko Umma kilugha ni tamko la Kiarabu kwalo wingi wake ni "Umaam" na hili hujumuisha watu wengi wenye kushirikiana juu ya mambo ya kijamii, kiada na shughuli nyinginezo.
 
Sasa wewe unajenga hoja alafu unanipa marejeo.
Lazima nikupe marejeo sababu Elimu ni amana, na kila amana hurudishwa kwa watu wake, na mimi nakurudisha kwa watu wa Elu, kasome, na ninayo kuandikia hapa ndiyo utayakuta humo humo, ili ujihukumu mwenyewe.

Pili, naweka marejeo kwa mtindo huo ili kuokoa muda.
Wewe unatakiwa uweke hapa hayo marejeo na hizo hadithi.
Mpaka sasa hivi nimeshakumulia ile hadithi, aliyo isimulia al Imaam Ahmad, sasa kama hujaisoma hilo ni tatizo lako la kutokuwa makini, na nikakupa marejeo mengine ili ukasome na upate faida zaidi.

Nafanya hivi, sababu hapa tunajadili jambo la kielimu, na hakuna kipya zaidi ya kunukuu toka kwa wakubwa zetu, walio tuzidi kwa ubora,elimu na maarifa bali mpaka umri.
Sioni kama ni sahihi unajadiliana na mtu alafu unajenga hoja kwa ushahidi ambao upo kwako.
Ushahidi upo kwangu kivipi wakati nimekuwekea marejeo, unakumbuka ile nukuu uliyo niwekea kuhusu maneno aliyo yasema al Imaam Muqbil na unajua kwanini sikuendelea na lile jambo, sababu nilienda kusoma zaidi, na mimi nakuwekea marejeo kwa uwazi na si wewe peke yako usome bali yeyote atakae pita hapa aone na akosome kwa faida zaidi.
Wewe ndo utoe hayo marejeo na sio unaniambia mimi nikapitie,wewe kwa nini usilete hapa.
Sasa nitoe marejeo mara ngapi wakati kila hoja nakupa marejeo ukasome ? Au unataka nini zaidi ya hivyo ?

Hivi kuna jambo bora kuliko ninalo lifanya mimi, la kukutajia kitabu na nina la muandishi wa kitabu hicho, ili ukasome mwenyewe kama hukuelewa ukaulize upate ufafanuzi zaidi. Sasa naona unataka kunipotezea muda mzee.
Kama mjumbe unakubali kuwa ni mtume kwa nini unakataa kuwa kila umma walipata mjumbe ?
Hakuna aliye kataa ya kila umma uliletewa mjumbe, bali nakataa ya kuwa si sawa ya kusema ya kuwa hakuna watu ambao hawakufikishiwa mtume, sasa sababu Qur'aan na Hadithi thi hazipingani, ulitakiwa ukawaulize wakubwa zako ni vipi wanao anisha nususi hizi mbili na kupata jibu moja.

Kwa maana hiyo kabisa iko wazi ni kuwa wewe hujaelewa maana ya aya.
 
Kundi la watu wangapi ili waitwe ummah ?

Kwa sababu
Kuanzia mtu mmoja huitwa umma kama akiwa kwenye haki,kama ilivyo kuja katika aya kumuhusu nabii Ibrahiim.
Tunakubaliana kuwa kila ummah ulipewa Mtume.
Hili nakubali ila kwa ile dhati ya watu husika ambao wamefikiwa na ujumbe ila si kwa ujumla.
Sasa nipe wewe maelezo yanayoonesha kuwa kuna nyumati ambazzo hazikupewa utume.
Nikupe maelezo mara ngapi na hadithi nimekuwekea hapa, iliyo simuliwa na Imaam Ahmad katika Musnad yake na al Imaam Al Bayhaaq katika kitabu chake "al 'Itiqaad" ? Inaonekana husomi hoja zangu, sina maelezo mengine zaidi ya kukunukulia nususi.
Na hayo maelezo uyaweke hapa yaseme kuwaa kuna ummah fulani haukupata mtume.

Maelezo yakisema kuwa kuna watu fulani hawakupata mtume hayo maelezo ni baatwil kwa sababu sio kila watu ni ummah.

Hayo marejeo yako yaweke hapa tuone usahihi wa mambo.
Naona sasa mada imekuzidi uwezo na unakataa maneno ya mtume yaliyo wazi kabisa, mtume amesema na watu hao huitwa "ahlul Fitrah" na hawa watapewa mtihani siku ile ile ya Hukumu.

