KAYGREKO
Member
- Jan 18, 2013
- 37
- 32
DIASPORA NA DENI LA TAIFA
Hakuna takwimu kamili, lakini inaaminika watanzania tuliopo ughaibuni tunafika milioni mbili.
Aidha wengi tunaoishi ughaibuni, tunajua nchi yetu ina deni la nje na la ndani japo wengi hawajui kiuhakika ni kiasi gani.
Leo ningependa kuja na ushauri ambao kwa wale wataouona ni ndoto za Abunuwasi ni vyema wakakaa kimya. Ama wale wataoona unafaa ila una makosa yatayohitaji kurekebishwa ni vyema warekebishe huenda tukapata pa kuanzia.
Hapa Ugiriki wakati ule wa Crisis iliyotufikisha kwenye Capital control,tukawa tunakadiriwa kiwango kidogo cha kutoa pesa kwenye ATM,na wengine walipoteza ajira wakashindwa hata kumudu mahitaji muhimu, ulibuniwa mfumo wa kusaidiana (HAUKUANZISHWA NA SERIKALI WALA VYAMA VYA KISIASA) Wagiriki waliopo nje ya nchi nao walishiriki ipasavyo.
Hapa sitopenda kufafanua nini walifanya bali nitapenda kujikita katika mazingira yetu sisi watanzania milioni mbili tuishio ughaibuni.
Nimejiuliza swali lifuatalo: Badala ya kutumia usd 50 kwenda angalia mechi moja, au kutumia euro 50 kunywa bia na nyama choma, au(,….) hivi kweli tutashindwa kujitolea japo usd MOJA TU? (au 2,5,10 au zozote atazoweza kila mmoja wetu kulingana na uwezo wake? Of course siyo wote watakaotoa lakini idadi yoyote itayopatikana itakuwa imesaidia. Hili linawezekana kama tutakuwa tumeelewa na kuuona umuhimu wa kupunguza deni.
Najua kuna wataohoji ni bora hiyo dola moja wakawatumia wazazi wao na wengine wataohoji kuwa hizo zitaibwa,zitatumika vibaya nk. Lakini inabidi tufike mahala kama taifa tuanze kujijengea utamaduni wa kupenda kusaidia taifa hadi tunaowapa majukumu nao wafike mahala wahisi uzito wa majukumu yao.
Huku ughaibuni kuna waTZ wana ujuzi na utaalam wa hali ya juu mno wakikaa wanaweza kutupatia mfumo mzuri wa kuhakikisha hizo pesa tutazochangia zinaonekana wapi zilipofika.
Je unaliboreshaje wazo hili ili tupate pa kuanzia ?
KAYU LIGOPORA
ATHENS – GREECE
28/10/2021
Hakuna takwimu kamili, lakini inaaminika watanzania tuliopo ughaibuni tunafika milioni mbili.
Aidha wengi tunaoishi ughaibuni, tunajua nchi yetu ina deni la nje na la ndani japo wengi hawajui kiuhakika ni kiasi gani.
Leo ningependa kuja na ushauri ambao kwa wale wataouona ni ndoto za Abunuwasi ni vyema wakakaa kimya. Ama wale wataoona unafaa ila una makosa yatayohitaji kurekebishwa ni vyema warekebishe huenda tukapata pa kuanzia.
Hapa Ugiriki wakati ule wa Crisis iliyotufikisha kwenye Capital control,tukawa tunakadiriwa kiwango kidogo cha kutoa pesa kwenye ATM,na wengine walipoteza ajira wakashindwa hata kumudu mahitaji muhimu, ulibuniwa mfumo wa kusaidiana (HAUKUANZISHWA NA SERIKALI WALA VYAMA VYA KISIASA) Wagiriki waliopo nje ya nchi nao walishiriki ipasavyo.
Hapa sitopenda kufafanua nini walifanya bali nitapenda kujikita katika mazingira yetu sisi watanzania milioni mbili tuishio ughaibuni.
Nimejiuliza swali lifuatalo: Badala ya kutumia usd 50 kwenda angalia mechi moja, au kutumia euro 50 kunywa bia na nyama choma, au(,….) hivi kweli tutashindwa kujitolea japo usd MOJA TU? (au 2,5,10 au zozote atazoweza kila mmoja wetu kulingana na uwezo wake? Of course siyo wote watakaotoa lakini idadi yoyote itayopatikana itakuwa imesaidia. Hili linawezekana kama tutakuwa tumeelewa na kuuona umuhimu wa kupunguza deni.
Najua kuna wataohoji ni bora hiyo dola moja wakawatumia wazazi wao na wengine wataohoji kuwa hizo zitaibwa,zitatumika vibaya nk. Lakini inabidi tufike mahala kama taifa tuanze kujijengea utamaduni wa kupenda kusaidia taifa hadi tunaowapa majukumu nao wafike mahala wahisi uzito wa majukumu yao.
Huku ughaibuni kuna waTZ wana ujuzi na utaalam wa hali ya juu mno wakikaa wanaweza kutupatia mfumo mzuri wa kuhakikisha hizo pesa tutazochangia zinaonekana wapi zilipofika.
Je unaliboreshaje wazo hili ili tupate pa kuanzia ?
KAYU LIGOPORA
ATHENS – GREECE
28/10/2021