Dhibiti muda anaospend mumeo kwa small house...

Dhibiti muda anaospend mumeo kwa small house...

Husninyo

Platinum Member
Joined
Oct 24, 2010
Posts
24,255
Reaction score
10,503
haya jamani.... kwa wale waliiolewa na wanahisi wanaume zao wana nyumba ndogo, hii inawahusu, siguarantee kuwa mmeo atamuacha huyo (kama anae) ila itasaidia kufanya nyumba yako isitetereke.

1.dhibiti matumizi ya simu.

kiukweli mawasiliano ndio msingi imara wa mahusiano yoyote. mawasiliano yanapokuwa lege lege hata penzi hufifia na linaweza kufa kabisa. hapa cha kufanya ni kumdhibiti baba watoto, akishaingia nyumbani hakuna kuchati chati tena, hakikisha hawi karibu na simu yake. sio mwanaume mpaka mnapanda kitandani yeye anachati tu, sa tano za usiku anachati na nani? hapo unaibiwa. akifika home ni muda wake yeye na familia tu, kismol house kama kipo kisubiri text msg kesho.

2. dhibiti mapato na matumizi.
small house siku zote yupo kipesa zaidi, kama mmeo anamwaga madolari ya kutosha si ajabu small house akang'ang'ania hapo mpaka azeekee kwa mmeo. katika kudhibiti mapato yenu mnaweza mkawa mnaandaa budgets zenu pamoja, mnapanga kiasi gani mnaiingiza kwa mwezi na vipi mtatumia.kudhibiti mapato itasaidia kupunguza fungu analokabidhiwa bi mdogo na si ajabu akakimbia mwenyewe baada ya kuona hakuna mavuno tena. kama mna mapato makubwa na matumizi mengi mnaweza kuajiri financial controller kabisa. lol.

3.verify safari zake za kikazi.

wanaume wenye vismall houses wakipata safari za kikazi unaweza kuta siku tatu kazini siku nne kwa bi mdogo wewe nyumbani unaambiwa safari ya siku saba kumbe mtu kasharudi amejichimbia sehemu wanakula bata. hapa unatakiwa kukaba, hakikisha siku ya safari unamsindikiza uwanja wa ndege au stand ya mkoa na siku ya kurudi ukampokee, hakikisha anarudi na risiti ya hotel na tickets za bus/ndege (tena hapa tafuta na file kabisa la kuwekea hizo receipts, mwambie umeanza utaratibu wa kutunza kumbukumbu. lol).

4.dhibiti ratiba zake za weekend.

uwe unatoka nae weekend, mnaweza kuwa mnaenda tembelea shamba, shopping na familia, beach, etc. jitahidi kuvurugua ratiba zake za weekend haswa zile ambazo una mashaka nazo... nyumba ndogo akikosa muda wa kuspend na mmeo ndio dalili nzuri la penzi lao kuchuja huku lako likishine.


5.timiza wajibu wako kama mke na ibada za pamoja.

hapa kila mtu anajua wajibu wake na anayoyafanya kudumisha furaha ya ndoa. usihesabu mazuri unayomfanyia mwenzio. we endelea kufanya tu. pia jiwekeni karibu na mungu kwa kusali pamoja na kufanya yale mema kwa pamoja.

mwageni mambinu jamani hata kama ni ya kialshabab! hizi zinafaa kwa mnaokaa nyumba moja.
 