Marejeo niweke mara ngapi, labda kama useme hujui Kiingereza, maana niliweka marejeo hayo kwa Kiingereza au hukuwa makini katika kusoma nilicho kiandika, moja ya majibu haya ni sahihi.

Huna uwezo wa kubatilisha maneno ya mtume kijana, unapoelekea unajiingiza kwenye madhambi, soma maneno ya Imaam Shawkaniy kuhusu ya kuwa Qur'aan na Hadithi havipingani na ukiona hilo ujue huna elimu na akili yako ni ndogo kung'amua nususi hizo.
 
Kwa hiyo kama ni hivyo sio kila watu ni ummah.

Na kila ummah lazima uwe na watu.

Sasa mbona hao watu ambao hawakupata mjumbe kwa nini uwatie katika ummah ilhali sio kila watu ni ummah ?
Hao ni umma kwa maana ya munasaba maalumu wa kilugha.
 
Hao ni umma kwa maana ya munasaba maalumu wa kilugha.

Nimepotea muda mrefu sana humu kutokana na uhaba wa wakati.

Nimefuatilia hoja zako kwa bahati mbaya sijaona dalili za wewe kunielewa japokuwa mimi nakuelewa unachomaanisha.

Ila yale ambayo nimeyamaanisha na ninayakusudia bado naona hujanielewa na ijaona dalili za kunielewa.

Kwa kuwa lengo langu sio kulaziminsha unielewe,na lengo sio kubishana basi mimi nimeona bora tuliwache hili kwa sababu kwa mfumo huu muafaka ni mgumu japo kuwa mengi ya kuuliza ninayo ila tungeishia hapo.
 
Nimepotea muda mrefu sana humu kutokana na uhaba wa wakati.

Nimefuatilia hoja zako kwa bahati mbaya sijaona dalili za wewe kunielewa japokuwa mimi nakuelewa unachomaanisha.

Ila yale ambayo nimeyamaanisha na ninayakusudia bado naona hujanielewa na ijaona dalili za kunielewa.

Kwa kuwa lengo langu sio kulaziminsha unielewe,na lengo sio kubishana basi mimi nimeona bora tuliwache hili kwa sababu kwa mfumo huu muafaka ni mgumu japo kuwa mengi ya kuuliza ninayo ila tungeishia hapo.
Usipate shida nenda kasome utabainikiea na mambo mengi usiyo yajua.

Marejeo yapo mengi sana ni wewe kurejea na kuwauliza unao waamini ambao wamekuzidi katika maarifa, hivi ndivyi huwa tunafanya.
 
kabisa, mtume amesema na watu hao huitwa "ahlul Fitrah" na hawa watapewa mtihani siku ile ile ya Hukumu
hapana ngoja niendelee.

Kwani Mtume kasema ummatul fitrah au ahlul fitrah ?

Kwani ahlul na ummah ni sawa kwa mujibu wa kauli hiyo ya Mtume ?
 
hapana ngoja niendelee.

Kwani Mtume kasema ummatul fitrah au ahlul fitrah ?

Kwani ahlul na ummah ni sawa kwa mujibu wa kauli hiyo ya Mtume ?
Mbona unauliza swali la kitoto mzee, kama Ibrahimu alikuwa ni umma na hali ya kuwa alikuwa mmoja, vipi ahlul fitrah wasiwe umma ?

Kaka usijiumize bure, rejea hadithi iko wazi sana ile katika musnad ya Imaam Ahmad.
 
Hili nakubali ila kwa ile dhati ya watu husika ambao wamefikiwa na ujumbe ila si kwa ujumla.
Alaaaa

Sasa hapa ulichomaanisha ni kuwa

"wale waliofikowa na mtume ama ujumbe wa Mtume hao ndio ummah,kwa maana wale ambao hawakufikiwa na utume sio ummah ?

Hapa nimekunuku vibaya mkuu ?
 
Mbona unauliza swali la kitoto mzee, kama Ibrahimu alikuwa ni umma na hali ya kuwa alikuwa mmoja, vipi ahlul fitrah wasiwe umma ?

Kaka usijiumize bure, rejea hadithi iko wazi sana ile katika musnad ya Imaam Ahmad.
Nabi ibrahim kuwa ummah maana yake ni ile ummah ya kuwa yupo katika haki na sio ummah ya watu.

Usijaalie ummah ya haki ukaifanya ummah ya watu huo sio ufahamu sahihi.

Au unataka kutuambia kuwa kila neno ummah lina maana kama ile ya nabi ibrahimu ?
 
