Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,502
- 9,283
Mkurugenzi wa kampuni ya Wasafi, msanii Diamond Platnumz ametoa msaada wa kodi ya pango kwa watu 57 ambao ni wajane, walemavu pamoja na wasiojiweza.
Msaada huo ni awamu ya kwanza katika ile dhamira yake ya kusaidia kodi ya pango kwa kaya 500 nchini zilizoathirika kiuchumi na janga la mlipuko wa virusi vya Corona.
Diamond Platnumz ametoa msaada huo leo katika makao makuu ya ofisi za kampuni ya WasafiMedia baada ya watu zaidi ya 100 kujitokeza ofisini hapo ambapo familia 57 zimeweza kupata msaada huo.
Kufuatia jambo hilo, familia zilizobakia kwenye orodha ya kaya 500 ni 443 ambapo mchakato unaendelea kwa ajili ya kuzipata kaya za wajane, walemavu na wasiojeweza.
==============
Fuatilia Diamond alivyoahidi:
Msanii Diamond Platnumz kulipa kodi ya nyumba ya miezi 3 kwa familia 500 za hali ya chini - JamiiForums