Husninyo dah sawa kabisa ila kumbuka kuwa mwanaume mwenye small house akiamua hata ule muda wa kazi atacheat tuu na wala huwezi kuzuia
Nitasafiri utanisindikiza na utakuja kunipokea ila kumbuka huko hotelini ninakolala hauko na mimi nalala na mtu ninayependa kuwa nae na nikitaka hata small house yangu naitumia nauli inanifuata nakaa nae na siku ya kurudi kila mtu na usafiri wake
 
Last edited by a moderator:
Mmimi nikifanyiwa yote hayo na ndoa itakufa.....hata kama sina nyumba ndogo

crazy women......danganyaneni humu msisahau ALL MEN NEED SPACE SOMETIMES...
The Boss umeongea
we need space bana simu yangu unipangie muda wa kuchat na kuongea
Safari niende na ofisi inidai risiti na wewe mke unadai risiti ahhh mambo gani hayo
 
Last edited by a moderator:
Husninyo dah sawa kabisa ila kumbuka kuwa mwanaume mwenye small house akiamua hata ule muda wa kazi atacheat tuu na wala huwezi kuzuia
Nitasafiri utanisindikiza na utakuja kunipokea ila kumbuka huko hotelini ninakolala hauko na mimi nalala na mtu ninayependa kuwa nae na nikitaka hata small house yangu naitumia nauli inanifuata nakaa nae na siku ya kurudi kila mtu na usafiri wake

ndio maana nimesema tunapunguza tu muda wa nyie kuspend na vismol house, haiguarantee kuwa mtaacha kuwa navyo. lol
 
Last edited by a moderator:
Mmimi nikifanyiwa yote hayo na ndoa itakufa.....hata kama sina nyumba ndogo

crazy women......danganyaneni humu msisahau ALL MEN NEED SPACE SOMETIMES...
anaekubana bana anakupenda the boss, hapendi uangukie huko.
 
Husninyo dah sawa kabisa ila kumbuka kuwa mwanaume mwenye small house akiamua hata ule muda wa kazi atacheat tuu na wala huwezi kuzuia
Nitasafiri utanisindikiza na utakuja kunipokea ila kumbuka huko hotelini ninakolala hauko na mimi nalala na mtu ninayependa kuwa nae na nikitaka hata small house yangu naitumia nauli inanifuata nakaa nae na siku ya kurudi kila mtu na usafiri wake

Ni kweli kabisa utajitia presha bure.....we uko busy kumdthibiti..........

Kama atafanya atafanya tu hata umfanyie nini!!!!!!!!!!!!Things are more complicated sana
 
mume muachie nafasi afanye yake,, ukiwa mke timiza wajibu ako kama mke!!!!!! mbona aman itakuwepo lkn kufanya hayo shoga unachimba kaburi la ndoa yako kwa mikono yako!!!
 
The Boss umeongea
we need space bana simu yangu unipangie muda wa kuchat na kuongea
Safari niende na ofisi inidai risiti na wewe mke unadai risiti ahhh mambo gani hayo

...waache wadanganyane hapa,,, then wabebe hizi theory wakapractice waone nini kitatokea......eti mapato yetu,,, risiti wazihifadhi,,, wakati ni lazima ziende ofcs as returns.......mwanaume haka ukifanya nae ofc 1 atakucheat tuu.....kuwa mpole na ridhika na upatayo,,,, basi...
 
Mh hiyo ya kumuharibia ratiba zake za weekend inaweza kuwork tena mara chache chache sana,ila kuanza kuchunguzana sijui lete risiti za hotel kwan we ndo office ulimtuma huko?
Kucontrol matumiz ni ngumu sana kama haujui mapato halisi ya mume wako,labda uwe HR wa anapofanyia kazi maana ni ngumu kujua pato lake halisi km c HR wala hajakushiriksha na haujawah kuona salary slip yake hata kwa bahat mbaya.
Ngumu kumcontrol mwanaume aisee ni kumuomba Mungu tu,kwanza cdhan kama kuna mwanaume ambaye anakuwa controled ivo...
Ndo unafanya yote hayo af mwisho wa siku unagundua c tu anacheat bali anafamilia kabs huko nje,pamoja na kumbana kote huko,lazima upaniki
 
Commitment ya ndoa haina maana ya kuuza uhuru wako wote,kuna degree inatakiwa iwe reserve kwa ajili ya mambo binafsi...though mimi sio muumini ya dhana ya ndoa mbili ila nikijua wife ananichimba to that extent ndoa itapiga mwereka!
 
Back
Top Bottom