Nabi ibrahim kuwa ummah maana yake ni ile ummah ya kuwa yupo katika haki na sio ummah ya watu.

Usijaalie ummah ya haki ukaifanya ummah ya watu huo sio ufahamu sahihi.

Au unataka kutuambia kuwa kila neno ummah lina maana kama ile ya nabi ibrahimu ?
Safi kabisa sasa maana ya ummah inafasiriwa kwa namna zaidi ya tano, na hao ahlul fitrah wanaingia katika ummah.
 
Kuna marejeo pale, tafuta kitabu Musnad cha al Imaam Ahmad bin Hanbal, chapa ya Kiarabu usome.
Mmi nakuhoji wewe.

Wewe kasome huko alafu lete marejeo kama ambavyo mimi nimekueletea ile kauli ya shekhe muqbili ukaiona.

Vile mimi ndo nafanya,mfumo wako siwezi kuufata kwa sababu ubainifu ni kwa yue mwenye madai ndo alete,sio aoneshe ubainifu ulipo bali aulete sehemu hiska watu wauone.

Kwa hiyo unapoenda mahakamani ushahidi usiuache nyumbani alafu ukawaambia watu kachukueni ushahidi nyumbani,wewe ndo uulete hapa mahakamani.

Utaratibu wako huo sio mzuri kwa mtazamo wangu ndio maana huwa naupuuza.
 
Safi kabisa sasa maana ya ummah inafasiriwa kwa namna zaidi ya tano, na hao ahlul fitrah wanaingia katika ummah.
Hhaha sasa mbona ukairejea maana ya ummah ya nabii ibrahimu wakati ile haiendani na maana ya ummah tunayoijadili hapa mzee zurri..

Kwa hoja gani waingie katika ummah hao ahlul fitrah ?
 
Mmi nakuhoji wewe.

Wewe kasome huko alafu lete marejeo kama ambavyo mimi nimekueletea ile kauli ya shekhe muqbili ukaiona.
Nikuwekee marejeo mara ngapi ? Wewe umedai hujui Kiingereza, sasa ukirejea katika yale marejeo itaona utafute yale marejeo kwa lugha unayo ielewa wewe ndiyo maana tunaweka marejeo na majina ya vitabu na waandishi, kwahiyo hilo la kuleta tena marejeo hali ya kuwa nimeshaleta ni kupotezeana muda.
Kwa hiyo unapoenda mahakamani ushahidi usiuache nyumbani alafu ukawaambia watu kachukueni ushahidi nyumbani,wewe ndo uulete hapa mahakamani
Hili tatizo lingine, kwa kuleta mambo ambayo si katika muktadha husika, nimekuwekea marejeo ukasema kiingereza hukijui, sasa unaposema hujapewa marejeo wakati unakiri ya kuwa kiingereza hukijui, huu ni utoto mwinginge, sasa nimekukumbusha ya kuwa, rejea yale marejeo niliyo kupa kisha tafuta chapa ya asili ya kiarabu usome.
Vile mimi ndo nafanya,mfumo wako siwezi kuufata kwa sababu ubainifu ni kwa yue mwenye madai ndo alete,sio aoneshe ubainifu ulipo bali aulete sehemu hiska watu wauone.
Ulicho kifanya wewe kwa Sheikh Abuu Adhulrahma Muqhil Allah Amrahamu, ndiyo nilochokifanya mimi kwa lugha Kiingereza, na ile nukuu toka katika ile tovuti ikakurudisha katika kitabu, sasa nimekupa marejeo na jina la kitabu na muandishi, sasa usisema uongo mzee.
 
Hhaha sasa mbona ukairejea maana ya ummah ya nabii ibrahimu wakati ile haiendani na maana ya ummah tunayoijadili hapa mzee zurri..
Nimekuonyesha ya kuwa hakuna ummah bila watu, hata ukiwa mtu mmoja leo hii ukiwa umeshikamana na haki, unaitwa ummah.

Ummah tunayo ijadili hapa nimeshakueleza huko nyuma kwamba kilugha ni mjumuiko wa watu fulani ambao wanaishi chini ya ada na kushurikiana katika mambo ya kimuamala, kotamaduni na kijamii, kwahiyo hata wakiwa kadhaa hao ni ummah.
Kwa hoja gani waingie katika ummah hao ahlul fitrah ?
Hoja ya maana ya ummah, wanaingia hao ahlul fitrah, na hadithi imethibitisha wazi kabisa ya kuwa kuna watu hawakufikiwa na ujumbe.
 
Back
Top Bottom